Ritz
JF-Expert Member
- Jan 1, 2011
- 46,918
- 32,335
Wanabodi,
Hii ndio wiki ya mwisho kwenye kampeni za uchaguzi mdogo jimbo la Arumeru Mashariki hali ni ngumu kwa Chadema.
Timu ya kampeni ya CCM inayoongozwa na Mwigulu Nchemba, Steven Wassira, Christopher Ole Sendeka, Livingstone Lusinde chini ya Edward Lowassa.
Hawa jamaa wamefanikiwa kufunika kabisa siasa za Chadema kwenye kampeni huko Arumeru Mashariki.
Timu ya kampeni ya Chadema inayoongozwa na Vincent Nyerere, Godbless Lema, chini ya W. Slaa na Freeman Mbowe.
Kuchelewa kurudi kwa Mbowe katika dulu lala salama kumesababishwa kushindwa kwake kuwashawishi wazee wa kimila kumunga mkono Nassari.
Tatizo lingine la Chadema wanahubiri mambo kiujumlajumla, hawasemi watatatuaje kero ambazo CCM wameshindwa kuzitatua.
Tathmini iliyofanywa huko Arumeru Mashariki inaonyesha Lowassa na Slaa wana ushawishi mkubwa ndani ya jimbo hilo, Lakini Slaa anazidiwa kete kutokana na mila na desturi za jamii yake ya Karatu kuwa na tofauti kubwa na za jamii ya Wamasai na Wameru.
Sasa hivi Chadema wamebaki kulalamika wanatukanwa wakati wamesahau kuwa kina Lema, ndio walianza siasa chafu za kumchafua Sioi Sumari.
Hii ndio wiki ya mwisho kwenye kampeni za uchaguzi mdogo jimbo la Arumeru Mashariki hali ni ngumu kwa Chadema.
Timu ya kampeni ya CCM inayoongozwa na Mwigulu Nchemba, Steven Wassira, Christopher Ole Sendeka, Livingstone Lusinde chini ya Edward Lowassa.
Hawa jamaa wamefanikiwa kufunika kabisa siasa za Chadema kwenye kampeni huko Arumeru Mashariki.
Timu ya kampeni ya Chadema inayoongozwa na Vincent Nyerere, Godbless Lema, chini ya W. Slaa na Freeman Mbowe.
Kuchelewa kurudi kwa Mbowe katika dulu lala salama kumesababishwa kushindwa kwake kuwashawishi wazee wa kimila kumunga mkono Nassari.
Tatizo lingine la Chadema wanahubiri mambo kiujumlajumla, hawasemi watatatuaje kero ambazo CCM wameshindwa kuzitatua.
Tathmini iliyofanywa huko Arumeru Mashariki inaonyesha Lowassa na Slaa wana ushawishi mkubwa ndani ya jimbo hilo, Lakini Slaa anazidiwa kete kutokana na mila na desturi za jamii yake ya Karatu kuwa na tofauti kubwa na za jamii ya Wamasai na Wameru.
Sasa hivi Chadema wamebaki kulalamika wanatukanwa wakati wamesahau kuwa kina Lema, ndio walianza siasa chafu za kumchafua Sioi Sumari.