Sokomoko
JF-Expert Member
- Mar 29, 2008
- 1,915
- 127
CHADEMA wazidi kuitesa CCM
Mwenyekiti Mbowe akihutubia Musoma mjini
na Kulwa Karedia
MAMIA ya wakazi wa mji wa Musoma na vitongoji vyake jana walijitokeza kwa wingi katika uzinduzi wa kampeni ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Operesheni Sangara, ambapo wito ulitolewa kwa Rais Jakaya Kikwete kuwafikisha mahakamani mafisadi wote walioiba fedha katika Akaunti ya Malipo ya Nje (EPA).
Wito huo ulitolewa mjini hapa na Katibu wa chama hicho, Dk. Willibrod Slaa, wakati akihutubia mamia ya wananchi kwenye uwanja wa Shule ya Msingi ya Mkendo.
Alisema endapo Rais Kikwete atashindwa kuwashughulikia mafisadi hao, ni bora kuwaachia wafungwa wote waliomo katika magereza mbalimbali nchini.
Mkakati wa Operesheni Sangara umelenga zaidi kupeleka madaraka kwa wananchi kuanzia ngazi za chini hadi taifa, ili kujenga uwezo wa chama.
Napenda kumwambia Rais Kikwete kwamba sasa muda wa Rais Kikwete kuona kipimo cha uongozi wake ni Oktoba 31 pale atakapowafikisha mahakamani mafisadi wote lakini kama hatafanya hivyo, tunasema wafungwa wote walioko gerezani waachiwe, ili haki itendeke kwa wote, alisema Dk. Slaa.
Alisema iwapo Rais Kikwete atashindwa kufanya hivyo atasababisha wananchi kuendelea kupoteza imani kwake, kama sasa ambapo wamefikia hatua ya kupiga mawe msafara wake.
Ni jambo la ajabu mkuu wa nchi kutupiwa mawe akiwa katika shughuli za serikali. Hii inaonyesha wazi jinsi wananchi walivyoanza kuchoshwa na serikali yake tunasema kama ataendelea na mwenendo huu anastahili kuondolewa hata kesho, alisema Dk. Slaaa.
Alisema kushindwa kwa serikali ya Kikwete kutoa maisha bora kwa kila Mtanzania kumetokana na wasaidizi wake wengi kujali masilahi binafsi, badala ya kutumikia umma.
Alisema tangu Rais Kikwete alipoingia madarakani wananchi walikuwa na matumaini makubwa, lakini hivi sasa wamekata tama, baada ya kunyanyaswa na watu waliopewa dhamana ya kuwasaidia.
Dk. Slaa alisema pamoja na hatua atakazochukua Rais Kikwete juu ya mafisadi, bado CHADEMA italipua bomu la ufisadi wa sh milioni 155 zilizoibiwa katika mgodi wa dhahabu wa Buhemba kupitia Kampuni ya Meremeta inayomilikiwa na Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ).
Rais tulimwambia mambo mengi kuhusu wizi wa fedha za umma, lakini tunashangaa kuona ameamua kushughulikia EPA peke yake, nawaambia jamani tulimwambia atupatie maelezo, lakini amekuwa akitukwepa kila siku.
Ufisadi mkubwa uliofanywa kwenye Kampuni ya Meremeta chini ya JWTZ sasa tunasema tutawasha moto hadi kuona waliochukua fedha hizi wanajulikana, alisema Dk. Slaa.
Kwa upande wake, Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho, Zitto Kabwe, alisema serikali ya CCM imechoka na sasa umefika wakati wa kukaa kando na kuachia kizazi kipya ambacho anaamini kuwa kitaleta mageuzi ya kweli.
Chama kimejaa mafisadi, wanalindana, wamechoka hata kwa mawazo, tunasema wakazi wa Musoma mna wakati wa kufanya maamuzi kama yaliyofanywa na ndugu zenu kule Tarime, ambako CCM tuliibwaga bila ubishi na leo hii tukifanya tathmini ya gharama za maisha, mtaona serikali ya Kikwete ilivyosababisha umaskini kuongezeka, alisema Zitto.
Huku akishangiliwa na maelfu ya wananchi, Zitto alisema taifa limeuzwa, kwani rasilimali zote muhimu zikiwemo madini, samaki, mbuga zimeuzwa kwa wakezaji kutoka nje ya nchi.
Tumekuwa na rasilimali nyingi ambazo zimeuzwa kwa wawekezaji wa nje hata bajeti yetu ya serikali imeendelea kubaki tegemezi, kwani mpaka sasa wafadhili wanatoa asilimia 34. Hii ni aibu kubwa, tukatae fedheha hii, alisema Zitto.
Aidha, Mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe, ambaye alifungua rasmi operesheni hiyo, alisema huo ni mpango uliobuniwa na CHADEMA bila kujali jinsia, rangi wala itikadi, kwa lengo la kulikomboa taifa.
Leo hii (jana) tumeanzisha vuguvugu la kweli lenye kuleta mapinduzi mapya na tumeamua kuzindulia hapa Musoma, kwa sababu ya kumuenzi hayati Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere, ambaye ni mzaliwa wa mkoa huu, alisema Mbowe.
Katika mkutano huo, wanachama zaidi ya 400 wa CCM walirudisha kadi zao na kukabidhiwa za CHADEMA, wakiwamo mjumbe wa Mkutano Mkuu wa Vijana (mkoa), Gewa Anthony, na aliyekuwa Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana Wilaya ya Musoma (UVCCM), Hamis Tumbo.
Source: Tanzania Daima
Mwenyekiti Mbowe akihutubia Musoma mjini
na Kulwa Karedia
MAMIA ya wakazi wa mji wa Musoma na vitongoji vyake jana walijitokeza kwa wingi katika uzinduzi wa kampeni ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Operesheni Sangara, ambapo wito ulitolewa kwa Rais Jakaya Kikwete kuwafikisha mahakamani mafisadi wote walioiba fedha katika Akaunti ya Malipo ya Nje (EPA).
Wito huo ulitolewa mjini hapa na Katibu wa chama hicho, Dk. Willibrod Slaa, wakati akihutubia mamia ya wananchi kwenye uwanja wa Shule ya Msingi ya Mkendo.
Alisema endapo Rais Kikwete atashindwa kuwashughulikia mafisadi hao, ni bora kuwaachia wafungwa wote waliomo katika magereza mbalimbali nchini.
Mkakati wa Operesheni Sangara umelenga zaidi kupeleka madaraka kwa wananchi kuanzia ngazi za chini hadi taifa, ili kujenga uwezo wa chama.
Napenda kumwambia Rais Kikwete kwamba sasa muda wa Rais Kikwete kuona kipimo cha uongozi wake ni Oktoba 31 pale atakapowafikisha mahakamani mafisadi wote lakini kama hatafanya hivyo, tunasema wafungwa wote walioko gerezani waachiwe, ili haki itendeke kwa wote, alisema Dk. Slaa.
Alisema iwapo Rais Kikwete atashindwa kufanya hivyo atasababisha wananchi kuendelea kupoteza imani kwake, kama sasa ambapo wamefikia hatua ya kupiga mawe msafara wake.
Ni jambo la ajabu mkuu wa nchi kutupiwa mawe akiwa katika shughuli za serikali. Hii inaonyesha wazi jinsi wananchi walivyoanza kuchoshwa na serikali yake tunasema kama ataendelea na mwenendo huu anastahili kuondolewa hata kesho, alisema Dk. Slaaa.
Alisema kushindwa kwa serikali ya Kikwete kutoa maisha bora kwa kila Mtanzania kumetokana na wasaidizi wake wengi kujali masilahi binafsi, badala ya kutumikia umma.
Alisema tangu Rais Kikwete alipoingia madarakani wananchi walikuwa na matumaini makubwa, lakini hivi sasa wamekata tama, baada ya kunyanyaswa na watu waliopewa dhamana ya kuwasaidia.
Dk. Slaa alisema pamoja na hatua atakazochukua Rais Kikwete juu ya mafisadi, bado CHADEMA italipua bomu la ufisadi wa sh milioni 155 zilizoibiwa katika mgodi wa dhahabu wa Buhemba kupitia Kampuni ya Meremeta inayomilikiwa na Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ).
Rais tulimwambia mambo mengi kuhusu wizi wa fedha za umma, lakini tunashangaa kuona ameamua kushughulikia EPA peke yake, nawaambia jamani tulimwambia atupatie maelezo, lakini amekuwa akitukwepa kila siku.
Ufisadi mkubwa uliofanywa kwenye Kampuni ya Meremeta chini ya JWTZ sasa tunasema tutawasha moto hadi kuona waliochukua fedha hizi wanajulikana, alisema Dk. Slaa.
Kwa upande wake, Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho, Zitto Kabwe, alisema serikali ya CCM imechoka na sasa umefika wakati wa kukaa kando na kuachia kizazi kipya ambacho anaamini kuwa kitaleta mageuzi ya kweli.
Chama kimejaa mafisadi, wanalindana, wamechoka hata kwa mawazo, tunasema wakazi wa Musoma mna wakati wa kufanya maamuzi kama yaliyofanywa na ndugu zenu kule Tarime, ambako CCM tuliibwaga bila ubishi na leo hii tukifanya tathmini ya gharama za maisha, mtaona serikali ya Kikwete ilivyosababisha umaskini kuongezeka, alisema Zitto.
Huku akishangiliwa na maelfu ya wananchi, Zitto alisema taifa limeuzwa, kwani rasilimali zote muhimu zikiwemo madini, samaki, mbuga zimeuzwa kwa wakezaji kutoka nje ya nchi.
Tumekuwa na rasilimali nyingi ambazo zimeuzwa kwa wawekezaji wa nje hata bajeti yetu ya serikali imeendelea kubaki tegemezi, kwani mpaka sasa wafadhili wanatoa asilimia 34. Hii ni aibu kubwa, tukatae fedheha hii, alisema Zitto.
Aidha, Mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe, ambaye alifungua rasmi operesheni hiyo, alisema huo ni mpango uliobuniwa na CHADEMA bila kujali jinsia, rangi wala itikadi, kwa lengo la kulikomboa taifa.
Leo hii (jana) tumeanzisha vuguvugu la kweli lenye kuleta mapinduzi mapya na tumeamua kuzindulia hapa Musoma, kwa sababu ya kumuenzi hayati Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere, ambaye ni mzaliwa wa mkoa huu, alisema Mbowe.
Katika mkutano huo, wanachama zaidi ya 400 wa CCM walirudisha kadi zao na kukabidhiwa za CHADEMA, wakiwamo mjumbe wa Mkutano Mkuu wa Vijana (mkoa), Gewa Anthony, na aliyekuwa Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana Wilaya ya Musoma (UVCCM), Hamis Tumbo.
Source: Tanzania Daima