Baraza la Vijana la Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Bavicha) wameomba msaada kwa vyama rafiki duniani ili kufanikisha maandalizi ya Uchaguzi Mkuu wa 2015.
Akihutubia katika Mkutano wa Kimataifa wa Vijana kuhusu demokrasia uliofanyika juzi kwenye Ukumbi wa Bunge la Australia (North Wales), Sydney, Katibu Mkuu wa Baraza la Vijana la Chadema (Bavicha), Deogratias Munish alisema: Chadema tumedhamiria kushika dola mwaka 2015, tunaomba msaada wenu wa hali na mali katika harakati zetu hizi.
Katika hotuba yake, Munishi alisema kutokana na matatizo mengi yanayoikumba Tanzania hasa katika mfumo wa uchaguzi, wameamua kufanya tathmini ya kukiwezesha kuingia Ikulu kwa kuwashirikisha vijana wa nchini nzima.Alisema ili kufanikisha hilo, kinahitaji kupata uzoefu wa nchi mbalimbali kabla ya kuingia kwenye mchakato wa uchaguzi.
Tunahitaji kufanya home work yetu vizuri kabla ya hapo. Ndiyo maana kama vijana wa chama, Baraza letu limeamua kwa makusudi kwenda kukijenga chama vizuri kwa kuwaunganisha vijana wote pamoja kwenye maeneo yao, alisema.
Alisema kabla ya Bavicha kujipanga kuhakikisha Chadema kinashinda katika Uchaguzi Mkuu ujao, Katibu Mkuu wake, Dk Willbrod Slaa alishaiagiza Bavicha kufuatilia kwa karibu migogoro yote inayohusu vyuo vikuu ambako ndiko iliko ngome kuu ya chama hicho.
Munish alisema Dk Slaa alisema vijana hao wanatakiwa kufuatilia na kuweka wazi hatua mwafaka zinazopaswa kuchukuliwa ili kukabiliana na matatizo ya vijana.
Alisema uwanja wa siasa nchini ni mchafu kutokana na kuwepo kwa katiba mbovu ambayo pamoja na mambo mengine, inakataza kuhoji matokeo ya urais pindi yatakapotangazwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi.Alisema ndiyo maana baraza hilo la vijana limeamua kukijenga chama kwa kuwaunganisha vijana wote pamoja kwenye maeneo yao ili kuhakikisha muungano wa ushindi 2015 unapatikana.
Alisema kutokana na vijana wengi duniani kuunganishwa na misingi ya vyama vyenye kusimamia na kuamini katika demokrasia, jambo la msingi ni kuhakikisha haki za binadamu na uhuru wa kweli unapatikana.
Ninaamini na nina uhakika mtatuunga mkono katika harakati zetu sisi vijana wa Tanzania katika kuhakikisha tunashinda 2015, alisema Munishi na kuongeza: Kukua kwa Chadema si kwa bahati mbaya, bali ni kutokana na nia na mipango yake thabiti ya kuutumikia umma wa Tanzania.
Alisema huduma mbovu za kijamii zimekuwa zikififisha ndoto za Watanzania kufikia maendeleo ya kweli hasa katika kipindi hiki cha kudorora kwa uchumi.Alisema kutokana na hali hiyo, Chadema kimeamua kupambana na rushwa bila woga kwa kuwafichua viongozi wala rushwa ambao wamekuwa wakilifilisi taifa kwa vitendo vyao hivyo.
Alisema Chadema na Watanzania hawajakata tamaa na huku akiwataka wajumbe waliohudhuria mkutano huo kuwaunga mkono katika kuendeleza mapambano ya kuongoza umma kueleza maovu yanayotendwa na Serikali.
Nchi wanachama wa umoja huo wenye wanachama 45 inashirikisha vyama vilivyopo madarakani na ambavyo havipo madarakani.
Baadhi ya nchi hizo wanachama ni Albania, Australia, Austria, Colombia, Croatia, Cyprus, Jamhuri ya Czech, Denmark, Ecuador, El Salvador, Finland, Ufaransa, Georgia, Ujerumani na Ghana.Katika orodha hiyo pia vipo vyama kutoka nchi za Ugiriki, Guatemala, Honduras, Hungary, Iceland, Korea Kusini, Macedonia, Maldives, Moldova na Mongolia.
Vingine vinatoka katika nchi za New Zealand, Nicaragua, Norway, Peru, Ureno, Serbia, Slovenia, Hispania, Sri Lanka, Sweden, Uganda, Uingereza, Venezuela, Belarus, Bolivia, Malta, Msumbiji, Namibia, Panama, Russia na Tanzania inayowakilishwa na Chadema.Katika mkutano wa aina hiyo uliofanyika nchini mwishoni mwa mwaka jana, ulihudhuriwa na nchi 24.
SOURCE:MWANANCHI
Akihutubia katika Mkutano wa Kimataifa wa Vijana kuhusu demokrasia uliofanyika juzi kwenye Ukumbi wa Bunge la Australia (North Wales), Sydney, Katibu Mkuu wa Baraza la Vijana la Chadema (Bavicha), Deogratias Munish alisema: Chadema tumedhamiria kushika dola mwaka 2015, tunaomba msaada wenu wa hali na mali katika harakati zetu hizi.
Katika hotuba yake, Munishi alisema kutokana na matatizo mengi yanayoikumba Tanzania hasa katika mfumo wa uchaguzi, wameamua kufanya tathmini ya kukiwezesha kuingia Ikulu kwa kuwashirikisha vijana wa nchini nzima.Alisema ili kufanikisha hilo, kinahitaji kupata uzoefu wa nchi mbalimbali kabla ya kuingia kwenye mchakato wa uchaguzi.
Tunahitaji kufanya home work yetu vizuri kabla ya hapo. Ndiyo maana kama vijana wa chama, Baraza letu limeamua kwa makusudi kwenda kukijenga chama vizuri kwa kuwaunganisha vijana wote pamoja kwenye maeneo yao, alisema.
Alisema kabla ya Bavicha kujipanga kuhakikisha Chadema kinashinda katika Uchaguzi Mkuu ujao, Katibu Mkuu wake, Dk Willbrod Slaa alishaiagiza Bavicha kufuatilia kwa karibu migogoro yote inayohusu vyuo vikuu ambako ndiko iliko ngome kuu ya chama hicho.
Munish alisema Dk Slaa alisema vijana hao wanatakiwa kufuatilia na kuweka wazi hatua mwafaka zinazopaswa kuchukuliwa ili kukabiliana na matatizo ya vijana.
Alisema uwanja wa siasa nchini ni mchafu kutokana na kuwepo kwa katiba mbovu ambayo pamoja na mambo mengine, inakataza kuhoji matokeo ya urais pindi yatakapotangazwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi.Alisema ndiyo maana baraza hilo la vijana limeamua kukijenga chama kwa kuwaunganisha vijana wote pamoja kwenye maeneo yao ili kuhakikisha muungano wa ushindi 2015 unapatikana.
Alisema kutokana na vijana wengi duniani kuunganishwa na misingi ya vyama vyenye kusimamia na kuamini katika demokrasia, jambo la msingi ni kuhakikisha haki za binadamu na uhuru wa kweli unapatikana.
Ninaamini na nina uhakika mtatuunga mkono katika harakati zetu sisi vijana wa Tanzania katika kuhakikisha tunashinda 2015, alisema Munishi na kuongeza: Kukua kwa Chadema si kwa bahati mbaya, bali ni kutokana na nia na mipango yake thabiti ya kuutumikia umma wa Tanzania.
Alisema huduma mbovu za kijamii zimekuwa zikififisha ndoto za Watanzania kufikia maendeleo ya kweli hasa katika kipindi hiki cha kudorora kwa uchumi.Alisema kutokana na hali hiyo, Chadema kimeamua kupambana na rushwa bila woga kwa kuwafichua viongozi wala rushwa ambao wamekuwa wakilifilisi taifa kwa vitendo vyao hivyo.
Alisema Chadema na Watanzania hawajakata tamaa na huku akiwataka wajumbe waliohudhuria mkutano huo kuwaunga mkono katika kuendeleza mapambano ya kuongoza umma kueleza maovu yanayotendwa na Serikali.
Nchi wanachama wa umoja huo wenye wanachama 45 inashirikisha vyama vilivyopo madarakani na ambavyo havipo madarakani.
Baadhi ya nchi hizo wanachama ni Albania, Australia, Austria, Colombia, Croatia, Cyprus, Jamhuri ya Czech, Denmark, Ecuador, El Salvador, Finland, Ufaransa, Georgia, Ujerumani na Ghana.Katika orodha hiyo pia vipo vyama kutoka nchi za Ugiriki, Guatemala, Honduras, Hungary, Iceland, Korea Kusini, Macedonia, Maldives, Moldova na Mongolia.
Vingine vinatoka katika nchi za New Zealand, Nicaragua, Norway, Peru, Ureno, Serbia, Slovenia, Hispania, Sri Lanka, Sweden, Uganda, Uingereza, Venezuela, Belarus, Bolivia, Malta, Msumbiji, Namibia, Panama, Russia na Tanzania inayowakilishwa na Chadema.Katika mkutano wa aina hiyo uliofanyika nchini mwishoni mwa mwaka jana, ulihudhuriwa na nchi 24.
SOURCE:MWANANCHI