Elections 2010 Chadema wanapaswa kuchakarika fasta

Mlalahoi

JF-Expert Member
Aug 31, 2006
2,182
883
Pingamizi ndio kama tulivyotarajia,Tendwa katekeleza maagizo aliyopewa Ikulu na JK.Sasa kila dakika ni mithili ya muujiza usiojirudia. Tumeshanyanyaswa vya kutosha, utawala wa sheria umeshachezewa sana, tunachohitaji ni immediate action.

Naamini hao wanasheria mahiri wa CHADEMA wameshapitia kila kifungu cha hoja mufilisi za Tendwa. What we now need ni shambulizi la nguvu. Kama ni uchaguzi kuahirishwa basi ni bora iwe hivyo lakini kamwe CHADEMA wasikubali haki yao-na ya Watanzania wapenda demokrasia-kuacha uhuni huu ukibarikiwa kirahisi.

Waiting....
 
Tena mahakamani kama nako hawaeleweki, mbele zaidi, ila mahakama nzuri ni sisi wenyewe wananchi ambao nao ni vichwa ngumu kama siyo hivyo, basi ccm watatawala miaka nenda.
 
Mi wanaiudhi sana has a hili lizee sijui linaitwa tendwa..natamani kutapika nikiliona kwenye tv
 
Mi wanaiudhi sana has a hili lizee sijui linaitwa tendwa..natamani kutapika nikiliona kwenye tv
Kigogo Tende ni mke wa kaka yao mkubwa thats y.. but hivi vitu sio vya kuachwa hivi hivi we must do somethin..
 
Wasiende mahakamani. Waanze kuwahamasisha wananchi kudai haki yao kwa mikono yao wenyewe,,,
 
Nadhani kama ni mahakama za Bongo, hawahitaji kamwe kwenda mahakamani c wot mnazielewa mahakana zetu? usijeambiwa "ni jambo la kisiasa" kama mgombea huru bali waendelee na kampeni zao huku wakitengeneza awareness kwa wabongo nao wataamua wenyewe. Kuna mwanafalsafa mmoja alisema kuwa mpaka wananchi wanyonywe vya kutosha ndipo watakapoamua kusimama na kuufulilia mbali utawala mbovu. Na yaja kwetu Bongo!
 
Wasiende mahakamani. Waanze kuwahamasisha wananchi kudai haki yao kwa mikono yao wenyewe,,,


unapozungumzia hapa, unaamanisha wavunje sheria ? wachukue sheria mikononi mwao.


wajaribu na waone kilichomtoa kanga manyowa
 
Tena mahakamani kama nako hawaeleweki, mbele zaidi, ila mahakama nzuri ni sisi wenyewe wananchi ambao nao ni vichwa ngumu kama siyo hivyo, basi ccm watatawala miaka nenda.

Nimeipenda hii. Nadhani mahakama yenye kuleta ukweli na kutenda haki ni sisi wenyewe, bila kuleta machafuko makubwa. Ni rahisi ni kuwaelimisha wananchi wetu kumkacha huyo kiongozi wa mafisadi anapokuja kutoa ahadi zake za uwongo. Au ikibidi kumfanyia kama alivyofanyiwa msaidizi wake Iringa na watetea haki wa nchi hii. Kwa hili tutafanikiwa.

Nadhani ataomba kujiuzulu mwenyewe tukifanikiwa kufikia hatua hiyo, sina hakika atakuwa na nguvu gani ya kustahimili hayo, kwanza ni mgonjwa. Kinachohitajika ni mapinduzi ya watu sio ya kijeshi. Watu wakifahamu wanataka nini, na wakifahamu nani ni kikwazo inawezekana.

Hasa wakati huu wa kampeni ambapo wanajipitisha pitisha kutoa ahadi za uwongo, ni muda mzuri wa kuwaeleza kuwa hatuwataki.

Mahakama ya serikali sifuri. Hukumbuki Jaki mkuu alivyoropoka wiki iliyopita? Ni wazi unatambua anakoegemea na kukandamiza.
 
USHAURI WA BURE KWA CHADEMA,

Hakuna hoja nzuri zinazowachanganya CCM kama za ufisadi, kwahiyo CHADEMA wanachoweza kukifanya ni kuwaweka ccm on defensive. ukitaka kushinda kampeni zozote zile siri ya kwanza ni kumuweka adui yako kwenye defensive position.

Na hoja kubwa inayoweza kuwaweka CCM ktk defensive zaidi ni swala la ufisadi na ndio maana kabla ya uchaguzi walitunga sheria nyingi za ajabu ajabu ili ku control speech kwamba uzungumzie ilani na siyo mambo mengine

Kwahiyo CHADEMA wanachotakiwa kukifanya sasa ni kuhubiri sera kwa bidii huku wakifanyia kazi hoja zote kifisadi kwa kina ili tukiingia October basi waanze kuwasha moto wa nguvu kuhusu ufisadi ili kuiweka CCM ktk hali ya kujitetea mpaka mwisho.

Na kwa kuwa hawana majibu ya hizi hoja za kuhusu ufisadi CCM watakuwa ktk hali mbaya maana watashindwa nini cha kuwaambia wananchi na hivyo kuiacha CHADEMA ikitamba uwanjani kwa kuzoa viti vyingi vya ubunge na hata urais.
 
Hivi inakuwaje kuhusu matangazo ya kampeni kwenye tv kama wanavyofanya marekani?au sheria inakataza?Kama haikatazi mi naona ni jambo zuri kufanya commercial ads kumnadi Dr. Slaa na kuzungumzia ufisadi ili kuwakumbusha wananchi.Nafikiri hilo litasaidia.
 
Hakuna hoja nzuri zinazowachanganyaCCM kama za ufisadi, kwahiyo CHADEMA wanachoweza kukifanya ni kuwaweka CCM on defensive.Ukitaka kushinda kampeni zozote zile siri ya kwanza ni kumuweka adui yako kwenye defensive position,ukitaka kupata attention(mshiko) ya mtu siku zote shika mfuko wake anakoweka pesa zake.

Kwahiyo pamoja na kwamba sera ni kitu kizuri lakini swala la kumuonyesha mtanzania jinsi anavyoibiwa pesa zake za kodi linaweza kumfanya ajiulize mara 10 kuliko swala la sera kwahiyo CHADEMA wana nafasi nzuri sana kwa maana wana hoja mshiko mkononi kuliko CCM na suala lao la mke wa mtu ambalo aligusi mfuko wa mtanzania.

Lakini CHADEMA wana hoja mshiko kubwa inayoweza kuwaweka CCM ktk defensive zaidi ni suala la ufisadi na ndio maana kabla ya uchaguzi walitunga sheria nyingi za ajabu ajabu ili ku control speech kwamba uzungumzie ilani na siyo mambo mengine.

Kwahiyo CHADEMA wanachotakiwa kukifanya sasa ni kuhubiri sera kwa bidii huku wakifanyia kazi hoja zote kifisadi kwa kina ili tukiingia october basi waanze kuwasha moto wa nguvu kuhusu ufisadi ili kuiweka CCM ktk hali ya kujitetea mpaka mwisho na kwa kuwa hawana majibu ya hizi hoja za kuhusu ufisadi ccm watakuwa ktk hali mbaya maana watashindwa nini cha kuwaambia wananchi na hivyo kuiacha chadema ikitamba uwanjani kwa kuzoa viti vyingi vya ubunge na hata urais.
 
Good idea; pumzi inatakiwa hapo; naamini come october CCM watamaliza hoja; mhimu Dr Slaa aiskubali kukatishwa tamaa na wajinga na ujinga wao eti kwa sababu ya smearing; wanatafuta mahala pa kutokea; aliwashika kwa kipindi cha wiki moja na sasa aendelee kuwashika zaidi na hoja yao itakuyfa kifo cha mende; najua watajitahidi kupeleka swala mahakamani ila mahakama haitegemei uchaguzi so hilo ni swala dogo tu litaisha
 
Hivi inakuwaje kuhusu matangazo ya kampeni kwenye tv kama wanavyofanya marekani?au sheria inakataza?Kama haikatazi mi naona ni jambo zuri kufanya commercial ads kumnadi Dr. Slaa na kuzungumzia ufisadi ili kuwakumbusha wananchi.Nafikiri hilo litasaidia.

Duh! Ni channel gani hiyo itakayotaka ku-commit suicide?
 
Back
Top Bottom