CHADEMA wanani dissapoint kwa kweli

Nimevumilia sana kutokusema but nimeshindwa sasa
inabidi niseme tu kilicho moyoni kwangu.

Kwa ufupi nashangazwa na busara za CHADEMA na Dk Slaa.

Mimi ni katika wale ambao nimesha give up na CCM.
Chochote watakachokifanya kikiwa kibaya sishangai na kikiwa kizuri
kwangu hakivutii.

Sasa nilitegemea CHADEMA wawe tofauti saana lakini
wanayoyafanya mimi naona kama hawapo serious kabisa.

1. La kwanza ni hili la kujaribu na kujibizana na watu wa CCM,
kwanza kwa nini chadema wana react na mambo ya CCM?
Mfano mkutano mkuu wa ccm na suala la kujivua gamba?

Kwa nini kwa mfano chadema walishindwa nini kudharau na
kutokuongea lolote, badala yake wakawa wanazungumzia
namna ya kupunguza gharama za maisha zinazopanda, na namna
ya kuwafaidisha watanzania na zoezi la mjadala wa katiba mpya?

2. Kwa nini wasizungumze ni vipi katiba mpya itawasaidia watanzania
kupambana na rushwa, ufisadi na matatizo mengine?

3. Imeandikwa kwenye media kuwa, watuhumiwa wa ufisadi
watawatumia viongozi wa vyama vya upinzani kumtukana Kikwete
na familia yake, na siku haipiti Dk Slaa anaanzisha madai ya Ridhiwani?

Imean hata kama yuko right,what about the wrong time?
kwa nini now wakati inatangazwa maadui wa Kikwete watakitumia chama cha upinzani?

4. Tazama hili la Nape na CHADEMA, nani anaefaidika kama sio
watuhumiwa wa ufisadi, maana sasa hawazungumzwi wao.
attention imehama kutoka kwao. Kwa msaada wa Dk Slaaa.

5. Hivi hata kama Nape alitaka kujiunga HADEMA au CCJ, kumuumbua huko
kunaleta faida au hasara kwa CHADEMA?

6. watu wengine walio CCM nao wangependa kuondoka, wanaonaje?


Hivi CHADEMA hawawezi kuzungumza kuhusu mustakabali wa tanzania bila
kuzungumzia CCM kwa jazba?

Mimi nakuwa dissapointed na CHADEMA.

Kwa sababu hata wakati wa uchaguzi, Mbowe na wenzie wa CHADEMA
walinishangaza walipomlalamikia Kikwete kufanya kampeni baada ya muda rasmi
kupita, badala ya CHADEMA kupinga hiyo sheria ya kipuuzi ya kuweka limit ya masaa ya kampeni.

i411 said:
Mimi nakubaliana kabisa na The Boss niwakati sasa CDM wawe wanatoa changamoto kwa serikali kuimarisha uchumi wetu na si kutupiana maneno. Yaani uongozi mzima wanatupiana maneno na kila mtu anaowarushia mfupa.

Mimi nazani wamuachie Mtikila kwa vile yeye ni kama anashinda mahakamani huko anaweza shinda mafisadi na kutupa updates. Viongozi wengine wawe mfano bora huko bungeni na kuiwajibisha serikali katika kutoa zile huduma tunazolipia kama umeme.

Waweke kama sera tukikosa umeme siku kazaa watufulani wajiuzuru manake watakuwa wameshindwa kutupa kipaumbele na kueka miundo mbinu ya vitu kama emegency power supply.

Hivi ndo tunaweza zuia ufisadi usitokeee kama wa Richmond. Walikiwa wanasema wanatupatia umeme wakati tulikua tunateseka tuu na mgao miaka nenda rudi. Kama kungekua na sera za kuwajibisha watu na wengine kujiuzuru tungewashutukia mapema, sio kushituka wakati tumeshaingia hasara mabilioni na watu tulishawachoka sasa na wanaendelea kudunda wana nyumba, magari na mabank akaunti yao yamenona siye tukitaabika na bado twa taabika.

You are very right mkuu.... kinachoendelea sasa kinatukumbusha - "MCHIMBA KISIMA, KAINGIA MWENYEWE" while it is important kwa chadema kuendelea kuanika uovu wa mafisadi, nadhani umefika wakati wa chama ku-mordenize, strategize na reform potentials ni nyingi sana


Kweli kabisa CHADEMA inabidi ishughulike na mambo ya wananchi kuendelea kujibizana na CCM ni kupoteza attention ya mambo ya msingi nakuunga mkono mkuu THE BOSS

Siasa za chuki siyo nzuri, kwani wewe waweza kufurahia kwa kupandikiza chuki ukidhani ndio upenyo wa kutokea lakini siku chuki ikiiva na ikalipuka hata mwenyewe utakuwa mhanga.

Chadema inatembea nchi nzima kupandikiza chuki kwa wananchi juu ya serikali yao, wanaweza kuona wako sawa lakini siyo sawa, kwani hata kama njia hiyo ikiweza kuwaingiza madarakani basi zile sentensi zao za nchi haitawaliki nadhani kipindi hicho ndio itakuwa wakati wake muafaka.

Uchaguzi uliopita kenya Laila alikuwa anakubalika sana lakini kaa na wakenya usikilize kama bado ana vote. The Boss nimekubali post yako iko kiuzalendo zaidi. Thanks Boss

Nakubaliana na mtoa mada kuna mambo ya msingi ambayo CHADEMA wanaweza kuzungumza zaidi ya CCM na ufisadi.

Sijaona PWENTI hata moja ........kama mmetumwa na Msekwa kamwambie CHADEMA ndio kwaaaaaaaaaaaanza kumekucha!
 
Jamani, ni pahali gani duniani penye vyama vingi vya siasa ambapo vyama hivyo vipo kwa ajili ya kusifiana na kujengana?! Upinzani upo kwa ajili ya kuzidiana kete kwa kufichuliana mapungufu na maovu kwa faida ya wananchi na maslahi ya Taifa husika. Else, turudi kwenye mfumo wa chama kimoja.
 
Nnakubaliana na mtoa mada lakini pia nnapingana nae kwa jambo moja:kuwa Chadema wasijibizane na ccm.Ikumbukwe uongo ukiachwa utawale kwa muda mrefu utaonekana kuwa ni ukweli.Hivyo Kama anatokea mtu anakunyooshea kidole waziwazi na kukwambia wewe upo hivi au upo vile lazima umjibu Tena mapema hasa jambo lenyewe likiwa ni baya.Sioni ubaya wowote kwa Chadema kuzijibu hoja hafifu za ccm.
 
Me nashangaa sana huu utamaduni wa watanzania kutokupenda kukosolewa au kuambiwa ukweli pale inapobidi. Naiona hii hali hata humu ndani JF Kila mtu akipost mada ya kuikosoa CHADEMA basi atatukanwa na kuitwa mtoto wa mafisadi.

People inabidi mjifunze kudigest different ideas. Inabidi tujenge utamaduni wa kukubali kutokubaliana. JUST BECAUSE NAIKOSOA CHADEMA IT DOESNT MEAN MIMI NI CCM, I CAN BE INDEPENDENT.

Katika chaguzi nyingi duniani wanaoamua mshindi ni watu kama mimi because sina chama so i can vote to chama chochote ambacho kina sera nzuri. Tofauti na watu ambao wenyewe ni wapenzi wa vyama, hata vyama vyao vikifanya madudu wanavipigia kura tu.

MAPENZI HULETA UPOFU, I dont support CCM 4 any mean kwani najua 80% ya matatizo yanayolikabili taifa letu yamesababishwa nao, na kama wangekuwa na gut wangeweza kuyamaliza yote.

The same time siwez tu kuisuport CHADEMA sababu tu ni chama cha upinzani kikuu wakati kuna madudu kibao nawaona wakifanya.

CHADEMA INABIDI WABADILIKE, UMAARUFU WAO UMEKUJA GHAFLA MNO AND THATS BAD, inabidi wafanye reform kubwa sana katika utawala na kurecruit watu.

ASIKWAMBIE MTU VINGINE, UKWELI NI KUWA NGUVU YA CHAMA CHOCHOTE CHA SIASA INAANZIA KWENYE MATAWI YA NYUMBA KUMI KUMI. HUKO NDIO KWA KUINVEST NA KUMWAGA MAPESA, NA SIO MAANDAMANO NA MIKUTANO ISIYO NA TIJA.

CHADEMA wafukuzeni CCM kimya kimya bila makelele kwa kukijenga chama katika nyumba kumi kumi.

Msinitukane wazee ni maoni tu.

Umeongea vizuri mkuu, hii nguvu ya umma ikianzia chini kwenye ngazi ya kitongoji impact yake nikubwa zaidi kuliko kuwekeza kwa watu wa msimu ambao hawatabiriki ni kama bendera fuata upepo CDM wakifanya maandamamo yupo CCM, CUF wakifanya maandamano utamuona kuliko kupoteza muda kwa watu hao ni bora kuweka mipango endelevu ya kuvua wanachama kwenye vitongoji kwa kuanzisha matawi madhalani ukiwa na matawi 120 kwa kila jimbo na kila tawi likawa na wanachama 150 katika majimbo 289 unapata wanachama zaidi ya 5mil. Kwanini ngùvu kubwa usiwekeze hapo penye uhakika kuliko kutumia muda mwingi kwa wasiyotabirika
 
Chadema inatembea nchi nzima kupandikiza chuki kwa wananchi juu ya serikali yao,.,.

Ndugu,
Inaonekana haujahudhuria mikutano ya Chadema! Hakuna swala la kupandikiza chuki. Wanawaonesha wananchi namna serikali ya ccm wanavyofuja na kufisadi kodi zao wakati walitakiwa kuzitumia kuwaletea maendeleo na kuwapunguzia hali ngumu ya maisha! Na hiyo ndio kazi yao kikatiba. Kuikosoa serikali. Nadhani tatizo lako ni kusikiliza TBC, Radio uhuru au bado upo kwenye enzi za zidumu fikra za m/kiti. Kwa vile kasema yeye tu, basi, unaichukua kama ilivyo. You need to change.
 
Mkuu wakati mwingine huwezi kushambulia tu bila kudefend, CCM walianza kutamba kuwa chama kimebadilika ilikuwa ni muhimu kwa CDM kuwakumbusha kuwa nyoka hata kama akivua gamba atabaki kuwa nyoka....Na huyu dogo Nape alianzisha yeye personal attck na kejeli kwa CDM ilikuwa ni muhimu kumjibu..baada ya hili bomu la Mpendazoe nape ataonekana ni msaliti ndani ya chama na ile imani kwa wenzake itakwisha, ndo maana unaona Chiligati na Mukama hawaatack personal za mtu, Nape anatakiwa alinganishe sera na kuwaonyesha wananchi jinsi sera zao zilivyo bora kuliko za chadema yeye anafanya personal attack...hiyo dozi iliyopata itamnyamazisha na kuwa CDM advantage sbb upande wa CCM kila mtu ataogopa kujiweka front
"bombs should be met by bombs".
 
The Boss, siasa ina manjonjo yake. Unakumbuka hivi majuzi huko USA yaliyomkuta OBAMA??? Pamoja na kuwa wote wanajua kuwa OBAMA ni Mzaliwa wa USA lakini REPUBLICAN walikuja na hoja ya kuwa inabidi OBAMA atoe Cheti cha kuzaliwa ili waweze kuhakikisha. Republican hawakuwa wajinga kuja na madai hayo, na wala si kuwa hawakuwa na hoja nyingine za kuongelea juu ya uchumi na au day to day activities. Hiyo ndio SIASA BOSS
 
Sijaona PWENTI hata moja ........kama mmetumwa na Msekwa kamwambie CHADEMA ndio kwaaaaaaaaaaaanza kumekucha!


Vibaraka wako wengi!!! Itasaidia kama wakati mwingine tukiangalia movie ikichezwa kuliko kusema inakudissapoint wakati wewe ni wa upande mwingine. Wenyewe wamekubali kujivua gamba sasa wewe hutaki wakosolewe? Ndiyo upinzani huo. tuvumiliane.
 
Hivi ukiwa vitani, akitokea mwenye panga utamwacha sbb wewe unamtafuta mwenye bunduki??....niwakumbushe kidogo, wakati ule wa uchaguzi mkuu Makamba alikuja na story ya unyumba wa Dk.Slaaa na upadri wake alipopigwa lile dongo la kumpa mimba mwanafunzi akawa mpole akafunga mdomo hatukumsikia tena, akaibuka Six na kupinga hoja ya elimu bure eti haiwezekani akaambiwa yeye si msafi na ni fisadi kama wenzake akakumbushwa ile ofisi ya spika ya millioni 500 kule jimboni kwake akawa mpole akanyamaza. Akaibuka Kinana, akapewa dozi yake kuhusu ufisadi wa zile meli zake na akaambiwa makombora mengine bado akatulia akaanza kuongea sera personal attack akaacha, akaibuka Shimbo, akapewa dozi yake ya tenda za kifisadi alizopewa na JK nae hatukumsikia tena. Kilichoponza Riz1 ni yeye na gazeti lake kumsakama kuisakama CDM kapewa dozi yake katulia...huyu Nape kajiingiza mwenyewe safari hii Dk katulia Marando na Mpendazoe wakampa dozi yake...Nape kashakuwa mpole baada ya hapo maandamano na kuwaeleza wananchi ukweli yako pale pale.

CHADEMA ni moto wa kuotea mbali, Nape mbwembwe zote zimemwisha
 
The Boss,

Nakushauri uendelee kujifunza siasa ndugu yangu.

Hayo unayoyasema hayawezi katu kuipotezea mwelekeo chadema. Kama unaifuatilia vizuri siasa ya dunia hii, chadema kuisema ccm ni suala ambalo haliepukiki kama ambavyo ccm isivyoweza kuepuka kupanga mikakati ya kuimaliza chadema.

ccm ndo wanaongoza nchi na kwahiyo mambo wanayoyafanya yana direct impact na maisha ya watanzania, kadhalika kazi inayofanywa na chadema ya kuwatetea watanzania na kuionyesha jamii ya watanzania ni kwa kiasi gani ccm inavyowajaza ufukara na jinsi gani viongozi wa ccm wasivyo wadilifu na kusababisha ugumu wa maisha ni jambo la kupongezwa.

Labda unithibitishie pasipo shaka kwamba umehudhuria mikutano ya chadema inayoendelea huko mikoani na ukagundua kwamba hawazungumzii kabisa masuala mengine yenye maslahi ya kitaifa yanayowagusa wananchi mmoja mmoja na wanarusha makombora tu kwa ccm basi hapo nitakuelewa na kukubaliana nawe. Lakini kama uko mjini na unategemea kupata taarifa za kinachojiri huko mikoani kupitia TBC, Radio uhuru, Mtanzania na Nipashe basi sitashangazwa kuona ukiwa na mtazamo ama mawazo kama haya.
 
The Boss

Nadhani unapotoka sana unapochukizwa na haya kwa kuwa hiyo ndio ushindani, siasa ni ushindani, kujenga hoja za mashiko, kueleza upungufu wa mwenzako na kuonyesha uwezo wako, CDM they have to do what they are doing now kwa kuwa CCM wamejifanya wamejivua gamba lazima wananchi waelezwe uhadaa wa CCM, lazima waelezwe udhaifu wa chama kilichowapeleka hapo walipo, lazima waambiwe ili waondokane na dhana kuwa CCM ndio imewalea na upinzani ni vita, lazima wajenge ushawishi mkubwa kwa wananchi na ushawishi ni kuwatembelea kila mara, kuwajengea hamasa kubwa na uelewa wa mambo.

Itakuwa dhambi kama watazungumzia masuala ya uzushi na uchochezi ila uzuri ni kwamba so far wanaeleza ukweli wakiwa na ushahidi, mara nyingi tu wanaolipuliwa hutishia kwenda mahakamani ila mpaka sasa hakuna aliyekwenda na hivyo kuthibitisha wana hoja za msingi, wana mashiko na uhakika na wanachizungumza

Hujasikia mkuu wa kaya akiwaambia maafisa habari serikalini watoe habari ili wapinzani wasiwe na cha kusema?hujasikia akiwaambia mawaziri waache urasimu na umungu mtu walete maendeleo?tunashuhudia semina elekezi nyingi zikiwa na lengo la kuwapa msasa watendaji wa serikali ili wakabilane na CDM na vuguvugu la kudai maendeleo japo semina zenyewe hazina tija?
 
Sawa, umenena vyema. Usiogope matusi unapokuwa na nguvu ya hoja. Chadema makini hawataki kusifiwa tuuuuuu!. Hukubali na kukabili changamoto zote hata kama zinatoka kwa maleria sugu!


A leader is someone who makes people do what they don't like and finally love it.
 
Nilidhani nipo peke yangu Mzito! Hivi hii ni forum ya SIASA au MMU? Nisije nikawa nimepotea njia....
Eti "CDM waifukuze CCM kimya kimya".....nyooooooo! Ni kama kumwambia Osama ende washington akajisalimishe! Eti "CDM ishugulike na mambo ya wanachi"...sasa kwani bei ya sukari na kodi kubwa ya bidhaa muhimu ni mambo ya vyura? Eti "waache kuandamana waende kwenye nyumba kumi kumi kufungua matawi"........wacheni kukariri kama watoto wa form one, kila jambo lina wakati wake na mahala pake muafaka. Kilichong'oa tawala dhalimu Tunisia,Misri na yanayoendelea Syria ni nyumba kumi kumi? nani kakwambia mabadiliko ya tawala kongwe Zanzibar, Zambia,Malawi,Kenya,Uganda (obote's time) yaliletwa na Nyumba kumikumi?
Hata Barcelona na flair yao wana mabeki na golikipa,unadhani ni kujazia tu ili wafike 11?
Wait a minute...Hivi toka lini siasa ikawa smart kama mchakato wa kuteu papa mpya? Isitoshe siasa yenyewe inapokua against chama kama CCM na utawala wake? Are you kidding guys? Infact vile kwamba CDM wanaendelea tu na siasa za majukwaani na maandamano ya amani,kwangu mie they deserve credits za uungwana. Otherwise wana uwezo kabisa wa kuchochea migomo ya wafanyakazi,maandamano yasiyo na mwisho na mengineyo ambayo sipendi kuyataja kabisa na nchi isitawalike hii. Waarabu hawa wana hali nzuri mnoo ukilinganisha na yetu lakini ona wanachokifanya.
Sijaona PWENTI hata moja ........kama mmetumwa na Msekwa kamwambie CHADEMA ndio kwaaaaaaaaaaaanza kumekucha!
 
Nimevumilia sana kutokusema but nimeshindwa sasa
inabidi niseme tu kilicho moyoni kwangu.

Kwa ufupi nashangazwa na busara za CHADEMA na Dk Slaa.

Mimi ni katika wale ambao nimesha give up na CCM.
Chochote watakachokifanya kikiwa kibaya sishangai na kikiwa kizuri
kwangu hakivutii.

Sasa nilitegemea CHADEMA wawe tofauti saana lakini
wanayoyafanya mimi naona kama hawapo serious kabisa.

1. La kwanza ni hili la kujaribu na kujibizana na watu wa CCM,
kwanza kwa nini chadema wana react na mambo ya CCM?
Mfano mkutano mkuu wa ccm na suala la kujivua gamba?

Kwa nini kwa mfano chadema walishindwa nini kudharau na
kutokuongea lolote, badala yake wakawa wanazungumzia
namna ya kupunguza gharama za maisha zinazopanda, na namna
ya kuwafaidisha watanzania na zoezi la mjadala wa katiba mpya?

2. Kwa nini wasizungumze ni vipi katiba mpya itawasaidia watanzania
kupambana na rushwa, ufisadi na matatizo mengine?

3. Imeandikwa kwenye media kuwa, watuhumiwa wa ufisadi
watawatumia viongozi wa vyama vya upinzani kumtukana Kikwete
na familia yake, na siku haipiti Dk Slaa anaanzisha madai ya Ridhiwani?

Imean hata kama yuko right,what about the wrong time?
kwa nini now wakati inatangazwa maadui wa Kikwete watakitumia chama cha upinzani?

4. Tazama hili la Nape na CHADEMA, nani anaefaidika kama sio
watuhumiwa wa ufisadi, maana sasa hawazungumzwi wao.
attention imehama kutoka kwao. Kwa msaada wa Dk Slaaa.

5. Hivi hata kama Nape alitaka kujiunga HADEMA au CCJ, kumuumbua huko
kunaleta faida au hasara kwa CHADEMA?

6. watu wengine walio CCM nao wangependa kuondoka, wanaonaje?


Hivi CHADEMA hawawezi kuzungumza kuhusu mustakabali wa tanzania bila
kuzungumzia CCM kwa jazba?

Mimi nakuwa dissapointed na CHADEMA.

Kwa sababu hata wakati wa uchaguzi, Mbowe na wenzie wa CHADEMA
walinishangaza walipomlalamikia Kikwete kufanya kampeni baada ya muda rasmi
kupita, badala ya CHADEMA kupinga hiyo sheria ya kipuuzi ya kuweka limit ya masaa ya kampeni.

NAIPENDA ZAIDI HII HAPA CHINI:
Wasaidizi wana nafuu kuliko rais?

Ansbert Ngurumo

BAADHI yetu hatujaelewa ari, nguvu na kasi ya Rais Jakaya Kikwete. Nina hakika naye ameiimba, lakini hajaielewa barabara.

Kaulimbiu hii iliyoasisiwa na kina Samuel Sitta mwaka 2005, ilitumika kumtafutia urais mgombea wa CCM, Jakaya Kikwete, kwa ari mpya, kasi mpya na nguvu mpya.


Waliomjua vema uwezo na udhaifu wake walidokeza mapema kwamba maisha ya Watanzania chini ya CCM ya Kikwete yangedorora na kuwa magumu zaidi - kwa ari mpya, nguvu mpya na kasi mpya.


Baadaye, sisi na baadhi ya watani wa CCM tuliifupisha kaulimbiu hiyo, tukaiita ANGUKA. Ni kweli! Miaka mitano baadaye, wameangukia pua.


CCM imeanguka. Rais Kikwete ameanguka. Mtandao wake umeanguka. Na kwa bahati mbaya, hata serikali yake imeanguka, ikaishia kuwa serikali kopa-kopa – hata mishahara ya watumishi – licha ya kodi kubwa tunazolipa.


Kuanguka huku, ndiko kumekuwa chanzo cha kura chache za mgombea urais wa CCM katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010. Kuanguka huku ndiko kumekuwa kichocheo cha vilio vya wananchi dhidi ya ufisadi. Kuanguka huku ndiko kumesababisha hata usanii mpya wa CCM wa ‘kujivua gamba.’


Kuanguka huku ndiko kumemkosanisha Rais Kikwete na maswahiba wake wa siku nyingi. Kuanguka huku ndiko kumemfanya Rais Kikwete aogope maandamano ya wananchi yanayoratibiwa na CHADEMA hata akalialia kwamba “wanataka kuniondoa kabla ya wakati.”


Kuanguka huku ndiko kumemwondoa Yusuf Makamba katika ukatibu mkuu wa CCM, yeye na sekretariati na Kamati Kuu. Kuanguka huku ndiko kumerutubisha na kukuza fitina na vita ya makundi ndani ya CCM.


Kuanguka huku ndiko kumewafanya Watanzania kuikataa CCM waziwazi kuliko wakati wote katika historia, na ndiko kumemwingiza Nape Nnauye (Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM) katika migogoro mipya ndani ya makundi ya CCM na kumwandalia anguko lake huko tunakokwenda, hasa baada ya Rais Kikwete kuondoka madarakani.


Anguko hili la ari mpya, kasi mpya na nguvu mpya limewagusa wananchi wenyewe. Sasa wanakabiliwa na ukali wa maisha usiofanana kabisa na ahadi kemkemu walizopewa na CCM mwaka 2005 na 2010.


Bahati mbaya waliosababisha anguko hili, bado wanajitapa kwamba wameleta maendeleo. Vipofu!


Na kwa sababu ya upofu huu, wanakosa mikakati mipya ya kujikwamua. Wanarudiarudia yale yale yaliyoshindwa kuwanusuru miaka mitano iliyopita.


Kwa mfano, mwaka 2006 mwanzoni, Rais Kikwete aliingia na mbinu ya kutembelea wizara moja moja, kutoa maelekezo na kupiga picha na watumishi wa wizara hizo. Ilikuwa propaganda na mapambo ya magazeti na televisheni.


Baadaye, aliwaita mawaziri na watumishi waandamizi wa serikali (mara mbili) katika semina elekezi kwenye Hoteli ya kifahari, Ngurdoto, Arusha.


Leo tunapotazama nyuma, ni nani anaweza kujivunia semina elekezi za Ngurdoto?


Lakini watu wasiojifunza hawafichiki. Mwaka jana, rais yule yule akagombea kwa kaulimbiu ya ari zaidi, kasi zaidi na nguvu zaidi. Yaani, hawa jamaa hawakuridhika na ’anguko jipya’ la 2006. Waliona hilo halitoshi, wakatuandaa “kuanguka zaidi” mwaka 2010!


Haikumwongezea kura mgombea wao. Haikuvuta hisia za vijana wala kina mama. Ili kupata watu wa kuhutubia ilibidi CCM itumie pesa nyingi kuchapisha na kugawa sare, kuwagawia watu na kuwapakia kwenye magari kuwapeleka kwenye mikutano ya mbali.


Haikuwaunganisha watawala wawe na sauti moja, hata baada ya kurejea madarakani. Haikuwasaidia kupata hekima ya kumaliza matatizo ya muda mrefu, kama ukosefu wa umeme ambao umezungumzwa tena na tena bila ufumbuzi.


Sasa kwa ari zaidi, nguvu zaidi na kasi zaidi, watawala wamerudi tena katika semina elekezi, chini ya mwelekezaji yule yule.


Walidhani zile zilishindikana kwa sababu zilifanyika Arusha. Sasa wamekimbilia Dodoma. Kwa wiki nzima, serikali iko Dodoma, imelala; inakula posho. Kazi zinakwama.


Rais naye, badala ya kuwaelekeza kwa hekima na ustadi, “akawananga” wasaidizi wake hadharani, kana kwamba huwa hapati fursa ya kukutana nao – wakati amekuwa akikutana nao kila mwezi katika vikao vya Baraza la Mawaziri. Ndio hao aliowatembelea na kuwasema wizarani kwao miezi miwili iliyopita, hata akawaamuru wengine waache ubabe.


Alitaka kuonewa huruma. Alitaka kuwashitaki kwa wananchi – waonekane wabaya, awe mzuri.


Rais anawasema mawaziri wake kama watoto wadogo wanaohangaika kuelewa kitu kidogo anachowafundisha. Anawaonyesha wananchi kwamba ana mawaziri mizigo, mbumbumbu – ambao kazi pekee wanayofanya ni “kumwangusha” rais.


Anataka turudi kwenye propaganda za kijinga walizoimba miaka mitano iliyopita, kwamba rais pekee ndiye anachapa kazi, bali mawaziri wake wanamwangusha.


Anawaambia mawaziri wake kuwa kama hawawezi kazi “waondoke,” kana kwamba hajui uwezo wao, hajui waliingiaje, wakati ndiye aliyewateua na ndiye ana mamlaka ya kuwaondoa.


Anataka “watoke” waende kwa wananchi kufafanua mafanikio ya serikali yake. Haamini kwamba wananchi wana uwezo wa kuona mazuri na mabaya ya serikali – bila kusubiri taarifa za mawaziri.


Haoni kwamba serikali inayofilisika na kulazimika kukopa hata mishahara ya watumishi wake, inahitaji kubana matumizi na kupunguza ziara na posho nono za viongozi hao waandamizi.


Lakini pia, tunapowatazama watu wenyewe aliokuwa anawapa somo, tunabaki kujiuliza: Rais amepata wapi hekima hii ya kudhani ana uelewa mpana kuliko mawaziri wake?


Amesomea wapi huko wasikojua wao, alikopata hicho cha kuwafunda? Tunapowatazama baadhi yao tunagundua kwamba kama rais angekuwa na busara ya kujifunza kutokana na miaka mitano iliyopita, asingewaita mawaziri kuwafunda, bali angewaita ili wakae kama timu, awaombe ushauri, awasikilize, wampe mang’amuzi yao na mipango mkakati; naye baada ya kuwasikiliza na kuongeza maono yake, awapangie kazi na kuwadai matokeo baada ya muda kadhaa.


Au basi angeunda kikosi kazi cha wasomi waliokubuhu kutoka taasisi mbalimbali zinazoheshimika, akawakutanisha na wasaidizi wake, wote pamoja wakavuna maarifa ya ziada katika kuboresha kazi zao na kukosoa kasoro za huko nyuma.


Angejenga mazingira ya kuambizana ukweli, naye akaambiwa kasoro zake; hasa kwamba serikali imekosa mipango mkakati mbadala na hata hiyo iliyopo imekosa msimamizi makini.


Kitendo cha rais kulialia mbele ya wateule wake na wananchi kupitia vyombo vya habari si ishara ya ushupavu anaostahili kuwa nao kiongozi mkuu wa nchi.


Ndiyo! Tuliona wameinama na kushika tama alipokuwa anafoka. Lakini ana uhakika gani kwamba walikubaliana naye? Ana uhakika gani kwamba walimwona shujaa?


Na kwa kiongozi ambaye ameongoza nchi kwa miaka mitano kwa hotuba na matamko yasiyotekelezeka, anadhani mawaziri wake watamwamini na kumheshimu baada ya kufokewa hadharani Dodoma?


Labda, watamshukuru kwa kuwatengenezea mazingira ya kula posho za safari. Lakini naamini mawaziri wenyewe wanajua fika kwamba hawana sababu ya kusafiri hadi vijijini kila mara, maana huko kuna watendaji wa ngazi za chini wanaopaswa kusimamia kazi na kuleta taarifa kwa ngazi za juu.


Sasa kama rais anaagiza mawaziri waende wenyewe vijijini, hao watendaji wa mikoani, wilayani na vijijini kwenyewe watafanya kazi gani?


Hivi waziri aliyekaa katika wizara ile ile kwa miaka mitatu au zaidi, ana kitu gani cha kujifunza kwa rais aliyekaa madarakani kwa miaka mitano bila maono na mafanikio yanayoshikika?


Rais Kikwete ana mfano gani wa utendaji uliotukuka anaoweza kuutumia kuwasuta mawaziri wake? Aliacha urithi gani katika wizara alizowahi kuongoza kabla hajawa rais?


Ni nani anayejua matatizo, changamoto, na suluhisho la matatizo yake, kati ya waziri aliye kwenye wizara hiyo hiyo, na rais “anayeishi kwenye ndege?”


Baadhi yetu tunajua kwamba mkwamo mkubwa wa kiutendaji unatokana na madaraka makubwa ya rais, nidhamu ya woga ya wasaidizi wake na utovu wa uzalendo wa baadhi yao.

Zipo taarifa kwamba siku hizi wasaidizi wa rais wameamua kumwambia yale anayotaka kusikia, kwa sababu anawafokea hovyo hovyo wanapomweleza asiyotaka, au wanapompa mapendekezo magumu.


Wanadai rais hataki kuambiwa asichotaka; nao hawako tayari kupoteza kazi zao.


Kwa mantiki hii, haiwezekani kwamba baadhi ya wasaidizi wa rais wana nafuu kuliko yeye? Kwanini tusiamini, basi, kwamba rais ndiye anawaangusha wasaidizi wake?
 
Boss umeongea vizuri lakini lazima CHADEMA wajibu hoja moja baada ya nyingine toka CCM, Kwa sababu uelewa wa watanzania walio wengi ni mdogo na kumbuka wengine hata kusoma na kuandika ni tatizo, sasa bila kujibu tuhuma zinazotolewa na wapinzani wao (CCM) watu watajua tuhuma hizo ni kweli wakati ni unafiki mtupu.

Unavyoelewa wewe si anavyoelewa mtanzania aliyeko kiguruira, inyonga nk, kumbuka kuna baadhi ya watanzania bado wanajua rais bado ni Nyerere.

Kwa mfano, hoja ya Udini, Ukabila, U padri wa Dr. Slaa na Ukatoriki, Ufisadi wa CHADEMA na viongozi wake wa juu ( Mbowe Magari na SLAA mshahara), Ubaguzi wa kikanda nk , Haya yanahitaji yajibiwe kwenye mikutano ya hadhara kwani huko coverage inakuwa kubwa kuliko magazeti na TV.

Kukuhakikishia hayo CHADEM imeeleweka kwamba si ya Ukabila, Udini na hata huu ufisadi wa juzi watu wanaelewa kwamba ni propaganda za CCM kwani wana ZIGO kubwa la ufisadi wameshindwa kulitua. Viongozi wa CHADEMA watazidi kuwaelewesha wananchi wajue kwamba mshahara as mshahara hauwezi kugeuka ukawa UFISADI - sasa inabidi kutumia majukwaa na lugha nyepesi ili watu waelewe na kuiamini CHADEMA zaidi na zaidi.

CHADEMA moto ule ule - NAPE tushammaliza sasa tunasuburi mwingine anyenyue pua.
 
Nnakubaliana na mtoa mada lakini pia nnapingana nae kwa jambo moja:kuwa Chadema wasijibizane na ccm.Ikumbukwe uongo ukiachwa utawale kwa muda mrefu utaonekana kuwa ni ukweli.Hivyo Kama anatokea mtu anakunyooshea kidole waziwazi na kukwambia wewe upo hivi au upo vile lazima umjibu Tena mapema hasa jambo lenyewe likiwa ni baya.Sioni ubaya wowote kwa Chadema kuzijibu hoja hafifu za ccm.

Your are very right mkuu, uwongo lazima uwekwe wazi, CDM haiwezi kuwapuuza tu na kusgughulika na mbinu za kupunguza gharama z amaisha au kuzungumzia katiba nk maana watekelezaji wakuu wa mambo hayo ni serilkali ya ccm, sasa bila kuwa na nguvu ya hoja inawezekana? Watu wengi lazima wajue true colors za CCM na hasa kauli zao na ahadi zao hewa
 
The Boss umepiga pazuri kabisa. Haya maoni yako ni sawa kabisa kwani inaonekana kama CDM wanaanza kucheza ngoma ya malumbano na CCM. Watanzania wanaonekana kuwa na imani na CDM kulingana na jinsi wanavyowatoa tongotongo za kisiasa. Sasa mtindo wa kuendelea kujibizana kwa mambo yasiyo na tija kwa watanzania ni kupoteza muda na nguvu bure.

CDM waendelee kuibua uozo wa CCM unaotufanya tuendelee kuwa maskini japo wenyewe wanadai hawajui kwanini nchi yetu ni maskini. malumbano na huyo dogo (Nape) hayawasaidii wala kuwasaidia wananchi. Wajenge chama, watoe hoja zenye uzito wa kutosha na wahakikishe kuwa Serikali inabanwa vilivyo bungeni ili kutekeleza ahadi lukuki zilizomwagwa wakati wa uchaguzi.

Mwisho kabisa wana JF inabidi wakubali kuwa jamvi hili ni la watanzania wenye uchungu na nchi yao. Wapo watu ambao ni neutral kabisa nikiwa na maana si CDM wala CCM. They have to be given a chance to speak their mind as well.....!

Alamsiki
 
Back
Top Bottom