Chadema wanamtambua rais: Jana, leo, kesho na keshokutwa

Albert Msando

JF-Expert Member
Nov 2, 2010
1,019
171
WanaJF,

Suala la CDM kumtambua au kutomtambua Raisi wa JMT limezua mijadala mbalimbali.

Kuweka rekodi sawa imebidi niweke hoja mbele yenu. Hoja yangu ni kwamba kama CDM tumeendelea kumtambua Raisi kwa matendo yetu ingawaje kwa vinywa vyetu imekuwa ngumu kutamka.

Nakubali kwamba ilitamkwa kwamba hatumtambui Raisi na haijawahi kutamkwa vinginevyo. Nakubali kwamba hata wakati wa sherehe za kumuapisha tuligoma kwenda na alipolihutubia Bunge tulitoka.

Lakini, muda huo huo tumeendelea kuhudhuria vikao vya Bunge na kuwahoji mawaziri aliowateua. Tunawahoji kwa nafasi zao za uwaziri na kutegemea watafanya yale tunayoyahoji.

Je inawezekana kuwatambua mawaziri na kazi zao kama humtambui aliyewateua?

Tunaishinikiza 'serikali' ifanye yale tunayoyataka, je serikali inaweza kuwepo kama Raisi hayupo? Au kutomtambua Raisikuna maana gani? Ni kutotambua mamlaka yake au ushindi wake?

Ufafanuzi huu haujatolewa na CDM hivyo ni salama kuamini kwamba CDM inatambua mamlaka ya Raisi na kuiheshimu.

Katika hili CDM lazima ibebe lawama za kutotoa ufafanuzi wa kauli au matamko kwamba haimtambui Raisi kwa wananchi waelewe. Kwa kiongozi yeyote kauli yake lazima iwe inayoeleweka na ya wazi kiasi kwamba mpokeaji wake anakuwa kwenye nafasi ya kuielewa ili kufanya uamuzi sahihi. Si salama kuacha matendo yakatumika kutoa tafsiri.

Kama CDM bado haimtambui Raisi ni vyema ikasemwa wazi na kwa lugha nyepesi. Huo ni ukomavu wa kisiasa na uthibitisho wa nia njema na thabiti ya kiuongozi.

Mimi binafsi kama mwanaCDM kwa maneno na kauli yangu namtambua Raisi. Napinga ushindi wake na sikubali daima kwamba alishinda kihalali. Kulikuwa na hila za kila aina ili aweze kushinda. Lakini nchi yetu inaongozwa kwa mujibu wa sheria, sheria zetu zimeruhusu Raisi anayeshinda kwa hila aongoze nchi hivyo namtambua kama Raisi wa JMT aliyeshinda kwa hila.

Nawatambua mawaziri na watendaji wengine walioteuliwa na Raisi aliyeshinda kwa hila.

Siwezi kuthibitisha hila hizo kwa sababu sheria hainiruhusu kuthibitisha baada ya NEC kumtangaza mshindi.

Jana, leo, kesho na keshokutwa Raisi wa JMT aliyeshinda kwa hila ndie Raisi na nimetambua na ninatambua na nitatambua hivyo!
 
Mkuu,
Hivi umeshawashauri viongozi wa chama chako kuhusu kutoa ufafanuzi mwepesi na unaoeleweka kwa wananchi kama unavyosema hapa?
"Katika hili CDM lazima ibebe lawama za kutotoa ufafanuzi wa kauli au matamko kwamba haimtambui Raisi kwa wananchi waelewe."

Au ungependa Dr. Slaa, Zitto, Regia nk wakusome hapa JF ndio waitishe vikao vyao ili kutengeneza huo ufafanuzi na tamko ambalo unaliona ni jambo muhimu kufanyika?
Umesema katika Post moja kuwa wewe ni Diwani wa CDM, sasa si ingekuwa busara kuwashauri hawa viongozi wako kwanza kupitia ofisi zenu za chama na Vikao vyenu? Au viongozi wako ni "hawaambiliki?","Hawashauriki?"

Hata hivyo, hongera kwa ujasiri huu uliouonesha na kutumia haki yako ya free speech! Nategemea viongozi wakuu wa CDM watapata ujumbe huu na pengine wataufanyia kazi ili kuonesha "ukomavu wa kisiasa na uthibitisho wa nia njema na thabiti ya kiuongozi."

Umepitia:: IPPMEDIA Kamanda anataniana na wanasiasa wenzake. Wamependeza.
 
MODS IUNGANISHE HII THREAD NA YA Pasco aliyomsingizia Mh.Mbowe.

Hatuwezi kurudia kujadili hoja ya Pasco, itakuwa ni kurudia rudia tu huu utumbo.
 
Acha kuzungusha mada. CDM hatumtambui kikwete kama rais wa JMT. Ninyi viongozi wa CDM mliotokea huko rombo mna matatizo. Mwenzio naye Selasini Hivyo hivyo, bungeni alitoa kauli zinazopingana na sera za chadema. MSITUCHANGANYE!
 
Nadhani iunganishwe na ile nyingine ya pasco tunayojadili sasa, ZINASHABIHIANA.
 
WanaJF,

Suala la CDM kumtambua au kutomtambua Raisi wa JMT limezua mijadala mbalimbali.

Kuweka rekodi sawa imebidi niweke hoja mbele yenu. Hoja yangu ni kwamba kama CDM tumeendelea kumtambua Raisi kwa matendo yetu ingawaje kwa vinywa vyetu imekuwa ngumu kutamka.

Nakubali kwamba ilitamkwa kwamba hatumtambui Raisi na haijawahi kutamkwa vinginevyo. Nakubali kwamba hata wakati wa sherehe za kumuapisha tuligoma kwenda na alipolihutubia Bunge tulitoka.

Lakini, muda huo huo tumeendelea kuhudhuria vikao vya Bunge na kuwahoji mawaziri aliowateua. Tunawahoji kwa nafasi zao za uwaziri na kutegemea watafanya yale tunayoyahoji.

Je inawezekana kuwatambua mawaziri na kazi zao kama humtambui aliyewateua?

Tunaishinikiza 'serikali' ifanye yale tunayoyataka, je serikali inaweza kuwepo kama Raisi hayupo? Au kutomtambua Raisikuna maana gani? Ni kutotambua mamlaka yake au ushindi wake?

Ufafanuzi huu haujatolewa na CDM hivyo ni salama kuamini kwamba CDM inatambua mamlaka ya Raisi na kuiheshimu.

Katika hili CDM lazima ibebe lawama za kutotoa ufafanuzi wa kauli au matamko kwamba haimtambui Raisi kwa wananchi waelewe. Kwa kiongozi yeyote kauli yake lazima iwe inayoeleweka na ya wazi kiasi kwamba mpokeaji wake anakuwa kwenye nafasi ya kuielewa ili kufanya uamuzi sahihi. Si salama kuacha matendo yakatumika kutoa tafsiri.

Kama CDM bado haimtambui Raisi ni vyema ikasemwa wazi na kwa lugha nyepesi. Huo ni ukomavu wa kisiasa na uthibitisho wa nia njema na thabiti ya kiuongozi.

Mimi binafsi kama mwanaCDM kwa maneno na kauli yangu namtambua Raisi. Napinga ushindi wake na sikubali daima kwamba alishinda kihalali. Kulikuwa na hila za kila aina ili aweze kushinda. Lakini nchi yetu inaongozwa kwa mujibu wa sheria, sheria zetu zimeruhusu Raisi anayeshinda kwa hila aongoze nchi hivyo namtambua kama Raisi wa JMT aliyeshinda kwa hila.

Nawatambua mawaziri na watendaji wengine walioteuliwa na Raisi aliyeshinda kwa hila.

Siwezi kuthibitisha hila hizo kwa sababu sheria hainiruhusu kuthibitisha baada ya NEC kumtangaza mshindi.

Jana, leo, kesho na keshokutwa Raisi wa JMT aliyeshinda kwa hila ndie Raisi na nimetambua na ninatambua na nitatambua hivyo!

Mkuu wewe ni kiongozi wa cdm kwahiyo unayo nafasi nzuri sana ya kutumia utaratibu wa kufikisha mawazo yako kwa viongozi wako wakuu.

Sitaki kuamini kwamba hujawasiliana na viongozi wako ili kuweka sawa msimamo wa chama chenu ama kutoa ufafanuzi ili watu wasishindwe kuwaelewa, manake sasa inaonekana kila mmoja anakuja na statement yake. Au viongozi wako hawaambiliki kwahiyo umeamua kuusema ukweli wa moyo wako hadharani?

Lakini pia nadhani ni muda muafaka kwa viongozi wa cdm kuwa clear kwa watanzania na washabiki wao kama kweli hawamtambui jk kinadharia ilihali kivitendo wanamtambua.

Anyway, ngoja tuendelee kusubiri muda si mrefu huenda tukapata kauli ya cdm manake viongozi wake ni members hapa watatujulisha msimamo wa cdm ni upi kwa rais jk.
 
Acha kuzungusha mada. CDM hatumtambui kikwete kama rais wa JMT. Ninyi viongozi wa CDM mliotokea huko rombo mna matatizo. Mwenzio naye Selasini Hivyo hivyo, bungeni alitoa kauli zinazopingana na sera za chadema. MSITUCHANGANYE!
Jibu hoja uache pumba na ubaguzi!
 
Labda niwe kama Zitto Bungeni jana. Hakuna chama cha siasa nchini kinaitwa CDM. Tuna CHADEMA.
 
Jamani ,
GT wa siku hizi wako kama wamepitia sec za kata hawasomi jambo wakalielewa unapobisha jambo toa sababu basi unabisha kama mpiga debe jamani upe uwanja huu hadhi yake wanaoingia kama wageni wavutiwe kuingia nao wachangie mawazo kwa maslahi ya Taifa .
Sasa ukiangalia mtoa mada ameeleza kwa ufasaha sababu za kumtambua Rais na hata viongozi wakuu wa CDM wanamtambua hila wanapinga taratibu zilizomweka madarakani yaani ushindi wa kimagumashi ambao kwa kuwa tume ya taifa ya uchaguzi imeshamtangaza hauruhusiwi kupinga eneo lolote zaidi ya kulalama kama hivi mnavyofanya lakini anabaki kuwa rais wako period
 
Alberto unataka timu nzima ya chadema wakufuate nyumbani kwako wakupe ufafanuzi... cuz hii ki2 walishatoa ufafanuzi zaidi ya maramoja... SORRY NAOMBA ELIMU YAKO MAANA DAH UELIMISHIKI.. Walisema hawatambui utaratibu ulimwoka rais madarakani... lakini wataudhuria na kushiriki bunge kwa mambo ya msingi na maslahi ya wananchi waliowaweka madarakani..
 
GTs,

Kuwa kiongozi wa wananchi kupitia CHADEMA (mimi ni Diwani ya Kata ya Mabogini, Moshi Vijijini) na sio kiongozi wa chama, hakuniondolei haki ya kusema kile ninachoamini humu JF.

Chadema ni chama ambacho kinaruhusu fikra binafsi. Naruhusiwa kusema mawazo yangu ndani na nje ya vikao ili mradi mawazo yangu na fikra zangu hazipingani na sera za chama. Kutomtambua Raisi sio sera ya Chadema!!

Unapokuwa mwanaChadema halafu hutaki kufikiri, huna ujasiri wa kutoa mawazo yako na huna utayari wa kusema ukweli hufai kuwa mwanachama! Viko vyama vinavyokufaa zaidi lakini sio CDM.

Ili chama kikue lazima kiruhusu changamoto za mawazo binafsi yanayotolewa na wanachama wake kwa kujali maslahi ya chama.

Kuhusu mkanganyiko wa kauli au tamko la kutomtambua Raisi sihitajiki kulipeleka kwenye vikao. Na kusema hapa JF haimaanishi kwamba sitalisema kwenye vyombo husika.

Tuache woga wa kutokusema ukweli. Mimi nitausema na mawazo yangu nitayasimamia iwe ni JF au kwenye vikao.
 
Msando,

Wakati mwenyekiti wa Chadema Mbowe anatangaza kutomtambuwa Raisi alisema kwamba ''' Katika mazingira haya ya kikatiba na kisheria njia pekee ya CDM kuonesha kwamba kulikuwa na ukiukwaji mkubwa katika uchaguzi 2010 ni kuendelea kutii dhamira zetu ( tunazoamini kwamba usalama wa taifa na tume ya uchaguzi uliingilia mchakato) kwa kukataa matokeo ya uraisi.

Wakatoka nje ya bunge kuonesha Dunia nzima kwamba kulikuwa na ukiukwaji mkubwa kwenye taratibu za kiuchaguzi.

Kwa sasa CDM wanafanya kazi na watu ambao wameteuliwa na raisi ambae kimsingi wanahoji mchakato wa upatikanaji wake.Lakini kwa upande wangu hatua za kutangaza kutomtambua na mambo yote waliyoyafanya yameamsha kitu.Kilio cha katiba mpya kimeshika kasi na hata ripoti ya ulaya imeponda muundo wa tume ya taifa ya uchaguzi.
 
Ihi ina maana CCM kimejaa vilaza sana au ? ni kwanini wanashindwa kuelewa simple statements ?
 
Alberto unataka timu nzima ya chadema wakufuate nyumbani kwako wakupe ufafanuzi... cuz hii ki2 walishatoa ufafanuzi zaidi ya maramoja... SORRY NAOMBA ELIMU YAKO MAANA DAH UELIMISHIKI.. Walisema hawatambui utaratibu ulimwoka rais madarakani... lakini wataudhuria na kushiriki bunge kwa mambo ya msingi na maslahi ya wananchi waliowaweka madarakani..

Straight,

Elimu yangu ni Shahada ya Kwanza ya Sheria, Chuo Kikuu Mlimani. Ni wakili wa kujitegemea.

Kwa sasa ndie wakili wa Chadema kanda ya Kaskazini.

Ni kweli sielewi kwanini tunazungusha maneno na kuwa wakali tunapoulizwa;

Je CHADEMA mnamtambua Raisi wa JMT?

Hakuna atakaye tuchapa tukijibu; Hatumtambui Raisi wa JMT. Sio Raisi wa JMT.

Haturudii hayo maneno ili wananchi waelewe. Hivi mwananchi aliyeko kijiji cha Chemchem anaelewa nini unaposema humtambui Raisi lakini anakusikia unamuuliza Waziri Mkuu Serikali itachukua hatua gani kumaliza tatizo la umeme?

Kusema kwamba msimamo wa CDM kuhusu kumtambua Raisi unaeleweka ni kujidanganya. Itatuumiza kama chama!

Hiyo ndio hoja yangu. Kwa nini kama CDM tusikae kimya kuona wengine wanasemaje ili tupime na kujua nini cha kufanya?

Kama hapa JF watu hawalewi unafikiri huko vijijini hali ikoje? Mimi naliona hili kila siku kwa wananchi wangu. Mkanganyiko huo sio kwamba naujua kwa kusoma post, hapana! Naujua kwa kuwepo kwenye kata na kuwasikia wananchi!

Hatuwezi kuruhusu uendelee! Ukisoma post yangu utaona nimemalizia kwa kusema napinga na nitapinga daima utaratibu uliotumika kumpata Raisi. Hata kama aliiba kura lakini sheria inamtambua, sisi ni nani hatumtambui?

You cant eat your cake and have it.

Kama hatumtambui basi tusitambue lolote analofanya kama Raisi. Tusipokee posho za vikao, tusiwatume mawaziri wake, tusitumie magari yao nk. Tuache siasa nyepesi na za kinafiki.

Unafikiri Misri wangesema hatumtambui Hosni Mubarak ila tutashirikiana na Makamu wake wa Raisi ingekuwaje?

Sitaki viongozi wa CDM waje kwangu, waende kwa wananchi na kuwapa ufafanuzi unaoleweka wa nini tunachosimamia!

Angalizo; humu ni JF sio kikao cha Chadema. Suala kwamba nipeleke hoja kwa viongozi wa CDM siliafiki. Nitapeleka muda ukifika kwa sasa hoja iko hapa tusikie mawazo ya wengine ili tujue tumekosea au tumepatia!
 
Straight,

Elimu yangu ni Shahada ya Kwanza ya Sheria, Chuo Kikuu Mlimani. Ni wakili wa kujitegemea.

Kwa sasa ndie wakili wa Chadema kanda ya Kaskazini.

Ni kweli sielewi kwanini tunazungusha maneno na kuwa wakali tunapoulizwa;

Je CHADEMA mnamtambua Raisi wa JMT?

Hakuna atakayetuchapa tukijibu;

Hatumtambui Raisi wa JMT. Haturudii hayo maneno ili wananchi waelewe. Hivi mwananchi aliyeko kijiji cha Chemchem anaelewa nini unaposema humtambui Raisi lakini nakusikia unamuuliza Waziri Mkuu Serikali itachukua hatua gani kumaliza tatizo la umeme?

Hiyo ndio hoja yangu. Kwa nini kama CDM tusikae kimya kuona wengine wanasemaje ili tupime na kujua nini cha kufanya?

Kama hapa JF watu hawalewi unafikiri huko vijijini hali ikoje? Mimi naliona hili kila siku kwa wananchi wangu. Mkanganyiko huo sio kwamba naujua kwa kusoma post, hapana! Naujua kwa kuwepo kwenye kata na kuwasikia wananchi!

Hatuwezi kuruhusu uendelee! Ukisoma post yangu utaona nimemalizia kwa kusema napinga na nitapinga daima utaratibu uliotumika kumpata Raisi. Hata kama aliiba kura lakini sheria inamtambua, sisi ni nani hatumtambui?

You cant eat your cake and have it. Kama hatumtambui basi tusitambue lolote analofanya kama Raisi. Tusipokee posho za vikao, tusiwatume mawaziri wake, tusitumie magari yao nk. Tuache siasa nyepesi na za kinafiki.

Unafikiri Misri wangesema hatumtambui Hosni Mubarak ila tutashirkiana na Makamu wake wa Raisi ingekuwaje?

Sitaki viongozi wa CDM waje kwangu, waende kwa wananchi na kuwapa ufafanuzi unaoleweka wa nini tunachosimamia!

Angalizo; humu ni JF sio kikao cha Chadema. Suala kwamba nipeleke hoja kwa viongozi wa CDM siliafiki. Nitapeleka muda ukifika kwa sasa hoja iko hapa tusikie mawazo ya wengine ili tujue tumekosea au tumepatia!

Kama ndivyo hivyo basi hoja yako ingekuja kwa mtazamo kuwa " msimamo wa chadema wa kutotambua mchakato wa kumpata Raisi unatatiza wananchi, nini kifanyike".........Lakini sasa wewe umekuja na uwongo wa kusema Chadema walisema hawamtambui Rais hivyo wananchi wanachanganyikiwa! Napata shida na dhamira yako!
 
Acha kuzungusha mada. CDM hatumtambui kikwete kama rais wa JMT. Ninyi viongozi wa CDM mliotokea huko rombo mna matatizo. Mwenzio naye Selasini Hivyo hivyo, bungeni alitoa kauli zinazopingana na sera za chadema. MSITUCHANGANYE!

1. Sijatokea Rombo.

2. Kauli kama hiyo ya 'urombo' haijengi.

3. Tunaonyeshaje kwamba hatumtambui? Tunafanikisha nini kwa kutomtambua Raisi?

4. Kutomtambua Raisi sio sera.

5. Tutaacha kuchanganyikiwa tu endapo tutakuwa wazi na tayari kuwa responsible kwa kauli zetu.

Jaribu kufikiri zaidi tujue nini cha kufanya kama chama badala ya kuwa mwepesi kusema kama ulivyosema! Tujenge chama makini kwa kukubali kufikiri!
 
Kama ndivyo hivyo basi hoja yako ingekuja kwa mtazamo kuwa " msimamo wa chadema wa kutotambua mchakato wa kumpata Raisi unatatiza wananchi, nini kifanyike".........Lakini sasa wewe umekuja na uwongo wa kusema Chadema walisema hawamtambui Rais hivyo wananchi wanachanganyikiwa! Napata shida na dhamira yako!

Ndio maana ya majadiliano. Unachokisema ni kwamba Chadema hawajawahi kutoa kauli kwamba hawamtambui Raisi?

Unasema kwamba Chadema ambacho hawatambui ni mchakato uliotumika?

Dhamira yangu ni kupata ukweli na kuelimika! Niambie ukweli na unielimishe!
 
GTs,

Kuwa kiongozi wa wananchi kupitia CHADEMA (mimi ni Diwani ya Kata ya Mabogini, Moshi Vijijini) na sio kiongozi wa chama, hakuniondolei haki ya kusema kile ninachoamini humu JF.

Chadema ni chama ambacho kinaruhusu fikra binafsi. Naruhusiwa kusema mawazo yangu ndani na nje ya vikao ili mradi mawazo yangu na fikra zangu hazipingani na sera za chama. Kutomtambua Raisi sio sera ya Chadema!!


Unapokuwa mwanaChadema halafu hutaki kufikiri, huna ujasiri wa kutoa mawazo yako na huna utayari wa kusema ukweli hufai kuwa mwanachama! Viko vyama vinavyokufaa zaidi lakini sio CDM.

Ili chama kikue lazima kiruhusu changamoto za mawazo binafsi yanayotolewa na wanachama wake kwa kujali maslahi ya chama.

Kuhusu mkanganyiko wa kauli au tamko la kutomtambua Raisi sihitajiki kulipeleka kwenye vikao. Na kusema hapa JF haimaanishi kwamba sitalisema kwenye vyombo husika.

Tuache woga wa kutokusema ukweli. Mimi nitausema na mawazo yangu nitayasimamia iwe ni JF au kwenye vikao.

Thanks Alberto! tunahitaji watu majasiri kama wewe, people who call things their names!. wewe ni kiongozi wa kweli nafikiri tutakuona mjengoni very soon.
 
Ndio maana ya majadiliano. Unachokisema ni kwamba Chadema hawajawahi kutoa kauli kwamba hawamtambui Raisi?

Unasema kwamba Chadema ambacho hawatambui ni mchakato uliotumika?

Dhamira yangu ni kupata ukweli na kuelimika! Niambie ukweli na unielimishe!

Ndicho ninachokisema na ninaamini ndicho viongozi wa Chadema kina Mbowe na Dk.Slaa wamekuwa wakihubiri mara kadhaa, kuwa wanamtambua Rais sababu ni halali kikatiba, sababu Rais akishatangazwa kwa mujibu wa sheria zetu hawezi kupingwa popote. Na kuwa Chadema walitoka nje ya Bunge wakati Kikwete anahutubia kuonyesha kutoridhishwa kwao na jinsi kanuni za Uchaguzi wa Rais zinavyonyima haki ya wananchi kupata Rais halali walomchagua...yapo mengi lakini moja ni hili la kutoweza kupinga matokeo ya Rais popote pale baada ya kutangazwa
 
Back
Top Bottom