kitalolo
JF-Expert Member
- Dec 4, 2006
- 1,827
- 707
Akihojiwa na radio moja mkoani Arusha jana, katibu wenezi wa ccm mkoa wa Arusha Bw. Semi Kiondo, amesema ushindi wa CDM jimbo la Arumeru Mashariki ni sawa na mtu aliyeokota pochi. akifafanua zaidi amesema pochi hilo CCM wamelidondosha na CDM wameliokota kwa bahati mbaya na kwamba CDM wasijitape sana kwani pochi sio lao.
Baada ya mahojiano hayo ilifuatiwa na maoni ya wananchi kwa njia ya simu ambapo kila aliyepiga simu alimchana live Bw. Kiondo hakukuwa na hata msikilizaji mmoja alirithika na maneno hayo ya kada huyu wa CCM.
Baada ya mahojiano hayo ilifuatiwa na maoni ya wananchi kwa njia ya simu ambapo kila aliyepiga simu alimchana live Bw. Kiondo hakukuwa na hata msikilizaji mmoja alirithika na maneno hayo ya kada huyu wa CCM.