Synthesizer
JF-Expert Member
- Feb 15, 2010
- 11,141
- 18,769
Wakuu wa mikoa na wilaya kutokuwa sehemu ya siasa ni jambo ambalo limepigiwa sana kelele na upinzani, na CCM kulizibia masikio. Hii ina maana Chadema wakishinda uraisi 2015, itabidi wabadilishe wakuu wote wa wilaya na mikoa kwa mpigo!
Tukiweka ushabiki wa kichama pembeni, nadhani hili ni suala linalopaswa kuangaliwa kwa umakini katika mabadiliko ya katiba. Huenda hata ni vema kutokuwa na nafasi za wakuu wa wilaya na mikoa bali wakurugenzi ambao hawapaswi kuwa na mfungo wa kisiasa. Wakuu wa wilaya na mikoa hawana lolote la maana wanalochangia zaidi ya propaganda, na mara nyingi kuwa kikwazo kwa wakurugenzi wa wilaya na mkoa.
Tukiweka ushabiki wa kichama pembeni, nadhani hili ni suala linalopaswa kuangaliwa kwa umakini katika mabadiliko ya katiba. Huenda hata ni vema kutokuwa na nafasi za wakuu wa wilaya na mikoa bali wakurugenzi ambao hawapaswi kuwa na mfungo wa kisiasa. Wakuu wa wilaya na mikoa hawana lolote la maana wanalochangia zaidi ya propaganda, na mara nyingi kuwa kikwazo kwa wakurugenzi wa wilaya na mkoa.