CUF Ngangari
JF-Expert Member
- Aug 11, 2011
- 273
- 51
Chama cha Demokrasia na Maendeleo kimeomba kukutana na kikwete kwa nia ya kuzungumzia mabadiliko ya mswada uliopitishwa juu ya uundaji kamati ya kukusanya maoni kwa wanainchi, huku wakiwa wamesahau kuwa walíisha wahi kutoka ndani ya bunge kwa madai eti hawatambui mchakato uliomuweka madarakani, yaani ni sawa na kusema "hawamtambui Rais" Leo mnajipeleka wenyewe bila kuitwa, wameshindwa chadema kutambua kuwa lugha wanayoisikia CCM, Kisiasa katika hili wamèfeli wao ndio walikuwa wanasema kuwa hawawezi kukaa meza moja na CCM Leo mnamuomba Raisi mkutane? mtambue hata CUF hawakuomba kukutana kukutana na CCM hata siku moja ila walitambua Lugha wanayoisikia CCM ni Maandamano yasiyo na kibali, ndio LUgha CCM wanayoisikia, wenyewe utawasikia njooni tuzungumze, kwa Chadema kujipeleka kwa kikwete mmejiuza bei sawa na bure, kwa kufanya hivyo mmetufadhaisha sana.