Mwiba
JF-Expert Member
- Oct 23, 2007
- 7,607
- 1,744
- Thread starter
- #41
yakhe maalim yupo katika kazi kwani kazi tuliyomtuma hajaimaliza na wewe kama shahidi ,angalia tu na utakuja kuona kuwa jamaa ni MasterMind wa kuiondoa CCM kwenye madaraka ,haya ya huku yawache kama yalivyo ,CUF inasema wameshaingiza mguu mmoja ndani ya Ikulu sasa wanapigania kuingiza wa pili.Kazi huko mnakogombea umeya !Naama Mwiba, Maalim Seif anaendeleaje na mnofu wa ngurue alioamua kuisaidia CCM kutafuna huko yakhe?
Tahadhari kubwa kwa wale ambao mawazo yao yanamuona Maalim Seif kama aliyepewa au kutupiwa fupa,mtakuwa mnakosea sana ,Msimamo waake na wa Chama Chake ni kuhakikisha CCM inaondoka madarakani,mwanzo walikuwa CCM watupu ,sasa hayo ni baada ya kusukumwa na CUF ,hivyo nguvu za kusukuma bado zinaendelea na hatimae kama yalivyomashindano ya mueleka ni kumsukuma hadi kumtoa nje ya ulingo,na hapa walipo wanendelea kumsukuma hadi wanahakikisha wametupa nje.
Ila Chadema wacheni kupelekwa puta na CCM ,mkifanya mchezo mtanasa,nasema tena washukuruni polisi wamewatoa kwenye mdomo wa chewa,naamini viongozi wenu watakuwa wameshajua.