EL MAGNIFICAL
JF-Expert Member
- Jan 11, 2011
- 938
- 125
Naibu katibu mkuu wa cuf ndg. Julius Mtatiro amesema pamoja na mbinu za wapinzani wenzentu jana kusambaza vipeperushi kuwa eti mgombea wa cuf amejitoa ktk kinyang'anyiro cha udiwani utaofanyika hivi punde ili wanabagamoyo wamchague mgombea wao wa cdm, bwana Mtatiro pia amewaomba wana bagamoyo waendelee na msimamo wao thabiti na wamchague mgombea wa cuf. Akiendelea kudadavua Naibu katibu mkuu wa cuf kuwa ikiwa wapinzani wenzao wataendelea kushughulika namna hii basi ccm wataondoka lini madarakani ? Alitegemea mchezo huo mchafu wangefanya ccm kuhofia upinzani lakini waliofanya kila hila ni wapinzani wenzao.
Amemaliza kwa kusema chuki, ubinafsi na umimi vinaharibu demokrasia ya vyama vingi hasa kwa tu-vyama twetu hutu tunatotafuta dola.
Source: page yake ya facebook.
Amemaliza kwa kusema chuki, ubinafsi na umimi vinaharibu demokrasia ya vyama vingi hasa kwa tu-vyama twetu hutu tunatotafuta dola.
Source: page yake ya facebook.