Mkwawa
JF-Expert Member
- Jun 8, 2011
- 1,334
- 1,464
Mjadala mkali unaendelea kati ya Ikulu na CDM unadhihirisha wazi kuwa wingi wa wabunge wa CCM ndani ya Bunge la muungano ni mzigo na hasara kubwa sana kwa wananchi na Taifa zima la Tanzania.
Bunge la JMT lilojaa wabunge wengi wa CCM ambao kati yao wapo wasomi waliobobea kwenye maswala ya katiba, sheria, utawala, uchumi, udaktari na maswala ya kijamii wakiwa baadhi yao wamesoma vyuo maarufu duniani kama harvard , st peters, Oxford, Yale, nk wameshindwa kuona hitaji muhimu la katiba na kuandaa muswada unaendana na mazingira na hali ya sasa na ya baadaye ya nchi yetu nzuri.
Wabunge hawa wa CCM wamekuwa stamp na kusahau taaluma zao mbali mbali. hili linadhirisha kuwa ukiwa na kadi ya CCM inafuta uwezo wako wa kufikiri na kubakia kama bua kavu linalopelekwa na upepo.
Hali hii imewafanya Viongzi wa chama na Serikali kushindwa kustahimili critics zinazotolewa na makundi ya kijamii na kuufanya Muswada uliosainiwa ili kurithisha vilaza wa CCM bungeni kufanyiwa kazi upya.
CDM wamejikita kuhakikisha katiba mpya inakuwa ya manufaa kwa wote inashirikisha makundi yote ya kijamii inajadiliwa kwa uhuru na upana, na mawazo yote yanafanyiwa kazi. Kupatikani kwa kamati huru na inayojitegemea ya kukusanya maoni na kupatikana kwa wataalalmu na watu huru ku-assemble katiba.
Je kwa nini wabunge wa CCM wanakubali kutumika kama madodoki? Je kwanini wanakuwa hamnazo hata kwenye mambo muhimu ya Kitaifa? haya yanatokea kwani huwa hawashindi kihalali hawawekwi na wananchi, kwao sanduku la kuraha haliwahusu, kwao demokrasia ni ngonjera kwao maisha ya kumkomboa mtanzania ni kujimaliza. Wanaahidiwa kupitisha upuuzi wowote bungeni kwani Tume ya Taifa ya Uchaguzi itawatangaza washindi hata wasipopata kura za kutosha hii ndio maana wabunge wa CCM wapo disconnected na wapiga kura.
CDM wanatumia karata ya mwisho kumlazimisha JK kurudisha mswada bungeni au kubadili muundo mzima wa kutafuta katiba mpya. Kwa hali ilivyo sasa JK hana jinsi kwani wabunge wake hawana la kuuza kwa wananchi, kwani mswada ni mbovu hata wao wenyewe wanauogopa.
Chief Mkwa wa Kalenga
Tanzania Huru Itajengwa na mimi na wewe.
Bunge la JMT lilojaa wabunge wengi wa CCM ambao kati yao wapo wasomi waliobobea kwenye maswala ya katiba, sheria, utawala, uchumi, udaktari na maswala ya kijamii wakiwa baadhi yao wamesoma vyuo maarufu duniani kama harvard , st peters, Oxford, Yale, nk wameshindwa kuona hitaji muhimu la katiba na kuandaa muswada unaendana na mazingira na hali ya sasa na ya baadaye ya nchi yetu nzuri.
Wabunge hawa wa CCM wamekuwa stamp na kusahau taaluma zao mbali mbali. hili linadhirisha kuwa ukiwa na kadi ya CCM inafuta uwezo wako wa kufikiri na kubakia kama bua kavu linalopelekwa na upepo.
Hali hii imewafanya Viongzi wa chama na Serikali kushindwa kustahimili critics zinazotolewa na makundi ya kijamii na kuufanya Muswada uliosainiwa ili kurithisha vilaza wa CCM bungeni kufanyiwa kazi upya.
CDM wamejikita kuhakikisha katiba mpya inakuwa ya manufaa kwa wote inashirikisha makundi yote ya kijamii inajadiliwa kwa uhuru na upana, na mawazo yote yanafanyiwa kazi. Kupatikani kwa kamati huru na inayojitegemea ya kukusanya maoni na kupatikana kwa wataalalmu na watu huru ku-assemble katiba.
Je kwa nini wabunge wa CCM wanakubali kutumika kama madodoki? Je kwanini wanakuwa hamnazo hata kwenye mambo muhimu ya Kitaifa? haya yanatokea kwani huwa hawashindi kihalali hawawekwi na wananchi, kwao sanduku la kuraha haliwahusu, kwao demokrasia ni ngonjera kwao maisha ya kumkomboa mtanzania ni kujimaliza. Wanaahidiwa kupitisha upuuzi wowote bungeni kwani Tume ya Taifa ya Uchaguzi itawatangaza washindi hata wasipopata kura za kutosha hii ndio maana wabunge wa CCM wapo disconnected na wapiga kura.
CDM wanatumia karata ya mwisho kumlazimisha JK kurudisha mswada bungeni au kubadili muundo mzima wa kutafuta katiba mpya. Kwa hali ilivyo sasa JK hana jinsi kwani wabunge wake hawana la kuuza kwa wananchi, kwani mswada ni mbovu hata wao wenyewe wanauogopa.
Chief Mkwa wa Kalenga
Tanzania Huru Itajengwa na mimi na wewe.