nzitunga
Senior Member
- Oct 31, 2010
- 193
- 53
I agree with you 100%, nawasikitikia hawa vijana, hawamjui Mbowe, ni dictator ile mbaya, na yupo Chadema si kwa maslahi ya waTanzania bali kuna mambo na malengo yake binafsi.
Mie nawashangaa sana wa Tanzania wenzangu wengine, hivi huyu jamaa ambae klabu zake za usiku zina uozo wa uadilifu kupindukia, na yule Dokta Slaa ndio kama tujuavyo, ana kesi ya kupora Mke wa mtu, ndio wanawashabikia na kuwasikiliza eti ni viongozi, wanaongoza nini?
Mbowe na wenzake wapo kwa ajili ya maslahi ya Watz. Watu utawajua kwa matendo yao. Kama CCM ama JK/Kayanja/na wengine wengi wangekuwa na mapenzi mema na nchi hii wasingefanya uchakachuaji mkubwa katika historia yetu. Wasingechochea chuki ya kidini ndani ya watz. Kama wanaipenda Tz, wasingekubali mali ya umma ipotee huku wenye mali wakifa kwa njaa, magonjwa na ujinga uliopindukia na ilihali wageni wanafaidi mali hiyohiyo na kuwa mabilionea huko kwao. Wasingekubali kutumia pesa ya umma kama EPA kuwaingiza madarakani. Wangeleta katiba mpya yenye kuwapa nguvu wananchi kuchagua kiongozi wamtakaye na kuifuta tume ya kichina inayowachagulia watu kiongozi na kuburuza matakwa ya watu.
Nataka kuwatia moyo CHADEMA, viongozi wake na wote wenye mapenzi mema na nchi hii, aruta continue, mpaka kieleweke. Hii sio nchi ya CCM, hii ni nchi ya watanzania. CCM ilizaliwa na ipo siku itakufa. Vyama vyote vina haki sawa. Na hata Mbowe/Slaa wakikaa kimya leo hii, nakuakikishia watainuka wengine kudai haki hii, tena watadai kwa nguvu ya ajabu. Watanzania wamechoka na manyanyaso ya CCM.