Curriculum Specialist
JF-Expert Member
- Oct 8, 2007
- 2,731
- 749
Wakati jana imeripotiwa kwamba CCM waliwashambulia kwa mawe wafuasi wa CDM huko Dodoma na kujeruhi vibaya mwandishi wa habari,leo gazeti la serikali Habari Leo limeripoti tofauti na kusema CDM ndiyo walivamia mkutano wa CCM na kujeruhi viongozi wawili kwa mawe.Kama gazeti la Habari Leo litakuwa limepotosha basi Taifa litaangamia kwa aina hii ya uandishi wa kishabiki!
Waongo hao, mimi niliongea na wananchi waliohudhuria mkutano walisema CCM ndo walioingilia msafara wa chadema na mgombea wao na kuanza kuwarushia mawe kitendo kilichosababisha vurugu na kuanza kurushiana mawe!