Chadema wakiongozwa na Mh. Godbless Lema wameandama mjini Arusha wakielekea ofisi za manispaa, lilikuwa kundi dogo la vijana, baada ya dk kama 2 hivi mlio mkubwa kama wa bomu ulisikika, wale vijana walisambatika wote. Hatukusikia kitu tena, nadhani ndio ulikuwa mwisho wa maandamano. Wengi walikuwa watu wa lower class (vijana waliopigika na maisha) na lilikuwa kundi dogo sana. Nawashauri CHADEMA waache kufanya mambo kwa kujaribisha kama wameamua kufanya maandamano wawahabarishe watu wote kwa njia mbalimbali kama mitandao au hata vipeperushi. Arusha barabara nyingi mbovu na muda unaenda. Kama adui anakushinda ungana nae wananchi wapate maendeleo.