CHADEMA tusilewe sifa za mjini!

JACADUOGO2.

JF-Expert Member
Dec 13, 2010
930
217
CHADEMA sasa inabidi tuamke na tuache kulewa sifa mijini wakati maeneo mengi ya vijiji hatujafanya chochote na tunasubiria mpaka uchaguzi mkuu au uchaguzi mdogo. Haipendezi hata kidogo.
Kumekuwa na tabia ya viongozi wa CHADEMA ngazi ya taifa kuongeza na kuzidisha nguvu pale ambapo tayari wananchi wameshapata mwanga kuliko maeneo mengine ambayo bado hayajaamka. Kwa mfano nguvu nyingi za Chama zinaelekezwa Arusha, Mwanza na Mbeya ambapo tayari kuna mwamko.
Maeneo ya vijijini yamesahauliwa sana. Kwa mfano wilaya nyingi zilizopo vijijini ni tabu tupu.
Naomba tujibu hoja badala ya kumshambulia mtoa hoja. Mimi ukiniuliza kuwa nimefanya nini, jibu ni kuwa nimewahi kugombea udiwani kwenye kata ya Nyahongo jimbo la Rorya kwa tiketi ya CHADEMA kwenye uchaguzi mdogo October 2011 na nilishindwa kwa tofauti ya kura 64 na CCM na tayari nimefungua matawi matatu ndani ya kata yangu na tuna ofisi ya kata safi sana na tumesimika viongozi wote ngazi msingi hadi kata na kila baada ya muda fulani narudi kuongeza nguvu ndani ya kata na jimbo!
Kwa sasa niko Sikonge Tabora katika kutafuta maisha na kwenye kampeni za uchaguzi mdogo wa madiwani hapa Sikonge (Ipole na Kiloleli) mchango wangu wa kihali na mali umeonekana na ninajivunia kuchangia ushindi katika kata ya Ipole. Kitu ambacho ni historia kwani tangu enzi na enzi CHADEMA haijaambulia kata yoyote ndani ya wilaya ya Sikonge.
Tuchangie namna ya kuongeza nguvu ya CHADEMA maeneo ya vijijini, tusisubiri 2015! Ahsanteni wadau.
 
CHADEMA sasa inabidi tuamke na tuache kulewa sifa mijini wakati maeneo mengi ya vijiji hatujafanya chochote na tunasubiria mpaka uchaguzi mkuu au uchaguzi mdogo. Haipendezi hata kidogo.
Kumekuwa na tabia ya viongozi wa CHADEMA ngazi ya taifa kuongeza na kuzidisha nguvu pale ambapo tayari wananchi wameshapata mwanga kuliko maeneo mengine ambayo bado hayajaamka. Kwa mfano nguvu nyingi za Chama zinaelekezwa Arusha, Mwanza na Mbeya ambapo tayari kuna mwamko.
Maeneo ya vijijini yamesahauliwa sana. Kwa mfano wilaya nyingi zilizopo vijijini ni tabu tupu.
Naomba tujibu hoja badala ya kumshambulia mtoa hoja. Mimi ukiniuliza kuwa nimefanya nini, jibu ni kuwa nimewahi kugombea udiwani kwenye kata ya Nyahongo jimbo la Rorya kwa tiketi ya CHADEMA kwenye uchaguzi mdogo October 2011 na nilishindwa kwa tofauti ya kura 64 na CCM na tayari nimefungua matawi matatu ndani ya kata yangu na tuna ofisi ya kata safi sana na tumesimika viongozi wote ngazi msingi hadi kata na kila baada ya muda fulani narudi kuongeza nguvu ndani ya kata na jimbo!
Kwa sasa niko Sikonge Tabora katika kutafuta maisha na kwenye kampeni za uchaguzi mdogo wa madiwani hapa Sikonge (Ipole na Kiloleli) mchango wangu wa kihali na mali umeonekana na ninajivunia kuchangia ushindi katika kata ya Ipole. Kitu ambacho ni historia kwani tangu enzi na enzi CHADEMA haijaambulia kata yoyote ndani ya wilaya ya Sikonge.
Tuchangie namna ya kuongeza nguvu ya CHADEMA maeneo ya vijijini, tusisubiri 2015! Ahsanteni wadau.

Uko sahihi. halafu bwana mdogo Zito anakigawa chama kwa kutaka URAIS
 
Hongera sana Mungu akubariki mkuu! Mi nakuunga mkono kweli kutokana na haya matokeo jamani cdm inabidi kubadilika na kutengeneza mimi kuanzia chini.
 
Halafu ningependa tuige siasa za nchi zilizoendelea kwa kueneza ''sera'' na kuwaelimisha wananchi umuhimu wa kujiandikisha na kupiga kura. Mimi nipo hapa Mbagala Dar es salaam yaani nilisikitika mno kuona hamna hata bendera ya CHADEMA. Nimejitolea kwa hali na mali kuhakikisha ofisi ya kata hapa Mbagala inakamilishwa. Nitawajulisha ikikamilika.!
 
YANI HAKUNA WATU AMBAO HUWA NAJIULIZA SIPATI MAJIBU KAMA HAWA VIONGOZI WA CDM.. NABAKI KUJIULIZA AU WANAENDA KUPATA POSHO NA KUTAFUNA ELA ZA&nbsp; CHAMA HUKO USA ,UK..YANI CHAMA HATA HUKU KWETU LINDI ,MTWARA NA SEHEMU KIBAO TZ KARIBU 90% ..WAMEKOMALIA KWENDA KUJENGA CHAMA NA KUFUNGUA MATAWI NJE YA NCHI WAKATI HUKU NDANI CHAMA HATA HAKIKUBALIKI.... USHAHIDI UCHAGUZI WA MADIWANI KWA KELELE ZA M4C TULIJUA WATACHUKUA KATA ZOTE LAKINI WAMEAMBULIA 5.<BR>USHAURI CDM ACHENI KUWEKA PESA MBELE JENGENI CHAMA NA SIO KUTAKA SIFA KUWA MNAMATAWI NJE YA NCHII,,,<BR>KWA SHERIA ZA TZ MTANZANIA ALIYEKO NJE YA NCHI HARUSIWI KUPIGA KURA NA WALA HAKUNA UTARATIBU HUO.<BR><BR>USHAURI NDO HUO INGAWA NAJUA WATUKUJA JIBU HOJA HII KWA MATUSI NA KEJELI LAKINI UKWELI NDO HUO... HATA LEO WAKIULIZWA MNAWANACHAMA WANGAPI TZ HATA HAWAJUI...LAKINI WANAWEZA SIASA ZA KULIPUA TU VIONGOZI WA NCHI.
 
Cdm tumefanya vizur sana,ila tume ya uchaguzi inapendelea ccm,wewe matokeo ya udiwani kura 3000 zinahesabiwa kuanzia saa kumi nanusu mpaka saa sita usiku!! Matokeo ya ushind wa ccm saa kumi namoja yamesha tangazwa.ya cdm mpaka watu waimbe nyimbo zoote huku wakikimbizana na mapolis.mpaka hapo nimegundua tz hakuna demokrasia.kaz sasa kwa asasi za kiraia na tume ya demokrasia nchini kudai daftar la mpiga kura na tume isiyo fungamana na chama chochote.nakama selikal haiwez kufanya hayo waende wakawaseme inje huko kwa wazamin wa tz tunyimwe misaada.hatuwez kuchaguli viongoz na kundi dogo la wazee vijana hatuna kad.fulu stop
 
Join Date : 13th December 2010
Posts : 692
Rep Power : 537
Likes Received 147
Likes Given 0

Nimevutiwa na kwenye RED
 

Similar Discussions

2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom