MKALIMOTTO
Senior Member
- Apr 7, 2012
- 136
- 9
Makamanda ninadhani sasa ni muda muafaka kwa majemedali wetu wa CDM kuanza kutuambia ni mikakati gani wameiweka juu ya sera ya utawala wa nchi hasa katika mambo ya ulinzi na usalama, sera ya nje ya nchi, uboreshaji wa maslahi ya watumishi, rasilimali za nchi dhidi ya uwekezaji dhulumifu. Ikumbukwe kuwa CDM yetu ndiyo mkombozi wa mtanzania maskini na kwamba tayari imefanikiwa kuwaamsha wananchi kutambua umuhimu wa kudai haki. Ni jambo la msingi sasa watueleze juu ya sera za utawala watakazozitumia ili kutuhakikishia umoja na utulivu wa nchi. Ninasema hivi kwasababu tangu awali Dr. Slaa ameonekana kuingia katika mgogoro na vyombo vya ulinzi na usala kama polisi, jwtz na usalama wa taifa kwa kuvituhumu kuilinda ccm. Je, akiwa Rais atavivunja na kuunda vya kwake?, atajenga urafiki ili vilinde maslahi yake?. Ikumbukwe ndugu zangu dola ndiyo nguvu ya nchi sehemu yoyote ile. Ni vyema basi viongozi wa CDM walione hilo ili wasije ingia kwa pupa, wakadhani kuivuruga dola itawasaidia la hasha. Karibuni kwa michango itakayojenga chama na utawala bora wa CDM 2015