CHADEMA: Tujadili Utayari wa Kutawala Nchi 2015

Mkuu wakati mwingine tunawalenga sana individuals na kuvilenga sana vyama. Kuna wakati naamini kuwa weakness kubwa tuliyonayo haiko kwenye individuals iko kwenye systems na institution. Ninaposema hili maana yangu ni kuwa hatuna mfumo (haupo) unaoweza kufanya mambo hapa Tanzania yaende, na hatuna institutions zinazoweza kutekeleza mambo.

Ukiangalia hapa Tanzania unaweza kuona kama Rais mzuri mambo mengi yanaenda vizuri, na kama si mzuri mambo mengi yanaenda hovyo. Ukiangalia wizara ni hivyo hivyo, kama waziri ni mzuri wizara inaenda vizuri na kama waziri si mzuri wizara inaenda hovyo...fuata utaratibu huo hadi ngazi ya chini kabisa.

Jaribu kuuangalia suala la msongamano wa magari hapa Dar, msongamano unaendelea kuwepo tangu JK aingine madarakani hakuna kilichofanyika (zaidi ya mipango na hatua ndogo ambavyo havitekelezeki), Angalia baraza la mawaziri limefanya nini, wizara ya ujenzi imefanya nini, polisi wa usalama barabarani wamefanya nini. Zaidi ya maneno hakuna chochote significant kimefanyika.

Au jaribu kuangalia akikatwa mwizi haadi kufikishwa mahakamani kusimewa mashatki na keshi yake kutolewa huku, utaona kuwa kuna mambo mengi sana hapo katikati hayafanyiki na hata kama yanafanyika ni kwa mwendo wa chura na kwa ubabaishaji mwingi.

Angalia kati ya serikali kuu, bunge, mahakama , civil society na media. Karibu kila moja haifanyi kazi inayostahili na kwa ufanisi, serikali kuu haiko united as one institution na haijui priorities zake ni zipi, bunge nalo liko kwenye sura ya kamati ya CCM zaidi kuliko bunge, mahakama ndio usiseme haina sautikabisa wakati kisheria ndio inatakiwa kuwa na sauti, civil society ndio njaa tu wao ni kama watu wanaoganga njaa, hakuna issue ya maana ambayo wameweza kupush kwa interest ya Tanzania, sana sana wanapush mambo ambayo hayana umuhimu mkubwa kwa maendeleo ya Tanzania, media ndio kabisa....apart from hapa JF na gazeti moja au mawili, majority ya waandishi na watangazaji ni vilaza na vibonde, wamebaki kufanya kazi ya entertainment zaidi ya kuelimisha na kuongopea watu.

Kwa hiyo naweza kusema pamoja na kuwa tunsema chama hiki kina itikadi hiki hakina, au huyu ni mgombea mzuri au yule si mgombea mzuri...the bottom line ni kwamba ni lazima tuweze kuwa na instututions zinazokuwa imara bila kujali nani anakuja nani anatoka.

Civilized states zote zina idara zinazojua majukumu yake, na sio kufanya kazi za zimamoto kwa amri ya katibu mkuu, mkuu wa mkoa au mkuu wa wilaya. hata mkuu wa mkoa akifanya fyongo anachukuliwa hatua mwa mujibu wa rules na regulations zilizowekwa kwa taasisi ile kufanya kazi.

Upo sahihi kabisa juu ya hili, especially umuhimu wa institutions in development; institutions zinaweka framework kwa ajili ya shughuli zote za uchumi katika taifa; tukiwa na institutions nzuri, it means kuna mazingira mazuri ya ku promote economic activity kwa mfano wananchi/wafanyakazi wanakuwa na motivation ya kufanya kazi, inventiveness n.k, lakini kama kuna bad institutions, nothing moves; Kuna njia nyingi za kupima institutional quality in a country, ikiwa ni pamoja na uwepo wa rule of law na pia democracy;

Lakini tukija kwenye suala la watu (people), hawa bado ni muhimu sana kwani bila uwepo wa watu wenye ari, mwamko, uzalendo n.k, institutions alone sio lolote;
 
Upo sahihi kabisa juu ya hili, especially umuhimu wa institutions in development; institutions zinaweka framework kwa ajili ya shughuli zote za uchumi katika taifa; tukiwa na institutions nzuri, it means kuna mazingira mazuri ya ku promote economic activity kwa mfano wananchi/wafanyakazi wanakuwa na motivation ya kufanya kazi, inventiveness n.k, lakini kama kuna bad institutions, nothing moves; Kuna njia nyingi za kupima institutional quality in a country, ikiwa ni pamoja na uwepo wa rule of law na pia democracy;

Lakini tukija kwenye suala la watu (people), hawa bado ni muhimu sana kwani bila uwepo wa watu wenye ari, mwamko, uzalendo n.k, institutions alone sio lolote;

Institutions are as good as the people who depend on them. In other words they are reflection of the people. If you can clean well your own toilet, why do you expect wonders somewhere else?
 
Labda na mie nitie neno humu..
Kiukweli vijana wengi sana hapa nchini hatuhitaji kujua TANU ilikua na malengo gani,na ni wachache sana hata wanaoelewa AZIMIO LA ARUSHA lilikua na contents gani....
Vijana wengi wanahitaji mabadiliko...THATS ALL,amini nakuambia vijana hawahitaji hata kujua CDM itawapa nini...lakini wako concern na kutoona CCM ikibaki madarakani.
Hata kama CDM wako na mapungufu kibao,lakini kuondoka kwa CCM ni moja kati ya mababiliko makubwa tunayoweza kufikia.

Mungu ibariki Tanzania,Mungu wabariki CDM.
 
Labda na mie nitie neno humu..
Kiukweli vijana wengi sana hapa nchini hatuhitaji kujua TANU ilikua na malengo gani...

Ningependa kuamini kwamba hapa hauna maana kwamba wewe kama kijana lakini pia vijana wengine wengi nchini Tanzania HAWANA ULAZIMA WA KUJUA TANU ILIUNDWA KUFANIKISHA KITU GANI TANGANYIKA. Kama hivyo ndivyo ulimaanisha, tafadhali nielimishe zaidi kwanini unafikiri hivyo ili na mimi nipate nafasi nzuri zaidi ya kujadili hoja yako;
 
Ningependa kuamini kwamba hapa hauna maana kwamba wewe kama kijana lakini pia vijana wengine wengi nchini Tanzania HAWANA ULAZIMA WA KUJUA TANU ILIUNDWA KUFANIKISHA KITU GANI TANGANYIKA. Kama hivyo ndivyo ulimaanisha, tafadhali nielimishe zaidi kwanini unafikiri hivyo ili na mimi nipate nafasi nzuri zaidi ya kujadili hoja yako;

HESHIMA KWAKO MKUU Mchambuzi,

Tukichora distribution curve ya vijana wa Tanzania against their age,bila shaka wengi wao wako katika miaka kati ya 18-30. Hawa watu wamezaliwa miaka ya kuanzia 1980 na kuendelea, yaani 1980,81,82......

Kimisingi wamekua na kukuta CCM ikitawala,na nchi tayari iko katika sintofaham ya ni itikadi ipi ya uchumi inayofuatwa na tifa husika,yan Yanzania.Hawa vijana wapo kichuuzi chuuzi tu.

Hawa vijana hawaichukulii uzito TANU ile iliyohubiriwa sana enzi zile,na hivyo ni wachache wanayoisoma,though they know baba wa Taifa kupitia hiyo TANu na vinginevyo walileta Uhuru na heshima kwa taifa letu.

Mkuu, Mchambuzi, hawa vijana hawana 'make up' (ya akili) kama waliyokuwa nayo wale wazee waliopo,kwa sababu ya mazingira waliyokulia, transformations wanazopitia na itikadi zinazowakuza. No wonder vijana hufurahia na kujionea ufahari pale wanapobadhiri fedha za uma,contrary na misingi ya TANU na ujamaa inavyosema.

Mchambuzi, hapo nilikua namaanisha vijana tulio nao, hao wanaoweza kuandamana pasi kujua lengo la maandamano hayo, vijana waliojaa ushabiki, vijana wanaotaka kuona kama nguvu zao zinaweza kubadili mizizi ya CCM na mafisadi wachache kuwa Tanzania mpya yenye neema kwao, vijana wanaotaka kuona mustakabali wao hauko tu kwenye makaratasi bali unatekelezwa kwa vitendo.

Sintasita kukwambia, CHANGE IS WHAT THEY NEED, hata CDM wangekuweka wewe, vijana wangekuchagua.... hatuhitaji siasa za kutulaghai kujua TANU na CCM vimefanya nini, tunataka kuona MABADILIKO.
 
majany

Nashukuru sana kwa mchango wako mkuu majany; nitakurudia baadae kidogo kwa kirefu ila kwa kuanzia ningependa kutamka mambo mawili:

Kwanza, TANU sio CCM, kwani TANU ilikufa na Tanganyika;

Pili, uelewa wa TANU ni muhimu sana kwa mafanikio ya chama chochote kile cha Siasa Tanzania, kukana hilo ni mwanzo wa kutofanikiwa kwa malengo yoyote yenye kulenga ukombozi wa nchi kwa nyanja yoyote ile au tabaka lolote lile ndani ya jamii; nitarudi kufafanua;
 
Last edited by a moderator:
Majany,

Tukichora distribution curve ya vijana wa Tanzania against their age,bila shaka wengi wao wako katika miaka kati ya 18-30.Hawa watu wamezaliwa miaka ya kuanzia 1980 na kuendelea,yaani 1980,81,82......;Kimisingi wamekua na kukuta CCM ikitawala,na nchi tayari iko katika sintofaham ya ni itikadi ipi ya uchumi inayofuatwa na tifa husika,yan Yanzania.Hawa vijana wapo kichuuzi chuuzi tu.

Upo sahihi kabisa na sasa naelewa msingi wa hoja yako. Ningependa kuongezea katika hili pia kwamba TANU SIO CCM; TANU na Malengo yake kwa taifa la Tanganyika huru ilikufa pamoja na Tanganyika mwaka 1977 pale CCM ilipozaliwa kutokana na ndoa baina ya TANU (kutoka upande wa Tanganyika) na Afro Shiraz Party (kutoka upande wa Zanzibar); Muungano baina ya nchi hizi mbili essentially ulikuwa ni muungano wa Vyama na mengine yangejengwa baada ya hapo, ujenzi ambao ulikwama na hadi sasa umekwama kutokana na mfumo mbovu wa muungano ambao ni kiini macho kama alivyotamka Lissu bungeni mwezi wa Sita, 2012; Muungano wa 1964 uliipiga TANU kichwani kwa silaha yenye ncha kali na kupelekea TANU kumbwa na hemorrhage (kuvuja kwa damu kwenye ubongo); kuanzia hapo TANU kikaenda kwenye ‘COMA' kwa miaka kumi na tatu, na hatimaye kufariki aidha kwa bahati mbaya au kwa makusudi mwaka 1977 ilipoundwa katiba mpya ya Tanzania iliyoipa CCM madaraka makubwa hata kuliko katiba ya nchi;

Ni katika kipindi hiki ndio tukaanza kuona nchi ikianza kukosa mwelekeo, na Mwalimu kuanza kulemewa katika kila nyanja kwani, pamoja na nia yakle nzuri, matokeo yake yakawa mabaya kwani CCM ilijitanua mno baada ya kushika hatamu na kuanza kutumia resources za umma kwa kasi kubwa kufanikisha malengo ya kisiasa kuliko yale yenye kulenga kuleta Maendeleo ya kiuchumi na kijamii; Yaliyokuja kujitokeza mwaka 1992 pale Azimio la Arusha lilipofutwa ndio ikawa ni mwisho wa TANU hata katika mazungumzo ya kisera za vitendo; Suala la sintofahamu na lile la vijana wengi wa leo kuwa kichuuzi chuuzi kwa kiasi kikubwa mizizi yake inatokana na masuala haya;

Hawa vijana hawaichukulii uzito TANU ile iliyohubiriwa sana enzi zile,na hivyo ni wachache wanayoisoma,though they know baba wa Taifa kupitia hiyo TANu na vinginevyo walileta Uhuru na heshima kwa taifa letu.

TANU ya wakati ule haikuwa TANU ya kuhubiri tu au TANU ya nadharia tu bali ilikuwa ni TANU ya vitendo, kupitia sera na principles mbalimbali in the context of a national vision ambayo ilieleweka wazi kwa kila mtanzania na kwa lugha nyepesi kueleweka hata kwa mwanafunzi wa darasa la saba; leo hii hatuna tena Dira, na badala yake kinachoendelea chini ya CCM ni Chauvism, Racism, udini and Ethnicity; hili ni timing bomb ambalo Nyerere alilionya dhidi ya CCM miaka michache kabla ya kufariki dunia;

Mkuu,Mtambuzi,hawa vijana hawana 'make up' (ya akili) kama waliyokuwa nayo wale wazee waliopo,kwa sababu ya mazingira waliyokulia,transformations wanazopitia na itikadi zinazowakuza.No wonder vijana hufurahia na kujionea ufahari pale wanapobadhiri fedha za uma,contrary na misingi ya TANU na ujamaa inavyosema.

Nakubaliana na wewe; muhimu pia hapa kuelewa ni kwamba, pamoja na mapungufu yake, Nyerere alitaifisha UCHUMI NA SIASA KWA MANUFAA YA WATANZANIA, huku viongozi waliomfuata walikuja KUTAIFISHA UCHUMI NA SIASA KWA MASLAHI YAO, FAMILIA ZAO NA WAPAMBE WAO, NA BADO VIJANA UNAOWAZUNGUMZIA WANAWAONA WANASIASA WA NAMNA HII KAMA HEROES;

Mtambuzi,hapo nilikua namaanisha vijana tulio nao,hao wanaoweza kuandamana pasi kujua lengo la maandamano hayo,vijana waliojaa ushabiki,vijana wanaotaka kuona kama nguvu zao zinaweza kubadili mizizi ya CCM na mafisadi wachache kuwa Tanzania mpya yenye neema kwao,vijana wanaotaka kuona mustakabali wao hauko tu kwenye makaratasi bali unatekelezwa kwa vitendo.

Enzi za TANU, vijana kwa wazee walikuwa na a common enemy ambae alikuwa ni mnyonyaji wa ndani na nje ya nchi; ni hili ndio lilipelekea vuguvugu la political movement miaka ya 1950s ambapo TANU ilizaliwa, na vijana kwa wazee kwa hiyari yao (sio kwa kulazimishwa) wakaamua kuiunga TANU mkono kwa wingi sasa ili kusaidia ifanikishe harakati za kuikomboa nchi kutokana kwenye utawala wa wanyonyaji; Kwa bahati mbaya CCM ikaja kuisaliti historia yan TANU; ndio maana leo hii vijana ambao ndio majority Tanzania wanashindwa tofautisha baina ya TANU na CCM; vijana hawa taratibu wanaanza kurudia historia ile ile ya kutaka mabadiliko (kama ilivyotokea chini ya TANU), kutokana na ukweli kwamba kumbe nafasi ya mkoloni ambae alikuwa ni mnyonyaji sasa imerithiwa na mtu mweusi ambae anaweka UFISADI mbele ya maslahi na matakwa ya UMMA; HAKI YA MUNGU aliyopewa mtanzania (rasilimali) imegeuzwa na watawala kuwa HAKI YA MZUNGU, huku Ufisadi ukifanikisha mradi huo;

Sintasita kukwambia,CHANGE IS WHAT THEY NEED, hata CDM wangekuweka wewe,vijana wangekuchagua....hatuhitaji siasa za kutulaghai kujua TANU na CCM vimefanya nini,tunataka kuona MABADILIKO.
Siasa au mjadala unao hoji TANU imefanya nini ni mtaji mkubwa wa kisiasa kwa CHADEMA kuliko CCM; nilishajadili hili elsewhere; Kwa maana nyingine, kufananisha TANU na Chadema ni mtaji wa kisiasa na ni ‘more of a political mileage' kwa Chadema kuliko CCM; Kumbuka tena, TANU ilikufa na Tanganyika, na TANU sio CCM; na CCM imeisaliti historia ya TANU;

Kinachonikwaza ni je, vijana hawa unaowazungumzia, kama kuna vitu vitatu ambavyo vinawafanya waamini kwamba CHADEMA ndio chaguo sahihi kuelekea ukombozi, sababu hizo tatu ni zipi? Nadhani pia you are in a position kuwajibia hilo;
 
Majany,



Upo sahihi kabisa na sasa naelewa msingi wa hoja yako. Ningependa kuongezea katika hili pia kwamba TANU SIO CCM; TANU na Malengo yake kwa taifa la Tanganyika huru ilikufa pamoja na Tanganyika mwaka 1977 pale CCM ilipozaliwa kutokana na ndoa baina ya TANU (kutoka upande wa Tanganyika) na Afro Shiraz Party (kutoka upande wa Zanzibar); Muungano baina ya nchi hizi mbili essentially ulikuwa ni muungano wa Vyama na mengine yangejengwa baada ya hapo, ujenzi ambao ulikwama na hadi sasa umekwama kutokana na mfumo mbovu wa muungano ambao ni kiini macho kama alivyotamka Lissu bungeni mwezi wa Sita, 2012; Muungano wa 1964 uliipiga TANU kichwani kwa silaha yenye ncha kali na kupelekea TANU kumbwa na hemorrhage (kuvuja kwa damu kwenye ubongo); kuanzia hapo TANU kikaenda kwenye ‘COMA' kwa miaka kumi na tatu, na hatimaye kufariki aidha kwa bahati mbaya au kwa makusudi mwaka 1977 ilipoundwa katiba mpya ya Tanzania iliyoipa CCM madaraka makubwa hata kuliko katiba ya nchi;

Ni katika kipindi hiki ndio tukaanza kuona nchi ikianza kukosa mwelekeo, na Mwalimu kuanza kulemewa katika kila nyanja kwani, pamoja na nia yakle nzuri, matokeo yake yakawa mabaya kwani CCM ilijitanua mno baada ya kushika hatamu na kuanza kutumia resources za umma kwa kasi kubwa kufanikisha malengo ya kisiasa kuliko yale yenye kulenga kuleta Maendeleo ya kiuchumi na kijamii; Yaliyokuja kujitokeza mwaka 1992 pale Azimio la Arusha lilipofutwa ndio ikawa ni mwisho wa TANU hata katika mazungumzo ya kisera za vitendo; Suala la sintofahamu na lile la vijana wengi wa leo kuwa kichuuzi chuuzi kwa kiasi kikubwa mizizi yake inatokana na masuala haya;



TANU ya wakati ule haikuwa TANU ya kuhubiri tu au TANU ya nadharia tu bali ilikuwa ni TANU ya vitendo, kupitia sera na principles mbalimbali in the context of a national vision ambayo ilieleweka wazi kwa kila mtanzania na kwa lugha nyepesi kueleweka hata kwa mwanafunzi wa darasa la saba; leo hii hatuna tena Dira, na badala yake kinachoendelea chini ya CCM ni Chauvism, Racism, udini and Ethnicity; hili ni timing bomb ambalo Nyerere alilionya dhidi ya CCM miaka michache kabla ya kufariki dunia;



Nakubaliana na wewe; muhimu pia hapa kuelewa ni kwamba, pamoja na mapungufu yake, Nyerere alitaifisha UCHUMI NA SIASA KWA MANUFAA YA WATANZANIA, huku viongozi waliomfuata walikuja KUTAIFISHA UCHUMI NA SIASA KWA MASLAHI YAO, FAMILIA ZAO NA WAPAMBE WAO, NA BADO VIJANA UNAOWAZUNGUMZIA WANAWAONA WANASIASA WA NAMNA HII KAMA HEROES;



Enzi za TANU, vijana kwa wazee walikuwa na a common enemy ambae alikuwa ni mnyonyaji wa ndani na nje ya nchi; ni hili ndio lilipelekea vuguvugu la political movement miaka ya 1950s ambapo TANU ilizaliwa, na vijana kwa wazee kwa hiyari yao (sio kwa kulazimishwa) wakaamua kuiunga TANU mkono kwa wingi sasa ili kusaidia ifanikishe harakati za kuikomboa nchi kutokana kwenye utawala wa wanyonyaji; Kwa bahati mbaya CCM ikaja kuisaliti historia yan TANU; ndio maana leo hii vijana ambao ndio majority Tanzania wanashindwa tofautisha baina ya TANU na CCM; vijana hawa taratibu wanaanza kurudia historia ile ile ya kutaka mabadiliko (kama ilivyotokea chini ya TANU), kutokana na ukweli kwamba kumbe nafasi ya mkoloni ambae alikuwa ni mnyonyaji sasa imerithiwa na mtu mweusi ambae anaweka UFISADI mbele ya maslahi na matakwa ya UMMA; HAKI YA MUNGU aliyopewa mtanzania (rasilimali) imegeuzwa na watawala kuwa HAKI YA MZUNGU, huku Ufisadi ukifanikisha mradi huo;


Siasa au mjadala unao hoji TANU imefanya nini ni mtaji mkubwa wa kisiasa kwa CHADEMA kuliko CCM; nilishajadili hili elsewhere; Kwa maana nyingine, kufananisha TANU na Chadema ni mtaji wa kisiasa na ni ‘more of a political mileage' kwa Chadema kuliko CCM; Kumbuka tena, TANU ilikufa na Tanganyika, na TANU sio CCM; na CCM imeisaliti historia ya TANU;

Kinachonikwaza ni je, vijana hawa unaowazungumzia, kama kuna vitu vitatu ambavyo vinawafanya waamini kwamba CHADEMA ndio chaguo sahihi kuelekea ukombozi, sababu hizo tatu ni zipi? Nadhani pia you are in a position kuwajibia hilo;

Ahsante sana mkuu Mchambuzi kwa kuzidi kunidadavulia kwa undani kabisa kuhusu hili tunalojadili....
Kabla sijakupa sababu naomba nirudi nyuma kidogo kwenye historia ya siasa na vyama vya siasa hapa nchine kwetu kwa kulinganisha na mwamko wa vijana,

Wakati tunaingia uchaguzi wa 1995,ambapo NCCR ilipokua imeshika hatamu kama chama mbadala ambacho vijana walianza kukiamini.Hiki chama kilifanikiwa saana kujileta karibu na wananchi,na ikapokewa kwa bashasha kubwa na vijana,nakiri kusema kwamba kukosekana kwa dira na mikakati kulifanya lile vuguvugu kufa.

Back in 2000,Ikaanza CUF ikaanza kushika hatamu,vijana pia walianza kuiona kama chama kitacholeta matumaini na mustakabali wao.Unajua kilichotokea...sihitaji kusema mengi.

Leo hii tunakiona CDM,chama ambacho kimeenda 'extra mile' kuliko vyote vilivyopita.Namaanisha kimeenda mbali zaidi ya vyama vyote nilivyovitaja.

Mkuu Mchambuzi,nimeamua kuandika hako ka historia(ingawaje hakako 'comprehensive sana) ili uone hii ari ya mabadiliko kwamba haikuanza leo wala jana,bali ilikosa kiongozi.

Mambo ambayo ninayaona ambayo yanasababisha hawa vijana kuamini CDM itawakomboa ni

i) Kukata tamaa(CCM haina matarajio yao,wanaona they better opt for the near solution available)
ii)Kukosekana na chama mbadala cha upinzani (apart from CDM) ambacho kina nguvu ya kuweza kuiondoa CCM madarakani na kuongoza dola,
iii)CDM wanaonekana kuwa na sera mbadala ambazo zina matarajio ya vijana wengi(though vijana wengi hawako informed,na hii ni challenge kwa CDM..

Mkuu Mchambuzi,kwa kifupi nimeweza kueleza kidogo kwenye huu mjadala wetu.
 
Ahsante sana mkuu Mchambuzi kwa kuzidi kunidadavulia kwa undani kabisa kuhusu hili tunalojadili....

Kabla sijakupa sababu naomba nirudi nyuma kidogo kwenye historia ya siasa na vyama vya siasa hapa nchine kwetu kwa kulinganisha na mwamko wa vijana,

Wakati tunaingia uchaguzi wa 1995,ambapo NCCR ilipokua imeshika hatamu kama chama mbadala ambacho vijana walianza kukiamini.Hiki chama kilifanikiwa saana kujileta karibu na wananchi,na ikapokewa kwa bashasha kubwa na vijana,nakiri kusema kwamba kukosekana kwa dira na mikakati kulifanya lile vuguvugu kufa.

Back in 2000,Ikaanza CUF ikaanza kushika hatamu,vijana pia walianza kuiona kama chama kitacholeta matumaini na mustakabali wao.Unajua kilichotokea...sihitaji kusema mengi.

Leo hii tunakiona CDM,chama ambacho kimeenda 'extra mile' kuliko vyote vilivyopita.Namaanisha kimeenda mbali zaidi ya vyama vyote nilivyovitaja.

Mkuu Mchambuzi,nimeamua kuandika hako ka historia(ingawaje hakako 'comprehensive sana) ili uone hii ari ya mabadiliko kwamba haikuanza leo wala jana,bali ilikosa kiongozi.

Mambo ambayo ninayaona ambayo yanasababisha hawa vijana kuamini CDM itawakomboa ni

i) Kukata tamaa(CCM haina matarajio yao,wanaona they better opt for the near solution available)
ii)Kukosekana na chama mbadala cha upinzani (apart from CDM) ambacho kina nguvu ya kuweza kuiondoa CCM madarakani na kuongoza dola,
iii)CDM wanaonekana kuwa na sera mbadala ambazo zina matarajio ya vijana wengi(though vijana wengi hawako informed,na hii ni challenge kwa CDM..

Mkuu Mchambuzi,kwa kifupi nimeweza kueleza kidogo kwenye huu mjadala wetu.

Well said Majany, nakubaliana na wewe katika yote hapo juu, na muhimu kuliko yote ni mawili: Kwanza, nimependa uliposema CUF ilishika hatamu; maana ya kushika hatamu ni chama kukubalika na wananchi na hivyo kuwa na mamlaka ya kufanya mambo au maamuzi mbalimbali kwa maslahi yao kama taifa; Hatamu haitokani na Chama kuwa na Power bali kuwa na authority, na source yake ni wananchi, sio silaha za moto au vitu kama hivyo; hatamu kwa sasa imehamia Chadema;

Suala la pili
ambalo naona ni muhimu pia katika hoja yako ni kuhusu changamoto walizonazo Chadema kwani kwa kweli upepo wote wa siasa upo in their favour, ni wao kujipanga na ku-manage vizuri such an opportunity, na kama ulivyoiweka vizuri, opportunity kama hii haiji mara mbili (rejea suala la NCCR miaka ya tisini wakati wa Lyatonga);
 
opportunity kama hii haiji mara mbili (rejea suala la NCCR miaka ya tisini wakati wa Lyatonga)

Well said Mchambuzi.....haswaaa hiki ndicho ninachomaanisha..ukiwa na vijana ambao hupelekwa na upepo,ambao hawako informed..ni rahisi sana kuwa 'swayed' na vyama ambavyo havitakua na tija kwa mtaji wa mabadiliko......

Umejibu vyema,na kama CDM wanaziona hizi changamoto,basi pasi nan shaka watachukua dola,kama hawazioni hizi changamoto pia,watakipata kilichowakuta NCCR na CUF...

Mungu ibariki Tanzania,Mungu uwaongoze vema CDM.....(I wish siku CCM ikianguka niwepo hai....don't get me wrong,it's just a WISH)
 
Mchambuzi,

Naomba nianze kwa kujadili hoja yako ya kwanza, Kwamba "CCM ndio kiongozi wa mageuzi nchini". Umeanza kwa kukumbushia matokeo ya Tume ya Nyalall, nadhani na wewe unafahamu hila zilizofanywa na chama cha Mapinduzi wakati wa utendaji kazi wa tume ile, tume iliandaliwa makada wa CCM ili kukusanya maoni yao, ndio maana ikaibuka na takwimu zile, hivyo sio sahihi kutumia takwimu zile bila kuweka angalizo, kudai kwamba watanzania hawakutaka vyama vingi bali CCM ndio iliyoruhusu kama zawadi vile, sababu naona hata kauli yako binafsi kwamba wanachofanya CHADEMA ni kama shukrani ya Punda ni mateke imejikita kwenye kukazia upotoshaji huo kwamba mfumo wa vyama vingi bila ridhaa ya CCM usingekuwapo.

Pili, CCM ilishindwa katika uchaguzi wa kwanza wa vyama vingi mwanga 1995, tena kote bara na zanzibar, dalili za kushindwa zilionekana kabla ya uchaguzi ndio maana Mwalimu aliingilia kati kuokoa chama chake, isingikuwa hivyo ni wazi asingeshiliki, uchaguzi wenyewe haukuwa huru na wenye haki kote bara na zanzibar, sitegemei mtu anayetoa maoni yake kama hasukumwi na msimamo wake wa kisiasa anaweza kuisifia ccm kwa kushinda uchaguzi ule bila kuweka angalizo la namna mchakato wa upigaji kura, uhesabuji na utangazaji ulivyogubikwa na sintofahamu kote bara na zanzibar, hivyo sio sahihi sana kusema ccm ilishinda katika uchaguzi wa kwanza wa vyama vingi nchini.

Vyama vingi ni asili yetu, sitaki kuliongelea hili sana, lakini natambua unajua kwamba vyama vingi vilikuwa nchi hii kabla hatujapata uhuru wa bendera mwaka 1961 na hata baada ya hapo kabla ya mwalimu kufanya mambo yake, Nadhani hii ingeweza kuwa sababu ya kutosha kabisa kukuzuia kuandika kwamba mfumo wa vyama vingi ni zawadi toka CCM.

Mwitikio wa wananchi, tuseme ulikuwa ni mdogo sana, sababu ya kwanza ni ukosefu wa elimu kwa watanzania, Je hili ni Jambo la kujivunia kisiasa? na inawezekana CCM ilishinda uchaguzi wa kwanza wa vyama vingi kihalali kabisa, lakini kama moja ya sababu ikiwa ni ukosefu wa elimu, hiki ni kitu cha kujivunia?

Inapofikia hatua wanasiasa wanatumia kigezo cha ukosefu wa ufahamu wa wananchi kujipigia chapuo za kisiasa inakuwa rahisi zaidi kusema siasa ni Dirty Game. Lakini ni wazi, siasa haipaswi na sio dirty game. Lakini ni dirty game hasa hapa kwetu na ndio maana tuko namna hii.

Katika hili labda kama unataka CHADEMA ijenge vyuo lakini nalazimika kuomba maelezo yako ya ziada, unategemea wafanye nini zaidi ya wanachokifanya sasa?
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Sangarara,

Asante sana kwa mchango wako. Naomba na mimi nichangia kama ifuatavyo:

naomba nianze kwa kujadili hoja yako ya kwanza, Kwamba "CCM ndio kiongozi wa mageuzi nchini". Umeanza kwa kukumbushia matokeo ya Tume ya Nyalall, nadhani na wewe unafahamu hila zilizofanywa na chama cha Mapinduzi wakati wa utendaji kazi wa tume ile, tume iliandaliwa makada wa ccm ili kukusanya maoni yao, ndio maana ikaibuka na takwimu zile, hivyo sio sahihi kutumia takwimu zile bila kuweka angalizo,kudai kwamba watanzania hawakutaka vyama vingi bali CCM ndio iliyoruhusu kama zawadi vile, sababu naona hata kauli yako binafsi kwamba wanachofanya CHADEMA ni kama shukrani ya Punda ni mateke imejikita kwenye kukazia upotoshaji huo kwamba mfumo wa vyama vingi bila ridhaa ya CCM usingekuwapo.

Sidhani kama kimsingi tunatofautiana sana na hoja yako kwani kama ulinisoma vizuri, nilichoeleza katika hili ni kwamba: ni dhahiri kwamba suala la vyama vingi lilikuwa haliepukiki lakini MKAKATI (STRATEGY) YA CCM wa kuhakikisha mageuzi ya kisiasa hayatokani na nguvu ya umma bali CCM na serikali yake imekijenga sana chama miongoni mwa wananchi; pia niliwahi kujadili kwamba CCM owned the political reform process kupitia tume ya nyalali, na ikajiwekea muda wa kutosha kujianga kabla ya uchaguzi mkuu wa kwanza wa vyama vingi tofauti na nchi nyingine karibia zote za dunia ya tatu ambapo suala la vyama vingi kwanza lilitokana na nguvu ya umma kutaka mabadiliko,lakini pili, chaguzi kuu za kwanza za vyama vingi zilikuja muda mfupi sana baada ya mabadiliko ya kisiasa na hivyo kupelekea vyama vingi tawala kuporomoka kwani havikujiandaa; Kwa CCM, imshukuru Nyerere kwa kulipanga hili vizuri kipindi kile;

Pili, CCM ilishindwa katika uchaguzi wa kwanza wa vyama vingi mwanga 1995, tena kote bara na zanzibar, dalili za kushindwa zilionekana kabla ya uchaguzi ndio maana Mwalimu aliingilia kati kuokoa chama chake, isingikuwa hivyo ni wazi asingeshiliki, uchaguzi wenyewe haukuwa huru na wenye haki kote bara na zanzibar, sitegemei mtu anayetoa maoni yake kama hasukumwi na msimamo wake wa kisiasa anaweza kuisifia ccm kwa kushinda uchaguzi ule bila kuweka angalizo la namna mchakato wa upigaji kura, uhesabuji na utangazaji ulivyogubikwa na sintofahamu kote bara na zanzibar, hivyo sio sahihi sana kusema ccm ilishinda katika uchaguzi wa kwanza wa vyama vingi nchini.

Sikubaliana na wewe kuhusu CCM kushindwa uchaguzi mkuu wa 1995 bara bali ningependa kuamini kwamba CCM ilishindwa Zanzibar; Kwa bara, ni Mwalimu ndiye aliyesaidia CCM ishinde kwa kumtembeza mgombea wa CCM nchi nzima huku akiaminisha UMMA kwamba Mrema hakuwa chaguo sahih, na bila ya juhudu hizi za Mwalimu, Mrema angeweza kabisa kuwa Rais;

Vyama vingi ni asili yetu, sitaki kuliongelea hili sana, lakini natambua unajua kwamba vyama vingi vilikuwa nchi hii kabla hatujapata uhuru wa bendera mwaka 1961 na hata baada ya hapo kabla ya mwalimu kufanya mambo yake, Nadhani hii ingeweza kuwa sababu ya kutosha kabisa kukuzuia kuandika kwamba mfumo wa vyama vingi ni zawadi toka ccm.

Upo sahihi kuhusu vyama vingi kuwepo Tanganyika kabla ya uhuru, hasa among the Chaggas ambao walikuwa na mfumo wa namna hiyo kwa muda mrefu tu; kwa mfano, Kilimanjaro Chagga Citizens Union (KCCU) mwaka 1949 na vingine kadhaa;
Mwitikio wa wananchi, tuseme ulikuwa ni mdogo sana, sababu ya kwanza ni ukosefu wa elimu kwa watanzania, Je hili ni Jambo la kujivunia kisiasa? na inawezekana ccm ilishinda uchaguzi wa kwanza wa vyama vingi kihalali kabisa, lakini kama moja ya sababu ikiwa ni ukosefu wa elimu, hiki ni kitu cha kujivunia?

Jibu ni hapana, hili sio suala la kujivunia hata kidogo; lakini kidogo umenichanganya hapa kwani sasa unaonyesha kuegemea upande wa hoja kwamba inawezekana CCM ilishinda uchaguzi wa 1995 kihalali, wakati hapo awali ulisema kwamba CCM ilianguka katika uchaguzi mkuu wa kwanza wa vyama vingi 1995 kote BARA na VISIWANI;

Inapofikia hatua wanasiasa wanatumia kigezo cha ukosefu wa ufahamu wa wananchi kujipigia chapuo za kisiasa inakuwa rahisi zaidi kusema siasa ni Dirty Game. Lakini ni wazi, siasa haipaswi na sio dirty game. Lakini ni dirty game hasa hapa kwetu na ndio maana tuko namna hii.

Binafsi sidhani kama politics is a dirty game but instead, PLAYERS IN THE GAME NDIO DIRTY; it's a game that consists of players who are LIARS, CORRUPT, BETRAYERS, AND EVEN MURDERERS;

Katika hili labda kama unataka CHADEMA ijenge vyuo lakini nalazimika kuomba maelezo yako ya ziada, unategemea wafanye nini zaidi ya wanachokifanya sasa?
Chadema imejitahidi sana, credit has to be given where its due, lakini chama hiki need to transform from being a party led by PERSONALITIES and become chama led by an ALTERNATIVE VISION for the nation ambayo Tanzanians will buy it for so many years to come, whether Chadema wins 2015 or not; ndio maana watu kama mzee sitta wanaishia kuishambulia chadema kwamba haina hazina ya uongozi kwasababu sasa kipimo cha chama bora kinageuzwa kuwa hazina ya viongozi, na cha kusikitisha, Chadema haikuja na majibu mazuri juu ya hili la uhaba wa viongozi na badala yake Dr. Slaa akajikita zaidi kuelezea kwamba Sitta ilikuwa aende Chadema meaning kuongezea hazina ya uongozi; ndio maana wapo viongozi wengi ndani ya CCM ambao wana hamu ya kuhamia chadema lakini kwa vile kipimo ni wingi wa personalities, wanasubiriana, wakati iwapo Chadema ingekuwa na nguvu kutokana na kuwa na alternatiev vision ya taifa ambayo imeota mizizi mijini hadi vijijini, hata kama Dr. Slaa angekuwa yupoe peke yake, bado viongozi wengi wangevutiwa kujiunga na Chadema kwani hiyo ingekuwa ni nguvu ya umma ya kudumu;

Hazina ya chama chochote cha siasa ni umma behind it, na hii inakuwa na nguvu zaidi iwapo umma unaona kuna alternative vision; tumeona ya NCCR na Mrema 1995, bado Chadema haipo tofauti sana na NCCR ya 1995; nina andaa makala on this and soon I'll share…
 
Mchambuzi,

Nashukuru kwa maelezo yako ya ziada kwenye mchango wangu kwa hoja yako ya kwanza, bado kuna mengi sana ya kujadiri katika hilo hasa katika msingi wa kufunguka zaidi, na kabla sijaenda mbali, naomba nikudokeze kwamba nimefika kwenye post hii baada ya kuelekezwa na mtu anaitwa pasco, ndio maana kama ambavyo naamini utakuwa umekwishang'amua approach yangu imekuwa too defensive, lakini kimsingi nimegundua Pasco anaitumia post yako kupotosha watu hapa ndani kwa kiwango kikubwa sana. tuyaache haya.

Umesema nimekuchanganya juu ya kushinda au kushindwa kwa ccm kwenye uchaguzi wa kwanza wa vyama vingi, msimamo wangu ni ule ule, ccm ilishindwa na kama ilishinda basi ilipata nafuu ya kura za mambumbumbu. Na hapa ieleweke kwamba simtukani mtu, mama yangu mzazi ni mmoja ya walioipigia kura ccm mwaka 1995, akawapigia tena 2000, na 2005, 2010 akawatosa. Hata yeye namtambulisha kama alikuwa anafanya maamuzi ya kimbumbumbu. Kama huu ulikuwa ni ushindi wa kujivunia basi nayo ni sababu ya kuikataa CCM zaidi na zaidi.

Nikirudi kwenye hoja ya msingi:

Umiliki na udhibiti wa vyombo vya habari. Naunga mkono hoja.

Uchumi mkubwa wa CCM, naunga mkono hoja.

Ujamaa bado ni relevant, hapa ninacho cha kuelezea.

Mchambuzi, mtoto wako akililia wembe utampa? Nategemea jibu lako litakuwa ni hapana. Wakati wa Kampeni za uchaguzi mkuu mwaka 2010, Ndugu Kikwete alifikia hatua ya kusema, "Ujamaa umepitwa na wakati" akashambuliwa sana na vyombo vya habari pamoja na wapiga kura. uzuri ni kwamba,kama ulivyoonyesha, wengi walimzodoa kwa kumuuliza mbona mnaendelea kujitambulisha kama mnasimamia uchumi wa nchi yetu katika misingi ya ujamaa?.

Nampinga Kikwete, lakini katika hili alikuwa sahihi, japo najua akiambiwa aeleze alikuwa anamaanisha nini anaweza akaja na maelezo tata zaidi, lakini maelezo sahihi (my opinion) ni kwamba, swala la ujamaa kupitwa na wakati ni FACT. mchakato wowote wa kuturudisha kwenye ujamaa ni kuturudisha nyuma, Na hakuna ushahidi wa kihistoria unaonyesha kwamba kuna wakati wowote ule, Jamii au Taifa lolote lile limewahi kufikia maendeleo makubwa yaliyopelekea kuwa na watu wenye furaha kwa utoshelevu walionao kupitia mfumo wa ujamaa. Mfumo wa ujamaa utaendelea kuwa wazo zuri sana ambalo haliwezekani kutekelezeka. Ujamaa kwa maana yake halisi ni sawa na ndoto.

Labda kama sijaelewa unamaanisha nini unaposema itikadi mbadala , tena itikadi itakayokidhi matakwa ya masikini wa kitanzania, to me its obvious, unamaanisha CHADEMA waanze kuimba ujamaa, sababu masikini wote wanautaka ujamaa, wote. Ujamaa ni uongo mkubwa kama ulivyo uongo wa kufuta umasikini.

Sasa Basi, kama ni kweli kabisa CHADEMA wanalazimika kwa mfano, kuupigia chapuo mfumo wa ujamaa eti kwa sababu wananchi wengi ama wameumiss sana, au wanaupenda sana kwa mategemeo kwamba watakuwa wameipiga bao ccm au kwenda nayo at pa. na mimi ntajitoa akili. ntawapigia kura ccm. Liwalo na liwe.
 
Sangarara,

Kwa mara nyingine tena, nashukuru kwa mchango wako na ningependa kujujibu kama ifuatavyo:

Nashukuru kwa maelezo yako ya ziada kwenye mchango wangu kwa hoja yako ya kwanza, bado kuna mengi sana ya kujadiri katika hilo hasa katika msingi wa kufunguka zaidi, na kabla sijaenda mbali, naomba nikudokeze kwamba nimefika kwenye post hii baada ya kuelekezwa na mtu anaitwa pasco, ndio maana kama ambavyo naamini utakuwa umekwishang'amua approach yangu imekuwa too defensive, lakini kimsingi nimegundua Pasco anaitumia post yako kupotosha watu hapa ndani kwa kiwango kikubwa sana. tuyaache haya.

Nashukuru kwa kunifahamisha hili; kwa uelewa wangu, Pasco yeye tayari inaelekea ana wagombea wake, na hoja zake nyingi huwa zinapima nguvu ya wagombea wake watatu ambao ni Lowassa kwa CCM, Zitto kwa Chadema na Jusa kwa CUF; vile vile hudai kwamba yeye sio mwanachama wa chama chochote cha siasa, Kwahiyo inakuwa vigumu kuelewa ananitumiaje kwani ni dhahiri yeye sio shabiki wa chama chochote bali ni WATU mbalimbali waliopo katika vyama vikuu vitatu, na hana interest sana kudadisi watu hawa watasimamia MASUALA gani wakati ukweli uliopo ni kwamba ushindi wa mgombea yoyote utatokana na WATU kupigia kura WATU wanaoamini watatosha katika nafasi hii ya juu kabisa ya uongozi wa taifa letu 2015;

Ni kutokana na ukweli huu, hasa wa watanzania kuzidi kuelimika juu ya ujinga wa kuchagua vyama au viongozi kwa MAZOEA, ndio maana nadhani watanzania wengi kwa sasa wanaendelea kujikita zaidi kupambanua kwa kina MASUALA ambayo yatakuwa muhimu kama vigezo vya kuchagua kiongozi atakae wafaa katika uchagauzi wa 2015; all that said and done, kama ulivyosema tuachane na hayo, lakini ukipata muda, naomba usome moja ya exchanges zangu na Pasco, hasa post number 233 na post number 235 kwenye link ifuatayo: https://www.jamiiforums.com/tanzani...ssa-then-2015-ni-ccm-tena-12.html#post4633031

Umesema nimekuchanganya juu ya kushinda au kushindwa kwa ccm kwenye uchaguzi wa kwanza wa vyama vingi, msimamo wangu ni ule ule, ccm ilishindwa na kama ilishinda basi ilipata nafuu ya kura za mambumbumbu. Na hapa ieleweke kwamba simtukani mtu, mama yangu mzazi ni mmoja ya walioipigia kura ccm mwaka 1995, akawapigia tena 2000, na 2005, 2010 akawatosa. Hata yeye namtambulisha kama alikuwa anafanya maamuzi ya kimbumbumbu. Kama huu ulikuwa ni ushindi wa kujivunia basi nayo ni sababu ya kuikataa CCM zaidi na zaidi.

Sishangai hoja yako kwamba kura za CCM mwaka 1995 zilikuwa ni kura za mambumbumbu na sidhani kama kutumia neno hil ni tusi; Mtu mbumbumbu ni mtu mjinga au zuzu, na hata Mwalimu katika moja ya hotuba zake alisema wazi kwamba kumwita mtu mjinga sio ajabu, na kwamba ni tofauti na kumuita mtu mpumbavu; Moja ya maadui watatu wa Maendeleo baada ya uhuru na hadi leo miaka hamsini baada ya uhuru ni umaskini, maradhi na UJINGA au UMBUMBUMBE au UZUZU;

Katika Tanzania ya leo, kumejaa watanzania ambao ni mbumbumbu wa SIASA, lakini pengine CCM kushinda kwa asimilia chache zaidi mwaka 2010 kulichangiwa kwa kupungua kwa umbumbumbu huo, kwani haingii akilini kwa watanzania kuwa maskini kwa miaka 50 halafu wachague chama kile kile kwa miaka 50 kwa asilimia 80; huu ni umbumbumbu, ujuha na uzuzu;

Kama CCM kushinda chaguzi kihalali, ni sawa iendelee kushinda lakini kwa asilimia ndogo kwani hiyo ni ishara ya demokrasia kukomaa, kwa mfano kama inavyotokeaga nchini marekani, UK n.k ambapo ushindi wa chama ngazi ya Urais haizidi 52%; huo ndio ushindi wa kujivunia kwa CCM kwani ni ishara kwamba UMBUMBUMBU unaisha lakini bado chama kinapendwa, lakini kupita kura kwa 80% na kushangilia, huu ni umbumbumu hata kwa viongozi wenyewe kwani ina maana wamechaguliwa na MAMBUMBUMBU na sio WAELEWA; ni muhimu CCM ianze kuukimbia ushindi Chama unaopenda kuuita ‘USHINDI WA MANYOYA", kama ukoma kwani HAKIKA, hakitafika mbali kwa mwendo huu, kitajimaliza chenyewe kwa UMBUMBUMBU!

Ujamaa bado ni relevant, hapa ninacho cha kuelezea. Mchambuzi, mtoto wako akililia wembe utampa? Nategemea jibu lako litakuwa ni hapana. Wakati wa Kampeni za uchaguzi mkuu mwaka 2010, Ndugu Kikwete alifikia hatua ya kusema, "Ujamaa umepitwa na wakati" akashambuliwa sana na vyombo vya habari pamoja na wapiga kura. uzuri ni kwamba,kama ulivyoonyesha, wengi walimzodoa kwa kumuuliza mbona mnaendelea kujitambulisha kama mnasimamia uchumi wa nchi yetu katika misingi ya ujamaa?.

Jibu kuhusu mtoto na wembe ni HAPANA pasipo shaka; Kwa kweli pamoja na mimi kuwepo kwenye zile kampeni za CCM 2010 kwa bahati mbaya nilipitwa na kauli hiyo kwamba Ujamaa Umepitwa na Wakati; Ni sahihi kwamba Katiba ya Chama bado inashikilia itikadi ile ile ya Ujamaa na Kujitegemea; Hata katiba ya nchi leo hii inasema taifa letu ni la Ujamaa na Kujitegemea; Hivi tunaelewa madhara ya kiongozi wa nchi kwenda kinyume na Katiba ni yepi? Kwa nchi zilizokomaa kidemokrasia, this would have been a disaster to the party and the candidate; Nisingependa kuamini kwamba Kikwete alitamka maneno hayo, lakini kama alitamka, basi hoja yako kwamba hili ni Taifa la Mbumbumbe (or rather wanaopigia kura CCM ni mbumbumu ina mashiko);

Iwapo wananchi wailipokea kauli hii kwamba Ujamaa umepitwa na wakati huku hata mchakato wa katiba mpya ulikuwa haujakubalika na chama tawala, kiongozi kupita kwenye kampeni na kusema Ujamaa umepitwa na wakati and get away with it ni nini kama sio umbumbumbe wa wananchi? naomba nirudie tena siamini bado kama Kikwete alitamka maneno haya; Vinginevyo kwa mujibu wa katiba yetu ya nchi, sehemu ya mwanzo kabisa ya katiba ya nchi ya mbumbumbu inasema hivi:

UTANGULIZI: SURA YA KWANZA: JAMHURI YA MUUNGANO, VYAMA VYA SIASA, WATU NA SIASA YA UJAMAA NA KUJITEGEMEA.

Nampinga Kikwete, lakini katika hili alikuwa sahihi, japo najua akiambiwa aeleze alikuwa anamaanisha nini anaweza akaja na maelezo tata zaidi, lakini maelezo sahihi (my opinion) ni kwamba, swala la ujamaa kupitwa na wakati ni FACT. mchakato wowote wa kuturudisha kwenye ujamaa ni kuturudisha nyuma, Na hakuna ushahidi wa kihistoria unaonyesha kwamba kuna wakati wowote ule, Jamii au Taifa lolote lile limewahi kufikia maendeleo makubwa yaliyopelekea kuwa na watu wenye furaha kwa utoshelevu walionao kupitia mfumo wa ujamaa. Mfumo wa ujamaa utaendelea kuwa wazo zuri sana ambalo haliwezekani kutekelezeka. Ujamaa kwa maana yake halisi ni sawa na ndoto.

Again iwapo Kikwete alitamka hivyo, basi kwa hili tupo pamoja;

Labda kama sijaelewa unamaanisha nini unaposema itikadi mbadala , tena itikadi itakayokidhi matakwa ya masikini wa kitanzania, to me its obvious, unamaanisha CHADEMA waanze kuimba ujamaa, sababu masikini wote wanautaka ujamaa, wote. Ujamaa ni uongo mkubwa kama ulivyo uongo wa kufuta umasikini.

Hapa naomba nitofautiane kidogo na wewe kama ifuatavyo: Tanzania ilikuwa chini ya Ujamaa kwa miaka "18" i.e. 1967 – 1985, na katika kipindi hiki, on average and in real terms, an average Tanzanian (wa kijijini) alisonga mbele kimaendeleo kuliko leo, kabla ya ile crisis ku-kick in at the end of 1970s; baada ya hapo, Ujamaa ukapigwa sana vita kwamba ndio sababu ya umaskini n.k, na badala yake soko huria likaingizwa na tumekuwa nalo kwa miaka "27" i.e. 1985 – 2012, lakini bado an average Tanzanian yule yule wa kijijini hali yake haijabadilika chini ya soko huria linaloungwa mkono na Chadema, yet M4C katika mwaka wa 27 wa soko huria inaonekana ni mkombozi; Iwapo nitamwita mtanzania huyu ambae kwa miaka 18 chini ya UJAMAA ni fukara, na miaka 27 ya Soko Huru bado maskini, kwamba pia ni mbumbumbu iwapo ataamini M4C ni mkombozi bila ya Chadema kufanya mabadiliko ya kidira na ki-itikadi, Je, utaona natenda haki au sio haki?

Mwalimu Nyerere miaka michache kabla hajafariki alialikwa na uongozi wa World Bank kule Washington na walimpa nafasi atoe hotuba kwa wafanyakazi wote wa taasisi hii; alisema kwamba kama angepata nafasi tena ya kuongoza nchi, angerudia karibia yale yale yale; the outcome ni kwamba alipigiwa makofi mengi sana mle ukumbini na kuambiwa na viongozi wale kwamba mengi aliyoyahimiza bado ni relevant ni kwamba tu circumstances have changed;

The bottom line hapa ni kwamba – hatuna haja ya kurudi kwenye Ujamaa lakini kuna mengi mazuri chini ya Ujamaa ambayo tunaweza kuyachukua, na hata hao wahisani waliotulazimisha serikali ijitoe katika kutoa huduma za kijamii, katika kuendesha uchumi , polepole wameanza to retract na kuhimiza umuhimu wa public sector katika afya, elimu n.k; vile vile wamebariki serikali kurudi katika kuendesha uchumi lakini kwa ujanja ujanja wa regulating the economy kupitia regulatory agencies mbalimbali kama vile EWURA, TCRA, SSRA, n.k;

Chadema iwapo wataingia madarakani 2015 kwa mwendo huu huu wa soko huria na kwa mwendo huu huu wa kukemea ufisadi bila ya kuwa na itikadi na dira mbadala yenye mashiko ya kweli kwa wananchi walio wengi, tukiwa wazima nitakukumbusha tena jinsi gani CCM au chama kingine kitakavyokuwa kinakamata kasi ya kuitoa Chadema madarakani 2020 kwani wananchi wataichoka Chadema haraka sana na hii itakuwa ni kwasababu za uzembe wa Chadema kwani hawawapi wananchi programu yao ya muda mfupi, muda wa kati na muda mrefu, badala yake wanahimiza mabadiliko ambayo hakika hawataweza kuyaleta ndani ya kipindi kifupi, hata kipindi cha muda wa kati; Chadema wajipange kwa hili mapema, vinginevyo as it stands, wanachotekeleza CCM kwa miaka 27 ni kile kile ambacho Mzee Mtei alitaka Serikali ikitekeleze baada ya kutofautiana na Mwalimu in early 1980s, na ni same policies Chadema itatekeleza 2015, na ndio maana wahisani hawajali who goes to the the State House kwani nje ya instability and chaos, mengine yote wana uhakika yatabakia intact, at their advantage i.e. foreign capital in mining, gas, oil, itafanya kazi iliyokusudiwa ambayo ni plundering our economies through unequal exchange, capital flight n.k.

Ni dira na itikadi mbadala pekee ya kuleta a WIN-WIN situation kati ya foreign capital ambayo tunahitaji sana lakini pia uplift ya majority ya watanzania ambao ni over 30 million vijijini, ndio chadema wanahitaji kuiuza kwa watanzania; Vision na Itikadi ambayo itakubali uwepo wa Soko Huria lakini pia itaweza kulikemea Soko Huria na kulirekebisha kwa vitendo kwa manufaa ya watanzania walio wengi; this would be close to a welfare state au zaidi itikadi na vision inayojikita zaidi katika social democracy;

Sasa Basi, kama ni kweli kabisa CHADEMA wanalazimika kwa mfano, kuupigia chapuo mfumo wa ujamaa eti kwa sababu wananchi wengi ama wameumiss sana, au wanaupenda sana kwa mategemeo kwamba watakuwa wameipiga bao ccm au kwenda nayo at pa. na mimi ntajitoa akili. ntawapigia kura ccm. Liwalo na liwe.

Natumaini baada ya maelezo yangu hapo juu, majibu ya hoja yako hii yapo wazi;
 
Mchambuzi,

Naendelea kukushukuru kwa ufafanuzi wa hali ya juu unaoendelea kuutoa, nimesoma na kutafakari maelezo yako kwa kina na nimeridhika kwamba yanafaa kwa matumizi. Nilikuwa nimedhamiria kuendelea kuchangia hoja zako zingine lakini katika kutafuta hoja ambayo ninaweza kuichangia haraka haraka bila kutumia muda mwingi wa kutafuta nini cha kuandika hapa nimegundua nalazimika kuendea na mjadala wa relevance ya ujamaa na umuhimu wa wapiga kura wa vijijini katika uchaguzi wa 2015.

Katika maelezo yako kwenye hoja namba saba, umerudia tena kusema.
"Nne, Upinzani dhidi ya Itikadi ya CCM, lakini bila ya kutoa dira na itikadi mbadala iliyo practical – Chadema wamekuwa wanapinga sera nyingi za CCM bila ya kutoa itikadi na dira mbadala kwa Ujamaa; mpaka sasa hawana itikadi yenye kusisimua na kuvutia wananchi walio wengi (vijijini) – [rejea mjadala wangu wa awali kuhusu relevance ya Ujamaa katika vijiji vya leo Tanzania]."
Hii imenifanya nione kwamba hauna mashaka na unachokizungumzia hapa, na mimi nawajibika kutaka maelezo ya ziada kwa mara nyingine tena.

Baada ya kukubaliana katika maswala mawili kwamba, Mtoto akililia wembe asipewe na kwamba kura za mambumbu hazina tija na sio busara kushangilia ushindi wa kura hizo. nadhani ni wakati muafaka tukakubaliana kuwa mikakati ya kupata usharwishi kwa watu wa vijijini na baadhi ya masikini wa mjini inapaswa kuwa tofauti na ile ya kupata ushawishi mijini.

Watanzania walio vijijini wanamatatizo makubwa mawili, kwanza hawana elimu yoyote ile, na pili ni masikini, Watanzania hawa wanachotaka kusikia ni sera za ujamaa, na sera za welfare economy kama ulivyotanabaisha ambazo kimsingi nakubaliana nazo asilimia mia moja.Kwa kipindi cha miaka hamsini watu hawa wamekuwa wakifundishwa na wanasiasa wetu wakati wa kampeni, kwamba serikali itawaletea maendeleo, na sasa wanachokijua na wanachotaka kukisikia kutoka kwa wanasiasa ni kwamba, wao wanasiasa watawafanyia nini, na wanarespond vizuri kwa wanasiasa wanaosema huku wanafanya na vitendo vyenye kubeba ishara ya utayari wa kutimiza ahadi zao, kwa mfano, wakiishaambiwa kwamba watajengewa barabara,hospitali,shule,madaraja,kupewa bei nzuri kwa mazao yao, kisha immedietly, wanapewa na kanga,kofia,t-shirts na shilingi elfu mbili mbili baada ya kula pilau na wao immediely wanafanya maamuzi ya kumchagua mtu huyo.
Mchambuzi, watu wetu wanataka kuwasikia wanasiasa wanaowaahidi vitu, hao ccm wenyewe mnaosema wana sera nzuri huwa sielewi mnatumia benchmarks gani kusema sera fulani ni nzuri, ukiangalia ilani ya uchaguzi ya ccm, kama nilivyokuwa nikisikia inasomwa na wagombea wao imejaa ahadi za vitu, na wanaofanya hivi wanafanya wakijua kwamba watu hawa wanaelewa na kurespond vizuri kwenye ahadi za vitu kuliko mambo ya msingi, Huku ni kumpa mtoto wembe.

Well, CHADEMA wanapigia kelele ufisadi, naomba utafakari vizuri kisha utazame kama ni sahihi sana kusema ufisadi ni swala la mpito alafu tujadiri kama Mapambano dhidi ya ufisadi sio sera mbadala, By the way ni kweli kelele za vita dhidi ya ufisadi hazijapelekea wananchi wa vijijini kurespond vizuri kwa CHADEMA?

Wakati ndio kwanza nchi hii inaanza kutambaa, Mwalimu nyerere alianza kutufunza kukabiriana na rushwa, ikawekwa na kwenye maandiko ya TANU kama sikosei pamoja na CCM. kwamba RUSHWA NI ADUI WA HAKI.Na yeye Binafsi akawa msitari wa mbele kupambana na Rushwa. Mwalimu huyo huyo nyakati za mwisho za uhai wake aliendelea kupigia kelele vitu vile vile tena in the end, katika namna ya kulalamika, Hata alipofikia hatua ya kusema CCM sio mama yake alikuwa kwenye muendelezo wa kulalamika kwamba Chama hiki kimechukua wrong direction, kwanza kimeua azimio la Arusha, pili kinanuka rushwa, na rushwa imepelekea serikali yake kushindwa kukusanya kodi nk nk nk.

Labda kama tunafikiria kwamba mapambano dhidi ya ufisadi ni mkakati wa kuwashughulikia mafisadi 10 wa mwembe Yanga. Lakini impact ya kupambana na ufisadi kwa dhati kabisa kabisa ni kubwa na yenye uwezo wa kuumua maendeleo ya Taifa letu kwa kasi na kwa muda mrefu zaidi ya hata asilimia 80% ya mirahaba kutoka kwenye hifadhi ya dhahabu chini ya ardhi yetu. Ufisadi unakwamisha mambo mengi sana katika Taifa letu in every aspect of our lives. Lakini leo Mchambuzi unatuambia mikakati ya kupambana na ufisadi ni jambo la mpito. Ufisadi is as old as both Poverty,Diseases,Illitrate,wars,Governments,Ujamaa, Ubepari,Christianity,Islamic,Budhaism, and even the mankind.

Nadhani ni wakati muafaka badala ya kuwalazimisha CHADEMA kuhubiri mambo wasiyoyajua au wanayotaka kuyasikia wapiga kura katika namna ya kumpatia mtoto wembe anaoulilia tuiunge mkono na tuisaidie kuelezea kwa ubunifu na uhalisia zaidi umuhimu wa Mapambano dhidi ya Ufisadi katika Taifa letu. HII NDIO SERA MBADALA WA POROJO ZA CCM.
Mchambuzi, ngoja nikudokeze kitu. Ikiwezekana, mambumbu wangenyimwa haki ya kupiga kura.
 
Last edited by a moderator:
Mchambuzi,

Sasa najielekeza kwenye hoja yako namba 7

Political Strategic Coherence and Consistency of CHADEMA. Kama nimeiweka kwa kiingereza sahihi. Unasema:

"Kwanza, Upinzani wenye utiifu na uaminifu kwa CCM – kuna nyakati viongozi wa Chadema huwa wanahubiri sera mbadala wa CCM huku wakiendelea kukitambua CCM kama ni chama halali chenye kuendesha serikali halali.

· Pili, Upinzani wa kuasi – Mara nyingine Chadema huonyesha umma kwamba chama kimejenga disloyalty na utawala wa CCM, lakini unakuta sio viongozi wote wanaoshikamana katika misimamo kama hii. Kwa mfano mwaka 2010 wabunge wa chadema walipotoka bungeni kukacha hotuba ya Rais Kikwete kufungua bunge, Zitto hakushiriki.

· Tatu, Upinzani dhidi ya muundo wa kisiasa (hasa katiba ya nchi) – Chadema wamekuwa wanapinga vipengele vingi vya katiba ya sasa, hasa vinavyohusiana na mapungufu ya current political system (mfano suala la muungano n.k), huku wakiendelea kuitambua serikali iliyopo madarakani kwamba ni halali kwa mujibu wa katiba ya nchi iliyopo sasa."
Ninaomba maelezo yako ya ziada kujustify kwamba, Kauli na misimamo binafsi ya viongozi wa CHADEMA inaweza kutumika kama kigezo cha kujustify kwamba Chama hakiko coherent and consistent katika mambo yake. Kwa bahati mbaya sana umemtaja ZITTO.

Kauli na misimamo binafsi ya viongozi wa Chama hasa wanapokuwa katika personal platforms ni vitu vya kuangalia kwa makini zaidi, Japo nakubali kwamba ni Tatizo, lakini sitegemei liwe ni lile linaloweza kukisambaratisha chama chochote kile, ama sivyo hicho sio chama tena bali genge fulani hivi la kihuni. ama sivyo tutakuwa tunataka kuua democrasia na uhuru binafsi wa watu. Mimi nadhani ni sahihi kusema kwamba mwanasiasa ambaye anakuwa hayuko coherent na political strategies za chama chake ndio anamatatizo badala ya chama chake.

Mchukulie mtu kama shibuda na kauli zake tata, hakuna mtu atakayekuelewa ukisema uongozi wa chadema umeparanganyika kutokana na kauli za shibuda, tena hata baada ya mwenyekiti kuaddress matamko yake once and strongly. Ukicompare CCM na CDM kama umbumbumbu wa wanasiasa wake kutokuthamini umuhimu wa kuwa coherent and consistent ni wazi utaona ccm walivyo na hali tete.

Mimi nadhani CHADEMA wamekuwa consistent for quite a long time now. UFISADI UFISADI UFISADI, Nadhani wana dhamira ya dhati kupambana na huu uchafu, na wako coherent as much kwa kuwa na viongozi ambao hawajachafuliwa na ufisadi.
 
Sangarara,

Nashukuru sana kwa mchango wako uliojaa mawazo mazuri sana; Lakini kabla sijaenda mbali, naomba niseme kwamba huu ni mtazamo wangu tu, hivyo nategemea mgongano mkubwa sana wa mawazo, lakini ninacho thamini zaidi ni kwamba mwisho wa siku, sote tunajifunza mengi toka kwa kila mmoja wetu, hivyo kuibuka waelewa zaidi; Nitajibu post zako mbili (post number 98 na number 99 kwa pamoja kama ifuatavyo:

Nianze na suala la wapiga kura wa mijini vi-a-vis wa vijijini; Kimsingi nakubaliana na wewe ila ningependa kuongeza tu kwamba – ni muhimu kwa Chadema kuanza kufanya an examination juu ya nani ni mpiga kura mijini na vijijini in terms of income, occupation, kiwango cha elimu, jinsia n.k, na kubaini factors zinapelekea wananchi wawe na tabia zinazotofautiana kwenye upigaji kura, hasa kwanini wapo wananchi wenye mazoea ya kupiga kura na kwani wengine hawana mazoea hayo, kote mijini na vijijini; Pengine nifafanue zaidi ni nizidi kueleweka juu ya hili: Kwa mfano, Chadema kama chama cha siasa, JE ni AGENT of mobilization au representation? Kwa mtazamo wangu, M4C inaegemea zaidi on Mobilization na kwa kiasi kikubwa ignores Representation; Ndio maana ukitazama umati wa M4C, wengi ni wanaume, wakati uhalisia wa mambo ni kwamba watanzania wengi (up to 54% of the population ni Wanawake), lakini muhimu zaidi, wapiga kura wengi (karibia 60%) ni wanawake;

Tukiwa bado kwenye suala la wapiga kura wa mijini versus vijijini, kumekuwa na trend katika chaguzi karibia zote barani Afrika kwa watu wa mijini kupigia kura zaidi vyama vya upinzani huku wale wa vijijini wakipigia kura zaidi vyama tawala; kwa kiasi kikubwa katika hoja zako umejaribu kulizungumzia hili, hasa katika jitihaha zako za kujaribu kubaini juu ya motivations za wapiga kura vijijini vis-à-vis mijini ni zipi; kwa mfano, umezungumzia suala la Ujamaa, illiteracy n.k, hoja ambazo binafsi pia nazikubali; Lakini tujiulize, JE: Wananchi wa mijini wanachagua vyama vya upinzani kwa sababu gani nje ya conventional factors tunazoelezwa: JE, is it because they feel the pinch of injustices kiuchumi, kisiasa na kijamii kwa kiwango tofauti na wenzao wa vijijini? Kwa maana nyingine, je, madhara ya soko huria na ubepari kwa wananchi/wapiga kura wa vijijini ni madogo kuliko kwa wenzao wa mijini? Hii itasaida sana kuzidi kutupatia uelewa juu ya relevance ya Ujamaa vijijini versus mijini;

Kwa mtazamo wangu ambapo pengine ni finyu, nadhani utofauti huu baina ya jamii za mijini na vijini unachangiwa sana ukweli kwamba - Wananchi wengi wa vijijini wana ufahamu mdogo sana kuhusu their civic duties (wajibu wao kama raia) na pia ufahamu mdogo sana juu ya state duties (wajibu wa serikali kwa wananchi), tofauti na wenzao wa mijini; Kwa mfano, among the most important civic duties ni katika any democracy ni pamoja na: VOTING & PAYING TAXES;


  1. VOTING
Huu ni wajibu mkubwa sana kwa mwananchi kwani wajibu huu unampa mwananchi fursa/ unamsaidia mwananchi kufanya maamuzi muhimu kuhusu mwenendo wa uongozi husika katika kumwendeleza yeye kiuchumi na kijamii; Ndio maana ni muhimu sana kwa wananchi wa vijijini kuanza kuwa na uelewa/kutofautisha kupigia kura MTU vis-à-vis MASUALA;

2.PAYING TAXES
Kulipa Kodi ni wajibu mwingine muhimu wa mwananchi; Pia Kodi ndio kiunganishi kikuu baina ya wajibu wa serikali na wajibu wa raia; ni katika uhusiano huu, suala la LEGITIMACY & CREDIBILITY ya serikali ndio hujitokeza kwani – credibility na legitimacy inatokana na jinsi gani serikali ipo accountable na kodi za wananchi wake; lakini tatizo lililopo Tanzania, hasa katika uhusiano baina na serikali na wanavijiji ni kwamba serikali kuu haiwajibiki moja kwa moja kwa wananchi kupitia kodi, na pia wananchi hawawajibiki moja kwa moja kwa serikali kuu kupitia kodi, na ni hapo ndipo mianya inayodumaza demokrasia hujitokeza;

Pengine nifafanue zaidi kidogo: Kodi represents mkataba baina ya serikali na wananchi ambapo wananchi hutegemea kuona faida ya kodi zao kwa serikali kupitia kwa mfano ongezeko au uboreshwaji wa huduma za kijamii, ongezeko au uboreshwaji wa miundo mbinu n.k, na haya yakitokea, ndio legitimacy na credibility inazidi kujengeka kwa serikali husika; Lakini huko vijijini kwetu Tanzania, contract ya namna hii haipo that straight forward; Ni katika mkanganyiko huu unakuta mara nyingi wananchi vijijini wanashindwa kufanya maamuzi ya maana during their civic duties, na mara nyingi huishia kupigia kura aidha MTU badala ya MASUALA anayosimamia au kupigia kura AHADI badala ya kuchambua practicalities za hizo ahadi. Suala la ahadi umelijadili na kimsingi tupo pamoja. Mwalimu Nyerere katika uchaguzi mkuu wa 1970 alipata kunena yafuatayo:

"I hope that both candidates in each election will be intelligent enough to recognize that not everything can be done at once, and that nothing in this world is FREE. For the fact is that if a person is urging more communal services or better communal services, he or she is probably also urging that you, as the voter, should be willing to pay more local rates or more taxes. For is they are promising lots of new activities if they are elected, and if they are promising that these will be done without any cost to you, or effort on your part, they are either deliberately misleading you – thinking you are fools or they themselves are fools."

Ni muhimu kwa Chadema kutumia Masomo kama haya Mwalimu aliyotuachia;


Hoja yako Juu ya mtazamo wangu juu ya ‘Consistency & Coherency' of Opposition Strategies

Kimsingi nakubaliana na hoja zako juu ya hili, hasa kuhusu umuhimu wa kutofautisha kauli na misimamo ya kiongozi vis-à-vis CHAMA, lakini pia umuhimu wa kutoa uhuru wa mawazo miongoni mwa viongozi; Nadhani hivyo ndivyo ulimaanisha, vinginevyo kama nimekosea naomba unisahihishe; Kama nipo sahihi, kimsingi tupo pamoja, ila niseme tu kwamba hoja yangu ililenga zaidi juu ya aina ya mikakati ya upinzani inayotumiwa na Chadema na kutafsiriwa na UMMA, hasa pale UMMA unapo consider matamshi na misimamo ya individual leaders kama ndio ya misimamo rasmi ya Chama;

Kama tunavyoelewa, moja ya kazi za chama cha upinzani ni kuja na mtazamo au msimamo tofauti na Serikali iliyopo madarakani, na ni muhimu mtazamo huo mbadala ukaonekana kuwa ni superior kuliko ule wa serikali mbele ya UMMA, mfano taxation policies, employment policies, etc; Ndio maana ili kufanikiwa in a consistent way, mara nyingi huwa ni muhimu sana kwa chama kuwa na mitazamo inayokingwa na itikadi fulani badala ya kuwa na misimamo au mitazamo ambayo haina a ‘strong base'; Chadema kwa bahati mbaya sana haina itikadi yenye mizizi mirefu kwa wananchi walio wengi (hasa vijijini), na badala yake kimekuwa ni chama kinachoendeshwa zaidi kwa personalities za viongozi wake; kwa bahati mbaya, CCM nayo pia imeanza mchezo huu; Hii ni kutokana na ukweli kwamba Vyama vyote viwili vinakabiliwa na ombwe la Itikadi.

Mwisho naomba nimalizie na suala la UFISADI na kwanini nasema hili ni suala la msimu.
Kwanza, naomba niseme kwamba mimi sikatai kwamba ufisadi unatugharimu kimaendeleo kama taifa; na nimependa sana ulipoliweka tatizo hili on PAR na maadui wengine wa Maendeleo kama vile umaskini, ujinga na maradhi; Ninaposema kwamba Ufisadi ni suala la msimu, maana yangu kuu ni kwamba – ni Kweli RUSHWA ni ADUI WA HAKI, lakini HAKI ina maadui wengi zaidi ya RUSHWA; kama tunakubaliana juu ya hili, JE, Rushwa ikipata ufumbuzi, suala la HAKI litakuwa limetatuliwa? Jibu ni Hapana; ndio maana huwa nahimiza juu ya umuhimu wa Chadema kuja na programu pana zaidi ya kujiandaa na uchaguzi mkuu wa 2015 ambayo itafanya Rushwa kuwa sehemu muhimu ya programu hiyo lakini huku ikikwepa kufanya UFISADI kuwa kete kubwa kuliko zote as a way ya kujitofautisha na CCM mbele ya wapiga kura; hii itawagharimu chadema, hasa ikizingatiwa kwamba Ufisadi hauna mashiko yoyote ya kiitikadi Kwahiyo chama chochote (including CCM) kinaweza kudandia hoja hiyo nap engine kuitumia kikamilifu kuliko Chadema 2015;

The bottom line hapa ni kwamba: Kwa miaka nenda, miaka rudi, majority of Tanzanians wamekuwa wanaishi kwa kuteseka sana kutokana na ukosefu wa HAKI kiuchumi, kisiasa na kijamii (political economic and social injustice), hivyo ni muhimu kwa Chadema inapoelekea 2015, ‘to approach' suala la HAKI in a more HOLISTIC WAY, kwani kama tunakubaliana kwamba HAKI ni the common denominator ya matatizo mengi kama sio yote ya Watanzania walio wengi, then ni muhimu tukakubaliana pia kwamba UFISADI is just an atom in the WHOLE;
 
Back
Top Bottom