CHADEMA: Tujadili Utayari wa Kutawala Nchi 2015

Mkuu FortJeasus kwanza inabidi tuangalie maana rahisi ya neno itikadi kwenye muktadha wa siasa, na hasa siasa za Tanzania. Kwa ufupi inaweza kuwa mkusanyiko wa imani, nadharia, mawazo na misimamo ya chama kuhusu mambo fulani.

Pili tuangalie Tanzania iko katika mazingira gani, na tuangalie ni vipi hizo itikadi zinaweza kutekelezwa.

Nikianza kuangalia itikadi(ideology) ya CCM ya ujamaa na kijitegemea, ambayo wengi tunaifahamu, kimsingi haipo. Imebaki tu kwenye vitabu, lakini kwa uhalisia ni kuwa haitekelezwi na haifuatwi hata kidogo, hata ukiangalia mwelekeo wa sasa hakuna dalili inayoonesha kuwa CCM itaelekea huko siku moja. Remnants wa itikadi hiyo kama Kina Mzee Kingunge kwa sasa ni makabaila wakubwa kama si mabepari. Uki-unpack the whole ideology na kuchambua element moja moja huwezi kuona hata kidogo kuwa CCM inatekeleza itikadi ya Ujamaa na kujitegemea. Kwa sasa kwenye aspect nyingi sana tunaona Tanzania inaegeemea zaidi kwenye ubepari.

Hata tukiangalia sera(policies) za CCM za sasa na election manifesto, hata ukiangalia ile vision 2025 which is 'implemented' based on ideology and policies of CCM, haina element zinazoweza kumconvince mtu mwenye akili kuwa tunaekelea kwenye ujamaa na kujitegemea. Zote zinalenga zaidi kwenye utengano, ubepari na kujitajirisha. Kwa maoni yangu, nikiangalia nini kipo kwenye katiba ya chama, ilani yake ya uchaguzi na kile kinachofanyika on the ground naweza kusema sielewi itikadi ya CCM ni ipi. Ujamaa ni kujitegemea? ubepari na kujitajirisha? ufisadi, fitna nk hakuna unachoweza kukiona wazi. Hakuna anayeweza kusema sasa hivi chama cha mapinduzi kinafanya kazi hii. Nina hakika leo ukimuuliza Nape hili swali hana jibu, leave Nape aside, muulize Mukama pia hana jibu.

Tukiangalia CHADEMA wao at least wako more ralistic, kwa kuwa wanaangalia mazingira ya sasa wanako-operate. Hata kama wana sera au itikadi, hawana uwanja wa kuzitekeleza. Majimboni ambako wana wabunge wawili au watatu bado hawana uwezo wa kufanya tofauti na kinachofanywa na wabunge wa CCM. Sidhani kama mkazi wa kinondoni ana tofauti na mkazi wa Ubungo kunakota na kuwa na wabunge tofauti. Sasa hivi hata kama kuna kitu kinaitwa sera ya Chadema naweza kusema bado hatuwezi kukiona wazi hadi washike rungu. Kidogo tumeona bungeni kwenye suala la ufisadi, wao hawaungi mkono ufisadi kama CCM (japo sera na itikadi zake zinapinga kivitendo wanaruhusu). So if there is such a thing as CDM ideology, we have to wait and see what is it.

Inawezekana Chadema na CCM wana maoni tofauti kuhusu mambo madogo madogo ambayo haya umuhimu sana katika mambo ya maendeleo na usalama wa nchi. Hayo kimsingi ni kwa ajili ya kukusanya wapiga kura tu. Lakini kuna makubwa kama defence, economy national unity , integration, etc huko ndio tunataka kujua itikadi hasa ya Chadema. Ya CCM tumeiona nadhani wengi hapa JF tunajua kuwa haifai, kwa sababu matokeo yake yameonekana.

Kulingana na hali ya sasa ya dunia, chama chochote makini kitafuata sera inayolenga kuinufaisha nchi katika mazigira ya sasa, ndani na nje, kitafuata sera inayoendana na upepo unaovuma. Kwa hiyo kikiwa madarakani ndio tutaweza kujua ndani kikoje.

Sasa hivi Chadema wamevaa Gwanda hatujui wakivua gwanda ndani kuna nini, CCM ingawa wamevaa Gamba tayari tumeona ndani kuna nini. Kwa hiyo bado hatuwezi kusema wazi ideology ya CHADEMA ikoje, hadi pale watakaoweza kuitekeleza, naamini kuwa haitakuwa tofauti na itikadi halisi ya CCM (sio iliyoandikwa kwenye mnakaratasi na inayoimbwa).

I stand to be corrected.
 
Last edited by a moderator:
Bongolander

'''Nikianza kuangalia itikadi(ideology) ya CCM ya ujamaa na kijitegemea, ambayo wengi tunaifahamu, kimsingi haipo. Imebaki tu kwenye vitabu, lakini kwa uhalisia ni kuwa haitekelezwi na haifuatwi hata kidogo, hata ukiangalia mwelekeo wa sasa hakuna dalili inayoonesha kuwa CCM itaelekea huko siku moja. Kwa sasa kwenye aspect nyingi sana tunaona Tanzania inaegeemea zaidi kwenye ubepari. Hata tukiangalia sera(policies) za CCM za sasa na election manifesto, hata ukiangalia ile vision 2025 which is 'implemented' based on ideology and policies of CCM, haina element zinazoweza kumconvince mtu mwenye akili kuwa tunaekelea kwenye ujamaa na kujitegemea. Zote zinalenga zaidi kwenye utengano, ubepari na kujitajirisha. Kwa maoni yangu, nikiangalia nini kipo kwenye katiba ya chama, ilani yake ya uchaguzi na kile kinachofanyika on the ground naweza kusema sielewi itikadi ya CCM ni ipi.

Tukiangalia CHADEMA wao at least wako more ralistic, kwa kuwa wanaangalia mazingira ya sasa wanako-operate. Hata kama wana sera au itikadi, hawana uwanja wa kuzitekeleza. Majimboni ambako wana wabunge wawili au watatu bado hawana uwezo wa kufanya tofauti na kinachofanywa na wabunge wa CCM. Sidhani kama mkazi wa kinondoni ana tofauti na mkazi wa Ubungo kunakota na kuwa na wabunge tofauti. Sasa hivi hata kama kuna kitu kinaitwa sera ya Chadema naweza kusema bado hatuwezi kukiona wazi hadi washike rungu.

....lakini kuna makubwa kama defence, economy national unity , integration, etc huko ndio tunataka kujua itikadi hasa ya Chadema''

Ndugu Bongonder, Kimsingi ninakubaliana na hoja zako.

Nilijaribu, katika bandiko langu la awali,kueleza kuwa CDM kama taasisi ya kisiasa inayo itikadi tofauti na madai ya baadhi ya wananchi wenzetu wanavyoamini. Kwa makusudi kabisa, sikufanya jitihada yoyote kuichambua itikadi ya CCM. Nililofanya hivyo kwa kuwa angalau tulipta kufahamu chama hiki kilipata kuamini katika nini. Kwa sasa, tunaelewa wazi kuwa kuna ombwe la kiitikadi katika chama hicho.Tutakubaliana kuwa ni hatari kuwa na vyama vya Upinzani visivyo na Itikadi..lakini ni hatari zaidi kuwa na chama tawala kisicho na itikadi iliyo wazi.Kama ulivyoonyesha katika bandiko lako, ni kweli kabisa kuwa Mipango yote ya Maendeleo huandaliwa kwa kuzingatia itikadi.

Ni hatari vile vile,tunapokuwa na Taifa lisilo na misimamo ama mikakati kuhusu mambo muhimu ya Kitaifa kama vile ulinzi ,uchumi na usalama.Hili linatokea wakati tunakabiliwa na ombwe la uongozi na mgogoro wa uhalali wa kuongoza(The crisis of Legitimacy). Nchini Marekani, kulipo na kiwango kikubwa cha uelewa na uwajibikaji wa kisiasa kutokana na historia na mazingira yake, kuna Sera na Mikakati iliyotungwa kuhusu masuala haya.Mathalani,kuna sera ya Marekani kuhusu Afrika ya mashariki, Kusini mwa Jangwa la Sahara, Middle East nk. Sera hizi hazibadiliki.

Chama chochote kinapoingia madarakani halazimika kuziteleza. Kwa sasa, tunatakiwa kuwa na Mjadala mpana wa Kitaifa kama wanazuoni wengi wanavyopendekeza na kisha tupate Muafaka wa Kitaifa ambao utatumiwa ku -base matendo na maaumuzi ya vyama vya siasa mara vinavyokamata dola.Tuna fursa ya kuwezesha hilo kama tutatumia Mchakato wa sasa wa Katiba Mpya kuamua ''Tanzania Tuitakayo''. Tunaweza pia kutunga Sera mahsusi katika maeneo muhimu kama vile Elimu, Ulinzi na Usalama na Maendeleo..Lengo la hatua hii ni kuhakikisha kuwa matendo yetu ya huko mbele yanakuwa predictable, na kuepusha hatari ya vyama vya siasa kuingia madarakani na kuratibu na kuendesha mabadiliko kulingana na matakwa yake.Tuanapokuwa na formalized procedures na systems hatuna sababu ya kuhofu Chama gani kitakamata dola.

Ni kweli kama ulivyosema ,kuwa, iweje wananchi wa Kinondoni wawe na Mbunge wa CCM wakati wenzao wa Ubungo na wawe na mbunge wa CHADEMA! Tunatambua kuwa maamuzi ya wapiga kura huongozwa na mambo kadhaa ikiwemo umaarufu wa mgombea, haiba yake, uwezo wake na juhudi zake katika kuvutia kura.(Soma Kitabu cha ''who Vote in Tanzania and Why'' (Maliyamkono)...mwaka( ). Hata hivyo katika mazingaira ambayo Uhuru wa Tume ya Uchaguzi unatiliwa mashaka,hayuwezi kusema kwa uhakika kama kweli Mgombea wa fulani alishinda kihalali.

Tukumbuke kuwa katika Tanzania,wapiga kura huwa hawajali sana kufahamu sera na itkadi za vyama vinavugombea. Hata hivyo, kadiri tunavyoenda mbele kuna matumaini kuwa Itikadi na Sera zitachukua nafasi kubwa katika kampeni za Chaguzi.
 
Last edited by a moderator:
FortJeasus,

Nashukuru wa kuendeleza mada hii. Nitazirudia hoja zako mbalimbali pamoja na wadau wengine muda mfupi ujao. Nadhani hoja yangu haikueleweka vizuri lakini nitafafanua baadae kidogo. Kwa sasa naomba niseme yafuatayo, hasa nikilenga hoja kwa mfano ya mwiba ambae anasema hivi:

Chadema hawana wenye sifa ambazo wataweza kutekeleza ,ukiangalia CDM hamna wana siasa wala wenye sifa za kiuongozi ,hapa walikuwa wamechachamaa kuanika CV za watu walipotakiwa waweke za kwao wakaingia mitini ndio mkatuletea mgombea mwenza wa uraisi aliekimbia dalasa la saba.

Naomba niseme kwamba tukubali ukweli wana CCM wenzangu. Kwa utafiti wangu ambao pengine sio credible, CCM kushinda urais 2015 ni vigumu sana, especially kama uchaguzi utakuwa fair and transparent; Mimi ni mwanachama wa CCM, lakini kama raia mwingine yoyote, na nina haki ya kutoa maoni yangu objectively, na kwa mujibu wa my immediate experience of actual things and events in this context, urais 2015 ni mgumu sana for CCM. Chadema stands a better chance kushinda 2015 kuliko CCM, but as long as they tie loose ends that exists, ambazo nilizijadili kwenye uzi mwingine titled:
Chadema: Tujadili Utayari Wa Kutawala Nchi 2015.

So ushindi wa Chadema 2015 upo imminent, but swali linalofuatia ni je, wataweza kutawala?

Binafsi sidhani kama wataweza kwa sababu, kama nilivyokwisha jadili elsewhere, umma umeichoka CCM na upo tayari kuiondoa CCM immediately; Chadema wanafanya kosa la kuaminisha umma kwamba fine, we can remove CCM immediately kwa ridhaa yenu and provide you with "immediate solutions"; hili ni tatizo kubwa sana Chadema inajijengea. Sina maana kwamba Chadema wanazunguka na kusema watatua hili na lile within a short time frame, lakini hawafanyi kazi kugeuza fikra za umma ambazo zina upeo huo mfupi;Chadema ilitakiwa kuaminisha umma kwamba we need to reconstruct this country together first then ndio tuje kujipanga to develop, na watakaofaidika na project hii ni watoto na wajukuu zenu, sio nyinyi, faida mtakayoiona nyinyi ni stoppage ya utawala wa kubabaisha na usio na manufaa kwa walio wengi. Vinginevyo iwapo watanzania wamevumilia kwa miaka 50, kwanini washindwe kuvumilia kwa miaka 15-20 ili reconstruction project ikimalizika, development ndio ianze to materialise kwao?

Ndio maana ninalazimika kuamini kwamba, unless Chadema inaanzisha project ya
RECONSTRUCTION AND DEVELOPMENT FOR 2015 AND BEYOND - na umma uelewe na ushibe dhana hii ,CCM itarudi 2020 kwa kishindo kikubwa sana na upinzani kushinda tena urais Tanzania itakuwa ngumu mno beyond 2025 and for the next foreseable future. Otherwise it is for Chadema themselves to loose;
 
FortJeasus,

Nashukuru wa kuendeleza mada hii. Nitazirudia hoja zako mbalimbali pamoja na wadau wengine muda mfupi ujao. Nadhani hoja yangu haikueleweka vizuri lakini nitafafanua baadae kidogo. Kwa sasa naomba niseme yafuatayo, hasa nikilenga hoja kwa mfano ya mwiba ambae anasema hivi:


Naomba niseme kwamba tukubali ukweli wana CCM wenzangu. Kwa utafiti wangu ambao pengine sio credible, CCM kushinda urais 2015 ni vigumu sana, especially kama uchaguzi utakuwa fair and transparent; Mimi ni mwanachama wa CCM, lakini kama raia mwingine yoyote, na nina haki ya kutoa maoni yangu objectively, na kwa mujibu wa my immediate experience of actual things and events in this context, urais 2015 ni mgumu sana for CCM. Chadema stands a better chance kushinda 2015 kuliko CCM, but as long as they tie loose ends that exists, ambazo nilizijadili kwenye uzi mwingine titled:
Chadema: Tujadili Utayari Wa Kutawala Nchi 2015.

So ushindi wa Chadema 2015 upo imminent, but swali linalofuatia ni je, wataweza kutawala?

Binafsi sidhani kama wataweza kwa sababu, kama nilivyokwisha jadili elsewhere, umma umeichoka CCM na upo tayari kuiondoa CCM immediately; Chadema wanafanya kosa la kuaminisha umma kwamba fine, we can remove CCM immediately kwa ridhaa yenu and provide you with "immediate solutions"; hili ni tatizo kubwa sana Chadema inajijengea. Sina maana kwamba Chadema wanazunguka na kusema watatua hili na lile within a short time frame, lakini hawafanyi kazi kugeuza fikra za umma ambazo zina upeo huo mfupi;Chadema ilitakiwa kuaminisha umma kwamba we need to reconstruct this country together first then ndio tuje kujipanga to develop, na watakaofaidika na project hii ni watoto na wajukuu zenu, sio nyinyi, faida mtakayoiona nyinyi ni stoppage ya utawala wa kubabaisha na usio na manufaa kwa walio wengi. Vinginevyo iwapo watanzania wamevumilia kwa miaka 50, kwanini washindwe kuvumilia kwa miaka 15-20 ili reconstruction project ikimalizika, development ndio ianze to materialise kwao?

Ndio maana ninalazimika kuamini kwamba, unless Chadema inaanzisha project ya
RECONSTRUCTION AND DEVELOPMENT FOR 2015 AND BEYOND - na umma uelewe na ushibe dhana hii ,CCM itarudi 2020 kwa kishindo kikubwa sana na upinzani kushinda tena urais Tanzania itakuwa ngumu mno beyond 2025 and for the next foreseable future. Otherwise it is for Chadema themselves to loose;

Hoja ya Mchambuzi ina ukweli ambao Chadema wanatakiwa kufanyia kazi. Ukiangalia safu ya viongozi wa Chadema waliopo sasa hivi ni wazuri, wanajiamini, wanauwezo wa kuhamasisha, kuelimisha nk. Kuna wasomi wengi tu kama wanaweza kutumia elimu yao vizuri inaweza kusaidi kuanza vizuri iwapo wanaweza kuchukua dola.

Jambo la msingi la kuangalia ni hili kwamba, uwezo na mafanikio katika uongozi si elimu pekee na mvuto wa watu walio nao, bali uzoefu nao huchangia sana katika kuleta mafanikio ya uongozi. Mfano Kenya baada ya sanduku la kura kuibwaga KANU safu ya upinzani ilisheheni wengi ambao walikuwa na uzoefu katika masuala ya uongozi kisiasa wakiongozwa na Mwai Kibaki mwenyewe ambaye alishawahi kuwa Makamu wa Rais katika awamu zilizotangulia, ambao waliamua kujiengua kutoka Chama tawala kwa sababu ya kutoridhishwa na uendeshaji wa serikali.

Kinachonivutia ni Chadema kufungua milango kwa wenye uzoefu kutoka serikali ya CCM kujiunga na Chadema ili kukipa nguvu na kwa namna fulani inaweza kusaidi kuchangia safu ya viongozi wazoefu wa uongozi wa serikali kuisaidia Chadema. Hata hivyo jambo hilo linaweza kuwa kitanzi kwa Chadema kwa vile uzoefu unaonyesha kwamba wengi walio madarakani sasa hivi mvuto kujiunga na chama kipya kinachoinukia kuwa na nguvu ni kutaka madaraka, na pale wanapokosa huishia kuanzisha mtifuano katika chama na hivyo kusababisha dhoruba zenye kuyumbisha uongozi mpya na chama kama ilivyotokea katika nchi kadhaa ikiwepo kesha kama tulivyoshuhudia.

Chadema mpaka sasa inazo sera nzuri zinazouzika lakini hazijapangwa kitaalamu na wala hazijawekwa wazi malengo ya mipango ya muda mfupi na mrefu. Kuna haja ya Chedema kuwatumia wataalamu walio nao na hata walio nje kuwasaidia kujenga sera zenye mtiririko ambao ni rahisi kueleweka na kuweka msimamo wazi katika mfumo wa utwala wanaotaka. Mara kadhaa wameshindwa kuainisha jambo hilo walipoulizwa katika majopo ya majadiliano au kampeni, kwani sera nzuri bila kuwa na mtiririko kitaalamu na kitaaluma huwa na kasoro ya kuonekana ni kama gari la zima moto linalohitajika wakati wa dharara.
 
Mchambuzi

Mkuu ni lazima utambue factor moja, wapiga kura wetu walio wengi bado hawajaamka na kujua umuhimu wa kura yao. They think in a very simplistic way, none thinks that CCM has brought us in a development quagmire we are in today. Hakuna anayefikiri sera, itikadi, mipango au vision yoyote........upepo ukija wanavuma nao. Ni kweli wapo wengi wameamka, lakini sio kwa kiasi cha kuifanya CCM ijue kuwa imefika mwisho. Kwa hiyo aliyosema Profesa baregu kuwa CCM inategemea mtaji wa wanyonge naamini kuwa yataendelea kuwa valid kama Chadema wataendelea na sytle ya 2010

I still believe kuwa CCM wana miaka mingine mitano ya kutawala baada ya JK, kwa sababu bado CCM ina monopoly ya vyombo vyote vya usalama ikiwemo NEC, kwa hiyo wanaweza kuingia madarakani kwa wizi kama walivyofanya 2010.

Njia peke ya CCM kushindwa ni kutokea kwa mpasuko mkubwa ndani ya Chama na kundi moja liistrengthen Chadema(hasa pale wale wanashiriki kuchakachua matokeo watakapoondoka CCM, itakosa namna ya kuiba kura tena), na ikiwa hivyo CCM itakufa itabaki kuwa kama KANU Kenya, mimi ni mwanaccm lakini nakubaliana na wewe kuwa CCM ile ya baba na babu zetu haifanani kabisa na ya sasa, uwezekano wa kurudi ile ya zamani ni mdogo sana. Ule ukuta wa Berlin aliousema Kolimba ukibomoka tu ndio hali itaanza kubadilika Tanzania, otherwise hali ya sasa itaendelea kuwepo.
 
Last edited by a moderator:
Mchambuzi

Mkuu ni lazima utambue factor moja, wapiga kura wetu walio wengi bado hawajaamka na kujua umuhimu wa kura yao. They think in a very simplistic way, none thinks that CCM has brought us in a development quagmire we are in today. Hakuna anayefikiri sera, itikadi, mipango au vision yoyote........upepo ukija wanavuma nao. Ni kweli wapo wengi wameamka, lakini sio kwa kiasi cha kuifanya CCM ijue kuwa imefika mwisho. Kwa hiyo aliyosema Profesa baregu kuwa CCM inategemea mtaji wa wanyonge naamini kuwa yataendelea kuwa valid kama Chadema wataendelea na sytle ya 2010

I still believe kuwa CCM wana miaka mingine mitano ya kutawala baada ya JK, kwa sababu bado CCM ina monopoly ya vyombo vyote vya usalama ikiwemo NEC, kwa hiyo wanaweza kuingia madarakani kwa wizi kama walivyofanya 2010.

Njia peke ya CCM kushindwa ni kutokea kwa mpasuko mkubwa ndani ya Chama na kundi moja liistrengthen Chadema(hasa pale wale wanashiriki kuchakachua matokeo watakapoondoka CCM, itakosa namna ya kuiba kura tena), na ikiwa hivyo CCM itakufa itabaki kuwa kama KANU Kenya, mimi ni mwanaccm lakini nakubaliana na wewe kuwa CCM ile ya baba na babu zetu haifanani kabisa na ya sasa, uwezekano wa kurudi ile ya zamani ni mdogo sana. Ule ukuta wa Berlin aliousema Kolimba ukibomoka tu ndio hali itaanza kubadilika Tanzania, otherwise hali ya sasa itaendelea kuwepo.

Tukitazama historia, upepo wa kisiasa unaonyesha kwamba unapokusudia kujenga mnara mrefu zaidi kupita yote ili uone kila kona ya dunia kama ilivyotokea kule kwa Waajemi (siku hizi Iraki), kwa vile kinachokusudiwa ni malengo binafsi tu ya kupoteza pesa nyingi kwa nia ya kuonwa na mnara mrefu duniani na hatimaye kufika mbinguni kwa urahisi kwa vile mnara huo umepunguza safari ya kufika mbinguni.

Kuna baadhi wataakaoona hoja hiyo haina mshiko kwa kuwa malengo ya mnara huo haina mshiko kwa wananchi wengi ambao kodi zao zinachangia kuujenga, na bado raia wangali katika lindi la umaskini, kitakachoshuhudiwa ni migomo baridi ambayo siku baada ya siku itasitisha kasi ya kumalizika kwa huo mnara mrefu kama wa babilonia.

Matokeo yake ni kutifuka kwa lugha ambayo inawaunganisha (system) huyu badala ya kuleta tofali analeta mwiko, anayetakiwa kuleta udongo atafikisha mbao, basi mambo ni mchanganyiko tupu, kwa nini lugha inayowaunanisha (system imeshatifuka) na hapo inafika no common goal sababu kila mmoja ana chake kwa kuwa ujenzi ule wa mnara unaonekana kusuasua na soon unaweza kusimama kabisa, kila mmoja ataamua kukusanya tu nguvu kujenga kajimnara kake. Whats wrong? Nyumba iliyogawanyika inaweza kusimama yenyewe?

Wiki iliyopita limetokea suala la utata mpaka wa Ziwa Nyasa, na baadhi ya waandamizi wa serikali akiwemo Waziri wa Mambo ya nje na ushirikiano wa kimataifa Mhesh. Bernard Membe kutoa kauli ya kuitishia Malawi akifuatiwa na Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge mambo ya Nje Mhesh. Edward Lowasa kufuata nyayo za Membe kujenga hoja ya kutetea sehemu ya nchi yetu. Membe ni mwakilinzi wa mkuu wa nchi kimataifa, wakati Lowasa naye vivyo kwa niaba ya Speaker wa Bunge la Jamhuri katika masuala ya kimataifa.

Kioja, Mkuu wa nchi Rais Kikwete alipokutana na Rais wa Malawi Joyce Banda na kumwita dada yake, alitamka kitu ambacho sikukitegemea kwamba waliotishia malawi ni wapinzani wake wa kisiasa wakati ni wateule wa kabinet yake. Hili linatofautiana vipi na historia ya ujenzi wa mnara wa babeli huko Babilonia?

Dalili hizi za utawala uliotukuka kati ya mataifa barani afrika ni kuonyesha kudhoofika, na kama upinzani usipotumia nafasi hii ambayo ni mwanya mzuri watakuja jutia baadaye. Nyufa hizi zinaweza kusaidia chama cha upinzani kuchukua serikali kiulaini, lakini uwezo wa kuendesha serikali usitazamiwe kuwa na matunda ya pekee awali, kwani wengi wataona afadhali ilipokuwa CCM, kwa nini? Uzoefu huchukua muda, na pengine awamu ya pili ndio unapoweza kuona matunda kama ilivyotokea Kenya.
 
Update.

Nimefanya mawasiliano na Ndugu Mchambuzi. Muda mfupi ujao atarejea hapa jamvini kufafanua na kujibu baadhi ya hoja.
 
Tatizo CHADEMA deep down hawaamini wanachukua nchi; bado wako bize kuikosoa serikali badala ya kujiandaa kuongoza vizuri

Ukimwamsha anayelala utalala wewe. Chadema inapokazana kuikosoa serikali maana yake inataka CCM iamke na kutenda vema ili kuwaridhisha wananchi. Je, kwa kufanya hivyo wananchi wataona kuna haja gani tena kuichagua CDM?
 
FortJeasus,

Samahani nilitingwa kidogo na shughuli, na pia uniwie radhi kama majibu yatakuwa marefu kidogo. Kwanza kabisa ningependa kuweka mambo yafuatayo sawa:

1. Kwanza - nadhani awali sikueleweka kwenye hoja yangu kuhusu "Utayari wa Chadema 2015". Msingi wa hoja yangu ilikuwa kwamba – kuna baadhi ya mambo ambayo Chadema haiyafanyii kazi, na nikatoa mfano wa perception ya "shukrani ya punda ni mateke", na kueleza kwamba sehemu kubwa ya umma inaendelea ‘kupotoshwa', aidha kwa bahati mbaya au kwa jitiada za makusudi, na kushauri Chadema ifanyie kazi maeneo kadhaa ili ifanikiwe. Mimi ni mwana CCM mpenda demokrasia na ushindani wa kisiasa wenye tija, na sioni vibaya kutoa mawazo yangu jinsi gani tunaweza boresha demokrasia yetu, hata ikibidi kukikosoa CCM as long as ni kwenye masuala ambayo in the ‘long run' yatatugharimu, kwa kujisahau na kuchukulia things for granted, hata kama kwa sasa yanaweza onekana yanaipa CCM ‘a competitive edge' dhidi ya upinzani. Na sehemu kubwa ya majibu yako umelenga katika kuonyesha ukweli upo wapi, na Chadema wanatakiwa kufanya mbele ya umma.

2. Pili, sikuwa na nia ya kuonyesha kwamba Chadema haipo tayari kupokea madaraka ya nchi 2015, na badala yake ‘to argue' kwamba ili kuiangusha CCM 2015, Chadema itahitaji mikakati ya aina mbili. Kwanza, kuendelea na kazi yake ‘to capitalize' kwenye udhaifu/mapungufu ya CCM, ambapo niliyajadili as "What Went Wrong For CCM"; lakini nikasema kwamba working on mapungufu ya CCM peke yake haitoshi, kwani ni kwa Chadema pia kuangalia na kuelewa "What Went Right For CCM", kwani in the long run, changamoto za Chadema zipo zaidi on the ‘later' kuliko the ‘former'.

Ningependa kutumia muda kidogo kujadili "dhana ya utayari", halafu baadae nitajadili hoja nyingine. Mimi nadhani wenye maamuzi ya mwisho kuhusu Utayari wa Chama fulani kutawala nchi ni umma. Nachoweza kufanya mimi au mtu mwingine ni kujadili au kuchambua tu mazingira ya utayari huo na kutoa mawazo huru, lakini sio maamuzi kwa niaba ya umma. Vinginevyo, tunazidi kushuhudia jinsi gani umma wa Tanzania ulivyochoka utawala wa CCM kwa sababu zilizo wazi. Suala on whether Chadema itafanikiwa kuwaletea wananchi suluhisho la kudumu, that remains to be seen.

Kuna factors kadhaa ambazo ni changamoto kwa vyama vingi vya upinzani, sio Tanzania tu bali all over the developing world. Hapa sina maana kwamba Chadema inakabiliwa na changamoto hizi moja kwa moja, bali nia yangu ni kuziorodhesha tu ili wafuasi wa Chadema wakipime chama chao. Changamoto hizi ni pamoja na:

i. Monocracy;
ii. Kuendesha Chama for private interest;
iii. Clientelism;
iv. Corruption/embezzlement;
v. Poor Organizational Structure;
vi. Lack of Internal Democracy; and
vii. Lack of Finance.

Niseme tu kwamba overtime, Chadema imejitahidi to overcome some of these challenges ingawa bado more work needs to be done in some areas.

Sasa niingine kwenye hoja zako nne kama ifuatavyo:

a) Hoja kuhusu CCM na Uongozi wa Mageuzi ya kisiasa nchini.
Katika hoja hii, umejadili mengi ambayo ndio ukweli halisi – kwa mfano the collapse of the soviet union and how that sent the wave of democracy in the third world. Upo sawa kabisa, na inatakiwa umma upewe elimu hiyo, na ndio ilikuwa hoja yangu ya msingi.

b) Relevance ya itikadi ya Ujamaa kwa wananchi vijijini.
Katika hili nina mtazamo tofauti kidogo na wewe. Ningependa kulizungumzia in the context of "Chadema na Maendeleo Vijijini". Kama nilivyokwisha argue elsewhere, itikadi na sera ambazo zipo practiced na CCM na Chadema leo hii hazina manufaa yoyote kwa watanzania wa vijijini. Vyama vyote hivi vina ambition ile ile – kwenda ikulu kutekeleza donor – led policies, not home grown policies kama enzi za Nyerere. Nimependa mjadala wako kuhusu the existing ‘rural-urban divide' na jinsi gani unaamini Chadema inaweza ktatua hili; hoja yako kwamba at independence Tanzania ilikuwa ni mainly vijiji (over 90%), ni sahihi; ndio maana I have argued elsewhere kwamba ni hali hii ndio provided the ‘social and material basis' for itikadi ya Ujamaa. In the 1960s, Sera yoyote nje ya Ujamaa ingekuwa ‘very short lived'. Ingawa Ujamaa haukufanikiwa sana, bad oleo hii kuna the same ‘social and material basis' for itikadi ya Ujamaa kuliko ya itikadi ya Uliberali au yoyote nyingine towards the right.

Hoja yako kuhusu kasi ya urbanization ni sahihi kabisa, lakini tatizo ni kwamba urbanization in Tanzania haileti maisha bora kwa wengi wanaohama, na mbaya zaidi, it makes things worse for wengi wanaobakia vijijini kwani it means nguvu kazi ya kilimo inahamia mijini, hence affect productivity ya kilimo. Urbanization yenye tija ni ile inayoenda sambamba na transformation katika sekta za kilimo na viwanda – rural and urban sector have to grow together – urbanization must involve transfer of manpower from the traditional sector (kilimo) to the modern sector (viwanda), determined by the demand for labour kwenye modern sector huku pia labour in the traditional sector ikiendelea kuhitajika kutokana na productivity/growth of the sector; urbanization isn't supposed to create or result from ‘idle labour', otherwise ni tatizo kubwa. Kwa Tanzania, tunaona jinsi gani migrants hawapati ajira mijini, hawapati nyumba za maana kuishi, lakini mbaya zaidi, wanaongeza more pressure to the already limited resources e.g. ardhi, public goods zilizopo mjini n.k. Matokeo yake ni more poverty mijini na potential violence.

Je, Urbanization ina faida gani kwa Chadema

In the short run, zipo faida, lakini sio in the medium to long term. Kwa mfano, faida zilizopo ni kwa Chadema kuendelea kufanikiwa kwenye majimbo ya mijini na yale ya barabara kuu kwenda mikoani na nchi jirani kwani tatizo la ‘Weak Civil Society in Tanzania' nililo jadili earlier, becomes less apparent. Faida nyingine ambayo inaendana na hii ni ukweli kwamba urbanization is one of the key determinants of democracy. Kwa mfano, kama tulivyokwisha ona kwenye mjadala wangu wa awali (on weakness of civil society), people in the villages have limited ability to organize…etc tofauti na wenzao in the urban areas ambako it is easier for people to meet, communicate, access the media etc. Lakini in the long run, urbanization can be a problem kama nilivyojadili earlier. Pia ni rahisi kwa Chama tawala to monitor and control wakazi wa mijini kuliko vijijini.

Je Chadema inaweza kulata rural development in Tanzania?
Kwa mujibu wa hoja zako, jibu ni ndio. Mimi sikatai lakini sidhani kama kazi hii ni rahisi kama unavyofikiri. Itakuwa vigumu sana kwa Chadema kufanya chochote tofauti na CCM.

Kwanini nasema hivi?
Historically, Vijiji vyetu vimekuwa a ‘failure' in terms of rural development despite the exhaustion ya karibia kila aina ya intervention:
1. Colonial State Failure – Serikali ya mkoloni haikufanikiwa kuleta rural development, and instead, made ths situation worse.
2. State Failure – Nyerere alijaribu kuleta rural development under Vijiji vya Ujamaa lakini yeye pia kwa kiasi kikubwa hakufanikiwa.
3. Market Failure (chini ya sera za SAPs 1985 – mid to late 1990s) – Baada ya Ujamaa kufeli, soko huria likaingia, huku wazee wetu kama Mzee Edwin Mtei (muasisi wa Chadema) wakiwa mbele katika kufanikisha mabadiliko haya. Hapa soko lilipewa nyenzo zote na serikali kutolewa katika equation ya rural development, lakini bado vijiji havikuendelea.
4. Market Failure (Chini ya Sera za PSRP na nyinginezo hadi kufikia leo). Baada ya SAPs kufeli, ikaonekana kwamba pengine tatizo lilikuwa ni kuitoa serikali in the development process, hivyo serikali ikarudishwa kushirikiana na sekta binafsi, lakini kwa miaka zaidi ya kumi na tano sasa, ndoa hii ya soko huria na serikali imezidi kumfanya mwanakijiji kuwa more excluded - socially, economically and politically.

Mchanganyiko wa State and the market katika hili has led to a ‘coordination failure', sababu kuu ikiwa kwamba - interest za soko na zile za serikali hazifanani.

Fortjeasus,

Given these four types of interventions on rural development, ambazo zote zimefeli, ningependa kusikia mawazo yako - Chadema watafanya nini tofauti, hasa in the context of itikadi yake ya Uliberali (yenye mrengo wa kati).

Vinginevyo I remain to believe kwamba Chadema haitaweza kukwepa kutambua umuhimu wa vijiji vya Ujamaa katika kufanikisha Rural Development kwani kwa kiasi kikubwa, watakutana na mazingira yale yale ya 1960s enzi za TANU. Kwa mfano, kama jinsi ilivyokuwa miaka ya 1960s, Tanzania leo bado ipo dominated na wanavijiji running a subsistence based economy kwenye vi-ardhi vidogo vidogo na katika maisha duni sana; Tanzania ina very low population density (the lowest in East and Southern Africa); Population outside town areas ipo very ‘sparse', so it becomes difficult to monitor, control na pia to intervene in terms of development projects, in a manner that is effective and sustainable.

Pia niseme tu kwamba, ingawa watu wengi wanaangalia vijiji vya Ujamaa kama it was more of a failure, wengi wanasahau kwamba kulikuwa na faida zake pia na baadhi ya hizi zipo wazi hata leo. Kwa mfano, there are studies today that show jinsi gani how maeneo haya have the highest completion rates of primary education compared to other areas ambazo hazikuguswa na operesheni ya vijiji vya Ujamaa au maeneo ambayo yalikuja endelezwa katika kipindi cha soko huria. Vile vile these studies reveal jinsi gani maeneo ya vijiji vya Ujamaa have greater availability of public goods and also report highest rates of participation in community projects kuliko maeneo yaliyoachwa na operesheni ya vijiji vya Ujamaa au yale yaliyokuja endelea chini ya soko huria.

c) Itikadi
Sikuwa na maana kwamba Chadema haina itikadi kwani kwa mujibu wa katiba ya Chadema, chama hiki kinafuata itikadi ya uliberali – mrengo wa kati. Hoja yangu ya msingi ilikuwa kwamba tuna tatizo la ombwe la itikadi miongoni mwa vyama vyote vya siasa Tanzania (including CCM), kwa maana ya kwamba itikadi zilizopo miongoni mwa vyama vyote ni aidha:

a) Ni itikadi za kwenye katiba tu, zilizoandikwa kukidhi moja ya requirements za msajili wa vyama kabla ya kupewa usajili; au
b) Ni itikadi zisizoakisi matakwa na uhalisia wa wananchi wengi (vijijini)/kwa maana nyingine, ni itikadi ambazo haziwezi kuleta majibu ya kweli kuhusu rural development in Tanzania.

Vinginevyo suala la ombwe la itikadi nilishajidili elsewhere kwenye uzi ufuatao: https://www.jamiiforums.com/great-thinkers/215953-nape-mnyika-mtatiro-wapi-itikadi-zenu.html.

Ningependa kumalizia kwa kuchambua kidogo itikadi ya Chadema ili sote tusaidiene kuona kama kweli itikadi hii ina tija kwa rural development in today's settings. Hapa pia tutilie maanani zile failures za rural development nilizojadili awali.

Traditionally, Itikadi ya Uliberali - mrengo wa kati], husimamia pamoja na mambo yafuatayo:
1. Ongezeko la kodi linaloendana sambamba na ongezeko la vipato na shughuli za uchumi (progression taxation);
2. Umiliki binafsi wa mali;
3. Kuwapatia wananchi uhuru wa kujiendeshea shughuli zao bila ya kuingiliwa na serikali;
4. Serikali kuratibu uchumi ila inapinga serikali kukwaza uhuru wa biashara na ushindani;

Ningependa kusikia mawazo yako kuhusu jinsi masuala haya yanaweza kutuletea sera zenye tija kwa maisha ya watanzania waliopo vijijini – hasa tukitilia maanani the failures nilizojadili awali i.e. COLONIAL STATE FAILURE, STATE FAILURE (Ujamaa), MARKET FAILURE;

c) Hoya kuhusu utamaduni wa kisiasa
Kimsingi nakubaliana na hoja zako, ila kama nilivyosema awali, ni vigumu to determine suala hili litakuja ‘play out' vipi katika siasa za 2015;
 
Last edited by a moderator:
Sasa hapa tunapata changamoto moja:
Je, ni kweli wananchi wa mijini wana utayari wa kushiriki siasa kikamilifu?

Mkuu ni percentage ndogo sana ya watanzania wana mwamko wa kisiasa. Kwa Tanzania naweza kusema ni Zanzniabr tu ambako naona wao wanapolitical awareness kubwa kiasi. Mkuu ukitaka kujua naweza kukupa mfano mmoja. Kuna mbunge mmoja alipopata ubunge hakuwenda jimboni kwake kwa muda mrefu mpaka wapiga kure wakamuuliza vipi? alichojibu ni kuwa si mlikula pilau mnataka nini tena? (sina hakika kama ni Kitwana Kondo alipokuwa mbunge wa Kigamboni)

Wenzetu marekani hatuwezi kujilinganisha nao, wao siasa si kama ni uchaguzi wa rais tu au masenetal, ukienda kwenye town halls ndio utajua hasa jinsi wanavyoperticipate kwenye siasa za mambo yanayowahusu.

Huku Tanzania, unaweza kuwa mbunge ukaendelea kuchaguliwa kwa kuwapa watu lift tu wakasema wewe ni mbunge mzuri. Wenzetu civic education iko juu sana, hata hapa Kenya au Nigeria kuna mwamko kiasi. NIgeria kwa mfano kama mbunge ukionekana kuwa ovyo unaitwa jimboni na kuvuliwa madaraka si kama hapa Tanzania, unaweza kuwa kilaza unaingia bungeni kupiga porojo tu kwa miaka mitano, wapiga kura hawana la kufanya.

Sasa hivi political awareness ya Tanzania inatokana na CDM ku sensitize issues na kujaribu kuwafikia watu kwa njia nyingi,lakini bado wengi hawajui itikadi, sera, mrengo na mengine mengi. Kwa hiyo ni wimbi tu linasaidia.
 
Chadema wakitaka mambo yawe mtiririko kama wakishika Dola, wahakikishe kuwa Bungeni kunakuwa angalau na nusu ya wabunge. Laiti cdm ingeshinda mwaka 2010, uongozi ungekuwa mgumu sana hasa katika suala zima la kupitisha bajeti na misuada. Mwisho wa siku cdm wangeonekana hawana uwezo kumbe mivutano ipo kwenye mihimili ya kitaifa
 
Chadema wakitaka mambo yawe mtiririko kama wakishika Dola, wahakikishe kuwa Bungeni kunakuwa angalau na nusu ya wabunge. Laiti cdm ingeshinda mwaka 2010, uongozi ungekuwa mgumu sana hasa katika suala zima la kupitisha bajeti na misuada. Mwisho wa siku cdm wangeonekana hawana uwezo kumbe mivutano ipo kwenye mihimili ya kitaifa

Ni dhahiri hili limekuwa lengo lao la muda mrefu lakini kufanikisha hilo sio kazi rahisi, na hata for 2015 hawataweza fikisha idadi hiyo ya wabunge ila watafanikiwa kukamata majimbo mengi zaidi; If I was CHADEMA, I would go for Quality ya wabunge wapya, sio Quantity ya wabunge wapya - tafuta vijana wa maana kama the likes of Mnyika na kuwasimamisha kwenye majimbo kadhaa, hasa yale yenye wakazi wengi, hasa kanda ya ziwa, dar-es-salaam na maeneo mengine machache; wakipata quality ya Mnyikas, Lissus and Zittos kama kumi hadi ishirini zaidi.

Mimi nadhani ni bora kuliko kuwa na just the quantity e.g. ya wabunge wapya 50-70 ambao hawajui kujenga hoja za ushawishi au kuchambua mambo na kubakia kutumika tu for 'walk outs' au voting purposes; I think kuna manufaa zaidi kwa umma kwa mfano kusikia/tazama on TV idadi kubwa ya wabunge (kihoja na kichambuzi) wenye uwezo wa mnyika and them wakipinga jambo fulani kwa maslahi ya taifa au kutetea jambo fulani kwa maslahi ya taifa, kuliko umma kusikia tu kwamba wabunge 100 wa CHADEMA wamepiga kura ya namna hii au they have walked out kwa sababu hii...; that's how i look at it, but i might be wrong....
 
Mkuu Mchambuzi, kuna kitu hujagusia ambacho nadhanni kingewasaidia CDM kuongezea uwezekano wa kuishinda ccm 2015. Sijui iwapo ni oversight au ulifikiri haiendani na context ya Bongo, ni juu ya Coalition ya opposition groups; hapa naagalia kujifunzia TEMPLATE waliyoitumia NARC Kenya kuing'oa KANU madarakani. Kabla ya 2002, walijaribu mwaka 1992 na 1997 lakini maara zote hawakuweza hadi walipokubali kuunganisha nguvu.

Hapa kwetu; pamoja na kwamba ccm iko mahututi, naona cdm bado wanaamini wataweza peke yao. Coalition pamoja na vyama kama cuf wenye nguvu visiwani na nccr huku bara inatosha kuhakikisha ushindi. Kumbuka, katika hili compromise ni muhimu la sivyo tutashuhudia baada ya 2015 watu wakiendelea kuitana ccm B.
 
Mkuu Mchambuzi, kuna kitu hujagusia ambacho nadhanni kingewasaidia CDM kuongezea uwezekano wa kuishinda ccm 2015. Coalition ya opposition groups; hapa naagalia kujifunzia TEMPLATE waliyoitumia NARC Kenya kuing'oa KANU madarakani. Kabla ya 2002, walijaribu mwaka 1992 na 1997 lakini maara zote hawakuweza hadi walipokubali kuunganisha nguvu.
Hapa kwetu; pamoja na kwamba ccm iko mahututi, naona cdm bado wanaamini wataweza peke yao. Coalition pamoja na vyama kama cuf wenye nguvu visiwani na nccr huku bara inatosha kuhakikisha ushindi. Kumbuka, katika hili compromise ni muhimu la sivyo tutashuhudia baada ya 2015 watu wakiendelea kuitana ccm B.

Ni kweli ila kwa dynamics za siasa zetu Tanzania, sioni such a thing happening na nadiriki kusema kwamba sio rahisi kwa Chadema kukubali kufanya hivyo, sana sana watajaribu kuwashawishi watanzania wenye mapenzi na vyama kama CUF, NCCR etc kukipigia kura Chadema 2015 lakini sio kuhimia muungano wa vyama vya siasa; Chadema has already burned the bridges, hawawezi kurudi nyuma na kutaka coalition government na vyama kama NCCR na CUF ambavyo wamekuwa wakivishutumu kuwa CCM B; tatizo lingine ni kwamba mpaka sasa sijasikia Chadema wakijaribu kupigania kanuni ya ushindi katika chaguzi kuu ibadilishwe kwani as we speak, CCM ikipata 50.1% na CDM 49.9%, mshindi atakuwa CCM, and i see chances ya hili kutokea ambapo inaweza pelekea CCM na Chadema kuunda serikali ya pamoja 2015, na kukiweka CDM katika nafasi ngumu sana kwani wamekuwa wakikebehi sana ndoa ya CCM na CUF Znz after 2010 elections;
 
Ni kweli ila kwa dynamics za siasa zetu Tanzania, sioni such a thing happening na nadiriki kusema kwamba sio rahisi kwa Chadema kukubali kufanya hivyo, sana sana watajaribu kuwashawishi watanzania wenye mapenzi na vyama kama CUF, NCCR etc kukipigia kura Chadema 2015 lakini sio kuhimia muungano wa vyama vya siasa; Chadema has already burned the bridges, hawawezi kurudi nyuma na kutaka coalition government na vyama kama NCCR na CUF ambavyo wamekuwa wakivishutumu kuwa CCM B; tatizo lingine ni kwamba mpaka sasa sijasikia Chadema wakijaribu kupigania kanuni ya ushindi katika chaguzi kuu ibadilishwe kwani as we speak, CCM ikipata 50.1% na CDM 49.9%, mshindi atakuwa CCM, and i see chances ya hili kutokea ambapo inaweza pelekea CCM na Chadema kuunda serikali ya pamoja 2015, na kukiweka CDM katika nafasi ngumu sana kwani wamekuwa wakikebehi sana ndoa ya CCM na CUF Znz after 2010 elections;

Mchambuzi,
Inaelekea Chadema wanajiamini kutokana na mvuto unaoonekana siku baada ya siku, kwani kuunganisha nguvu za vyama vingine vya upinzania kinachowatisha ni tofauti za kiitikadi na pia some political parties they just join for personal leadership interest.

Hoja nyingine ni hiyo uliyosema Mchambuzi kuhusu challenges ambazo CUF wamezipata kwa kuwa na serikali ya mseto, kwani mwenye % kubwa ndiye mwenye kauli, kwani Vice President kule visiwani ni image ndani ya serikali isiyokuwa na kauli, Utaona Vice President wa pili ndiye mwenye kuongoza serikali, mambo kama haya iwapo nafasi inakuruhusu bora kujenga mazingira ya kujiamini kujenga nguvu za kujitegemea.

Hilo linaeleweka kutokana na Chadema kutangaza dhamira ya wanaopenda kujiunga nao wapeleke barua za maombi yao kwa siri na kuonyesha majimbo wanayokusudia kugombea, ina maana anayetaka kujiunga na Chadema kutoka chama kingine ni ruksa, lakini si kuunganisha nguvu za vyama vyote.

Ideology ya Mbowe mara baada ya uchaguzi mkuu uliopita ilitoa uwazi zaidi kutokana na kusema makovu katika kipindi cha Uchaguzi mkuu, kwani ilionekana wazi vyama vingine vya upinzani Tanzania haviegemei kusaidia chama cha upinzani chenye nguvu, bali kuna kuwa na dalili fulani za wivu na hivi kuwa wapiga debe wa chama tawala.
 
Mchambuzi,
Inaelekea Chadema wanajiamini kutokana na mvuto unaoonekana siku baada ya siku, kwani kuunganisha nguvu za vyama vingine vya upinzania kinachowatisha ni tofauti za kiitikadi na pia some political parties they just join for personal leadership interest.

Hoja nyingine ni hiyo uliyosema Mchambuzi kuhusu challenges ambazo CUF wamezipata kwa kuwa na serikali ya mseto, kwani mwenye % kubwa ndiye mwenye kauli, kwani Vice President kule visiwani ni image ndani ya serikali isiyokuwa na kauli, Utaona Vice President wa pili ndiye mwenye kuongoza serikali, mambo kama haya iwapo nafasi inakuruhusu bora kujenga mazingira ya kujiamini kujenga nguvu za kujitegemea.

Hilo linaeleweka kutokana na Chadema kutangaza dhamira ya wanaopenda kujiunga nao wapeleke barua za maombi yao kwa siri na kuonyesha majimbo wanayokusudia kugombea, ina maana anayetaka kujiunga na Chadema kutoka chama kingine ni ruksa, lakini si kuunganisha nguvu za vyama vyote.

Ideology ya Mbowe mara baada ya uchaguzi mkuu uliopita ilitoa uwazi zaidi kutokana na kusema makovu katika kipindi cha Uchaguzi mkuu, kwani ilionekana wazi vyama vingine vya upinzani Tanzania haviegemei kusaidia chama cha upinzani chenye nguvu, bali kuna kuwa na dalili fulani za wivu na hivi kuwa wapiga debe wa chama tawala.

tatizo linakuja hapo kujiamini kuwa wanaweza bila ya coalition, Wakati Raila na wenzake wanaungana na Mzee Kibaki 2002, walikuwa na mtaji wa wabunge wa majimbo zaidi ya 100 lakini bado waliungana ndipo makaitoa kanu, jamaa wa cdm hawa idadi ndogo huo ujasiri wa kuendelea bila wengine sana sana u itawanufaisha ccm.
 
nMkuu Mchambuzi,
Nashukuru sana kwa majibu yako kuhusu hoja zilizoibuliwa na wanajamvi wenzangu pamoja na zile zangu.
Ni matumaini yangu kuwa mjadala huu umekuwa na utakuwa faida kwa watu wanaotamani kujua.Ni matumaini yangu vile vile Wakuu wa vyama husika watafanyia kazi yaliyojadiliwa na yatakayojadiliwa huko mbele ya safari maana wengine tunapata tulizo la moyo na nafsi kwa kujadili masuala ya aina hii.Hatimaye, wataona umuhimu wa kuendesha siasa za kistaarabu na za hoja mwaka 2015.Wafuatiliaji wa uzi huu watakubaliana nasi kuwa tumeweka nguvu kubwa kujadili masuala badala ya watu binafsi.Naweza kutamka kuwa huu ni mjadala mzito sana niliopata kushiriki tangu nijiunge rasmi na kuwa mwanachama wa JF,January 2012. Moja ya faida za kushiriki mijadala ya aina hii ni kujenga hulka ya kujisomea na kusaka maarifa.Haiwezekani hata kidogo kushiriki mjadala kama huu bila kufanya maandalizi.

Nieleze kwa dhati kabisa kuwa nimeridhika kwa kiasi kikubwa na majibu ya hoja zangu nilizozielekeza kwako.Kama ulivyoshauri,kuhusu hoja yako ya awali kuwa''CCM inataka kuonekana ndicho kinamiliki Mageuzi ya kisissa nchini''sasa ni wakati wa viongozi wa CHADEMA kuchukua hatua za makusudi kufafanua historia ya Vyama vya Vingi vya Siasa nchini ili kujenga uelewa sahihi kwa wapiga kura watarajiwa na kuepusha upotoshaji wa CCM.Ninataka kuamini CHADEMA inaweza kutumia fursa ya Operesheni ya M4C ya sasa kuelimisha umma kufanikisha hilo.Vile vile pamoja na mambo mengine ifafanua falsafa,itikadi, sera ,imani, mikakati ya chama kwa Wananchi.Wakifanya hivyo,watakuwa wamejenga mtaji juu ya mwamba imara ambao porojo za CCM hazitaweza kuubomoa.

Kimsingi tumekubaliana katika maeneo karibu yote.Eneo lililobaki ni ''relevance ya Itikadi ya Ujamaa kwa wananchi waishio vijijini''katika mazingira ya sasa.Msingi wa hoja hii ni Itikadi ya chama.
Ninaamini ili kuweza kuja na sera na mikakati sahihi na thabiti kuhusu wakazi wa vijijini ni vyema CHADEMA,kupitia Kurugenzi yake ya Sera & Utafiti ifanye utafiti kuhusu mafanikio yliyopatikana na matatizo yanakabili maeneo ya vijijini.Pia chama kijiulize kwa nini pamoja mipango,sera,programu na mikakati kadhaa iliyowahi kubuniwa na kutekelezwa bado hatujashuhudia maendeleo yaliyotarajiwa! Wakati tunangoja matokeo ya utafiti,(kama wakuu wa chama wataona ni muhimu) bado tunaweza kuendeleza mjadala tukitumia uwezo wetu wa kutafuta,kuchakata na kuchambua vyanzo vya maarifa na taarifa.
Mtazamo wangu kuhusu namna bora ya kuwakomboa wananchi wa vijijini kutoka katika lindi la umaskini unabaki ule ule.
Kwamba lazima kuwe na sera,mipango,programu na mikakati shirikishi,inayochochea mapinduzi ya kweli ya kilimo tena kilimo cha kisasa na cha kibiashara,kinachotumia ardhi kubwa na teknolojia ya kisasa na lengo likiwa ni kuchozalisha ziada ya kuuzwa ng'ambo.Ili hili litokee ni sharti ,kilimo-kama nilivyojadili katika bandiko langa la awali-kifanywe na watu wachache na wenye mitaji.Kisha lile kundi linaoacha kilimo kwa kukosa ardhi na kushindwa kuhimili ushindani,liende mijini kufanya kazi zinazozalisha.Kwa sasa wananchi wa vijijini hawazalishi na wanaishi maisha magumu.Wanatazamia kupata ahueni kwa kuhamia mijjini! Mijini hakuna uzalishaji /wazalishaji wa kutosha na vijijini pia hakuna uzalishaji /wazalishaji.Nguvu kazi kubwa haitumiki.Hapo ndipo tulipokwama.Matokeo ya uwekezaji katika kilimo ni uboreshaji wa maisha ya wakazi wa vijijini na mijini.Na kilimo, kama ulivyoonyesha, kitaleta mabadiliko ya viwanda.Viwanda vitaboresha maisha ya wakazi wa mijini.Na maisha ya maendeleo ya miji yatahamasisha maendeleo ya vijijini.Miji na vijiji vinategemeana sana.Ile ''idle labour'' itageuzwa kirahisi kuwa a working labour.

Siasa ni sayansi.Ni sayansi kwa kuwa inaendeshwa kwa kuzingitia misingi na kanuni ya kisayansi.Na moja ya misingi hiyo ni uendeshaji wa tafiti zinazoibua kweli(facts) kadha wa kadha.Ninaamini kuwa tafiti nyingi zimekwisha kufanywa na wanataluma na wakuu wa CHADEMA wanalazimika kuzitumia tafiti hizo katika kufikia maamuzi kuhusu maendeleo vijijini.Wakati tukingoja matokeo ya tafiti zao ,tutaweka bidii kuendesha mijadala hadi tuweze kupata jawabu sahihi na mwafaka.Tutaendelea kutoa maoni yetu kwa kuzingatia dainamiksi za kijamii,kisiasa, kiuchumi na kiutamaduni.

Moja ya maoni yangu ni kuwa,ikiwa CHADEMA itakamata dola 2015,na kufanya jitihada kuwezesha mapinduzi katika sekta ya kilimo na viwanda nchini sina shaka kabisa itakuwa imetekeleza itikadi yake ya Uliberali Mrengo wa Kati.Kivipi?Serikali yake itakuwa imejenga viwanda,itaweka mazingira mwafaka/wezeshi kwa sekta binafsi kuwekeza kiviwanda kitalinda bei ya wakulima na kuwawezesha kimitaji kitaasisi,kisera ,kimfumo na kiteknolojia.Ni rahisi as that ingawa itachukua muda kuweza kuzaa matunda yanayotarajiwa.

Hoja za Bongolander nimezipokea.Nimemshauri,tangu awali atumie muda asome kitabu cha ''Who Vote in Tanzania and Why'' cha Maliyamkono.Humo kuna majibu ya maswali yake.
 
FortJeasus,

Nashukuru sana kwa mchango wako, lakini hasa jitihada zako za kuendeleza mjadala huu muhimu kwani manufaa yake ni kwa taifa kuliko vyama vya siasa kwani hakika nchi yetu inatangulia kwanza, na siasa huja baadae;

Kwanza nianze na hoja yako pale unapozungumzia suala la mapinduzi ya kilimo yatakayopelekea mapinduzi ya viwanda na kuonya kwamba shughuli hii itachukua muda mrefu kukamilika; Upo sahihi kuhusu suala la muda na nimekuwa naonya sana Chadema kulifanyia kazi suala hili la muda ili wananchi wasiwe na matarajio ya kuona mabadiliko ndani ya muda mfupi kwani kilichopo vichwani mwa wananchi wengi hasa vijana ni kwamba CCM lazima iondoke ili waanze kupata neema; ni muhimu Chadema kuwaelimisha kwamba wao (vijana) ndio nguzo muhimu katika kufanikisha mabadiliko hayo kwenye sanduku la kura 2015 lakini wasitegemee kuona matunda ya mabadiliko hayo mpaka pengine uzeeni au wakifikia umri wa kati; ni muhimu kwa chadema kuelezea umma huu ni mambo gani yatakayo badilika:


  • Ndani ya kipindi kifupi (e.g. 3 - 5 years);
  • yepi ndani ya kipindi cha muda wa kati (e.g. 5 - 10 years) ; na
  • yepi itachukua muda mrefu pengine kuja shuhudiwa na watoto wao au wajukuu zao (e.g. 10 to 25 years);
​
Iwapo huwa unafuatilia siasa za wenzetu waliotutangulia kiuchumi, kidemokrasia n.k, unasikia jinsi gani viongozi wa nchi hizi wanavyo lay out mikakati yao ya muda mrefu; ni kawaida kumsikia Rais Bush (enzi zake), Obama, hata viongozi wa nchi kama Brazil, South Korea n.k wakizungumzia mikakati ya muda mrefu, hata miaka 30 ijayo na wananchi kuvutiwa nayo;

Kuhusu suala la M4C, kama nilivyosema elsewhere, itakuwa jambo la busara kwa Chadema kugeuza M4C kuwa a fact finding mission kama ziara ya Mwalimu mwaka 1962 alipojiuzulu siasa na kuamua kwenda vijijini kwa muda mrefu sana kufanya utafiti juu ya nini ni matumaini, matarajio na shauku za watanzania wengi; ni baada ya safari hii ndio akaja na Azimio La Arusha lililozaa Ujamaa; Ni muhimu sana kwa Chadema kugeuza M4C kuwa ziara ya namna hii au ku attach watu kadhaa ndani ya M4C kufanya kazi hii kwani amsha amsha ya wanavijiji juu ya umuhimu wa mabadiliko itakuwa haina maana kama Chadema watakuwa ndio wenye maamuzi juu ya nini ni matumaini, shauku na matarajio ya wananchi; ni muhimu sana kuwapa wananchi nafasi watoe shauku zao ili hapo baadae Chadema ikija na mipango yake ya maendeleo, basi iende sambamba na matakwa ya walio wengi - hii ni dhana ya bottom - up approach to development vis a vis top - down approach; Nashawishika kusema kwamba ndugu zetu vijijini hakika wana issues zinazowakabili na wanazohitaji zifanyiwe kazi lakini issues hizi wanaziweka katika makundi ya urgent and important; tusiwaamulie na tusiwapangie masuala yepi kwao ni urgent na yepi ni important kwao bali tuwasikilize wao katika hilo;

Kuhusu itikadi, lazima itikadi ya chama iakisi reality iliyopo kwenye jamii; kama ni uliberali, basi iakisi (reflect)social reality iliyopo, kama ni ujamaa, pia iakisi social reality iliyopo; sasa hapa ni suala la ushindani baina ya CCM na CDM juu ya ubora wa itikadi zao, hasa jinsi gani wanadhani zinaweza kuzaa sera ambazo zitasaidia kutatua matatizo ya wananchi walio wengi; ushindani wa kisiasa uelekezwe huko, sio kwenye masuala ya sijui Dr. Slaa katekeleza mke, sijui kiongozi gani wa CCM kafanya hivi; tuache siasa za kwenda kusemeana kwa wananchi na badala yake tuendeshae siasa za kwenda kuuza itikadi zetu, sera zetu, mikakati yetu kwa wananchi;

Mimi bado nina amini kwamba majibu juu ya matatizo mengi ya wananchi vijijini na maskini kwa ujumla yapo katika itikadi ya ujamaa, lakini sio ujamaa ule wa enzi za TANu bali ujamaa ambao utafanyiwa marekebisho, hasa ujamaa wa kidemokrasia i.e social democracy; Itikadi hii ina akisi social reality iliyopo vijijini na hata miongoni mwa wakazi wengi wa mijini (maskini) lakini pia inatambua umuhimu wa soko/soko huria katika uchumi, lakini muhimu zaidi inakemea mapungufu ya soko huria huku ikiwalinda maskini dhidi ya Marketization, Privatization and Liberalization, kuliko ilivyo hivi sasa chini ya uliberali; Vinginevyo itikadi ya Uliberali haitaki urafiki wa aina yoyote baina yake na maskini wa mijini na vijijini, urafiki wake na kundi hili ni pale tu wanapokuwa na uwezo wa kifedha/purchasing power, huku ikifanya jitiada ndogo sana kujenga hiyo purchasing power; tumekuwa na uliberali kwa miaka zaidi ya 25 sasa na hatujaona lolote la maana on that end;

Binafsi sioni jinsi gani uliberali per se utamsaidia mwanakijiji na maskini kwa ujumla, lakini ningependa kusikia zaidi kutoka kwako juu ya hili; Je ni wapi uliberali umesaidia maskini katika dunia ya tatu? iwe mrengo wa kati, kulia au kushoto?
 
Hao ni CDM wazee wa kucheza na maneno, CCM ikishinda Mbowe atasema alimaanisha uchaguzi wa ubunge wa Hai!!!
Slaa si alisema hagombei Urais 2015 kwa sababu atakuwa mzee, lakini sasa tayari swala la uzee halipo anajiandaa kwa kinyang'anyiro!
hivi kuna wanaoongoza kubadili maneno kama viongozi wa ccm? nitajie mmoja tu ambaye hajawahi kubadili maneno, si kwenye kujenga barabara, kukanusha ufisadi, majibu bungeni, mikutano ya hadhara nk

Anyway; hoja yako nyepesi na si ajabu ulidhani uko jukwaa la habari mchanganyiko, maana kule uko fit

Mchambuzi, umeiweka vyema, Boss umekosoa vyema...

Lakini je; Utayari unatokana na kauli tu??/
utayari unatokana na siasa tu?
utayari unaazia wapi??

nauliza haya kwani nimeona (naweza kuwa nimekosea sana, samahani) chadema imejikita kwenye kilekile kilichoidhoofisha ccm, nacho ni siasa. sioni jitihada za kweli za kujenga au kuandaa mipango imara ya kiuchumi, kisayansi, huduma za jamii kwa ujumla wala kuweka mbele champions vijana au wazee watakoongoza kuinua uchumi, we need to start knowing htem now!!! tujue wapi tunaweza kuchangia japo kidogo kusukuma mbele; tunataka sasa kuanza kusikia wataalam wa uchumi wa chadema ni hawa, na hii ndio philosophy yao, sio zitto kusoma hotuba ya bajeti mbadala, maana hiyo ndio inafanya baadhi ya wanasias kudhani kwa kusoma bajeti tu, basi wewe ni guru wa eneo husika, la ahsha

niliwahi mwambia haya zitto, mkumbo, na vijana wao wengi sana.... kwamba sioni base ya nguvu ya professsional wing, naona saisa nyingi sana, mwisho zitakua za kupachikana kwani kutakua na kukosa maandalizi ya muda mrefu, vetting nk.

rafiki yangu mmoja (member humu) alikiambia, majority ya technocrats wataoka ccm kuendesha serikali chadema ikishinda, nikashika kichwa, nikashushia bia, na kwenda kulala ---kwani nilipata jibu jepesi kwenye swali zito, yaani jamaa ameshapumzika kwamba tukishinda kisiasa, tunabeba wachezaji wa timu ya ccm na maisha yanaendelea. sisemi hilo ni kosa, lakini sioni kama tutakua tunabadilika... we need a mix of things

yawezekana sijajua undani wa tactics za chadema, lakini general strategies need to come out now, we only have 3 years sasa kama hadi badi miezi 24 wataalam wa uchumi na mbinu zinakua siri, sijui utaziuzaje na kuzidefend vipi in 12 months or so
 
hivi kuna wanaoongoza kubadili maneno kama viongozi wa ccm? nitajie mmoja tu ambaye hajawahi kubadili maneno, si kwenye kujenga barabara, kukanusha ufisadi, majibu bungeni, mikutano ya hadhara nk

Anyway; hoja yako nyepesi na si ajabu ulidhani uko jukwaa la habari mchanganyiko, maana kule uko fit

Mchambuzi, umeiweka vyema, Boss umekosoa vyema...

Lakini je; Utayari unatokana na kauli tu??/
utayari unatokana na siasa tu?
utayari unaazia wapi??

nauliza haya kwani nimeona (naweza kuwa nimekosea sana, samahani) chadema imejikita kwenye kilekile kilichoidhoofisha ccm, nacho ni siasa. sioni jitihada za kweli za kujenga au kuandaa mipango imara ya kiuchumi, kisayansi, huduma za jamii kwa ujumla wala kuweka mbele champions vijana au wazee watakoongoza kuinua uchumi, we need to start knowing htem now!!! tujue wapi tunaweza kuchangia japo kidogo kusukuma mbele; tunataka sasa kuanza kusikia wataalam wa uchumi wa chadema ni hawa, na hii ndio philosophy yao, sio zitto kusoma hotuba ya bajeti mbadala, maana hiyo ndio inafanya baadhi ya wanasias kudhani kwa kusoma bajeti tu, basi wewe ni guru wa eneo husika, la ahsha

niliwahi mwambia haya zitto, mkumbo, na vijana wao wengi sana.... kwamba sioni base ya nguvu ya professsional wing, naona saisa nyingi sana, mwisho zitakua za kupachikana kwani kutakua na kukosa maandalizi ya muda mrefu, vetting nk.

rafiki yangu mmoja (member humu) alikiambia, majority ya technocrats wataoka ccm kuendesha serikali chadema ikishinda, nikashika kichwa, nikashushia bia, na kwenda kulala ---kwani nilipata jibu jepesi kwenye swali zito, yaani jamaa ameshapumzika kwamba tukishinda kisiasa, tunabeba wachezaji wa timu ya ccm na maisha yanaendelea. sisemi hilo ni kosa, lakini sioni kama tutakua tunabadilika... we need a mix of things

yawezekana sijajua undani wa tactics za chadema, lakini general strategies need to come out now, we only have 3 years sasa kama hadi badi miezi 24 wataalam wa uchumi na mbinu zinakua siri, sijui utaziuzaje na kuzidefend vipi in 12 months or so

Mkuu wakati mwingine tunawalenga sana individuals na kuvilenga sana vyama. Kuna wakati naamini kuwa weakness kubwa tuliyonayo haiko kwenye individuals iko kwenye systems na institution. Ninaposema hili maana yangu ni kuwa hatuna mfumo (haupo) unaoweza kufanya mambo hapa Tanzania yaende, na hatuna institutions zinazoweza kutekeleza mambo.

Ukiangalia hapa Tanzania unaweza kuona kama Rais mzuri mambo mengi yanaenda vizuri, na kama si mzuri mambo mengi yanaenda hovyo. Ukiangalia wizara ni hivyo hivyo, kama waziri ni mzuri wizara inaenda vizuri na kama waziri si mzuri wizara inaenda hovyo...fuata utaratibu huo hadi ngazi ya chini kabisa.

Jaribu kuuangalia suala la msongamano wa magari hapa Dar, msongamano unaendelea kuwepo tangu JK aingine madarakani hakuna kilichofanyika (zaidi ya mipango na hatua ndogo ambavyo havitekelezeki), Angalia baraza la mawaziri limefanya nini, wizara ya ujenzi imefanya nini, polisi wa usalama barabarani wamefanya nini. Zaidi ya maneno hakuna chochote significant kimefanyika.

Au jaribu kuangalia akikatwa mwizi haadi kufikishwa mahakamani kusimewa mashatki na keshi yake kutolewa huku, utaona kuwa kuna mambo mengi sana hapo katikati hayafanyiki na hata kama yanafanyika ni kwa mwendo wa chura na kwa ubabaishaji mwingi.

Angalia kati ya serikali kuu, bunge, mahakama , civil society na media. Karibu kila moja haifanyi kazi inayostahili na kwa ufanisi, serikali kuu haiko united as one institution na haijui priorities zake ni zipi, bunge nalo liko kwenye sura ya kamati ya CCM zaidi kuliko bunge, mahakama ndio usiseme haina sautikabisa wakati kisheria ndio inatakiwa kuwa na sauti, civil society ndio njaa tu wao ni kama watu wanaoganga njaa, hakuna issue ya maana ambayo wameweza kupush kwa interest ya Tanzania, sana sana wanapush mambo ambayo hayana umuhimu mkubwa kwa maendeleo ya Tanzania, media ndio kabisa....apart from hapa JF na gazeti moja au mawili, majority ya waandishi na watangazaji ni vilaza na vibonde, wamebaki kufanya kazi ya entertainment zaidi ya kuelimisha na kuongopea watu.

Kwa hiyo naweza kusema pamoja na kuwa tunsema chama hiki kina itikadi hiki hakina, au huyu ni mgombea mzuri au yule si mgombea mzuri...the bottom line ni kwamba ni lazima tuweze kuwa na instututions zinazokuwa imara bila kujali nani anakuja nani anatoka.

Civilized states zote zina idara zinazojua majukumu yake, na sio kufanya kazi za zimamoto kwa amri ya katibu mkuu, mkuu wa mkoa au mkuu wa wilaya. hata mkuu wa mkoa akifanya fyongo anachukuliwa hatua mwa mujibu wa rules na regulations zilizowekwa kwa taasisi ile kufanya kazi.
 
Back
Top Bottom