Mpaka Kieleweke
JF-Expert Member
- Feb 27, 2007
- 4,132
- 1,571
Lissu alimaanisha hiki;
Mheshimiwa Spika,
Tarehe 11 Machi 2011, Serikali ilichapisha Muswada wa Sheria ya Mapitio ya Katiba ya mwaka 2011 (The Constitutional Review Bill, 2011) katika Gazeti la Serikali la tarehe hiyo. Muswada huo uliletwa katika Mkutano wa Tatu wa Bunge hili tukufu kwa Hati ya Dharura. Hata hivyo, baada ya upinzani mkubwa dhidi ya Muswada huo kujitokeza karibu nchi nzima, Serikali ililazimika kuundoa katika ratiba ya shughuli za Bunge kwa maelezo kwamba itaufanyia marekebisho na kuurudisha Bungeni katika Mkutano huu wa Bunge. Hata hivyo, licha ya Muswada huo kuwepo katika ratiba ya awali ya shughuli za Bunge, baadae ratiba hiyo ilifanyiwa mabadiliko kwa kuuondoa Muswada kwenye ratiba hiyo.
Mheshimiwa Spika,
Dana dana yote hii inaonyesha jinsi suala la utaratibu wa namna ya kupata Katiba mpya kwa ajili ya nchi yetu lilivyo muhimu. Tofauti na kauli za awali za Serikali, Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni inaamini kwamba sheria inayoweka utaratibu wa kupatikana kwa Katiba mpya ina umuhimu mkubwa wa karibu sawa na Katiba yenyewe. Utaratibu wa kidemokrasia, shirikishi wa makundi makuu ya kijamii na ulio wazi utapelekea nchi yetu kuwa na Katiba mpya ambayo sisi wote tutaweza kujivunia. Kwa upande mwingine, utaratibu uliojaa ukiritimba wa kirasimu, unaohodhiwa na watu au taasisi chache na unaofanyika gizani na/au kwa siri utaleta Katiba mpya kwa jina tu. Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni inaamini kwamba katika hali ya sasa ya kisiasa ya nchi yetu, utaratibu huu hauwezi kukubalika na wananchi walio wengi na utasababisha machafuko makubwa ya kisiasa na kijamii.
Kwa bahati mbaya, Mheshimiwa Spika, Serikali inaelekea kufikiri kwamba inaweza kuwalazimisha Watanzania kukubali utaratibu wa aina hiyo. Hii ni kwa sababu Kambi Rasmi ya Upinzani imepata nakala ya Rasimu ya Muswada wa Sheria ya Mapitio ya Katiba, 2011 iliyofanyiwa marekebisho ambayo inatazamiwa kuletwa Bungeni kwa tarehe ambayo haijulikani bado. Rasimu ya Muswada huu inathibitisha kwamba Serikali haina nia yoyote ya kuweka utaratibu wa kidemokrasia, ulio shirikishi wa makundi makuu ya kijamii na kisiasa katika kupata Katiba Mpya. Kwa upande mwingine, Rasimu inapendekeza utaratibu wa kupata Katiba Mpya uliojaa urasimu na unaoendeleza hodhi ya Urais wa Kifalme ambayo ndiyo imekuwa hulka kuu ya mfumo wetu wa kikatiba na kisiasa.
Mheshimiwa Spika,
Rasimu ya Muswada inapendekeza kumpa mamlaka makubwa Rais wa Jamhuri ya Muungano kwa mashauriano na/au makubaliano na Rais wa Zanzibar ya kuteua Tume ya Kupitia Katiba yenye wajumbe wasiozidi thelathini. Aidha, Rasimu ya Muswada inapendekeza kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano kwa mashauriano na/au makubaliano na Rais wa Zanzibar ataipatia Tume hiyo hadidu za rejea na muda wa kumaliza kazi yake na kuwasilisha taarifa. Utaratibu huo huo wa mashauriano na makubaliano utatumika katika uteuzi wa Katibu wa Tume; na Sekretariati ya Tume ambayo itateuliwa na Waziri wa Katiba na Sheria kwa makubaliano na Waziri mwenzake wa Zanzibar. Katibu na wajumbe wa Sekretariati wanatakiwa kuwa watumishi wa umma ambao, hata kwa mujibu wa utaratibu wa sasa wa kikatiba, wanawajibika kwa Rais.
Mheshimiwa Spika,
Rasimu ya Muswada wa Sheria ya Mapitio ya Katiba inaendeleza pia mfumo wa Urais wa Kifalme kwa mapendekezo juu ya uwasilishaji wa taarifa ya Tume. Hapa inapendekezwa kwamba Tume ya Mapitio ya Katiba itawasilisha taarifa yake kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano na Rais wa Zanzibar. Aidha, "baada ya mashauriano na makubaliano na Rais wa Zanzibar na baada ya kumalizika kwa taratibu za ndani zinazohusu utungaji wa sera, Rais atamwelekeza Waziri kuwasilisha Muswada wa Katiba katika Bunge la Katiba kwa ajili ya kupitishwa kwa vifungu vya Katiba." Pendekezo hili ni la hatari kubwa. Kwanza, ‘kumalizika kwa taratibu za ndani zinazohusu utungaji wa sera' maana yake ni kwamba mpaka Baraza la Mawaziri liridhie Muswada huo ndio utapelekwa kwenye Bunge la Katiba! Kwa mujibu wa Katiba, wajumbe wote wa Baraza la Mawaziri ni wateuliwa wa Rais.
Mheshimiwa Spika,
Mfumo wa Urais wa Kifalme pia unaonekana katika mapendekezo yanayohusu Baraza la Katiba. Kwa mujibu wa kifungu cha 20 cha Rasimu ya Muswada, Rais – kwa makubaliano na Rais wa Zanzibar – na baada ya kushauriwa na Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano na yule wa Zanzibar ataunda Baraza la Katiba na kuteua wajumbe wake. Baada ya kuundwa, Baraza la Katiba litateua Spika na Naibu Spika ambao watatakiwa kutoka katika sehemu tofauti za Jamhuri ya Muungano. Spika na Naibu Spika watatakiwa kula kiapo mbele ya Makatibu wa Baraza la Katiba ambao ni Katibu wa Bunge wa sasa na Katibu wa Baraza la Wawakilishi la Zanzibar wa sasa. Wote hawa, kwa mujibu wa Katiba na Katiba ya Zanzibar ya 1984, ni wateuliwa wa Rais na/au wa Rais wa Zanzibar na wanatakiwa kula kiapo kwa Rais!
Mheshimiwa Spika, Rasimu ya Muswada wa Sheria ya Mapitio ya Katiba inapendekeza kwamba kazi ya Baraza la Katiba iwe moja tu: kutunga Katiba Mpya na mambo yanayohusiana nayo. Baada ya kufanya kazi hiyo, Baraza litakuwa limejifuta lenyewe, ijapokuwa kujifuta huko kwa Baraza hakutamzuia Rais kuliunda upya Baraza siku za baadae likiwa na wajumbe wale wale kwa lengo la kufanya mabadiliko ya Rasimu ya Katiba Mpya kabla Rasimu hiyo haijapitishwa! Rasimu inapendekeza kwamba ili Katiba Mpya ipitishwe ni lazima ipate ridhaa ya theluthi mbili ya wajumbe wote wanaotoka Tanzania Bara na idadi hiyo hiyo ya wajumbe wanaotoka Tanzania Zanzibar.
Mheshimiwa Spika, Rasimu ya Muswada wa Sheria ya Mapitio ya Katiba inapendekeza pia kwamba Katiba Mpya ipatiwe nguvu na uhalali wa kisheria kwa kupitia kura ya maoni itakayoratibiwa na kusimamiwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi kwa kushirikiana na Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar. Tume hizi mbili – kwa mashauriano na Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano na Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar - ndizo zitakazotengeneza swali litakaloulizwa kwenye kura ya maoni. Utaratibu utakaotumika katika kura ya maoni ni ule unaotumika katika chaguzi za kawaida katika nchi yetu, yaani Sheria ya Uchaguzi wa Taifa, Sura ya 343, Sheria ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa, Sura ya 292 na Sheria ya Uchaguzi ya Zanzibar, 1984. Ijapokuwa kura ya maoni itaamuliwa kwa wingi wa wapiga kura (simple majority), Rasimu ya Muswada inapendekeza kwamba ili kura hiyo iwe halali ni lazima angalau 65% ya wapiga kura wote waliojiandikisha Tanzania Bara na Tanzania Zanzibar washiriki katika kupiga kura. Rasimu ya Muswada inapendekeza kwamba Rais ndiye atakayeamua, kwa namna atakavyoona inafaa, kuanza kutumika kwa Katiba Mpya!
Mheshimiwa Spika, Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni inaitaka Serikali kutoa kauli rasmi kama Rasimu ya Muswada wa Sheria ya Mapitio ya Katiba ndio inawakilisha msimamo wa Serikali juu ya mchakato wa kutungwa kwa Katiba Mpya. Kama ni hivyo, basi Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni inapenda kuweka wazi msimamo wake Muswada huu haukubaliki hata kidogo. Kwanza, Kambi Rasmi ya Upinzani haikubaliani na mamlaka makubwa yanayopendekezwa kupewa Rais wa Jamhuri ya Muungano na Rais wa Zanzibar chini ya Muswada huu. Urais wa Kifalme kama kanuni kuu ya kikatiba na kisiasa ndiyo ambayo imetufikisha hapa tulipo leo: taifa lenye wananchi maskini, lililojaa ufisadi, lisilojali demokrasia na haki za binadamu na lenye kuongozwa na watawala wasiowajibika kwa wananchi au kwa vyombo vya uwakilishi vya wananchi. Mfumo huu hauwezi kutumika tena kulipatia taifa letu Katiba Mpya ya kidemokrasia itakayokidhi mahitaji ya karne hii na nyingine zijazo.
Pili, Mheshimiwa Spika, mapendekezo ya Rasimu ya Muswada hayakubaliki kwa sababu yanaweka mchakato wa Katiba Mpya kwenye huruma na/au fadhila ya Rais wa Zanzibar na siasa za Zanzibar kwa ujumla. Kwa mapendekezo haya, Rais wa Zanzibar asipokubaliana na jambo lolote linalohitaji ridhaa yake basi mchakato mzima utasimama au kusitishwa. Aidha, endapo katika kura ya maoni inayopendekezwa, theluthi mbili ya Wazanzibari hawatakubaliana na Katiba Mpya basi Katiba hiyo haitapitishwa hata kama inakubaliwa kwa kiasi kikubwa na wananchi wa Tanzania Bara. Mustakbala wa taifa letu hauwezi kuwekwa tena rehani kwenye siasa za Zanzibar na kwenye matakwa ya Wazanzibari kwa kiasi hicho. Kuhusiana na jambo hili, Kambi Rasmi ya Upinzani inapendekeza kwamba Rais wa Zanzibar ahusishwe tu katika masuala ya kikatiba ambayo ni ya Muungano tu. Nje ya masuala hayo, Rais wa Zanzibar hana sababu yoyote ya kuhusishwa na mchakato wa kikatiba unaohusu mambo ya Tanzania Bara.
Aidha, wajumbe wa Tume ya Mapitio ya Katiba ambao watatoka Zanzibar wahusike tu katika mchakato wa masuala ya kikatiba ambayo ni ya Muungano tu. Vile vile, Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni inapendekeza wananchi wa Zanzibar washiriki katika kura ya maoni inayohusu mfumo mpya wa Muungano tu. Hii ndio kusema kwamba, kama vile ambavyo viongozi, wawakilishi na wananchi wa Tanzania Bara hawajashirikishwa katika mchakato wa kikatiba wa Zanzibar kwa sababu ulihusu mambo yasiyokuwa ya Muungano, vivyo hivyo viongozi, wawakilishi na wananchi wa Zanzibar wasishiriki katika mchakato wa kikatiba wa mambo yasiyokuwa ya kikatiba kwa upande wa Tanzania Bara.
Mheshimiwa Spika, Kwa kuzingatia historia halisi ya Muungano wetu, Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni inaamini kwamba wakati umefika kwa wananchi wa Tanzania Bara na Tanzania Zanzibar kuamua - kwa mara ya kwanza katika historia yetu na kwa uhuru kabisa - kama wanataka kuendelea kuwa na Muungano na wa aina gani. Hili halijawahi kufanyika na ndio maana Muungano umeendelea kuwa kero kwa wananchi wengi wa nchi hizi mbili. Kambi Rasmi ya Upinzani inaamini kwamba suala la ridhaa ya wananchi ni la umuhimu mkubwa na ni lazima lishughulikiwe kwanza kabla ya mchakato unaopendekezwa na Rasimu ya Muswada wa Sheria ya Mapitio ya Katiba kuanza na/au kupitishwa.
Aidha, kwa kuzingatia historia yetu halisi ya kikatiba na kisiasa, Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni inapendekeza mfumo mpya wa kutunga Katiba Mpya ambao hautatawaliwa na kivuli kirefu cha Urais wa Kifalme. Kikubwa hapa ni kwamba, badala ya wajumbe wa Tume ya Katiba kuteuliwa na Rais kama inavyopendekezwa na Rasimu ya Muswada, wajumbe hao wateuliwe kutokana na mapendekezo ya vyama vya siasa, hasa hasa vile ambavyo vina uwakilishi Bungeni, taasisi zisizokuwa za kiserikali na za kitaaluma, makundi maalum ya kijamii pamoja na Serikali yenyewe. Aidha, badala ya Sekretariati ya Tume kujazwa warasimu wa Serikali ambao ni wateuliwa wa Rais kama inavyopendekezwa, Sekretariati hiyo itokane na wajumbe watakaoteuliwa na Tume yenyewe na ambao watawajibika moja kwa moja kwa Tume yenyewe badala ya kuwajibika kwa Rais kama ilivyo sasa.
Mheshimiwa Spika, Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni haina imani, sio tu na Tume ya Taifa ya Uchaguzi, bali pia na mfumo mzima wa kisheria na kitaasisi unaoendesha chaguzi za nchi yetu. Mfumo huu na watendaji wake wameonyesha wazi kutokuwa huru na kutumiwa na Chama cha Mapinduzi kuchakachua matokeo ya chaguzi mbali mbali hapa nchini. Kwa maana hiyo, Tume ya Uchaguzi ya Taifa, na ile ya Zanzibar, haiwezi kuachiwa jukumu kubwa la kuendesha kura ya maoni kwa ajili ya kupata Katiba Mpya. Kambi Rasmi ya Upinzani inapendekeza kwamba Serikali ilete bungeni muswada wa mapendekezo ya mabadiliko ya Katiba na ya sheria husika za uchaguzi kwa lengo la kuiunda upya Tume ya Taifa ya Uchaguzi kwa lengo la kuhakikisha inasimamia zoezi la kura ya maoni kwa uhuru na bila upendeleo kwa chama tawala. Muswada huu vile vile utatoa fursa kwa Bunge hili tukufu kutunga vifungu vinavyowezesha Katiba Mpya kutungwa ambavyo havipo kwa Katiba ya sasa. Kutofanya marekebisho haya kutafanya sheria yoyote ya kuweka utaratibu wa kupata Katiba Mpya kuwa batili kwa kwenda kinyume na matakwa ya Katiba ya sasa ambayo hairuhusu Katiba Mpya kutungwa ila inaruhusu tu marekebisho ya Katiba yenyewe.
MCHAKATO WA KATIBA MPYA
Tarehe 11 Machi 2011, Serikali ilichapisha Muswada wa Sheria ya Mapitio ya Katiba ya mwaka 2011 (The Constitutional Review Bill, 2011) katika Gazeti la Serikali la tarehe hiyo. Muswada huo uliletwa katika Mkutano wa Tatu wa Bunge hili tukufu kwa Hati ya Dharura. Hata hivyo, baada ya upinzani mkubwa dhidi ya Muswada huo kujitokeza karibu nchi nzima, Serikali ililazimika kuundoa katika ratiba ya shughuli za Bunge kwa maelezo kwamba itaufanyia marekebisho na kuurudisha Bungeni katika Mkutano huu wa Bunge. Hata hivyo, licha ya Muswada huo kuwepo katika ratiba ya awali ya shughuli za Bunge, baadae ratiba hiyo ilifanyiwa mabadiliko kwa kuuondoa Muswada kwenye ratiba hiyo.
Mheshimiwa Spika,
Dana dana yote hii inaonyesha jinsi suala la utaratibu wa namna ya kupata Katiba mpya kwa ajili ya nchi yetu lilivyo muhimu. Tofauti na kauli za awali za Serikali, Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni inaamini kwamba sheria inayoweka utaratibu wa kupatikana kwa Katiba mpya ina umuhimu mkubwa wa karibu sawa na Katiba yenyewe. Utaratibu wa kidemokrasia, shirikishi wa makundi makuu ya kijamii na ulio wazi utapelekea nchi yetu kuwa na Katiba mpya ambayo sisi wote tutaweza kujivunia. Kwa upande mwingine, utaratibu uliojaa ukiritimba wa kirasimu, unaohodhiwa na watu au taasisi chache na unaofanyika gizani na/au kwa siri utaleta Katiba mpya kwa jina tu. Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni inaamini kwamba katika hali ya sasa ya kisiasa ya nchi yetu, utaratibu huu hauwezi kukubalika na wananchi walio wengi na utasababisha machafuko makubwa ya kisiasa na kijamii.
Kwa bahati mbaya, Mheshimiwa Spika, Serikali inaelekea kufikiri kwamba inaweza kuwalazimisha Watanzania kukubali utaratibu wa aina hiyo. Hii ni kwa sababu Kambi Rasmi ya Upinzani imepata nakala ya Rasimu ya Muswada wa Sheria ya Mapitio ya Katiba, 2011 iliyofanyiwa marekebisho ambayo inatazamiwa kuletwa Bungeni kwa tarehe ambayo haijulikani bado. Rasimu ya Muswada huu inathibitisha kwamba Serikali haina nia yoyote ya kuweka utaratibu wa kidemokrasia, ulio shirikishi wa makundi makuu ya kijamii na kisiasa katika kupata Katiba Mpya. Kwa upande mwingine, Rasimu inapendekeza utaratibu wa kupata Katiba Mpya uliojaa urasimu na unaoendeleza hodhi ya Urais wa Kifalme ambayo ndiyo imekuwa hulka kuu ya mfumo wetu wa kikatiba na kisiasa.
Mheshimiwa Spika,
Rasimu ya Muswada inapendekeza kumpa mamlaka makubwa Rais wa Jamhuri ya Muungano kwa mashauriano na/au makubaliano na Rais wa Zanzibar ya kuteua Tume ya Kupitia Katiba yenye wajumbe wasiozidi thelathini. Aidha, Rasimu ya Muswada inapendekeza kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano kwa mashauriano na/au makubaliano na Rais wa Zanzibar ataipatia Tume hiyo hadidu za rejea na muda wa kumaliza kazi yake na kuwasilisha taarifa. Utaratibu huo huo wa mashauriano na makubaliano utatumika katika uteuzi wa Katibu wa Tume; na Sekretariati ya Tume ambayo itateuliwa na Waziri wa Katiba na Sheria kwa makubaliano na Waziri mwenzake wa Zanzibar. Katibu na wajumbe wa Sekretariati wanatakiwa kuwa watumishi wa umma ambao, hata kwa mujibu wa utaratibu wa sasa wa kikatiba, wanawajibika kwa Rais.
Mheshimiwa Spika,
Rasimu ya Muswada wa Sheria ya Mapitio ya Katiba inaendeleza pia mfumo wa Urais wa Kifalme kwa mapendekezo juu ya uwasilishaji wa taarifa ya Tume. Hapa inapendekezwa kwamba Tume ya Mapitio ya Katiba itawasilisha taarifa yake kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano na Rais wa Zanzibar. Aidha, "baada ya mashauriano na makubaliano na Rais wa Zanzibar na baada ya kumalizika kwa taratibu za ndani zinazohusu utungaji wa sera, Rais atamwelekeza Waziri kuwasilisha Muswada wa Katiba katika Bunge la Katiba kwa ajili ya kupitishwa kwa vifungu vya Katiba." Pendekezo hili ni la hatari kubwa. Kwanza, ‘kumalizika kwa taratibu za ndani zinazohusu utungaji wa sera' maana yake ni kwamba mpaka Baraza la Mawaziri liridhie Muswada huo ndio utapelekwa kwenye Bunge la Katiba! Kwa mujibu wa Katiba, wajumbe wote wa Baraza la Mawaziri ni wateuliwa wa Rais.
Mheshimiwa Spika,
Mfumo wa Urais wa Kifalme pia unaonekana katika mapendekezo yanayohusu Baraza la Katiba. Kwa mujibu wa kifungu cha 20 cha Rasimu ya Muswada, Rais – kwa makubaliano na Rais wa Zanzibar – na baada ya kushauriwa na Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano na yule wa Zanzibar ataunda Baraza la Katiba na kuteua wajumbe wake. Baada ya kuundwa, Baraza la Katiba litateua Spika na Naibu Spika ambao watatakiwa kutoka katika sehemu tofauti za Jamhuri ya Muungano. Spika na Naibu Spika watatakiwa kula kiapo mbele ya Makatibu wa Baraza la Katiba ambao ni Katibu wa Bunge wa sasa na Katibu wa Baraza la Wawakilishi la Zanzibar wa sasa. Wote hawa, kwa mujibu wa Katiba na Katiba ya Zanzibar ya 1984, ni wateuliwa wa Rais na/au wa Rais wa Zanzibar na wanatakiwa kula kiapo kwa Rais!
Mheshimiwa Spika, Rasimu ya Muswada wa Sheria ya Mapitio ya Katiba inapendekeza kwamba kazi ya Baraza la Katiba iwe moja tu: kutunga Katiba Mpya na mambo yanayohusiana nayo. Baada ya kufanya kazi hiyo, Baraza litakuwa limejifuta lenyewe, ijapokuwa kujifuta huko kwa Baraza hakutamzuia Rais kuliunda upya Baraza siku za baadae likiwa na wajumbe wale wale kwa lengo la kufanya mabadiliko ya Rasimu ya Katiba Mpya kabla Rasimu hiyo haijapitishwa! Rasimu inapendekeza kwamba ili Katiba Mpya ipitishwe ni lazima ipate ridhaa ya theluthi mbili ya wajumbe wote wanaotoka Tanzania Bara na idadi hiyo hiyo ya wajumbe wanaotoka Tanzania Zanzibar.
Mheshimiwa Spika, Rasimu ya Muswada wa Sheria ya Mapitio ya Katiba inapendekeza pia kwamba Katiba Mpya ipatiwe nguvu na uhalali wa kisheria kwa kupitia kura ya maoni itakayoratibiwa na kusimamiwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi kwa kushirikiana na Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar. Tume hizi mbili – kwa mashauriano na Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano na Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar - ndizo zitakazotengeneza swali litakaloulizwa kwenye kura ya maoni. Utaratibu utakaotumika katika kura ya maoni ni ule unaotumika katika chaguzi za kawaida katika nchi yetu, yaani Sheria ya Uchaguzi wa Taifa, Sura ya 343, Sheria ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa, Sura ya 292 na Sheria ya Uchaguzi ya Zanzibar, 1984. Ijapokuwa kura ya maoni itaamuliwa kwa wingi wa wapiga kura (simple majority), Rasimu ya Muswada inapendekeza kwamba ili kura hiyo iwe halali ni lazima angalau 65% ya wapiga kura wote waliojiandikisha Tanzania Bara na Tanzania Zanzibar washiriki katika kupiga kura. Rasimu ya Muswada inapendekeza kwamba Rais ndiye atakayeamua, kwa namna atakavyoona inafaa, kuanza kutumika kwa Katiba Mpya!
Mheshimiwa Spika, Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni inaitaka Serikali kutoa kauli rasmi kama Rasimu ya Muswada wa Sheria ya Mapitio ya Katiba ndio inawakilisha msimamo wa Serikali juu ya mchakato wa kutungwa kwa Katiba Mpya. Kama ni hivyo, basi Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni inapenda kuweka wazi msimamo wake Muswada huu haukubaliki hata kidogo. Kwanza, Kambi Rasmi ya Upinzani haikubaliani na mamlaka makubwa yanayopendekezwa kupewa Rais wa Jamhuri ya Muungano na Rais wa Zanzibar chini ya Muswada huu. Urais wa Kifalme kama kanuni kuu ya kikatiba na kisiasa ndiyo ambayo imetufikisha hapa tulipo leo: taifa lenye wananchi maskini, lililojaa ufisadi, lisilojali demokrasia na haki za binadamu na lenye kuongozwa na watawala wasiowajibika kwa wananchi au kwa vyombo vya uwakilishi vya wananchi. Mfumo huu hauwezi kutumika tena kulipatia taifa letu Katiba Mpya ya kidemokrasia itakayokidhi mahitaji ya karne hii na nyingine zijazo.
Pili, Mheshimiwa Spika, mapendekezo ya Rasimu ya Muswada hayakubaliki kwa sababu yanaweka mchakato wa Katiba Mpya kwenye huruma na/au fadhila ya Rais wa Zanzibar na siasa za Zanzibar kwa ujumla. Kwa mapendekezo haya, Rais wa Zanzibar asipokubaliana na jambo lolote linalohitaji ridhaa yake basi mchakato mzima utasimama au kusitishwa. Aidha, endapo katika kura ya maoni inayopendekezwa, theluthi mbili ya Wazanzibari hawatakubaliana na Katiba Mpya basi Katiba hiyo haitapitishwa hata kama inakubaliwa kwa kiasi kikubwa na wananchi wa Tanzania Bara. Mustakbala wa taifa letu hauwezi kuwekwa tena rehani kwenye siasa za Zanzibar na kwenye matakwa ya Wazanzibari kwa kiasi hicho. Kuhusiana na jambo hili, Kambi Rasmi ya Upinzani inapendekeza kwamba Rais wa Zanzibar ahusishwe tu katika masuala ya kikatiba ambayo ni ya Muungano tu. Nje ya masuala hayo, Rais wa Zanzibar hana sababu yoyote ya kuhusishwa na mchakato wa kikatiba unaohusu mambo ya Tanzania Bara.
Aidha, wajumbe wa Tume ya Mapitio ya Katiba ambao watatoka Zanzibar wahusike tu katika mchakato wa masuala ya kikatiba ambayo ni ya Muungano tu. Vile vile, Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni inapendekeza wananchi wa Zanzibar washiriki katika kura ya maoni inayohusu mfumo mpya wa Muungano tu. Hii ndio kusema kwamba, kama vile ambavyo viongozi, wawakilishi na wananchi wa Tanzania Bara hawajashirikishwa katika mchakato wa kikatiba wa Zanzibar kwa sababu ulihusu mambo yasiyokuwa ya Muungano, vivyo hivyo viongozi, wawakilishi na wananchi wa Zanzibar wasishiriki katika mchakato wa kikatiba wa mambo yasiyokuwa ya kikatiba kwa upande wa Tanzania Bara.
Mheshimiwa Spika, Kwa kuzingatia historia halisi ya Muungano wetu, Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni inaamini kwamba wakati umefika kwa wananchi wa Tanzania Bara na Tanzania Zanzibar kuamua - kwa mara ya kwanza katika historia yetu na kwa uhuru kabisa - kama wanataka kuendelea kuwa na Muungano na wa aina gani. Hili halijawahi kufanyika na ndio maana Muungano umeendelea kuwa kero kwa wananchi wengi wa nchi hizi mbili. Kambi Rasmi ya Upinzani inaamini kwamba suala la ridhaa ya wananchi ni la umuhimu mkubwa na ni lazima lishughulikiwe kwanza kabla ya mchakato unaopendekezwa na Rasimu ya Muswada wa Sheria ya Mapitio ya Katiba kuanza na/au kupitishwa.
Aidha, kwa kuzingatia historia yetu halisi ya kikatiba na kisiasa, Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni inapendekeza mfumo mpya wa kutunga Katiba Mpya ambao hautatawaliwa na kivuli kirefu cha Urais wa Kifalme. Kikubwa hapa ni kwamba, badala ya wajumbe wa Tume ya Katiba kuteuliwa na Rais kama inavyopendekezwa na Rasimu ya Muswada, wajumbe hao wateuliwe kutokana na mapendekezo ya vyama vya siasa, hasa hasa vile ambavyo vina uwakilishi Bungeni, taasisi zisizokuwa za kiserikali na za kitaaluma, makundi maalum ya kijamii pamoja na Serikali yenyewe. Aidha, badala ya Sekretariati ya Tume kujazwa warasimu wa Serikali ambao ni wateuliwa wa Rais kama inavyopendekezwa, Sekretariati hiyo itokane na wajumbe watakaoteuliwa na Tume yenyewe na ambao watawajibika moja kwa moja kwa Tume yenyewe badala ya kuwajibika kwa Rais kama ilivyo sasa.
Mheshimiwa Spika, Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni haina imani, sio tu na Tume ya Taifa ya Uchaguzi, bali pia na mfumo mzima wa kisheria na kitaasisi unaoendesha chaguzi za nchi yetu. Mfumo huu na watendaji wake wameonyesha wazi kutokuwa huru na kutumiwa na Chama cha Mapinduzi kuchakachua matokeo ya chaguzi mbali mbali hapa nchini. Kwa maana hiyo, Tume ya Uchaguzi ya Taifa, na ile ya Zanzibar, haiwezi kuachiwa jukumu kubwa la kuendesha kura ya maoni kwa ajili ya kupata Katiba Mpya. Kambi Rasmi ya Upinzani inapendekeza kwamba Serikali ilete bungeni muswada wa mapendekezo ya mabadiliko ya Katiba na ya sheria husika za uchaguzi kwa lengo la kuiunda upya Tume ya Taifa ya Uchaguzi kwa lengo la kuhakikisha inasimamia zoezi la kura ya maoni kwa uhuru na bila upendeleo kwa chama tawala. Muswada huu vile vile utatoa fursa kwa Bunge hili tukufu kutunga vifungu vinavyowezesha Katiba Mpya kutungwa ambavyo havipo kwa Katiba ya sasa. Kutofanya marekebisho haya kutafanya sheria yoyote ya kuweka utaratibu wa kupata Katiba Mpya kuwa batili kwa kwenda kinyume na matakwa ya Katiba ya sasa ambayo hairuhusu Katiba Mpya kutungwa ila inaruhusu tu marekebisho ya Katiba yenyewe.