GHIBUU
JF-Expert Member
- Jan 13, 2011
- 4,432
- 3,006
Unaposema tanzania it means unaijumuisha na zanzibar ambayo sasa hivi wengi ya watanganyika ndio wamegundua kuwa ni nchi yenye mipaka yake.
Sasa hivi kuna mjadala wa katiba,katika mijadala inayokwenda Tanzania hapa zanzibar wao wanajadili muungano,kwa sababu katiba ya muungano imeingizwa ndani ya katiba ya tanganyika na kuwa kama vile magaragwe na kunde kuchanganya hujui ya muungano na yepi sio yamuungano.
Before muungano wetu ulikuwa unaitwa jamuhuri ya watu wa tanganyika na zanzibar,ambapo wakati huo tanganyika ilikuwa na katiba yake,ila rais alokuwa wa muungano pia alikuwa rais wa tanganyika wakati rais wa zanzbar alikuwa makamo wa kwanza wa muungano.
Kilicho fanyika Nyerere alifanya ujanja kuifuta Tanganyika ambayo nchi kamili iliyojipatia uhuru wake 1961,na kuita tanzania-Tan zania eti Tan imetoka katika tanganyika herufi za mwanzo tatu,na zania imetoka katika zanzibar sijui hapo nichambue vipi imetoka vipi katika zanzibar.
Halafu kachukua katiba ya tanyanyika na kutia yale makubaliano ya muungano ( article of union) kuchanganya pamoja na kuongeza viraka na kuita katiba ya tanzania. Ni kichekesho.
Nashangazwa sana kuona chadema wanapotamka neno tanzania wakisema kuwa wanatetea wakati unasema tanzania unaijumisha na zanzibar,na zanzibar sasa hivi wanajadili muungano,wanacho hitaji sasa hivi kujadiliwa muungano aidha kuleta serikali tatu kama ilivyokuwa hapo mwanzo tena ujadiliwe upya,au kuuvunja muungano.
Kwa nini chadema wasitamke tanganyika wanaposema wanataka katiba mpya kwa sababu wanaposema tanzania inawajumuisha na zanzibar wakati hawatetei watanzania wote ? Ikiwa wao wanatetea watanzania wote basi pia wafike zanzibar kutetea maslahi yao wazanzibari ,na moja ya maslahi hayo wanayohitaji ni zanzibar kuwa nchi yenye mamlaka yake yote,kimataifa na kitaifa.
Ikiwa kweli chadema munatetea watanzania pasi musitetee upande mmoja ambao ni tanzania bara,kwa jina jengine tanganyika.
Sasa hivi kuna mjadala wa katiba,katika mijadala inayokwenda Tanzania hapa zanzibar wao wanajadili muungano,kwa sababu katiba ya muungano imeingizwa ndani ya katiba ya tanganyika na kuwa kama vile magaragwe na kunde kuchanganya hujui ya muungano na yepi sio yamuungano.
Before muungano wetu ulikuwa unaitwa jamuhuri ya watu wa tanganyika na zanzibar,ambapo wakati huo tanganyika ilikuwa na katiba yake,ila rais alokuwa wa muungano pia alikuwa rais wa tanganyika wakati rais wa zanzbar alikuwa makamo wa kwanza wa muungano.
Kilicho fanyika Nyerere alifanya ujanja kuifuta Tanganyika ambayo nchi kamili iliyojipatia uhuru wake 1961,na kuita tanzania-Tan zania eti Tan imetoka katika tanganyika herufi za mwanzo tatu,na zania imetoka katika zanzibar sijui hapo nichambue vipi imetoka vipi katika zanzibar.
Halafu kachukua katiba ya tanyanyika na kutia yale makubaliano ya muungano ( article of union) kuchanganya pamoja na kuongeza viraka na kuita katiba ya tanzania. Ni kichekesho.
Nashangazwa sana kuona chadema wanapotamka neno tanzania wakisema kuwa wanatetea wakati unasema tanzania unaijumisha na zanzibar,na zanzibar sasa hivi wanajadili muungano,wanacho hitaji sasa hivi kujadiliwa muungano aidha kuleta serikali tatu kama ilivyokuwa hapo mwanzo tena ujadiliwe upya,au kuuvunja muungano.
Kwa nini chadema wasitamke tanganyika wanaposema wanataka katiba mpya kwa sababu wanaposema tanzania inawajumuisha na zanzibar wakati hawatetei watanzania wote ? Ikiwa wao wanatetea watanzania wote basi pia wafike zanzibar kutetea maslahi yao wazanzibari ,na moja ya maslahi hayo wanayohitaji ni zanzibar kuwa nchi yenye mamlaka yake yote,kimataifa na kitaifa.
Ikiwa kweli chadema munatetea watanzania pasi musitetee upande mmoja ambao ni tanzania bara,kwa jina jengine tanganyika.