Mwana Kwetu
JF-Expert Member
- Jul 12, 2011
- 652
- 562
Kwenye power breakfast kwenye dondoo za magazeti Mwigulu mchemba anasemekana amewaambia wakazi wa Mbuguni kwamba CHADEMA wamemwambia hawahitaji jimbo la Arumeru bali wanajenga Chama kitu ambacho kila mtu anajua ni uongo mtupu. amewadanganya wananchi hao kwamba CHADEMA hata ikishinda jimbo mbunge wake hataweza leta maendeleo yoyote kwani chama kilichoko madarakani ni CCM na hivyo mbunge wa CHADEMA akishinda ni sawa na kutokuwa na Mbunge.
Hii hoja hata mimi binafsi nimemsikia Mchemba akiongea kwenye kampeni na ni hoja potofu na inabidi CHADEMA waivalie njuga kumkomesha huyu mpotoshaji mkubwa. Mbunge inajulikana ni mwakilishi wa wananchi awe CDM, CUF, TLP au CCM na wananchi wanamchagua kidemokrasia kwa kuona ni mbunge kutoka chama gani anayewafaa zaidi na kwamba vyama vinavyogombea ubunge vipo kisheria kwa maendeleo ya wananchi. Iweje mchemba avuruge wananchi kwa kauli za uongo halafu anaachwa. Mbona kuna maeneo mengi wabunge wanatoka vyama vya upinzani na shughuli za kimaendeleo zinafanyika.
Basi mchemba aeleze ni kifungu gani katika katiba ya Jamhuri ya Tanzania kinachosema mbunge kutoka upinzani akiomba fungu la maendeleo la wilaya hatapewa mpaka atoke cham tawala. ijulikane na wanachi waambiwe kuwa fedha za shughuli za maendeleo ya majimbo na sehemu yoyote nchini hazitoki katika mfuko wa CCM bali serikalini zikiwa zinatokana na kodi za watanzania ambao ni kutoka vyama vyote. Mchemba atuambie ni CCm inatoa fedha za shughuli za maendeleo au serikali?. Ninavyojua CCM wana hali mbaya kifedha hata ya kujiendesha inapatikana kwa manati je iweje Mchemba adanganye wananchi kwa kauli za uongo tena majukwaani halafu anaachwa?
Atuambie kama walipa kodi wamegawanywa kiitikadi ya vyama vingi hadi aseme CDM haitaleta maendeleo Arumeru kwa sababu walipa kodi wa CHADEMA ni wachache?
Hizi kauli za kihuni, kejeli na kupotosha zinatakiwa zisisikike tena na CDM kama mlivyomjibu Mkapa kwa habari ya Vicent nyerere pambaneni na huu upotoshaji.
Mchemba ni MHUNI NA ANATAKA KUFANYA KAMPENI ZA KIHUNI NA ASIVUMILIWE
Kampeni zikifanyika kistaarabu CDM lazima waibuke washindi tu
Hii hoja hata mimi binafsi nimemsikia Mchemba akiongea kwenye kampeni na ni hoja potofu na inabidi CHADEMA waivalie njuga kumkomesha huyu mpotoshaji mkubwa. Mbunge inajulikana ni mwakilishi wa wananchi awe CDM, CUF, TLP au CCM na wananchi wanamchagua kidemokrasia kwa kuona ni mbunge kutoka chama gani anayewafaa zaidi na kwamba vyama vinavyogombea ubunge vipo kisheria kwa maendeleo ya wananchi. Iweje mchemba avuruge wananchi kwa kauli za uongo halafu anaachwa. Mbona kuna maeneo mengi wabunge wanatoka vyama vya upinzani na shughuli za kimaendeleo zinafanyika.
Basi mchemba aeleze ni kifungu gani katika katiba ya Jamhuri ya Tanzania kinachosema mbunge kutoka upinzani akiomba fungu la maendeleo la wilaya hatapewa mpaka atoke cham tawala. ijulikane na wanachi waambiwe kuwa fedha za shughuli za maendeleo ya majimbo na sehemu yoyote nchini hazitoki katika mfuko wa CCM bali serikalini zikiwa zinatokana na kodi za watanzania ambao ni kutoka vyama vyote. Mchemba atuambie ni CCm inatoa fedha za shughuli za maendeleo au serikali?. Ninavyojua CCM wana hali mbaya kifedha hata ya kujiendesha inapatikana kwa manati je iweje Mchemba adanganye wananchi kwa kauli za uongo tena majukwaani halafu anaachwa?
Atuambie kama walipa kodi wamegawanywa kiitikadi ya vyama vingi hadi aseme CDM haitaleta maendeleo Arumeru kwa sababu walipa kodi wa CHADEMA ni wachache?
Hizi kauli za kihuni, kejeli na kupotosha zinatakiwa zisisikike tena na CDM kama mlivyomjibu Mkapa kwa habari ya Vicent nyerere pambaneni na huu upotoshaji.
Mchemba ni MHUNI NA ANATAKA KUFANYA KAMPENI ZA KIHUNI NA ASIVUMILIWE
Kampeni zikifanyika kistaarabu CDM lazima waibuke washindi tu