Mwanamosi
Member
- Aug 9, 2010
- 73
- 0
Nadhani mengi yamesemwa mengine kwa jazba nk...lakini hebu tuutazame ukweli wa mambo? kwa nini hawa waheshimiwa wanapotoswa ndio wanahama vyama? na huko wanakokimbilia kitu cha kwanza ni kutaka kugombea? hivi wamekaa na kutafakari kwa nini wameshindwa walikotoka?na je wameshazijua vema sera za chama wanachoingia? na je wameshakubalika miongoni mwa wanachama wa vyama vyao vipya?(yaweza kuwa sio relevant ila ni muhimu kukubalika). Nahisi iko haja ya kuwapa uanachama wa kawaida kwa miaka mitano ndipo wagombee coz nina hofu yasitokee ya 1995 watu walipodhani Mrema and Co wangechukua nchi kumbe wametumwa kuvuruga upinzani.
Hao wanaoenda upinzani toka CCM nadhani baadhi yao ni waroho wa madaraka,kwani wanaona kwa kukosa nafasi CCM basi hawawezi kukaa bila madaraka ndio maana wanaona ni bora wakajaribu kupata madaraka haya kupitia vyama vingine..wachekiwe nia zao kabla ya kupewa nafasi kuwakilisha upinzani kwani nahofu kuwa iko siku wakitoswa upinzani watarejea CCM na mifano mingi tumeiona. yawezekana wana uchungu kweli wa kuleta maendeleo ila nadhani wakae kwanza wakijue chama walichokwenda au la watakuwa ni sawa na wale waliohama CCM 1995 na badae kurudi baada ya kuua iliyokuwa NCCR-Mageuzi ya kumsukuma mrema na kumbeba.
Ni maamuzi ya Chadema kuwapa nafasi wagombee ila kwa mtazamo wa kisiasa hilo laweza kuwa kosa kwa namna moja au nyingine kwani hawa bado ni wageni sana..nadhani tumeona waliokosa Chadema wameenda CUF kama alivyofanya Mwera na hii inaonesha kuwa kuna watu wao wanachotaka ni madaraka tu na si kingine,bila kujali ni wapi anakopatia madaraka hayo. mtu kakaa CCM miaka20 au 30 leo anadai chama kimeoza wakati angepita kwenye maoni sidhani kama angesema hayo yote...
Kazi kwa Chadema kupembua pumba na mchele kabla ya kuwapa nafasi waheshimiwa hawa ambao kama si mbinu ya CCM basi wachunguzwe utashi wao wa kujiunga Chadema, what is their motive? watu wanaweza kudanganyika nao au kwa umati unaotokea pindi CHADEMA wakifanya mikutano lakini kumbe ni yale yale ya Mrema and company ya 1995 yakabaki yakiumiza watu mioyo na kulia kuwa matokeo hayakuwa halali. chonde wanajamii tuwachunguze wote wanaohama baada ya kutoswa wawe wa CCm au Upinzani na nia zao huko waendako . hapo ndipo tutajua wanaimarisha au kubomoa upinzani...
Binafsi siungi mkono hawa jamaa kupewa nafasi za kugombea kwa tiketi ya upinzani bali wapewe muda ndipo wagombee..ni mtazamo tu
Hao wanaoenda upinzani toka CCM nadhani baadhi yao ni waroho wa madaraka,kwani wanaona kwa kukosa nafasi CCM basi hawawezi kukaa bila madaraka ndio maana wanaona ni bora wakajaribu kupata madaraka haya kupitia vyama vingine..wachekiwe nia zao kabla ya kupewa nafasi kuwakilisha upinzani kwani nahofu kuwa iko siku wakitoswa upinzani watarejea CCM na mifano mingi tumeiona. yawezekana wana uchungu kweli wa kuleta maendeleo ila nadhani wakae kwanza wakijue chama walichokwenda au la watakuwa ni sawa na wale waliohama CCM 1995 na badae kurudi baada ya kuua iliyokuwa NCCR-Mageuzi ya kumsukuma mrema na kumbeba.
Ni maamuzi ya Chadema kuwapa nafasi wagombee ila kwa mtazamo wa kisiasa hilo laweza kuwa kosa kwa namna moja au nyingine kwani hawa bado ni wageni sana..nadhani tumeona waliokosa Chadema wameenda CUF kama alivyofanya Mwera na hii inaonesha kuwa kuna watu wao wanachotaka ni madaraka tu na si kingine,bila kujali ni wapi anakopatia madaraka hayo. mtu kakaa CCM miaka20 au 30 leo anadai chama kimeoza wakati angepita kwenye maoni sidhani kama angesema hayo yote...
Kazi kwa Chadema kupembua pumba na mchele kabla ya kuwapa nafasi waheshimiwa hawa ambao kama si mbinu ya CCM basi wachunguzwe utashi wao wa kujiunga Chadema, what is their motive? watu wanaweza kudanganyika nao au kwa umati unaotokea pindi CHADEMA wakifanya mikutano lakini kumbe ni yale yale ya Mrema and company ya 1995 yakabaki yakiumiza watu mioyo na kulia kuwa matokeo hayakuwa halali. chonde wanajamii tuwachunguze wote wanaohama baada ya kutoswa wawe wa CCm au Upinzani na nia zao huko waendako . hapo ndipo tutajua wanaimarisha au kubomoa upinzani...
Binafsi siungi mkono hawa jamaa kupewa nafasi za kugombea kwa tiketi ya upinzani bali wapewe muda ndipo wagombee..ni mtazamo tu