Mpaka Kieleweke
JF-Expert Member
- Feb 27, 2007
- 4,132
- 1,571
Kujenga demokrasia ni ngumu, mimi nampongeza sana Mboe mpaka hapo alipofikisha CHADEMA, ndo maana alipoulizwa kuwa makosa waliyofanya ndani ya uongozi wake akukataa, alisema yapo.
Swala la kumshauri mgombea kujitoa kumwachia mwingine ni la kawaida ndani ya vyama. Hilary Clinton alishauriwa hivyo, na aligundua hivyo kuwa kuendelea na kinyanganyiro na Obama ni kuumiza Chama chake, hivyo alikubali kujiondoa kabla ya mkutano mkuu wa Democrat ili amuunge mkono Obama na kuomba wafuasi wake wamkubali Obama.
Hivyo kufanya hivyo kwa namna moja ni kujenga demokrasia kwani mgombea anabaki na uhuru wa kuamua kuendelea au kuachia.
Naitakia Mboe na CHADEMA mafanikio zaidi.
Kuna watu haya maandishi mekundu hawataki kuyasoma na kuyatafakari, wao wanaona tuu kwa jicho moja hawataki kuona upande wa pili .well articulated.