Ben Saanane
JF-Expert Member
- Jan 18, 2007
- 14,581
- 18,123
- Thread starter
- #41
Nitakwambia unapokosea mku wangu..
Kwanza ni mahala nilipoweka nyekundu utaona panapingana na maelezo ya mahala Blue..kuna vitu vinaingiliana kimakosa.
Na sijui hii habari vijana mnaipata wapi kwamba mnaweza kuongoza Taifa.. Hivi kweli ukiwa daranani kwa sababu mko wanafunzi 2000 unafikiri nyie mnajua zaidi ya walimu 45 wanaoongoza shule na kuwafundisha! Kwa nini usikubali kugombea uongozi wa wanafunzi wa shule au chuo isipokuwa uongozi wa shule nzima kama kipimo halisi cha mahusiano badala ya asilimia za wahusika kuwa sababu?.. Hili ni kosa la kwanza. Vijana mnatakiwa kupikwa kisiasa na mpikike, kama bado mungali wabichi msitake sana kuonyesha mnaweza ili hali bado mnatakiwa kujifunza siasa. Tumeyaona ya kila Lusinde na bado tunayaona mengi hapa JF hawa wote ni reflection yenu vijana.
Pili, Umezungumzia vizuri kuhusu vijana kutosikilizwa, sidhani kama hilo ni kweli vijana wanasikilizwa isipokuwa madai yao ndiyo yanavuka mipaka kama wale madaktari (vijana) ambao walikuwa wakihoji mishahara, posho na vifaa vya kazi madai mazuri kabisa...kisha wakageuza madai ya kuwa lazima Waziri fulani ajiuzuru ndio warudi kazini.. toka hapo mkuu walipotosha picha nzima ilihali wakiongea na waziri mkuu na rais. Kama vijana wanataka kusikilizwa na haswa mahitaji yao au wananchi sidhani kama suluhu ya kazi kwa vijana itatokana na vijana wenyewe kuongoza isipokuwa mfumo mzima wa uwekezaji na Ajira nchini maana wanaoweza kufanya kazi ni vijana na tusipoweza kuzalisha kazi inakula kwa vijana zaidi...
Na amini maneno yangu hutapenda kabisa uwe ktk nafasi ya wazee ambao nguvu ya kazi hawana, hawana pension, wanazeeka bila mtaji wala limbikizo la mali kwa manufaa ya watoto wao.. Wewe kkama kijana unatakiwa kupingana na mfumo ulowakwaza wazee wako, unatazama walikotoka na walipo na kuchambua hitilafu na mapungufu ambayo hutapenda vijana na watoto wetu kupitie mfumo wa maisha yale yale. Kumbuka tu kwamba hata hawa wazee maskini walikuwa vijana na walishindwa kulitengeneza Taifa letu kuwa bora wakiwa vijana..Hivyo ni mfumo zaidi ya umri wao kuwa sababu ya kushindwa kwetu..
My advice kwenu vijana, Pinganeni na mfumo unashindwa kuzalisha kazi, mfumo unaoshindwa kuzalisha kuujenga miundombinu, kujenga viwanda, kukuza kilimo kwa sababu hizi ndizo nguzo za kuzalisha kazi na maendeleo ya vijana na Taifa zima...Lakini sio kukazania uongozi mbona hamsemi vijana wapewe mashamba mkalime? vijana mkavue samaki na kadhalika isipokuwa Uongozi wa vyama na nchi..
Asante sana kwa kunikosoa mkuu.Mkuu wangu mkandara ninachoongelea kwenye mabadiliko ya fikra,ideologies na principles naongelea Mfumo.Ndiyo maana mara nyingi nikikosoa wazee wanapokemea vijana na kutaka tuendelee na status quo najikuta mara nyingi matatani hata hapa JF.
Mara nyingi nimekuwa nikijadili juu ya vijana kuaminiwa na kusikilizwa.Kama hautasikilizwa,ukatishwa kwa vyovyote ni njia ya kuziba vijana mdomo ili wasipambane na mfumo.Ndiyo maana nikiongelea radical reform watu wanapata shida kelewa.ni radical reform kiuchumi,kisiasa na kijamii.Na hizi haziwezi kuwa na maana kama hatutabadili fikra.kubadili fikra ni kufungua akili,ni kama maua yanayochanua kupokea kitu fulani.Hata katiba mpya ije kama hatutaendesha vita kali ya mapambano ya fikra bado tutageuka taifa la malumbano.tutaanza kulumbana juu ya katiba mpya badala ya kusugua fikra kujadili fursa zilizoletwa na katiba mpya
Mkuu wangu,ndiyo maana signature yangu na kaulimbiu yangu nikiwa nagombea uenyekiti wa BAVICHA ya MOVEMENT FOR RADICL CHANGE ilileta utata.Ni juu ya kufanya overhaul kisiasa,kiuchumi na kisiasa kwa kuanza na uhamasishaji wa kifikra zaidi.Nashukuru tunaelekea huko.Chama changu kimeanza sasa na movement for change.hii ni dhana pana kifalsafa
Mfumo tulio nao wa kisera ni wa kupeleka mambo kikawaida.Business as usual,hatuonyeshi kuwajibika kitaifa,hatuonyeshi kama ni watu wenye ambition duniani ukilinganisha na mataifa mengine.mfumo wetu zaidi ya facebook,twitter na google hautufanyi tuonekane kama tuko aware na kinachoendelea kwingine.tunaishi kama vyura bwawani tukidhani hiyo ndiyo dunia nzima kumbe kuna nchi kavu.
Msomi akiwa na digrii moja hawajibiki katika jamii inayomzunguka.haleti tofauti yoyote kifikra,kwetu elimu inatumika kama bastola ya kutishia watu.Hatujichanganyi na watu na kuambukiza fikra mpya bila majigambo.Ufisadi unaouona leo ni matokeo ya mfumo na ndiyo tunatakiwa tupambane nao.Kwa taifa ambitious huwezi kuona uthubutu wa serikali na makampuni ya kigeni yakikandamiza raia kama ninavyoshuhudia leo hii huku Geita
Leo hii hatuwaandai vijana kuwa na sauti au capacity ya kukosoa mfumo.wazee hawa walishindwa kufanya hivyo na sasa baadhi yao wanataka vijana ambao ni wazee wa baadae waendelee hivyo hivyo,yaani kilichobadilika ni kujua kuingia tu facebook,twitter,mavazi na mbwembwe kwenye harusi zetu na za marafiki.tunajenga taifa la ovyo.Sera ya kilimo kwa mfano hakuna kijana mwenye mwamko kwa kuwa amelelewa hivyo kimfumo.hajalelewa kuona fursa na kuwa aggressive.Mawazo yake hayaaminiki.Youths patriotic Movement inakuja kuongoza mapambano haya.Itakuwa kielelezo cha haya tunayopigania.Tunaandaa vision 2025 kupambana na vision 2030 ya washindani wetu kisiasa na kiuchumi ukanda huu wa Afrika mashariki (Kenya) huku wenzetu wakijitahidi kuweka mazingira ya kupambana na mfumo huku sisi tumweka Embargo.Kwa mazingira haya tutarajie fedheha huko baadae hapa A.Mashariki.Hiki ni kitu ambacho siko tayari kukiona nikiwa hai.hata sasa tumeshafikia alarming stage
Taifa hili na jamii unayoiona ni mfumo ulioandaliwa kuzuia ukosoaji,au kukinga fikra mpya za kupambana na mfumo.Tumekuwa taifa la kupambana na watu.Hata mimi kidogo niingie katika mtego wa kupambana na kundi la watu kama wazee kama nisingekuwa makini na baadhi ya wakuu kama ninyi kunikumbusha hapa