CHADEMA ni kama CCM..,ama mbaya kuliko CCM...!

Ama kweli CCM puppets are now on air. Ngoja tukutoe tongotongo machoni na threads zako zisizo fanyiwa utafiti pamoja na nduguyo maralia sugu.

1. Dhamira ya dhati ya kupambana na rushwa na ufisadi sio nyimbo za majukwaani, ama machozi bungeni bali ni kwa vitendo. Rushwa ni kosa la jinai ambalo kwa mujibu wa sheria mtuhumiwa hushitakiwa mahakamani na mwendesha mashtaka wa jamii (Public Prosecutor).

Huyu ni mteule wa Rais aliye madarakani, ingawa anapaswa kufanya kazi kwa mujibu wa katiba. Katiba haijatoa uhuru kwa mtu mwingine kuendesha kesi za jinai. Tueleze ni kwa namna gani CDM watamwagiza DPP awakamate mafisadi na kuwafungulia mashtaka?

Kazi ya kushughulikia rushwa, kuanzia kupeleleza, kukamata na kufikisha mtuhumiwa kwa DPP ni ya TAKUKURU na POLISI (Mkurugenzi wa PCCB na IGP ni wateule wa rais na wanawajibika kwa rais), CDM watatumia njia gani na kwa sheria ipi kumwagiza Hosea au Mwema kutafuta ushahidi kuhusu ufisadi, kuwakamata na kuwafungulia mashtaka mafisadi?

Haiyumkini mahakama zetu pamoja na kuzionesha kama ni vyombo huru, lakini si huru abadani. Jaji Mkuu, Jaji kiongozi na majaji wengine wote ni wateule wa Rais (CCM), mishahara yao na marupurupu inapangwa na serikali, bajeti yao inapangwa na serikali (Celina Kombani), hata kiutendaji ni sehemu ya serikali (Rejea semina elekezi Dodoma na Hotuba toka kwa Jaji mkuu).

Unategemea CDM wataweza vipi kupambana na ufisadi kwa njia mbadala zaidi ya kushitaki kwa wananchi? Katika mfumo ambao Serikali, Bunge na Mahakama zinafanya kazi kama kitu kimoja (Mapacha watatu, baba mmoja CCM), unategemea kundi la wananchi na asasi nyingine watapata wapi haki zao wanazoamini zimenyang'anywa?

2. CDM haijapinga matokeo bila kufanya study kama unavyotaka Dunia iamini. Wana ushahidi wa wazi na waliutoa, lakini CDM ni chama cha wapenda amani kupita kiasi, ndio sababu hawakutaka kuingia barabarani kuandamani kupinga kuporwa ushindi wao. Na kwa kukupa ushahidi dhahiri si tume ya uchaguzi wala CCM ama JK waliokanusha madai ya CDM. Na mpaka leo tume ya uchaguzi haijatoa matokeo kamili ya kura za urais (Tembelea tovuti yao uone).

3. Nadhani hujui unachokiongea unakurupuka tuu. Mwelekeo wa uchumi wa nchi hautolewi na vyama vya siasa ama asasi za kiraia. Mwelekeo wa uchumi wa nchi hutolewa na serikali iliyo madarakani kupitia tume za mipango, wizara ya fedha, Benki kuu na vyombo vingine vya kifedha kama TRA. Hivi ni chombo gani kati ya hivi CDM wanaweza kuvitumia kutoa mwelekeo wa uchumi?

Dunia nzima kushindwa kwa uchumi wa nchi ni kushindwa kwa serikali iliyo madarakani. Jamani, muwe mnaangalia hata TV, fuatilia yanayoendelea sasa Ugiriki, Uturuki japo ufunguke akili kidogo. Na kudorora kwa uchumi wa Tanzania ni matokeo ya kushindwa kwa serikali ya JK na si visingizio vingine.

4. Suala la undugunisation fanya utafiti usikurupuke.

5. Thread yako haijafanyiwa utafiti, kwa wakati huu CDM ndicho chama kinachoungwa mkono na watanzania wengi zaidi kuliko chama chochote cha siasa. Tafiti za sasa zinaonyesha wazi, na matokeo ya Igunga ni sehemu ya ushahidi tosha. Licha ya CCM kununua shahada, kugawa pesa, kupeleka viongozi wake wote wanaoungwa mkono na watanzania wengi, wamerudisha jimbo kwa tofauti ya kura 3000, CDM imenyang'anya kura za CUF 9000, CCM 9000 na kupata nyingine 4000.

Na hii ni tishio kwa CCM ndio maana hawaishi kutisha watu na kubambikiza kesi viongozi wa CDM. Ikiwemo hii ya kizushi kabisa ya Mh. Lema.

6. Siasa ni propaganda, lakini hii yako ni unafiki uliokithiri. CDM wana mgogoro gani? Vipi dhana ya kuvuana magamba na kukatazana kutangaza nia ya kugombea urais? Vipi makundi yanayotafunana ndani ya CCM?

Umesahau mkutano wa wenyeviti na makatibu wa mikoa ulivyoisha kwa kuwa na misimamo inayosigana (Kundi la Makongoro na la Mwenyekiti wa mkoa wa DSM?), kauli ya Sita kuhusu kuenguliwa uspika kwamba ni njama za mafisadi? Je, uamuzi wa chama chenu ulitoka kwa mafisadi?

Vipi kuhusu CCJ vs Magamba? Mgogoro ndani ya CCM ni wa maangamizi, CDM hawana mgogoro wowote ila CCM wanajaribu kuipandikiza bila mafanikio. Wanaweza kufanikiwa kuisambaratisha NCCR na si chama makini CDM.

PUNGUZA UNAZI JADILI HOJA ZA KWELI NDUGU.
Mara zote ninapojadiliana juu ya suala fulani lengo la majadiliano yangu ni kufikia solution na kuelewesha kwa kufikisha ufahamu.

Na sina lengo la kuonekana mshindi kwa kupayuka kwingi..,unaweza kudhani kuwa i'm too harsh in critique but believe me kama nisingelikuwa modest basi post yako yote ningeliijaza rangi za makosa ila nimejitahidi sana kuwa fair..,kwa kifupi haujui yafuatayo;

1; utawala wa sheria na namna unavyofanya kazi.
2; haujui nini maana ya "study" ikiwa ni neno ulilolitumia katika hoja yako juu ya kupinga matokeo na pia neno "ushahidi";
3; haujui misingi na kanuni zinazoongoza sera za kiuchumi na namna ya upatikanaji wake, haujui ni nini "uelekeo wa uchumi"
4&5; haujui ni nini "utafiti" usingelisema kuwa CDM ni chama kinachoungwa mkono na watz wengi na takwimu zako ni irrelevant kuhusu igunga.
6; haujui, aidha maana ya mgogoro ama haujui nini kinaendelea ktk chama chako;

Hayo ni katika baadhi ya usiyoyajua..,jaribu kuleta yale unayoyajua tujadiliane..,kwa haya hakuna mjadala....!
 
N awewe nae pumba zote hizo za nini> ndio uonekane unajuwa kuandika sna? kumbukeni hapa tunatazama screen za kompyuta na si makaratasi haya. hebu fungeni kidogo, muwe mnajuwa namna ya ku "summarize". Mnakuwa Mzee Mwanakijiji aliyepitwa na wakati.
Watu mmeshindwa kufikiri, mmepoteza muelekeo na sasa mnatamani na wengine wapotee....!
 
[h=6]
"ACHA UKWELI UONGELEWE"
wakati hali iko namna hii maeneo ya vijijini na kwenye vitongoji ambako maelfu ya watanzania na wapiga kura wanapatikana, ambako huduma za jamii hazifiki, ambako watu wamepoteza matumaini, ambako umasikini umeshamiri bado sisi tupo tukilala nje Arusha tukiamini hilo ndilo suluhisho la watu hawa walioko huku. Ofisi ikiwa katika hali hii inatoa picha kuwa wanachama wako wangapi na wanaari na hamasa kiasi gani, inajulisha ni kwa namna gani watu hawa hawafikiwi na hawathaminiki.


[/h]
View attachment 40952

Hii ni moja kati ya very weak arguement unayojaribu kujenga. Anayekusanya kodi za wananchi ambae anapaswa kuboresha huduma za msingi kwa hao watu ni ccm ama chadema? Mbona watu mnakuwa wepesi wa kutumika na kushindwa kutumia taaluma zenu effectively?
 
Kwa heshima zote, kwa moyo wangu wote na akili zangu zote, naunga mkono hoja zako.

Mimi pia ni mmoja ya watu waliokuwa disappointed na CDM, CDM are turning out to be traitors of innocent men and women of Tanzania tuliokuwa tumetoa trust yetu kwa CDM.

Kama CDM watazingatia ulichokiandika watalinda heshima ya chama na kujirejeshea imani ya watanzania. Wakipuuza wana options mbili:

1. Kufa
2. Au kusababisha kumwagika damu ya watanzania wasiokuwa na hatia. Au kumissuse trust ya watu waliotoa mioyo yao kwa CDM

Fortunately, this is just a wishful thinking from haters!
Chadema haihitaji ushauri toka kwa wanamagamba na wapambe wake. Wewe ni gamba unajaribu kuuhadaa umma kwamba ulikuwa na mapenzi na chadema wakati maandiko yako yanakuumbua!
 
Mara zote ninapojadiliana juu ya suala fulani lengo la majadiliano yangu ni kufikia solution na kuelewesha kwa kufikisha ufahamu.,na sina lengo la kuonekana mshindi kwa kupayuka kwingi..,unaweza kudhani kuwa i'm too harsh in critique but believe me kama nisingelikuwa modest basi post yako yote ningeliijaza rangi za makosa ila nimejitahidi sana kuwa fair..,kwa kifupi haujui yafuatayo;
1; utawala wa sheria na namna unavyofanya kazi.
2; haujui nini maana ya "study" ikiwa ni neno ulilolitumia katika hoja yako juu ya kupinga matokeo na pia neno "ushahidi";
3; haujui misingi na kanuni zinazoongoza sera za kiuchumi na namna ya upatikanaji wake, haujui ni nini "uelekeo wa uchumi"
4&5; haujui ni nini "utafiti" usingelisema kuwa CDM ni chama kinachoungwa mkono na watz wengi na takwimu zako ni irrelevant kuhusu igunga.
6; haujui, aidha maana ya mgogoro ama haujui nini kinaendelea ktk chama chako;

hayo ni katika baadhi ya usiyoyajua..,jaribu kuleta yale unayoyajua tujadiliane..,kwa haya hakuna mjadala....!

Mdau amejitahidi kukutoa tongotongo na ulipaswa kumshukuru lakini umeamua kucheza kiduku(dill dallying)!
Kajipange vizuri hapa umechemsha, chadema iko imara na haitayumba hata mpandikize mamluki.
 
Wewe una jipya unamawazo na uelewa mdogo cdm ni chama cha haki na cha wanyonge tatizo wewe unafaidika na uwizi unaofanya na ccm,mshahara wa dk slaa na mdogo mno ukilinganisha na mambo isitoshe ni mtu mmoja anyepata,acha kulopoka lopoka,huoni wenzio wanamkalibisha mtoto wa mfalme kisha na wewe unachekacheka ukiangalia upumbavu.TOA HOJA MBOVU HIZO.
 
Mkuu TandaleOne bandiko lako limetulia sana tumekuelewa lakini jaribu kusummarize kutomchosha msomaji bana.
 
Mwaka 2010 tulishuhudia matukio mengi yakijiri ndani ya taifa letu, ni matukio yaliyonasibishwa na siasa na kukua kwa demokrasia.,kulingana na muundo na mitindo ya utokeaji wake wengi tuliamini kuwa siasa katika Tanzania imepata muamko mpya na inashika hatamu katika kuleta mabadiliko ya kinchi katika Nyanja zote ambako siasa inagusa ama inahusika moja kwa moja, hapa nikijumuisha uchumi, tamaduni na jamii.


Katika matukio, lipo moja lilikuwa very significant and relative to what I am writing today.,nalo ni kukua na kutanuka kwa CDM mpaka kufikia kuwa chama kikubwa cha upinzani chenye mikiki na mabavu tele tena shupavu mbele ya CCM.,kushindwa na kufanikiwa kwake.


Kukua kwa chama hiki hakujatokea ghafla ama kwa bahati nasibu ni kwa kuwa kulikuwapo na mipango thabiti tena ya muda mrefu ya kuhakikisha chama hiki kinakua na kufikia malengo yake ya kuchukua nchi na kutawala dola. Kwa kuwa lengo langu si kuelezea historia ya kukua kwa CDM sitaingia ndani katika kulieleza hili.

Lengo kuu la waraka huu ni kueleza kupoteza kwangu matumaini na hamu ya kuwa shabiki wa siasa za Tanzania na imani yangu kuwa Siasa na wanasiasa wetu wanao uwezo wa kuleta mabadiliko ya kweli ndani ya jamii ya watanzania ambao wapo katika dimbwi la umasikini na dhiki kuu.

Kutokana na propaganda zilizopenyeshwa na kukubalika katika vichwa vya wengi ni kuwa hali ngumu ya maisha ya watanzania imeletwa na uongozi mbaya wa serikali ya CCM, ambayo wizi, ujambazi, uporaji, ufisadi, rushwa, elimu isiyo na tija(hafifu), uongozi wa kupeana (unprofessionalism) njaa,magonjwa,miundombinu hafifu,na mengineyo yameonekana kutawala. Kwa kiasi kikubwa kama si kwa asilimia zote nilikubaliana na hili, na nikawa attentive, makini na kujiaminisha kuwa hawa wanao address matatizo haya wanakuja na mbinu mbadala na mawazo tatuzi katika kushughulikia hali hii, na si mimi pekee bali watanzania walio wengi hasa wa mijini tuliamini hivyo.

Kushindwa kwa CDM;
Kulingana na yanayoendelea hivi sasa ndani ya CDM kikiwa kama chama kikubwa cha upinzani kunaonyesha dhairi kushindwa kwake katika kufikiri juu ya njia sahihi na mbinu piganizi katika kuyashughulikia matatizo yanayowakabili watanzania kiuchumi, kiutawala, pamoja na kijamii.
Na nitayazungumza machache na kwa mifano ili watu wapate kuelewa kiunaga ubaga

1: Katika ufisadi, CDM haijaonesha mipango thabiti juu ya kulishughulikia suala la ufisadi nchini zaidi ya kuitisha maandamano ya kupinga kulipwa mafisadi ambao wanabebwa na mahakama, hili linaonyesha ni kwa kiasi gani hakuna mipango thabiti,ya muda mrefu na endelevu juu ya kuzuia miaya ya rushwa, hali zinazopelekea rushwa na hata kutoa direction ya adhabu na kanuni zinazosimamia utekelezaji wa mikakati hiyo ya kupambana na rushwa bali tumeona kuwa wapo viongozi katika CDM ambao wanapropagate ufisadi katika nafasi zao ndogo walizonazo hali inayotoa ishara ni kwa kiasi gani wanaweza kuwa pindi wakipata nafasi kubwa, kumbuka ya Mshahara wa Dk Slaa, kumbuka Magari ya Mbowe, kumbuka ukwepaji wa kodi wa chama, yale ya diwani kule Mara, n.k

2: Katika nchi ambayo demokrasia ni msingi na daraja la kuendea utawala wa sheria, wananchi (wapiga kura) lazima wawe na ufahamu wa kutosha juu ya maamuzi wanayotakiwa kuyachukua pindi wanapotumia fursa yao ya kupiga kura, Katika hili CDM wamekuwa mbele kulalamika na kupinga matokeo bila kufanya study yakinifu juu ya uhalisia wa wapiga kura Tanzania, wakiwa wanatumia sample space ambayo ni irrelevant kwa wakazi wa mijini na watumiaji wa mitandao katika kufanya tathmini zao za ushindi ama kushindwa., katika uchaguzi mkuu uliopita na zingine ndogondogo tathmini za kwenye mitandao zilionyesha kuwa CDM itashinda kwa kishindo na matokeo yamekuja tofauti mara zote katika chaguzi zote, na ni baada ya matokeo ndipo CDM hukakamaa na kunadi kuibiwa kura baada ya kutulia na kujifanyia tathmini yakinifu. UKWELI NI KUWA..,wapiga kura walio wengi ni watu wa vijijini ambao wengi katika wao ni masikini wa kutupwa , kulingana na ripoti ya benki ya dunia iliyotolewa October mwaka huu ni kuwa asilimia 83 ya masikini huishi vijijini,ambao katika hao milioni 6.4 wanaishi katika mstari wa umasikini wa kukosa chakula, milioni 10 wanakabiliwa na kukosa chakula kwa msimu-kwa maana wanakuwa nacho kipindi cha mavuno na kabla ya kipindi cha masika kinawaishia.,wengine milioni 12.7 hawapati mahitaji yao ya msingi, hii ikimaanisha kuwa zaidi ya watanzania milioni 30 wanaishi katika umasikini wa kutupwa idadi ambayo ni kubwa maradufu ukulinganisha na hapo nyuma na ni idadi inaonyesha kukua kwa umasikini na kufilisika kwa serikali inayotakiwa kuwahudumia watu hawa.
Katika hali kama hiyo watu hawa lazima watadanganyika kwa kupikiwa wali, kupewa t-shirt na kofia lakini pia watanunulika kwa bei rahisi sana, hali inayowawezesha viongozi wasio na nia ya kweli ya kuwaletea maendeleo kujipenyeza kwa urahisi na kupata uongozi, wakati hali iko hiovi huko vijijini CDM wao wako busy ARUSHA wakiandamana na kulala nje, mambo ambayo hayana mashiko yeyote wala sababu za msingi.

Lakini kama hayo hayatoshi, ni kuwa wakati serikali ikishindwa kusimamia fedha na miradi inayoelekezwa katika maeneo ya vijijini CDM inashindwa kuweka mkakati wa ufuatiliaji na taasisi ya kuhoji matumizi na utekelezaji ( hili linawezekana kisheria) ambapo kupitia taasisi hiyo usimamizi utaimarika lakini pia wapiga kura watapata mrejesho na kushuhudia nia ya kweli ya wanasiasa wao ya kuwaletea maendeleo.

3:Kulingana na mfumo wa sasa wa kiuchumi wa soko holela ambapo wenye nacho hupata fursa ya kujitajirisha zaidi kwa kupitia migongo ya walalahoi, CDM inayofursa ya kutoa muelekeo wa uchumi na mfumo unaojali na kugusa pande zote kwa kushauriana na wachumi walionao na kuandaa proposal ya sera zenye kulenga mabadiliko chanya kwenye sekta ya fedha,kodi, biashara, mishahara,na miamala mbalimbali katika sekta tofauti za kiuchumi hususani kilimo, ambapo watanzania walio wengi wamejiajiri huko. Na hili lazima lifanyike chini ya wataalamu wa uchumi na fedha.

4: katika mambo yanayopigiwa kelele katika uongozi chini ya serikali ya CCM ni undugunization katika ajira na mgawanyo wa vyeo na madaraka, katika hili CDM tuliamini watakuja na mbinu tofauti ya kuhakikisha kuwa vyeo na madaraja ya kazi yanagawanywa kulingana na uwezo, elimu na nafasi ya mtu,lakini tofauti na matarajio ya wengi bado ipo system ya kulimbikiziana vyeo ndani ya CDM, watu kama mnyika na wengineo wanavyo vyeo zaidi ya vitatu wakati mmoja kana kwamba hakuna vijana wengine katika CDM walio na uwezo na elimu ya kushika nafasi hizo.

5: kupoteza umaarufu na kushindwa ushawishi kwa jamii.,hivi sasa kwa mtu aliye makini na siasa za ndani ya nchi, anaweza kugundua kwa urahisi kuwa CDM wamepoteza umaarufu na ushawishi kwa watanzania, umaarufu ambao ulipatikana kwa gharama kubwa na akili nyingi, hii inatokana na kupoteza uelekeo kwa media outlet zinazotumiwa na chadema, mfano wa magazeti kama mwanahalisi,mtanzania,Tanzania daima,mwananchi, the citizen na social medias kama jamii forums ambazo kwa mara ya kwanza zilikuwa na mvuto mkubwa kwa watanzania wapenda habari lakini kutokana na kuandika kwa mlengwa mmoja na kwa muda mrefu bila kubadilika zimepoteza ladha na thamani yake kwa watanzania.

6: Migogoro ndani ya chama.,CDM kikiwa chama kilichojitokeza mbele ya watanzania kama chama cha wapenda mabadiliko, wapenda vijana na wanaharakati wa kweli wenye kutaka Tanzania yenye neema ipatikane, bahati mbaya CDM kimekuwa kikijiingiza ndani ya migogoro ya mara kwa mara tena kwa viongozi wake wa ngazi za juu., ili linatokana na ukweli kuwa wapo wapenda madaraka wasiotaka kupisha wenzi wao na hasa vijana katika nafasi nafasi za kiutawala ndani ya chama, wenye kutaka kutoa kauli za mwisho zisizopingwa wala kukosolewa.,hali hii inatia mashaka kwa watanzania walio wengi hivyo kupoteza ari na hamasa katika kukipenda na kukiamini CDM.,wengi wakiamini kuwa tofauti pekee ya CDM na CCM ni herufi “D” tu na si vinginevyo.

Kwa kuhofia kuwachosha wasomaji, nitasitisha hapo na mengine naweza nikayazungumza kama sehemu ya comments, ila kwa kumaliza nitasema kuwa MTANZANIA TAMBUA WAZI KUWA MABADILIKO YANAANZA NA WEWE NA NI JUKUMU LAKO WALA SI LA YULE.,ACHA KULALAMIKA, ACHA KULALA NJE, ACHA KUPIGA MAYOWE, CHUKUA HATUA ZA KWELI ZA KULETA MABADILIKO YA KWELI BILA KUFUNGWA KATIKA ITIKADI AMA IMANI.,BALI KWA MSUKUMO WA UTANZANIA WAKO NA UTAIFA WAKO.
MAANDAMANO NI NJIA YA KUFIKISHA UJUMBE LAKINI SI NJIA PEKEE YA KUFIKISHA UJUMBE.,MAANDAMANO PEKEE HAYATUTOI KATIKA UMASIKINI NA KUTUTAJIRISHA BALI UZIDISHA UMASIKINI NI NJIA ILIYOSHINDWA,INAYOSHINDWA NA ITAKAYOSHINDWA TANZANIA…!

Umenena vyema!

ukweli siku zote utasimama, wengi watakaokutukana nawaliokutukana aidha wameuona ukweli na kujilinganisha jinsi walivyoingizwa mjini na aibu imewakumba!

nafurahi kuwa wewe ni mwanamageuzi...unapenda mabadiliko, umesema kama hakimu au refa.

Nimepigana na kusema mara nyingi sana humu kuhusu chadema, taswira yake na mission zao.

Ninapoona wengine mnaamka na kusema yaleyale na style nyingine nafarajiki, si kwa sababu chadema umeisema vibaya la hasha! bali nina hamu kuona chadema inabadilika na kujitayarisha kushika nchi! si chadema ya sasa si kwa style hiii...they ar just a bunc of loosers who think their preaches wil sink down in our head...

we need solutions
we need visions
we need clear strategies to remove ccm from power
we need to see logical thinking in everything we do
we need to have many songs other than ufisadi of which we have failed to say how we can deal with it

Niliwahi kuuliza swali, Mbowe ni mfanyabiashara.........akiwa waziri mkuu, au rais atawezaje kutojipendelea tenda na fursa zingine za kibiashara?? sio kuwa tutamtengeneza Rostam na Lowasa mwingine?? wakabaki kuangaliana na kukaa kimya

we need to think deeper

wanasiasa hawaaminiki, sio malaika we need to monitor them
 
Ama kweli CCM puppets are now on air. Ngoja tukutoe tongotongo machoni na threads zako zisizo fanyiwa utafiti pamoja na nduguyo maralia sugu.
1. Dhamira ya dhati ya kupambana na rushwa na ufisadi sio nyimbo za majukwaani, ama machozi bungeni bali ni kwa vitendo. Rushwa ni kosa la jinai ambalo kwa mujibu wa sheria mtuhumiwa hushitakiwa mahakamani na mwendesha mashtaka wa jamii (Public Prosecutor). Huyu ni mteule wa Rais aliye madarakani, ingawa anapaswa kufanya kazi kwa mujibu wa katiba. Katiba haijatoa uhuru kwa mtu mwingine kuendesha kesi za jinai. Tueleze ni kwa namna gani CDM watamwagiza DPP awakamate mafisadi na kuwafungulia mashtaka? Kazi ya kushughulikia rushwa, kuanzia kupeleleza, kukamata na kufikisha mtuhumiwa kwa DPP ni ya TAKUKURU na POLISI (Mkurugenzi wa PCCB na IGP ni wateule wa rais na wanawajibika kwa rais), CDM watatumia njia gani na kwa sheria ipi kumwagiza Hosea au Mwema kutafuta ushahidi kuhusu ufisadi, kuwakamata na kuwafungulia mashtaka mafisadi? Haiyumkini mahakama zetu pamoja na kuzionesha kama ni vyombo huru, lakini si huru abadani. Jaji Mkuu, Jaji kiongozi na majaji wengine wote ni wateule wa Rais (CCM), mishahara yao na marupurupu inapangwa na serikali, bajeti yao inapangwa na serikali (Celina Kombani), hata kiutendaji ni sehemu ya serikali (Rejea semina elekezi Dodoma na Hotuba toka kwa Jaji mkuu). Unategemea CDM wataweza vipi kupambana na ufisadi kwa njia mbadala zaidi ya kushitaki kwa wananchi? Katika mfumo ambao Serikali, Bunge na Mahakama zinafanya kazi kama kitu kimoja (Mapacha watatu, baba mmoja CCM), unategemea kundi la wananchi na asasi nyingine watapata wapi haki zao wanazoamini zimenyang'anywa?
2. CDM haijapinga matokeo bila kufanya study kama unavyotaka Dunia iamini. Wana ushahidi wa wazi na waliutoa, lakini CDM ni chama cha wapenda amani kupita kiasi, ndio sababu hawakutaka kuingia barabarani kuandamani kupinga kuporwa ushindi wao. Na kwa kukupa ushahidi dhahiri si tume ya uchaguzi wala CCM ama JK waliokanusha madai ya CDM. Na mpaka leo tume ya uchaguzi haijatoa matokeo kamili ya kura za urais (Tembelea tovuti yao uone).
3. Nadhani hujui unachokiongea unakurupuka tuu. Mwelekeo wa uchumi wa nchi hautolewi na vyama vya siasa ama asasi za kiraia. Mwelekeo wa uchumi wa nchi hutolewa na serikali iliyo madarakani kupitia tume za mipango, wizara ya fedha, Benki kuu na vyombo vingine vya kifedha kama TRA. Hivi ni chombo gani kati ya hivi CDM wanaweza kuvitumia kutoa mwelekeo wa uchumi? Dunia nzima kushindwa kwa uchumi wa nchi ni kushindwa kwa serikali iliyo madarakani. Jamani, muwe mnaangalia hata TV, fuatilia yanayoendelea sasa Ugiriki, Uturuki japo ufunguke akili kidogo. Na kudorora kwa uchumi wa Tanzania ni matokeo ya kushindwa kwa serikali ya JK na si visingizio vingine.
4. Suala la undugunisation fanya utafiti usikurupuke.
5. Thread yako haijafanyiwa utafiti, kwa wakati huu CDM ndicho chama kinachoungwa mkono na watanzania wengi zaidi kuliko chama chochote cha siasa. Tafiti za sasa zinaonyesha wazi, na matokeo ya Igunga ni sehemu ya ushahidi tosha. Licha ya CCM kununua shahada, kugawa pesa, kupeleka viongozi wake wote wanaoungwa mkono na watanzania wengi, wamerudisha jimbo kwa tofauti ya kura 3000, CDM imenyang'anya kura za CUF 9000, CCM 9000 na kupata nyingine 4000. Na hii ni tishio kwa CCM ndio maana hawaishi kutisha watu na kubambikiza kesi viongozi wa CDM. Ikiwemo hii ya kizushi kabisa ya Mh. Lema.
6. Siasa ni propaganda, lakini hii yako ni unafiki uliokithiri. CDM wana mgogoro gani? Vipi dhana ya kuvuana magamba na kukatazana kutangaza nia ya kugombea urais? Vipi makundi yanayotafunana ndani ya CCM? Umesahau mkutano wa wenyeviti na makatibu wa mikoa ulivyoisha kwa kuwa na misimamo inayosigana (Kundi la Makongoro na la Mwenyekiti wa mkoa wa DSM?), kauli ya Sita kuhusu kuenguliwa uspika kwamba ni njama za mafisadi? Je, uamuzi wa chama chenu ulitoka kwa mafisadi? Vipi kuhusu CCJ vs Magamba? Mgogoro ndani ya CCM ni wa maangamizi, CDM hawana mgogoro wowote ila CCM wanajaribu kuipandikiza bila mafanikio. Wanaweza kufanikiwa kuisambaratisha NCCR na si chama makini CDM.

PUNGUZA UNAZI JADILI HOJA ZA KWELI NDUGU.

siasa za africa ziko hivyo..... wanaoshabikia CCM kwa sasa wanaonekana wajinga...kipya kinyemi
wanaoshabikia Chadema wanaonekana wana akili, lakini kumbe wanafanya kile kile cha washabiki wa cmm...nao ni wajinga kwa namna ya kipekee zaidi

If you are serious, usipende wanasiasa, evaluate them!

kwa mfano ukiwaevaluate wanasiasa wa chadema, utagundua mtu kama zito yuko juu na kamwacha mbali sana Slaa na Mbowe kwa kila kitu, kuanzia akili na kutoa solutions

Ila kwa sababu ya upenzi mtu bogas anayejipeleka NMC kama Slaa utamsifia, kesho atakupotezea muda wa yeye kwenda mahakamani, badala ya kupoteza muda kukiweka chama kwenye mazingira mazuri ya ushindi 2015!

ukifikiria sana, japo ni ngumu kumeza..utagundua dhamira yao ni ruzuku , na kupata fedha zingine na kuishi vizuri na familia zao....na si kukusaidia wewe

1. wabunge wote wa chadema wanapokea posho ile ile tunayoilalamikia

2. chadema wana-breach tendering procedure na wanauziana magari mabovu

3. mbowe amekopesha chadema fedha ambazo hazijulikani mpaka leo, na anajilipa malipo kwa deni lisiloisha

4. mbowe ni mkwe wa mwenyekiti wa zamani wa chadema...na ndiye aliyeamuru uchaguzi usifanyike ila mbowe aendelee? kulikuwa na sababu gani kuitisha uchaguzi wa mwenyekiti wa taifa na uchaguzi usifanyike?

5. hakuna demokrasia ndani ya chadema

6. chadema haijaweza kujiondoa kwenye tuhuma za kuwa ni cha kikristo..na kamwe hawajafanya lolote kuuaminisha umma kuwa si wakristo

7. Chadema kwenye baadhi ya vituo huwa haiweki mawakala, na hawana mpango huo, wana majimbo yao tu na mahesabu ya kibiashara zaidi na si ya kitaifa

8. chadema hawakufanya kampeni mikoa ya lindi, mtwara na pwani......??? hii ni sura ya kitaifa?

9. chadema hawataki muungano, ila kipindi cha uchaguzi watamtafuta mgombea mwenza toka zanzibar!

10. chadema hawajafanya lolote (notable) kupinga tume ya uchaguzi ( hata kwa maandamo na kwenye jela kama Lema) wanasubiri kulia tume ya uchaguzi mbovu baada ya uchaguzi? ukiwa unashindana na timu unayojua refa atapendela upinzani una haja gani ya kuingia kwenye chaguzi?? fikiri

11. Nguvu ya chadema kudai katiba haipo au imepungua na utaisikia tena january 2016 baada ya kushindwa uchaguzi mwingine


haipo kwa maslahi ya taifa..haiko kuindoa ccm, ni NGO ni wajasiriamali...hawakufahamu ww na kelele zako, haukumona mke wa slaa wala wa mbowe NMC usiku!!!

mwenzako Slaa anasubiri million 7 mwisho wa mwezi ambazo zilikuwa hazilipiwi kodi ( mpaka TRA walipoingilia kati)

Igunga chadema wametumia million 400!!! kama mafisadi wadogo walio nje ya ulingo...na ukiwauliza wanasema mbona CCM wametumia zaidi ya hizo?????

La mwisho ni chadema hawahawa waliokuwa tayari kumkaribisha Lowasa na Kikwete mwaka 2005 kama kikwete au Lowasa asingepitishwa na NEC ya CCM kugombea urais!!!! leo Kikwete na Chadema ni maadui?..THINK??
 
Tandaleone nakushukuru kwa mawazo yako lakini naomba nikuulize yafuatayo:

(1) Kwa nini Tanzania ni masikini wakati ina almasi (Mwadui), makaa ya mawe (Kiwira), Chuma, Dhahabu (Geita, Kahama, Nzega, Chunya, Tunduru, Singida), Mbuga za wanyama (Serengeti, Mikumi, Selous etc), Ardhi ya kutosha kutoka Mtwara hadi Mtukula, Namanga hadi Tunduma, Rusumo hadi Holoholo.
(2) Kwa nini Watanzania waishi kwenye nyumba za Tembe baada ya miaka 50 ya uhuru?
(3) Kwa nini tatizo la umeme liwe kama donda ndugu?
(4) Kwa nini Tanzania isiweze kuuza nyama na mazao yake nchi za nje wakati kuna wengi sana Usukumani, Ugogoni na umasaini?
(5) Kwa nini ubora wa elimu unaporomoka kutoka shule za awali mpaka vyuo kikuu? (Je tutaweza kushindana kwenye EAC)?
(6) Kwa nini uchumi wetu unaendelea kuwa tegemezi?
(7) Kwa nini CCM imeanza kukosa uungwaji mkono kwenye ngoma zake kama Mwanza, Shinyanga, Mbeya?
(8) Kwa nini ufisadi unazidi kuenea badala ya kutokomezwa?
(9) Kwa nini uchumi wetu unakua kwa kasi ndogo sana ukilinganisha na the existing latent potential?
(10) Kwa nini Katiba mpya ni muhimu kwa ustawi wa Tanzania? Kwa nini watawala wanajaribu kuichelewesha au kuruhusu mabadiliko yasiyo na tija?

Ukiwa mkweli katika nafsi yako, utaafiki kuwa maswali yaho yametolewa majibu kwenye Ilani ya uchaguzi, bajeti mbadala na hotuba mbalimbali za viongozi wa CDM.
 
siasa za africa ziko hivyo..... wanaoshabikia CCM kwa sasa wanaonekana wajinga...kipya kinyemi
wanaoshabikia Chadema wanaonekana wana akili, lakini kumbe wanafanya kile kile cha washabiki wa cmm...nao ni wajinga kwa namna ya kipekee zaidi

If you are serious, usipende wanasiasa, evaluate them!

kwa mfano ukiwaevaluate wanasiasa wa chadema, utagundua mtu kama zito yuko juu na kamwacha mbali sana Slaa na Mbowe kwa kila kitu, kuanzia akili na kutoa solutions

Ila kwa sababu ya upenzi mtu bogas anayejipeleka NMC kama Slaa utamsifia, kesho atakupotezea muda wa yeye kwenda mahakamani, badala ya kupoteza muda kukiweka chama kwenye mazingira mazuri ya ushindi 2015!

ukifikiria sana, japo ni ngumu kumeza..utagundua dhamira yao ni ruzuku , na kupata fedha zingine na kuishi vizuri na familia zao....na si kukusaidia wewe

1. wabunge wote wa chadema wanapokea posho ile ile tunayoilalamikia

2. chadema wana-breach tendering procedure na wanauziana magari mabovu

3. mbowe amekopesha chadema fedha ambazo hazijulikani mpaka leo, na anajilipa malipo kwa deni lisiloisha

4. mbowe ni mkwe wa mwenyekiti wa zamani wa chadema...na ndiye aliyeamuru uchaguzi usifanyike ila mbowe aendelee? kulikuwa na sababu gani kuitisha uchaguzi wa mwenyekiti wa taifa na uchaguzi usifanyike?

5. hakuna demokrasia ndani ya chadema

6. chadema haijaweza kujiondoa kwenye tuhuma za kuwa ni cha kikristo..na kamwe hawajafanya lolote kuuaminisha umma kuwa si wakristo

7. Chadema kwenye baadhi ya vituo huwa haiweki mawakala, na hawana mpango huo, wana majimbo yao tu na mahesabu ya kibiashara zaidi na si ya kitaifa

8. chadema hawakufanya kampeni mikoa ya lindi, mtwara na pwani......??? hii ni sura ya kitaifa?

9. chadema hawataki muungano, ila kipindi cha uchaguzi watamtafuta mgombea mwenza toka zanzibar!

10. chadema hawajafanya lolote (notable) kupinga tume ya uchaguzi ( hata kwa maandamo na kwenye jela kama Lema) wanasubiri kulia tume ya uchaguzi mbovu baada ya uchaguzi? ukiwa unashindana na timu unayojua refa atapendela upinzani una haja gani ya kuingia kwenye chaguzi?? fikiri

11. Nguvu ya chadema kudai katiba haipo au imepungua na utaisikia tena january 2016 baada ya kushindwa uchaguzi mwingine


haipo kwa maslahi ya taifa..haiko kuindoa ccm, ni NGO ni wajasiriamali...hawakufahamu ww na kelele zako, haukumona mke wa slaa wala wa mbowe NMC usiku!!!

mwenzako Slaa anasubiri million 7 mwisho wa mwezi ambazo zilikuwa hazilipiwi kodi ( mpaka TRA walipoingilia kati)

Igunga chadema wametumia million 400!!! kama mafisadi wadogo walio nje ya ulingo...na ukiwauliza wanasema mbona CCM wametumia zaidi ya hizo?????

La mwisho ni chadema hawahawa waliokuwa tayari kumkaribisha Lowasa na Kikwete mwaka 2005 kama kikwete au Lowasa asingepitishwa na NEC ya CCM kugombea urais!!!! leo Kikwete na Chadema ni maadui?..THINK??
Mkuu kuna vitu umevitaja nakuunga mkono kabisa kuwa hatuwezi kuitoa ccm bila mipango ya kueleweka.mipango hiyo ilikuwa inatakiwa sasa! Mfano swala la katiba ndani ya miaka 2 lilipaswa kusimamiwa vyema toka wananchi walipopata mwamko,lakini mwaka unaisha hapachimbiki bungeni wala mitaani,ajenda tunazokomaa nazo haziwezi kutoa watu barabarani bali tunaishia kugawanyika! Ila mkuu kwa namna unavyomlinganisha Zitto na akina Mbowe na Slaa hutendi haki kabisa na hujengi namna hiyo.tujifunze kutoa mawazo yetu mazuri kama haya bila kuingiza maneno kama haya yatayoleta mgawanyiko usio na msingi.kama ungeweza ku edit hicho kipengele kila mtu angesoma with open mind! Waberoya una mawazo mazuri tu ila kwa nyakati hizi toa ujumbe bila kuzungumzia watu.
 
Back
Top Bottom