CHADEMA ndio wamesababisha mgomo wa madaktari

Kama WanaJF wanavyofahamu, mimi binafsi nilihusika sana na uasisi wa CHADEMA, na licha ya kwamba niliachia uenyekiti (taifa) tangu 1998 nimeendelea kuwa mjumbe wa Kamati Kuu. Nimefarijika sana na hatua na mwenendo wa hiki chama ktk miaka hii ya karibuni. Mzee Mtei ni mzee mwenye furaha sana kutokana na mafanikio ya chama alichokiasisi.

Lakini nimefadhaishwa sana na makala iliyoandikwa na "Wanabidii" ktk Gazeti la TzDaima la jana Jumapili ikizusha eti Chadema ndio kimesababisha mgomo wa madaktari!! Madaktari wamegoma kutokana maslahi duni, wakati viongozi wengi, wakiwemo Wabunge wanajiongezea posho!!

Madai mengine ni kwamba CDM wamesababisha thamani ya Shilingi kushuka na kuleta mfumko wa bei. Eti Mheshimiwa Rais wetu anakutana na Bill Gates huko Davos, na huyu tajiri wa Kimerikani atatusaidia! Lazima tutambue matatizo ya mfumko wa bei yatatatuliwa na sisi wenyewe kisiasa kwa kushusha au kuondoa kodi katika bidhaa muhimu na kuzalisha kwa wingi.

Makala hii imeendelea kutoa lawama likuki kwamba CDM ndio tunasababisha taabu na matatizo ya WaTz., hata kwamba minong'ono ya viongozi wa CCM kulishwa sumu ni sisi tumeanzisha! Pale hawa "Wanabidii" walipofikia kulaumu eti Chadema ndio walisababisha mafuriko yaliyolikumba jiji la Dar es Salaam, ndipo nilipofikia uamuzu kwamba nishauri Makala hii ipuuzwe!!

Nimeandika jibu hili kwa hii Makala, kwa vile najua Watanzania wengi wanasoma Tanzania Daima na huenda wengi wao wakadhani kuna chembe ya ukweli. Hakuna!!! Chadema ni chama makini, kinachoongozwa na WaTz wazalendo, wenye kupenda nchi yao. Wanajali matatizo na adha zinazowakabili wananchi na wananuia kwa dhati kukabiliana nazo kwa umakini,ujasiri na uzalendo. Ni lazima uongozi wa nchi upige vita rushwa na ubadhirifu wa fedha za umma unaofanywa na baadhi yao.

Kauli mbiu yetu ni HAKUNA KULALA, MPAKA KIELEWEKE!!!!!!.

Edwin Mtei.
 
Ile makala hata mimi niliisoma. kikweli nadhani muandishi alikuwa anafanya masihara. hofu yangu ikaja kwamba baadhi ya wenzetu hasa huko tulikozaliwa wakiisoma makala kama ile wanaweza kuamini kuwa ni kweli. na ubaya wa fasihi andishi ni kwamba huwa haibadiliki.
 
Nimeisoma ile nakala Jana, ila nilichogundua ni kuwa alieandika vile alikuwa kama anaibeza Serikali kuwa sio kila mgomo umesababishwa na Chadema. Ukiisoma kwa makini zaidi naona imeandikwa kwa kuikejeli Serikali dhaifu iliyoshindwa kuliongoza Taifa letu la Tanganyika. Siwezi kuamini kilichoandikwa ni chaukweli bali ni Joke.

Upuumzike kwa amani Mzee wetu
 
Mzee E Mtei.

Ni vizuri kama ungeibandika hiyo makala hapa jamvini unajua sisi wengine tulishalidharau Tanzania daima siku nyingi hasa baada ya kusoma makala nyingi zilizokuwa na muelekeo wa kuwatetea mafisadi.
 
Kweli kabisa hawa CHADEMA wanahusika na mgomo huu kwa kuwa hata mbunge wao kama vile Dr Hamisi Kingwangala wa Nzega alikuwa akishiriki katika mikutano ya madakatarikushawushi na kupitisha mgomo na kuonekan hata katika vyombo vya habari.​
 
Kama WanaJF wanavyofahamu, mimi binafsi nilihusika sana na uasisi wa CHADEMA, na licha ya kwamba niliachia uenyekiti (taifa) tangu 1998 nimeendelea kuwa mjumbe wa Kamati Kuu. Nimefarijika sana na hatua na mwenendo wa hiki chama ktk miaka hii ya karibuni. Mzee Mtei ni mzee mwenye furaha sana kutokana na mafanikio ya chama alichokiasisi.

Lakini nimefadhaishwa sana na makala iliyoandikwa na "Wanabidii" ktk Gazeti la TzDaima la jana Jumapili ikizusha eti Chadema ndio kimesababisha mgomo wa madaktari!! Madaktari wamegoma kutokana maslahi duni, wakati viongozi wengi, wakiwemo Wabunge wanajiongezea posho!!

Madai mengine ni kwamba CDM wamesababisha thamani ya Shilingi kushuka na kuleta mfumko wa bei. Eti Mheshimiwa Rais wetu anakutana na Bill Gates huko Davos, na huyu tajiri wa Kimerikani atatusaidia! Lazima tutambue matatizo ya mfumko wa bei yatatatuliwa na sisi wenyewe kisiasa kwa kushusha au kuondoa kodi katika bidhaa muhimu na kuzalisha kwa wingi.

Makala hii imeendelea kutoa lawama likuki kwamba CDM ndio tunasababisha taabu na matatizo ya WaTz., hata kwamba minong'ono ya viongozi wa CCM kulishwa sumu ni sisi tumeanzisha! Pale hawa "Wanabidii" walipofikia kulaumu eti Chadema ndio walisababisha mafuriko yaliyolikumba jiji la Dar es Salaam, ndipo nilipofikia uamuzu kwamba nishauri Makala hii ipuuzwe!!

Nimeandika jibu hili kwa hii Makala, kwa vile najua Watanzania wengi wanasoma Tanzania Daima na huenda wengi wao wakadhani kuna chembe ya ukweli. Hakuna!!! Chadema ni chama makini, kinachoongozwa na WaTz wazalendo, wenye kupenda nchi yao. Wanajali matatizo na adha zinazowakabili wananchi na wananuia kwa dhati kukabiliana nazo kwa umakini,ujasiri na uzalendo. Ni lazima uongozi wa nchi upige vita rushwa na ubadhirifu wa fedha za umma unaofanywa na baadhi yao.

Kauli mbiu yetu ni HAKUNA KULALA, MPAKA KIELEWEKE!!!!!!.

Edwin Mtei.


Mzee Chikamoo, Nimefarijika sana kujua kuwa na wewe ni mfatiliaji wa habari ndani ya ukumbi huu ulio huru. Mzee kuna namna nyingi za kufikisha habari na pia kuna namna nyingi za kupokea habari, kama uliisoma kwa umakini ile habari haikuwa ikilaumu chadema wala kuisema vibaya, ilikuwa inaonyesha jinsi serikali yetu isivyo wajibika, na imekuwa ikitafuta kondoo wa kafara katika kila jambo linalo husu jamii badala ya kutafuta suluhisho.

Kwa mtanzamo wangu mwandishi wa habari ile ni mshabiki na mkereketwa mzuri tu wa CDM, alikuwa akionyesha jinsi gani CDM ilivyo jinamizi kwa viongozi na watawala wa nchi hii, viongozi wa nchi hii hata watoto wao nyumbani wakikataa kuoga shutuma zitapelekwa kwa chadema, Hii inaonyesha kuwa CCM inaongoza nchi lakini CDM inawaongoza wananchi.

Mzee uwapo ndani ya ukumbii huu wa jamii lazima kwanza uisome habari kwa umakini, si kila jambo linawekwa wazi ndo maana likaitwa jukwaa la wafikiriaji wakuu, unaweza ukatukanwa kwa mfumo wa kusikfiwa na ukasifiwa kwa mfumo wa kutukanwa, cha muhimu ni kujua kuwa mwandishi analenga nini kabla haujachangia.

LONG LIVE MZEE.
 
Mzee Mtei, Awali ya yote heshima nyingi sana kwako.
Mimi nadhani umefanya jambo jema kutushtua kuhusu "makala" hii ambayo inavyosomeka imeandikwa kukejeli serikali iliyo madarakani ilivyo dhaifu. Visingizio vya udhaifu na kushindwa kutatua matatizo kuitupia CDM! Serikali hii imeshindwa, ingelikuwa kwenye nchi zilizoendelea ingelikwisha jiuzulu.
 
Pale hawa "Wanabidii" walipofikia kulaumu eti Chadema ndio walisababisha mafuriko yaliyolikumba jiji la Dar es Salaam, ndipo nilipofikia uamuzu kwamba nishauri Makala hii ipuuzwe!!

Edwin Mtei.

Umri na kazi! Unalalamiiiiiika, soma tena
 
ikisomwa na mtu mwenye upeo ataipambanua lakini je ikitokea imesomwana mtu wa tofauti na hapo nini madhara yake....


Mtu wa tofauti na hapo anafuata nini humu? hii ni nyumba ya wafikiriaji wakubwa, watu wenye fikara fupi hapawafai hapa.
 
Back
Top Bottom