Mkondakaiye
JF-Expert Member
- Dec 5, 2011
- 838
- 174
Katika vyama vya siasa vilivyopo hapa Tanzania CDM ndicho chama pekee kilichobaki kuwa chama makini na kinachoshughulika na matatizo ya watanzania kwa sababu zifuatazo:
CDM kazeni buti, Msikae mjini nendeni vijijini mkawaamushe watu waliolala ili magamba wasiwaibie kura tena.
Tujadili
- CDM Toka uchaguzi umalizike wamekuwa msitari wa mbele kupigania haki za wananchi na kuibana serikali kwa kusababisha uchumi wa Tanzania kushuka na kufanya maisha ya watanzania kuwa magumu. Na hata ilipofukuza wanachama hakuna malalamiko yaliyotolewa.
- CCM wao toka uchaguzi umalizike wamekalia kulalama kuvuana magamba ambayo yameshindikana kuto na huku wananchi wakiumia na hali ngumu ya uchumi na wala hawajali.
- NCCR-MAGEUZI na CUF Toka uchaguzi uishe wamebaki kuwatukana CDM kwa kufadhiliwa na CCM na wananchi kuwaita CCM B na laana iliyowapata wameanza kufukuzana.
- TLP na UDP Toka uchaguzi umalizike wamejikita kutafuta maslahi yao binafsi huku wakiunga mkono CCM na kuacha kutetea wananchi
- Vyama vingine ni vya musimu wakati wa uchaguzi kuitibulia CDM
CDM kazeni buti, Msikae mjini nendeni vijijini mkawaamushe watu waliolala ili magamba wasiwaibie kura tena.
Tujadili