Sobangeja
JF-Expert Member
- Apr 10, 2011
- 401
- 354
Nami ndo narejea toka katika mkutano,wacha kabisa watu walifurika katika viwanja vya Msakila sekondari haijapata tokea.Mkutano umeisha saa 07.49.wanachama zaidi ya 600 wamejiunga na CHADEMA!Wengine wamerejesha kadi za Magamba,lililonifurahisha zaidi wazee muhimu sana wa kifipa,mzee Zeno Nkoswe mzee Mtuka nao pia wamerejesha kadi za chama cha Magamba na kujiunga na CHADEMA.kumbuka hawa wazee ndio walihamasisha sana wananchi wa Sumbawanga kuchagua viongozi wadilifu katika nkoa huu!Hii naona ni hatua moja kubwa sana katika mkoa wa Rukwa kuelekea mageuzi juu ya nchi hii.T-Shirts,holders na promotools zimenunuliwa kama njugu.Jamani CHADEMA inatisha,Mbowe,Slaa,Zitto,Mpendazowe wachache walioongea wakati nafika kwa mkutano.