sajosojo
JF-Expert Member
- Apr 14, 2010
- 1,017
- 619
Kuna kauli inasema hivi ITS BETTER TO REMAIN SILENT AT RISK OF BEING THOUGHT FOOL,THAN TO TALK AND REMOVE ALL DOUBT OF IT
kwa muda mrefu nimekuwa nikitazama siasa za afrika na sehemu nyingine za Dunia nilichokigindua kwa afrika zinaendeshwa na upepo sana tena unaovuma pasipo UELEKEO na siku zote siasa za afrika zimelenga kuwapata emotional voters na si rational voters, Tanzania kama nchi ya afrika haijapona kuzikwepa siasa za kipuuzi na kihuni.
Nakumbuka nikiwa chuo niliwahi kuhudhuria MKUTANO wa CHADEMA VIWANJA VYA MAKUBURI KARIBU NA MABIBO HOSTEL , moja ya kauli ninayoikumbuka na ilitolewa na DR SLAA kuwaTANZANIA hakuna udini na kama kuna udini ni jukumu la serikali kutatatua hilo suala,
KWA muda wa mwaka mzima nimekuwa nikisikia fujo sehemu mbali mbali zikuhusisha masuala ya kidini, kwa mwenye kumbukumbu zangu nakumbuka FUJO ZA MWANZA ,ZANZIBAR, TUNDULU, DAR NA SONGEA na siku zote nilikuwa sijasikia kauli za vyama vya kisiasa Vikizungumzia HIZO FUJO, nakumbuka pia kwenye MKUTANO WA CUF kuna mtu aliwaomba waislam kukiunga MKONO CUF eti kwa hoja CCM IMEWASALITI,
lakini juzi jumapili nikiwa nasikiliza radio WAPO FM nilisikia mahojiano ya MABERE MARANDO(mwanasheria wa CHADEMA) akitoa msimamo wa chama chake kuhusu fujo za kidini ZA ijumaa iliyopita ,alisema hivi" Tanzania hakuna UDINI ILA KUNA MGOGORO WA WAISLAM NA serikali ya CCM, NA HATA WALE WANAOCHOMA MAKANISA NI WAHUNI NA AKAIKOSOA MAHAKAMA KWA KITENDO CHA KUTO KUMPA SHEIKH PONDA DHAMANA,na akamalizia kwa KUIKOSOA Bakwata na kudai haiungwi mkono na WAISLAM WA tanzania baaada ya Hii kauli kuna maswali ya ufahamu ambayo CHADEMA WANGEWAPA MAJIBU WATANZANIA ILI tuweze kutofatisha CHADEMA NA CCM ,
- Je kama wanaochoma makanisa ni wahuni kwa nini WANACHOMA makanisa TU na si MISIKITI AU NYUMBA NYINGINE ZA IBADA
- Kama kweli wanaochoma makanisa ni wahuni, chadema wanaushahidi upi unaothibitisha uhuni wa hao wachoma makanisa
- kwa sababu CHADEMA WAMESEMA wanaochoma makanisa ni wahuni beyond a reasonable doubt chadema wanawajua hao wahuni , je wamechukua hatua gani katika kuwasaidia polisi ili wawakamate hao wahuni au wamechukua hatua gani kuhakisha hao wahuni hawarudii tena kuchoma makanisa
- Anadai BAKWATA haiungwi mkono na waislam wa TANZANIA HASA MUFTI WATU HAWAMTAKI, JE ni kura gani ya maoni CHADEMA WAMEWAHI KUITISHA ILI tujue ni waislam wangapi hawaitaki BAKWATA NA mufti
- marando ni mwanasheria mzuri tu je hajui dhamana ni nini na hoja iliyotolewa na makahama ni mpya kwake na haipo kwenye procuderes
- Kwa kuwa KUCHOMWA makanisa na hizi fujo hazijanza leo je CHADEMA WALIKUWA WAPI KUTOA MSIMAMO WAO YALIPOCHOMWA MAKANISA
- Kwa kuwa chadema ni wasemaji wa waislam kuna madai ya MSINGI AMBAYO WAISLAM WANATAKA moja wapo ni la kadhi MSIMAMO WA CHADEMA NI UPI
- KWA KUWA ZANZIBAR ni sehemu ya Tanzania na kuna uchomaji wa makanisa huko je tamko la chadema ni lipi Pia bado sijaelewa vyombo vya habari vya Tanzania kazi zake zipi, vingi vimetoa kauli za kulani fujo za ijumaa na kuponda sana, mbona waislam wanapodai haki zao vinaponda kuwa hawakufuta utaratibu lakini kwa nini havipondi pale wafuasi wa vyama vya siasa wanapogoma kufuata taratibu za nchi AU WAFUASI WA VYAMA FLANI WAKIDAI HAKI ZAO PASIPO KUFUATA UTARATIBU NI HAKI ILA SIE WAFUASI WA DINI TUKIDAI HAKI ZETU NI UHUNI FLANI EE,
Ikumbukwe utashi wa wanasiasa wetu hauwezi kumaliza migogoro ya kidini , dini si kitu cha kuchezea na kutafutia UMarufu mnatupoteza kwa majibu yenu mepesi mepesi, Ntaendelea kuipenda Tanzania na si chama cha siasa hivyo sitakuwa mnafiki kwa nchi yangu