Chadema na usimamizi wa fedha zake; mgongano wa maslahi?

Pole sana Dr.Kitila

Kwa hiyo unakiri wazi kabisa kuwa wenye fedha ndio wanaanzisha vyama

1. Kwa nini vyama hivi vinakosa michango ya watu?
2. Je ni mpaka lini Vyama hivi vitaendelea kuwategema viongozi tu wenye fedha , je wakifilisika chama ndio kimekufa?
3. badala ya kusema tu kuwa 'mnawategema viongozi kifedha' je mmefanya juhudi gani kuepuka tegemezi hizi za viongozi? Obama ansema walichangiwa mpaka dola 1 na watoto wa shule ili washinde uchaguzi

4. Je kama mnategema fedha za viongozi, lengo lao na dhumuni lao ni nini? maana kwa namna hii
(a) Chama kinakuwa hakina demokrasia
(b)kuwapinga kama wakikosea ni kazi..YES si watazira na kuondoka na fedha zao

5.Hivi hao viongozi hizo fedha wanazokopesha wanapolipwa wanalipwa na Interest?


6. Is this project of opposition parties is viable? to you?

Kama mpaka leo ni miaka zaidi ya 15 bado hamjaweza kuwa na uhakika wa michango ya wanachama wanaokipenda, hauoni CHADEMA SIO CHAMA CHA WATU.. CHAMA CHA WAJASIRIAMALI WACHACHE WHICH IS WRONG!

7.Ili nishike nafasi ya Mbowe ninatakiwa kuwa na Capital ya shiling ngapi Dr.??


teh teh teh teh
Wenye fedha wanapoanzisha chama lazima waweke kanuni zitakazolinda masilahi yao. Kama hiyo signatory lazima awe mwenyekiti na mwingine akijaribu kuuwania huo uenyekiti kutokana na kanuni zao ni za kimasilahi wanaona signatory itatoke nje ya control yao.

Wanamkanya kijana kaa chini tunaomba jitoe ,kijana akijitoa wazee wa kanuni wanaona masilahi yao ya u signatory kijana anayatia ktk hali tete ,huyu kijana pamoja amejitoa leo lakini siku za usoni atautaka tena u signatory. sasa kinachofuata ni kuhakikisha tuna m-changanya kijana ama ahame chama ama a give up.
 
Mimi nafikiri hii ilikuwa sababu tosha kabisa ya kumuengua Zitto katika kugombea uenyekiti. Kwani Mbowe anakidai chama.
 
Wewe spinning huiwezi....kachukue shule kwanza kwa wenzako then uje. Kamuuliza angalau Makamba namna ya ku-spin, hii ya kwako ni nyeupe mno....

Umeninyanyua sana kunipeleka kwa Makamba kujifunza, wakati napata "shule" ya bure hapa hapa JF kuwa Mbowe ni mdai mkubwa wa chama, 42m na huenda zikaongezeka! Wakati huo huo yeye ni Mwenyeki na mtia saini wa cheque kuna soma zuri la spinning kushinda hili?

Kama spinning ukajifunze wewe hii yako ni aibu hata kuita ni spinning!

Ukweli utabaki chama aanzishe Mbowe na familia yake, wahangaike nacho mpaka kufika hapo kilipofika halafu mje wa kuja kuleta mambo yenu accounting concepts na blah blah zenu.

Mimi toka nimeijua Chadema nimekuwa nikisikia hizi nyimbo za Mbowe kudai chama, madeni hayaishi na hakuna mchanganuo wa madeni mnapewa figure tu. Akina Kafulila walio jaribu kuhoji yaliyo wakuta ni historia. Wahenga walisema kapu la mjanja mjinga hatii mkono Mbowe ataendelea kukamua tu after all shamba la bwana Kheri na Mbuzi wa bwana Kheri!
 
Labda kwa sababu wameshiriki kikamilifu katika kupambana VITA dhidi ya Ufisadi(kwa kuanzia na ile list of shame)

Wao hawakufanya hilo; wao walilikuza tu hilo zaidi ya yote sioni.

.......
kingine sikioni so far kinachoweza kunifanya niwachangie,nina wasiwasi hela nitakazowachangia zaweza kutumika kulipa madeni kwa Mbowe na Ndesa(nisieleweke vibaya hapa)..

Hofu yako hiyo ni ya msingi.

Cha msingi CHADEMA muwe wabunifu katika kuanzisha miradi/vyanzo vya mapato badala ya kutegemea kukopa kutoka kwa akina Mbowe&Co..Pia muliangalie kwa umakini hilo suala la Mwenyekiti kuwa signatory(ambalo limeleta msuguano mkubwa dani ya chama na ninaamini litaendelea kuleta msuguano lisipofanyiwa ufumbuzi wa haraka) na mjithidi kuwa na utulivu ndani ya chama hasa katika kipindi hiki kigumu cha kuelekea uchaguzi mkuu...

Nililiuliza hili wiki chache hapo nyuma juu ya vitega uchumi vya Chadema.. watu wakadhani nawawangia!
 
Shalom, Mku tunazungumzia tanzania na sii nchi ambazo zinafanya malipo ama transfer ya fedha kwa njia hizo. Bongo inafahamika kabisa uwezo wa signatory na ndicho kinacholeta matatizo yote haya. Hakuna mtu hapa anasema Mbowe kaiba fredha ama hatuna imani na Mbowe isipokuwa ni utaratibu mbaya uimetumika na ndio sababu kubwa ya matatizo yote ndani ya Chadema toka nimsikie Kabourou hadi hawa kina Juju.

Na waswahili husema lisemwalo sana mwisho huaminika na maadam tumaona wapi matatizo yameanzia na upo uwezekano mkubwa wa Mbowe kutokuwa msaini wa cheque, mimi sioni tatizo liko wapi maadam hatua hiyo itaondoa kinyongo na fikra mbaya ambazo zinaweza kukigharimu chama. Kuweka sign cheque ni hatua ya mwisho kabisa ya malipo na bahati mbaya biashara nzima ya chama Chadema ni kazi za kanisa yaani kinachoingia hakizai isipokuwa kinatumika na bahati mbaya kuliko yote ni mali ya wanachama wote...Hii ni kazi ya kuaminiana na bahati mbaya Wadanganyika hatuwezi kuaminiana inapofikia ktk maswala ya fedha hasa pale mshika fedha ama mweka sahihi anaposhamiri kimaisha kuwashinda wengine, hoja huzuka!

Na amini maneno yangu watu hawatajali una mali kiasi gani ama umekikopesha chama kiasi gani maadam wanahisi kuna kamchezo wataendelea kudhani hivyo..Kibaya kwa Chadema mtu wanayemdhania hayo ndiye mwenyekiti wa chama..Angekuwa Mkandara hapa wala wasingekuwa na shida kwa sababu wanajua wanaweza kunivaa wakati wowote..Hivyo kuwepo kwa misingi bora za uhasibu kulingana na mazingira yetu ni muhimu zaidi..

Naomba ifahamike kwamba hapa tunatoa mawazo yetu ktk kujaribu kuboresha hali ya kisiasa ndani ya chama na sii kubisha tu ili mradi kubisha pasipo kuangalia misingi ya ulipaji na hasa uwekaji sahihi ikiwa ndio mamlaka ya mwisho ktk matumizi..

Hivyo sioni shida kubwa ya kuweka mtu mwingine badala ya Mbowe kwani sidhani kama kazi za mwenyekiti ni pamoja na uwekaji sahihi malipo ya chama.. Sidhani kama hiyo ndio kazi ya wenyeviti hata hao CCM wasiaminika kabisa hawafanbyi hivyo...Ila kama kuna mchango kwa sababu ya Mgombea aidha iwe Urais ama Ubunge hapa naweza kubali mgombea kuwa mweka sahihi kinyume cha hapo mkuu hutaweza kubadilisha mawazo ya Wadanganyika wengi. na kila mnavyojaribu kuweka sababu ndo mnavyo wapa mashaka na watazidi kuhoiji vitu ambavyo hata hawana uhakika navyo...
 
Shalom, Mku tunazungumzia tanzania na sii nchi ambazo zinafanya malipo ama transfer ya fedha kwa njia hizo. Bongo inafahamika kabisa uwezo wa signatory na ndicho kinacholeta matatizo yote haya. Hakuna mtu hapa anasema Mbowe kaiba fredha ama hatuna imani na Mbowe isipokuwa ni utaratibu mbaya uimetumika na ndio sababu kubwa ya matatizo yote ndani ya Chadema toka nimsikie Kabourou hadi hawa kina Juju.

Na waswahili husema lisemwalo sana mwisho huaminika na maadam tumaona wapi matatizo yameanzia na upo uwezekano mkubwa wa Mbowe kutokuwa msaini wa cheque, mimi sioni tatizo liko wapi maadam hatua hiyo itaondoa kinyongo na fikra mbaya ambazo zinaweza kukigharimu chama. Kuweka sign cheque ni hatua ya mwisho kabisa ya malipo na bahati mbaya biashara nzima ya chama Chadema ni kazi za kanisa yaani kinachoingia hakizai isipokuwa kinatumika na bahati mbaya kuliko yote ni mali ya wanachama wote...Hii ni kazi ya kuaminiana na bahati mbaya Wadanganyika hatuwezi kuaminiana inapofikia ktk maswala ya fedha hasa pale mshika fedha ama mweka sahihi anaposhamiri kimaisha kuwashinda wengine, hoja huzuka!

Na amini maneno yangu watu hawatajali una mali kiasi gani ama umekikopesha chama kiasi gani maadam wanahisi kuna kamchezo wataendelea kudhani hivyo..Kibaya kwa Chadema mtu wanayemdhania hayo ndiye mwenyekiti wa chama..Angekuwa Mkandara hapa wala wasingekuwa na shida kwa sababu wanajua wanaweza kunivaa wakati wowote..Hivyo kuwepo kwa misingi bora za uhasibu kulingana na mazingira yetu ni muhimu zaidi..

Naomba ifahamike kwamba hapa tunatoa mawazo yetu ktk kujaribu kuboresha hali ya kisiasa ndani ya chama na sii kubisha tu ili mradi kubisha pasipo kuangalia misingi ya ulipaji na hasa uwekaji sahihi ikiwa ndio mamlaka ya mwisho ktk matumizi..

Hivyo sioni shida kubwa ya kuweka mtu mwingine badala ya Mbowe kwani sidhani kama kazi za mwenyekiti ni pamoja na uwekaji sahihi malipo ya chama.. Sidhani kama hiyo ndio kazi ya wenyeviti hata hao CCM wasiaminika kabisa hawafanbyi hivyo...Ila kama kuna mchango kwa sababu ya Mgombea aidha iwe Urais ama Ubunge hapa naweza kubali mgombea kuwa mweka sahihi kinyume cha hapo mkuu hutaweza kubadilisha mawazo ya Wadanganyika wengi. na kila mnavyojaribu kuweka sababu ndo mnavyo wapa mashaka na watazidi kuhoiji vitu ambavyo hata hawana uhakika navyo...

kwa kuandika hayo ulioandika je huoni kama the so called wapiganaji wenzako watakuchukia?
 
This is great. Lakini so far Mbowe kuwa signatory wa account ni kwa mujibu wa kanuni za chama. Kwamba kuna haja ya kuziangalia hizi kanuni, this is absolutely fine; ni jambo ambalo tutaliangalia katika vikao vyetu vya ndani. Being one of the wawakilishi wa sauti za wapenzi wa mageuzi ndani ya chadema naahidi kabisa kuwa tutaliangalia hili katika vikao vyetu ili kuona uwezekano huo.

Ambacho binafsi nimekuwa napinga ni kitendo cha baadhi ya watu kumlaumu Mbowe kuwa signatory as as if amejiamulia kinyume na taratibu. Tufike mahala tutofautishe kati ya kosa la kikanuni na kosa la kiongozi kama kiongozi. Ambacho kimekuwa kikiendelea katika siku za karibuni ni kumshambulia Mbowe kana kwamba amevunja kanuni na katiba ya chadema. Sasa ukweli ni kwamba Mbowe hajavunja kanuni au sheria yeyote ndani ya chadema na ya nchi kwa kuwa signatory wa account. Sasa kama tatizo ni kanuni tusema hivyo, na kama ni kosa ni la kamati kuu na hivyo kazi yeu kama viona mbali kupitia forum hii ni kuishauri na hata kuiagiza (ushauri wa wengi ni amri) kamati kuu ya chama hiki kuziangalia upya kanuni hizi. Kwa kuwa CHADEMA ni chama cha watu chenye masikio makubwa ya kusikia, watasikia na watalifanyia kazi hili.

Mimi binafsi nawashukuru sana wana JF kwa kutoa ushauri murua kwa chama chetu; hii ni ishara kwamba mnataka kuona hiki chama kinaongoza nchi katika kuleta mabadiliko ambayo wananchi wanayalilia kwa miongo na miongo.

Mbali ya mawazo haya mazuri, mnaweza pia kuichangia kwa kutuma neno CHADEMA kwenda namba 15710 (mitandao ya Zain na Vodacom pekee).

- Hewala mkuu, wala hakuna cha kuongeza hapa!

Respect.


FMEs!
 
kwa kuandika hayo ulioandika je huoni kama the so called wapiganaji wenzako watakuchukia?
Wanichukie kwa sababu gani?..Umemsikia Kitila Mkumbo akizungumza na kutoa shukran zake. Mbowe wangu, anafahamu nachozungumza sii kwa kulenga maslahi yake bali kuondokana na adha hizi zote ambazo hazina mpango..Kwani biashara zake tu kwa mwaka ni mtaji mzima wa Chadema, na hizi fujo ni lazima zikome na pengine njia bora zaidi ni yeye kuwa mbali na cheque hizo. Ni ushauri, taabu iko wapi?
 
Back
Top Bottom