Mag3
Platinum Member
- May 31, 2008
- 13,060
- 22,755
Mkuu mwiba, wewe pamoja na Lipumba, Duni, Hamad na Malaria Sugu wote mnakaribishwa viwanja vya Jangwani kama mpo Dar es Salaam, huenda mkapewa nafasi ya kuwasalimia wananchi.Lipumba ameona uzezeta wa CHADEMA na ni kweli kabisa kwa wewe Mtanzania uliepo nje utaona CHADEMA kama ni chama chenye mvuto na kufahamika sana katika TZ ,lakini ukweli sio huo CHADEMA ni Chama kidogo sana na ni chama zaidi kilichojikita katika udini ,maana mara utasikia wakiimba nyimbo za kanisani ile wanaiita kwaya wakimalizia na haleluya .
Duh, punguza munkari Mkuu Mwiba na vuta subira, mwali atafunuliwa muda si kitambo. Baada ya ndoa ya mkeka ya CCM na CUF, hawa wamekuwa wamoja hakuna wa kuwatenganisha tena. Chadema kwa ufahamisho wako hawana kawaida ya kuwa na wagombea wa kudumu.Chama mnajiandaa kugombea uraisi halafu eti unahitajia watu kutoka Chama fulani ili wawe wasaidizi au sijui ndio siku izi wanaitwa wagombea mwenza ,jamaini hivi Chama aina hii huwa kimekamilika kwa nini msiwape wagombea mwenza akina Shaibu na Lwakatare au Zitto ,Mbowe au yeyote ndani ya chadema ?
Hamna taabu hilo hata lisikupe homa, mwali kachumbiwa lakini kwa kuwa keshamchagua mume fisadi, kaonyesha ulipo uaminifu wake. Kadanganyika kwa kudhani yote yanayong'aa ni dhahabu lakini October 31 atabaki akilalama tu laiti angejua !Mnaenda kuomba watu wa chama kingine kama si utaahira ni kitu gani ? Ipo kasoro ndani ya Chadema au kwa luga ingine naweza kusema kuna tatizo ndani ya Chadema na lazima mlitatue kabla hamjafika mbali ni aibu kabisa kwenda kudai eti Juma Duni au Hamad waipe tafu Chadema ,watu wa Chadema mnahuzunisha sana ,na hapa ndipo nilipoona udhaifu wenu na kuwa hamfai kabisa kusimamisha mgombea uraisi ikiwa hamjiamini na hamjakamilika ,maana huku ni kutokujiamini ,mbele ya jamii .
Ungekuwa mkweli ungejua wanaokuzwa na magazeti ni akina nani. Jaribu tu kufungua Daily Noise au Issa Supu blog au RadioTV ya Mafisadi utawaona bila wasi wasi.Chadema mnakuzwa na vyombo vya habari vinawasifu sana na inakuwa kama mnavishwa kilemba cha ukoka tatizo mnavyotoka kwenye magazeti sivyo mlivyo ,mtu atashangaa akifanikiwa kuona live mambo yenu.mnatia huruma sana hapa kwa jinsi mnavyojipa moyo mnadanganyana wenyewe kwa wenyewe ,likianguka sijui atalaumiwa nani ?
Mkuu Mwiba jaribu kuwa na heshima kidogo unapowataja hao makamanda lakini uko sahihi kudai kuwa CUF ndio wanaweza kuwasiliza (sic!) CCM - si wana chanja kitanda ? Chadema hawana cha mseto, ebo !Hawa akina Slaa Mbowe Zitto si walikuwemo humu jamii forum mbona wameingia mitini ? CUF wataongoza tena katika ushindi na wataendelea kuwa ni chama hiki tu kinachoweza kuwasiliza CCM na si vinginevyo.
Waulize Mpanda, Morogoro, Iringa, Mtwara, Kigoma, Mbeya, Mwanza, Kagera, Mara, Tabora...... bila kusahau Dar es Salaam. Haya Mkuu Mwiba, Chadema ni wababaishaji !Nikiongezea CHADEMA mnajiona ni nyinyi tu kwa vile mnaendesha hicho Chama kikabila ,na mtu hawezi kuona mpaka awemo ndani humo ndio ukaona kunatokea mizozano ya hali ya juu ndani ya CHADEMA kwa sababu za kuongozana kimila na kuwemo kwa ukabila katika sehemu nyeti kwamba akina hawa tu ndio wanaoweza kushika nafasi hizi. Ukimaliza uchaguzi huu au kabla basi Chadema itasambaratika ,jamani hiki Chama hakina muelekeo ni wababaishaji tu. tusiandikie mate bado ka miezi miwili unusu ,mtaelewa popo nundu sio ndege.