MNYISANZU
JF-Expert Member
- Oct 21, 2011
- 7,048
- 1,102
Wananchi wa jimbo la Iramba mashariki wameelezea kuchoshwa na ulaghai unaofanywa na Chama Cha Mapinduzi kupitia mbunge wao Salome D. Mwambu na wameapa kufanya mabadiliko makubwa 2015.
Katika hatua nyingine wananchi hao wamewataka viongozi wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo [ CHADEMA] kufika jimboni humo ili wazungumze nao mambo mbali mbali ikiwamo uimarishaje wa chama jimboni, kadi za uanachama, bendera na kufungua matawi, nk.
Jimbo la Iramba Mashariki linasumbuliwa na uhaba mkubwa wa maji, huduma za afya, miundombinu ni duni mno, shule zina upungufu mkubwa wa walimu na vitabu, nk. Pia mbunge wao amewatelekeza na haonekani jimboni mwao.
Source: Ni mimi mwenyewe nipo Iramba mashariki.
Katika hatua nyingine wananchi hao wamewataka viongozi wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo [ CHADEMA] kufika jimboni humo ili wazungumze nao mambo mbali mbali ikiwamo uimarishaje wa chama jimboni, kadi za uanachama, bendera na kufungua matawi, nk.
Jimbo la Iramba Mashariki linasumbuliwa na uhaba mkubwa wa maji, huduma za afya, miundombinu ni duni mno, shule zina upungufu mkubwa wa walimu na vitabu, nk. Pia mbunge wao amewatelekeza na haonekani jimboni mwao.
Source: Ni mimi mwenyewe nipo Iramba mashariki.