Jana nilienda buguruni nikitafta makamanda wa chadema manually,watu wengine niliouliza hawakuwa na taharifa sahihi kuhusu hao makamanda hivyo wakanielekeza makao makuu ya CUF kwa minajili kwamba hawa upinzani watakuwa wanafahamiana.Safari ya kwa mzee Lipumba ikaanza,moja mbili moja mbili moja mbili,mpaka kwa ngangari,jamani mpo?tupo karibu.Nawaulizia makamanda so and so naweza wapata mitaa gani kwani nilijua chadema wanamsingi ila sikujua wapi specific.Matusi niliyoporomoshewa Mungu anajua......Hichi chama ci hatukitaki kabisa,kwanza hawana chao hapo,nawe kichaa unaulizia chadema buguruni?umepotoka,haumfahamu profesa wa uchumi?ataja komboa taifa,hata marekani wanamtambua we si mwanaCUF au mwenzetu mchaga?na story nyingi tu,sitasema zote.Sikukata tamaa nikanyosha huyooooooooo kwa magamba,huwezi amini ushirikiano nilipewa mpaka kufikishwa kwenye tawi ilo la chadema.Nimeshindwa kuelewa labda wadau nijuze kuna nini kati ya chadema na cuf na c CCM hasimu wao namba moja?