Mkwawa
JF-Expert Member
- Jun 8, 2011
- 1,334
- 1,464
Chama cha Maendeleo na Demokrasia kinakua kwa kasi nzuri sana. sera zake na viongozi wake na wabunge wengi wanakubalika kwa Jamii ya tanzania ya leo.
Kuna angalizo muhimu sana linahitajika kufanyiwa kazi kubwa sana na kulichukulia kwa uzito wake. Chama kinapokuwa na kuleta upinzani mkubwa kwa chama tawala tayari kinatengeneza mwanya wa kubomolewa kwa siasa za kiafrika na hasa east afrika. Makada na wagombea wa nafasi mbali mbali lazima wawe ni watu wanaokijua chama kwa undani na kuelewa sera za chama, itikadi na mfumo. Viongozi wote lazima wajua misingi na imani za chama na nini wanasimamia, huo ndio msingi wa kujenga chama imara na serikali imara. Chama legelege kinazaa serikali legelege.
Napendekeza utaratibu ambao tumekuwa tukiutumia wa kuwapata wagombea kuubadilisha haraka iwezekanavyo. Najua Viongozi waliopo wamepitia kwenye vipindi vigumu sana, wanahitaji pongezi ya namna ya pekee na sifa kubwa na kuenziwa ndani ya chama. Wamefanya kazi katika mazingira magumu na kwa wakati mgumu sana. Viongozi wote wa CDM kuanzia 1992 hadi leo poleni sana na hongereni sana. Utaratibu ambao umetumika wa kuwapata wagombea wa nafasi mbali mbali za kitaifa, wilaya, mkoa, ubunge, udiwani nk lazima ubadilike. mabadiliko haya lazima yafanyiwe mabadilko kwenye katiba ili kutoa mwanya wa malalamiko na uonevu.
Moja mwanachama ambaye anataka kugombea nafasi yeyote ile ya uongozi, ndani ya chama au ile ya udiwani, ubunge lazima awe na muda utakaokubalika ndani ya chama, awe mwanachama hai, anayeshiriki shughuli za chama pale alipo, napendekeza walau awe mwanachama kwa miaka miwili kabla ya kuomba au kupewa nafasi yeyote ya uongozi. Hii itasaidia kuwapata viongozi imara na wenye kuelewa chama na sera zake.
Mchakato huu utasaidia kuwa na viongozi wanajua misingi na uimara wa chama badala ya sasa kuvizia wanaotemwa au wanaovizia vyeo au wanaopima upepo kwa faida za matumbo au kusaidia vyama vingine kwa kuingiza mamluki. Najua kunagharama zake ila hii itasaidia kuwa na chama imara chenye watu madhubuti.
Chama kinakua kinahitaji misingi imara, wimbi la wasaliti linakuwa kwani chama tawala kinaangamia, kinatumia hila, fedha, na ushushu kuua upinzani kwa kununua wapinzani. Njaa za viongozi wasio na mwelekeo wa kuwakomboa wananchi, wasioelewa nini CDM wanafanya wananunulika kirahisi na kutengeneza makundi, fujo, tamaa nk.
Ni mimi
Chief Mkwawa wa Karenga
Kuna angalizo muhimu sana linahitajika kufanyiwa kazi kubwa sana na kulichukulia kwa uzito wake. Chama kinapokuwa na kuleta upinzani mkubwa kwa chama tawala tayari kinatengeneza mwanya wa kubomolewa kwa siasa za kiafrika na hasa east afrika. Makada na wagombea wa nafasi mbali mbali lazima wawe ni watu wanaokijua chama kwa undani na kuelewa sera za chama, itikadi na mfumo. Viongozi wote lazima wajua misingi na imani za chama na nini wanasimamia, huo ndio msingi wa kujenga chama imara na serikali imara. Chama legelege kinazaa serikali legelege.
Napendekeza utaratibu ambao tumekuwa tukiutumia wa kuwapata wagombea kuubadilisha haraka iwezekanavyo. Najua Viongozi waliopo wamepitia kwenye vipindi vigumu sana, wanahitaji pongezi ya namna ya pekee na sifa kubwa na kuenziwa ndani ya chama. Wamefanya kazi katika mazingira magumu na kwa wakati mgumu sana. Viongozi wote wa CDM kuanzia 1992 hadi leo poleni sana na hongereni sana. Utaratibu ambao umetumika wa kuwapata wagombea wa nafasi mbali mbali za kitaifa, wilaya, mkoa, ubunge, udiwani nk lazima ubadilike. mabadiliko haya lazima yafanyiwe mabadilko kwenye katiba ili kutoa mwanya wa malalamiko na uonevu.
Moja mwanachama ambaye anataka kugombea nafasi yeyote ile ya uongozi, ndani ya chama au ile ya udiwani, ubunge lazima awe na muda utakaokubalika ndani ya chama, awe mwanachama hai, anayeshiriki shughuli za chama pale alipo, napendekeza walau awe mwanachama kwa miaka miwili kabla ya kuomba au kupewa nafasi yeyote ya uongozi. Hii itasaidia kuwapata viongozi imara na wenye kuelewa chama na sera zake.
Mchakato huu utasaidia kuwa na viongozi wanajua misingi na uimara wa chama badala ya sasa kuvizia wanaotemwa au wanaovizia vyeo au wanaopima upepo kwa faida za matumbo au kusaidia vyama vingine kwa kuingiza mamluki. Najua kunagharama zake ila hii itasaidia kuwa na chama imara chenye watu madhubuti.
Chama kinakua kinahitaji misingi imara, wimbi la wasaliti linakuwa kwani chama tawala kinaangamia, kinatumia hila, fedha, na ushushu kuua upinzani kwa kununua wapinzani. Njaa za viongozi wasio na mwelekeo wa kuwakomboa wananchi, wasioelewa nini CDM wanafanya wananunulika kirahisi na kutengeneza makundi, fujo, tamaa nk.
Ni mimi
Chief Mkwawa wa Karenga