commited
JF-Expert Member
- Feb 27, 2012
- 1,626
- 870
Iko wazi kuwa ccm kama chama tawala, kinafahamu fika kuwa kimeshindwa kuondoa kero muhimu kwa maisha ya mtanzania kwa zaidi ya miaka 50, matatizo hayo makubwa ni rushwa,ujinga, na umaskini. Na chama hiki kinafahamu kuwa watanzania wa miaka ya 1990, siyo hawa wa 2012, na wala hawatakuwa wale wa 2015, zaidi ya yoote chama hiki kinafahamu kuwa wananchi wengi wamekata tamaa ya kusikia ahadi za kila uchaguzi kwa zaidi ya miaka 50 sasa, baadhi ya hila zake zimeanza kufahamika KWA WANACHI WA KAWAIDA na hata kwa vyama pinzani hasa chama kikuu cha upinzani chadema. Hila za ccm ilizozitumia katika kushinda baadhi ya chaguzi zikiwemo zile za uchaguzi mkuu wa raisi 2010, ambapo chama hiki (ccm)kilitumia nguvu nyingi na pesa nyingi sana kuhonga mitandao ya simu kuwachafua wagombea mbalimbali hasa dr Slaa, kutumia tume ya uchaguzi kubadili matokeo, kuwatumia polisi katika kuhalalisha wizi wa kura wa majimbo mbalimbali kama mvomero, shinyanga mjini, ifakara na Kilimanjaro na kadhalika. CCM inafahamu kuwa kwa sasa inakabiliwa na tatizo sugu machoni pa wanachi hasa wa mjini na hata baadhi ya vijijnii juu ya matumizi mabaya ya madaraka, ukiukwaji wa haki za binaadamu, wizi wa rasilimali za taifa(madini,ardhi na kadhalika), wizi wa fedha za uma kama(mabilioni ya shimbo, mabilioni ya Epa, meremeta,kagoda na mengine mengi).MIKAKATI YA CCM KUMALIZA UPINZANI NA HASA CHADEMA KUELEKEA 20151.CCM Kwa ujumla wake kinajua hatari ya anguko kubwa liliyoko mbele yake hasa kuelekea uchaguzi mkuu 2015,na hata sasa kwenye chaguzi zake za nec inapanga watu ambao wanaushawishi mkubwa wa kifedha ili wakati huo wa chaguzi utakapofika rushwa iwe wazi wazi hasa maeneo ya vijijini, ikiwemo ununuaji wa shahada ya kupigia kura lakini pia CCM inajiandaa kugawa pesa kwa wanachi bila kificho,2. zimetengwa bilioni zaidi ya milioni 400 (safety net)" na chanzo cha fedha hizi ni kutoka mifuko ya jamii kama NSSF,na pia zimekusanywa toka kwa wafanya biashara wakubwa ambao wamekuwa na mikutano ya siri na mkuu wa nchi, lengo kuu ni kuhakikisha popote pale patakapooneka kunahatari ya kukosa kura hasa za uraisi( mchuno mkubwa utakuwa kati ya EL, Bilali, na Nchimbi na Membe) pesa hizi zitumike kuwapa wananchi!.3. Kati ya mwaka 2013-2015 Serikali ya sisiemu inajiandaa kutangaza huduma za afya, elimu kuwa bure, lengo ni kujaribu kupunguza nguvu ya chadema katika ajenda hizo, ili wahakikishe vile vitu amabavyo vinawapa nguvu chadema katika majukwaa vinapungua4. Hujuma katika maboresho ya daftari la wapiga kura ( Hili ntalieleza muda utakapofika)5. Pia kunamkakati ambao ulisha sukwa tangu 2009 hasa kwa chadema kuwatumia baadhi ya viongozi ambao ni rahisi kuhongeka, wapewe pesa, na wengine kuelekea uchaguzi mkuu watajitoa chamani na kugombea kama wagombea binafsi, (divide and rule)6. Lakini pia taassisi ya msajili wa vyama vya siasa, imepewa rungu la kuhakikisha anakimonita chadema na hata pale watakapoingia katika kumi na 18 zake akifute, zaidi ya yoote ili kuongeza ugawanyaji wa kura za wapinzani vyama vingi sana vitasajiliwa kuelekea uchaguzi mkuu na vingine vikiwa na mlengo wa kidini wazi wazi. Pia viongozi wa vyama vingi vya upinzani mbali ya cdm wameshapewa maelekezo ya kuwaatack live CDM, na hata kuwahujumu katika mikakati yao (oparesheni mbalimbali mikoani) na matamko yao mbalimbali lengo ni kuhakikisha cdm inapunguzwa kasi na hata kufa kabisa.CHADEMA IJIPANGE SANA, IWE NA PLAN B, C NA D KWANI CCM WANAJUA HATARI ILIYOPO MBELEYAO.. NA HAWAKO TAYARI KUACHIA NCHII HII KIRAHISI, WANAJIPANGA KUTUMIA KILA AINA YA NGUVU, HILA MAUAJI YA VIONGOZI WA CDM& WANAHARAKATI, VITISHO NA KADHALIKA, LENGO NI KUHAKIKSHA CCM INABAKI MADARAKANI.Mungu ibariki Tanzania.