Chadema msione aibu kuiga NCCR-Mageuzi kwa kuthubutu

MAFILILI

JF-Expert Member
Apr 28, 2011
2,377
1,194
Nachukua fursa hii adimu kutoa hongera kwa viongozi wa NCCR Mageuzi kwa kuonyesha UJASIRI wa kuwaita viongozi na wanachama mbele ya vikao halali na kuchukua maamuzi magumu ya kuwavua uanachama akiwemo mbunge wa Kigoma Kusini, Kafulila.

Wakati CUF nayo leo wakitarajia kumweka kiti moto mbunge wa Wawi, Hamad Rashidi, CHADEMA wamekuwa butu kumwita mbunge wao, John Shibuda anayeonekana anawasaliti kupitia kauli zake na vitendo vyake vya kutufuata mwenendo wa viongozi wake wa CHADEMA.


Kulikoni CHADEMA kwa nini mnakuwa wagumu kumweka kiti moto Shibuda????? Mie nafikiri Shibuda kawashika pabaya hivyo mwaogopa mkimpiga chini, atamwaga uozo wenu wote mbele ya jamii.

Poleni kwa kushindwa kufanya maamuzi dhidi ya Shibuda ama mwaogopa ruzuku kupungua????
 
Nachukua fursa hii adimu kutoa hongera kwa viongozi wa NCCR Mageuzi kwa kuonyesha UJASIRI wa kuwaita viongozi na wanachama mbele ya vikao halali na kuchukua maamuzi magumu ya kuwavua uanachama akiwemo mbunge wa Kigoma Kusini, Kafulila.

Wakati CUF nayo leo wakitarajia kumweka kiti moto mbunge wa Wawi, Hamad Rashidi, CHADEMA wamekuwa butu kumwita mbunge wao, John Shibuda anayeonekana anawasaliti kupitia kauli zake na vitendo vyake vya kutufuata mwenendo wa viongozi wake wa CHADEMA.


Kulikoni CHADEMA kwa nini mnakuwa wagumu kumweka kiti moto Shibuda????? Mie nafikiri Shibuda kawashika pabaya hivyo mwaogopa mkimpiga chini, atamwaga uozo wenu wote mbele ya jamii.

Poleni kwa kushindwa kufanya maamuzi dhidi ya Shibuda ama mwaogopa ruzuku kupungua????

Hakuna mwenye ubavu ndani ya CDM kumgusa Shibuda, na yeye aliisha sema wao wakimwaga ugali na yeye anamwaga mboga

 
MAFILILI,
Hivi huona uamuzi wa CDM kuendelea kumvumilia Shibuda ni sehemu ya Uamuzi Mgumu ambao NCCR wameushindwa kwa Kafulila na kwamba CUF nao wanapaswa waige mfano huu wa CDM katika kumkabili Hamad Rashid?
 
Nachukua fursa hii adimu kutoa hongera kwa viongozi wa NCCR Mageuzi kwa kuonyesha UJASIRI wa kuwaita viongozi na wanachama mbele ya vikao halali na kuchukua maamuzi magumu ya kuwavua uanachama akiwemo mbunge wa Kigoma Kusini, Kafulila.

Wakati CUF nayo leo wakitarajia kumweka kiti moto mbunge wa Wawi, Hamad Rashidi, CHADEMA wamekuwa butu kumwita mbunge wao, John Shibuda anayeonekana anawasaliti kupitia kauli zake na vitendo vyake vya kutufuata mwenendo wa viongozi wake wa CHADEMA.


Kulikoni CHADEMA kwa nini mnakuwa wagumu kumweka kiti moto Shibuda????? Mie nafikiri Shibuda kawashika pabaya hivyo mwaogopa mkimpiga chini, atamwaga uozo wenu wote mbele ya jamii.

Poleni kwa kushindwa kufanya maamuzi dhidi ya Shibuda ama mwaogopa ruzuku kupungua????

Sio kila kitu akifanya mwenzako na wewe lazima ukiige kizima kizima. Muda mwaafaka ukifika na kama kweli SHIBUDA ataonekana amefanya kosa linalositahili adhabu ya kufukuzwa uanachama nadhani CHADEMA watafanya hivyo . Kwanza wameshafanya hivyo kwa madiwani wake watano huko ARUSHA
 
Nachukua fursa hii adimu kutoa hongera kwa viongozi wa NCCR Mageuzi kwa kuonyesha UJASIRI wa kuwaita viongozi na wanachama mbele ya vikao halali na kuchukua maamuzi magumu ya kuwavua uanachama akiwemo mbunge wa Kigoma Kusini, Kafulila.
...
Hapo kwenye bold... kulikuwa na madai kwua wajumbe wa kikao kile wengui walichomekwa baada ya wengine wengi kufutwa bila maelezo ya kueleweka. Nina mashaka iwapo tunaweza kukiita kikao kile kuwa ni halali.
Lakini kwa ujumla wa hoja yako, nitaishangaa sana Chadema iwapo itaamua kuanza kuiga mambo yanayofanywa na vyama vingine
 
Hapo kwenye bold... kulikuwa na madai kwua wajumbe wa kikao kile wengui walichomekwa baada ya wengine wengi kufutwa bila maelezo ya kueleweka. Nina mashaka iwapo tunaweza kukiita kikao kile kuwa ni halali.
Lakini kwa ujumla wa hoja yako, nitaishangaa sana Chadema iwapo itaamua kuanza kuiga mambo yanayofanywa na vyama vingine

Siyo siri tena, Shibuda akiwa bungeni alitofautiana na hadi leo yupo tofauti na mtazamo wa CDM kuhusu na suala la posho. Itakumbukwa Shibuda tangia siku ya kwanza ya bunge alikuwa tofauti na wenziwe juu ya kumtambua JK. Sina budi kuamini kuwa CDM wakimwaga ugali, Shibuda atamwaga mboga, Kazi ipo kweli kweli CDM wameshikwa pabaya na Shibuda!!!
 
Mimi nafikiri kufukuzana siyo njia pekee ya kumaliza migogoro katika vyama vya siasa,cha msingi ni kukubali kutokubaliana.Kufukuzana kutakuwa na maana pale tu mwanachama atakapokwenda kinyume na sera cha chama.
 
Maamuzi magumu ni pamoja na kutotoa maamuzi ya kipuuzi kwa kufuata mkumbo.
 
CDM kuna mambo ya muhimu ya kufanya kwa sasa zaidi ya kumjadili Shibuda - nani asiyemjua shibuda? Leo kaibukia kete ya kuwalaumu viongozi wa dini wasimseme Rais wake kabla hata hajafanya utafiti wowote, tena huku alikoibukia ndiko kubaya zaidi bora livyokuwa anawasema viongozi wake bungeni. kuitisha kikao kumjadili mtu huyu ni gharama ni vyema muda na hela hiyo itumike kuimarisha chama.

Viongozi wa dini wamefanya mambo mengi sana kuishauri serikali hii hadi wakatoa miongozo - sasa sijui jamaa alikuwa muda wote anafikiria POSHO tu hata hafuatilii jambo hili.
 
MAFILILI,
Hivi huona uamuzi wa CDM kuendelea kumvumilia Shibuda ni sehemu ya Uamuzi Mgumu ambao NCCR wameushindwa kwa Kafulila na kwamba CUF nao wanapaswa waige mfano huu wa CDM katika kumkabili Hamad Rashid?

kama kumvumilia mtu ndio uamuzi mgumu, kwanini chadema walishindwa kuchukua maamuzi hayo "uyaitayo" magumu zidi ya madiwani wa Arusha?
 
Siyo siri tena, Shibuda akiwa bungeni alitofautiana na hadi leo yupo tofauti na mtazamo wa CDM kuhusu na suala la posho. Itakumbukwa Shibuda tangia siku ya kwanza ya bunge alikuwa tofauti na wenziwe juu ya kumtambua JK. Sina budi kuamini kuwa CDM wakimwaga ugali, Shibuda atamwaga mboga, Kazi ipo kweli kweli CDM wameshikwa pabaya na Shibuda!!!
kaka CDM ni taasisi makini, haifikiri kwa kiwango chako and who is Shibuda ndani ya CDM?
 
Siyo siri tena, Shibuda akiwa bungeni alitofautiana na hadi leo yupo tofauti na mtazamo wa CDM kuhusu na suala la posho. Itakumbukwa Shibuda tangia siku ya kwanza ya bunge alikuwa tofauti na wenziwe juu ya kumtambua JK. Sina budi kuamini kuwa CDM wakimwaga ugali, Shibuda atamwaga mboga, Kazi ipo kweli kweli CDM wameshikwa pabaya na Shibuda!!!
Ebu niambie kitu ambacho Shibuda anacho ambacho iwapo atakisema au kikfanya itasababisha Chadema iwe katika hali mbaya
 
Back
Top Bottom