Chadema mnamuogopa lema?..anafanya nini mpaka leo cc??

shebby1

Member
May 26, 2012
27
0
Ndugu zangu, kwa Hali ya kawaida mbunge ni Yule mwenye access ya kuingia bungeni na kufanya shuhuli za kibunge Kama kamati za kudumu nakadhalika. Ndugu yangu GODBLESS LEMA yeye alichaguliwa na wabunge kuwa mjumbe wa kamati kuu kupitia zile nafasi tano za Wajumbe wa kamati kuu kupitia wabunge..swali la kujiuliza ni kwanini hata baada ya kuenguliwa na mahakama kuwa mbunge bado anaruhusiwa kuingia kwenye kamati kuu ya chadema? Ni kwanini wabunge wasipewe nafasi ya kuchagua mbunge mwingine awe mjumbe wa kamati kuu?...na kwanini Chama kinamtumia LEMA mtu asiye hata na sifa yoyote kwenye jamii kwenda Kuje ga Chama mikoani?..sehemu nyingi alizopita amekuwa akilalamikiwa kuwa anafanya siasa za kibaguzi, je ni kuitimiza ile kauli kuwa kiongozi yeyote wa CDM ni lazima atokee sehemu Fulani Fulani maw nchi hii?...nimefuatilia wasifu wake akiwa bungeni kwa makini, na nimegundua tangu Ameingia
mpaka ametoka bungeni ameuliza swali la msingi moja tu na la nyongeza moja, na amechangia Mara kumi tu kwa siku zone zaidi ya 200 alizokaa bungeni....nafahamu kuwa kuna watu nitawakwaza lakini ninawaomba muyajadili niliyoyasema na Msiende nje ya mada.
 
Ni ruiz FAA pia kusikia Kama nimetumwa, Mimi gamba, kijana wa nape, usalama n.k....ila ninachosisitiza ni kwamba ninataka tu ufafanuzi juu ya hayo.
 
Back
Top Bottom