Chadema mnalalamika nini? Mbeya maji, Moshi beer.

zomba

JF-Expert Member
Nov 27, 2007
17,261
3,909
[h=2]Sunday, July 22, 2012[/h] [h=3]Rais Kikwete azindua mradi wa maji Mbeya[/h]
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete,Kamishna wa Maendeleo katika Jumuiya ya Ulaya Andris Piebalgs(wapili kushoto), balozi wa jumuiya ya ulaya nchini Cerian Philberto Sebregondi(kushoto),Balozi wa Ujerumani nchini Klaus Peter Brandes na Waziri wa Maji Profesa Jumanne Maghembe wakikata utepe kuzindua rasmi mradi wa maji safi na mazingira Mjini Mbeya leo mchana.
Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete,Kamishna wa Maendeleo Jumuiya ya Ulaya Andris Piebalgs(Watau kushoto) na Waziri wa Maji Profesa JumANNE Maghembe wakikagua chanzo cha maji eneo la Swaya mjini Mbeya wakati wa uzinduzi wa mradi maji safi na mazingira mjni humo leo mchana.

Source:FULL SHANGWE: Rais Kikwete azindua mradi wa maji Mbeya

[h=3]Pinda azindua Kiwanda cha Serengeti mjini Moshi[/h]

Waziri Mkuu Mizengo Pinda, jana amezindua kiwanda cha Bia cha Serengeti tawi la Moshi mkaoni Kilimanjaro. Kinwanda hicho cha kisasa na kikubwa kipo eneo la Pasua Boma Mbuzi katika barabara ya Sukari.

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akisalimiana na Mmoja wa Wanahisa wa SBL, Christopher Gachuma mara baada ya kuwasili kiwandano hapo.

Pinda akizungumza jambo na Mkurugenzi wa Mawasiliano wa SBL, Teddy Mapunda.

Pinda akisalimiana na Mkurugenzi wa Masoko wa SBL, Ephraim Mafuru

Waziri Mkuu Mizengo Pinda akikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa Kiwanda cha SBL mjini Moshi.

Pinda akifunia kitambaa katika moja ya shughuli za uzinduzi wa mjini mosha. Pamoja nae ni Mwenyekiti wa Badi ya SBL, Jaji Mark Bomani na kati kati yao ni Mkuu wa Moa wa Iringa, Leonidas Gama.

Waziri Mkuu akipata maelezo juu ya uzalishaji wa Kiwanda hicho

Pinda akitembezwa katika maeneo mbalimbali ya Kiwanda.


Sehemu ya ujazaji kinywaji cha Serengeti katika kiwanda hicho.

Akiendelea kupata maelezo ya uzalishaji.

chanzo father kidevu
Source:
KIMKEV ENTERTAINMENT: Pinda azindua Kiwanda cha Serengeti mjini Moshi

 
Kazi ipo. Akiifungua ile airport ntampa salute maana imekuwa kama gofu tu pale Songwe....ushuru utakuwa mdogo sana mwezi huu maana hivi viwanda vya bia kushoto na kulia duuh
 
Kazi ipo. Akiifungua ile airport ntampa salute maana imekuwa kama gofu tu pale Songwe....ushuru utakuwa mdogo sana mwezi huu maana hivi viwanda vya bia kushoto na kulia duuh

Ulitaka Moshi mpewe nini? cha mbege?
 
Ulitaka Moshi mpewe nini? cha mbege?

zomba, yaani utafikiri na wewe ni mtabiri. Moshi tunakunywa mbege. Haina VAT ile...haya maviwanda kila kona yanatusaidia kulewa zaidi na kusahau kufuatilia uporaji wa mali yetu ya asili. Think well about it
 
Kwani moshi na mbeya ni mikoa ya chadema? Mbona mwandishi hueleweki?
 
Zomba kwa misemo yako hiyo mwishowe utasema Mwanza Sato... Katavi tunguli.. walianza kipele kipele.. mwishowe.....
 
Mtu hasifiwi kwa kazi ambayo anapaswa kuifanya katika hali ya kawaida..........tusifie pale ambapo amefanya la ziada
 
Hongera walipa kodi wa Jumuiya ya Ulaya na walipa kodi wa Ujerumani kwa msaada huu, Mungu awajalie zaidi. na Ujerumani ndipo kinapotoka kile chama cha CDU.
 
kila kitu ni kutegemea tufanyiwe tu, yaani hadi hata vitu vidogo mpaka tulete umatonya. Pesa za wananchi walalahoi zinaenda kufichwa nje na mafisadi. Wananchi wakihoji jibu ni kwamba "tumewaambia watafakari na wajipime then wajiwajibishe wenyewe". Sipati picha utendaji wa aina hii, hata katika ngazi ya familia tu kuna disciplinary principles. lakini cha kushangaza serikali na taasisi zake zinakiuka ili tu kuendelea kuifisadi nchi.
 
Moshi tulishavuka vyote hivyo,kazi iliyobaki ni kusambaza maujanja kona nyingine za nchi zilizokuwa zimefunikwa uso na blanket chafu la ccm,ipo mbege,denge,kibo gold nk,hivi zomba kwao ni wapi?au nae ni kati ya wahanga wa jiji,wakataa kwao?
 
Baada ya kelele nyingi mkapelekewa kiwanda cha beer hukohuko nyumbani. Kwi kwi kwi teh teh teh!
 
tatizo anayekulipa kumfanyia kazi ni zoba kama wewe maana huna jipya mpaka utaingia kaburini na ufinyu wa mawazo
 
du hulali kwa mdundo wa chadema mbona bado tunafunga viatu kamba mpambano bado tukianza utajificha wapi sijui masikiniQUOTE=zomba;4298560]Baada ya kelele nyingi mkapelekewa kiwanda cha beer hukohuko nyumbani. Kwi kwi kwi teh teh teh![/QUOTE]
 
zomba, yaani utafikiri na wewe ni mtabiri. Moshi tunakunywa mbege. Haina VAT ile...haya maviwanda kila kona yanatusaidia kulewa zaidi na kusahau kufuatilia uporaji wa mali yetu ya asili. Think well about it
Niliwahi kusikia kuwa hivyo viwanda vya bia ndiyo wateja wakubwa wa madawa ya kulevya. sijataka kuamini sana lakini wajomba zangu kule Moshi wawe macho sana maana kule wamekushindwa watataka kumaliza watu akili kiaina!

Maneno ya Zomba siyo ya kupuuza hata kidogo! Watu wa Moshi wanatakiwa kuwa makini sana. Ni kheri wakahakikisha zinazozalishwa hapo hazinyweki pale. Na watafute soko nje!
 
mtoa mada ana matege ya ubongo,aliyekuambia moshi kuna shida ya maji nani?huko tumemaliza enzi ya mwalimu,lami mpaka migombani,umeme mpaka mikahawani kamuulize cptn komba.ttz kwenu mnaohangaika na kansa ccm
 
Mtu hasifiwi kwa kazi ambayo anapaswa kuifanya katika hali ya kawaida..........tusifie pale ambapo amefanya la ziada

Kazi w/aliyotakiwa kukamilisha miaka ishirini na tano iliyopta Mkuu.
Nchi ikiwa na siasa mbaya ni sawa na iliyo katika vita ya kupambana na magaidi. Mfano Tanzania haina tofauti kubwa sana na Columbia. Ila sisi tumeelemewa zaidi maana magaidi-aka-mafisadi-aka-magaidi ndiyo wako madarakani.
 
Kikwete hana lolote alochangia mradi huo, Tunawashukuru Jumuiya ya watu wa ulaya na watu wa ujerumani CCM msitafute sifa ambazo si zenu
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom