Kwa muda kumekuwepo na tetesi kwamba Mbowe angependa sana kuwania nafasi ya urais 2015. Kama hili ni kweli CHADEMA watakuwa na wakati mgumu kwa sababu pamoja na kwamba ametoa mchango mzuri kwenye chama chake lakini kukubalika kwa Mbowe ni tofauti sana na Dr. Slaa. Hapa Mbowe na uongozi mzima wa CHADEMA wanatakiwa wawe very realistic na wajue ni kwanini watanzania wengi wamekikubali hiki chama kwa kasi ya ajabu mara pale tu Dr Slaa alipotangazwa kuwa mgombea wa nafasi ya urais.