EasyFit
JF-Expert Member
- Jul 4, 2011
- 1,269
- 1,082
CHADEMA imesema licha ya Rais Jakaya Kikwete kutia saini Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Katiba ya mwaka 2011, itafanya kila linalowezekana kuhakikisha Tanzania inapata Katiba bora.
Matamko haya yametolewa jana na viongozi wa Chadema walipokuwa wakizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kufungua semina ya siku moja ya viongozi wa chama hicho kutoka katika mikoa 26 ya Tanzania Bara.
Slaa:
"Sisi tuliomba tuonane na rais ili tumshauri aache kusaini katiba ile lakini hatuna uwezo wa kumzuia kwa kuwa katiba yenyewe inamruhusu, hivyo kama ameisaini shauri yake, sisi bado tunaendelea na msimamo wetu wa kuipinga sheria hiyo," alisema.
Alisema kuwa kitendo hicho kimeonesha kuwa Kikwete hakujali hoja za Watanzania na wadau wengine kwa ujumla. Alisema pamoja na yote yaliyotokea, CHADEMA wataendelea kupeleka maoni yao kwa ajili ya marekebisho hayo kama ambavyo walikubaliana kwa pamoja.
Zitto:
"Ni vema juhudi hizi ziendelee, tusikubali kushindwa kupata mwafaka wa kitaifa," alisema Zitto na kusisitiza; "Kwa namna yoyote ile Chadema itaendelea kuchukua hatua zote muafaka kuhakikisha Watanzania wanapata Katiba nzuri na yenye manufaa kwa taifa.
"Watanzania waelewe kwamba hakuna ushindani katika jambo hili. Tunaandaa mazingira mazuri ya kuliandaa Taifa letu liwe na demokrasia zaidi na liweze kutumia rasilimali za nchi kwa maendeleo ya Watanzania," aliongeza.
"Nimewahi kusema na ninarudia kusema tena, Katiba ya nchi inaweza kutafutwa barabarani, lakini kamwe haiandikwi barabarani. Katiba huandikwa mezani kutokana na mazungumzo yanayozaa mwafaka wa Kitaifa," alionya Zitto
Lissu:
"Ninachosema ni kuwa Rais alitukatalia mapendekezo yetu kwa sababu katika kikao kile hatukukubaliana kuwa hataisani muswada huo," alisema Lissu na kuongeza:
"Sisi tunaendelea kufanya efforts (juhudi), kuendelea kusimamia hoja zetu na tunajiandaa kupeleka hoja bungeni kubadilishwa kwa sheria hii," alisema.
"Tutawaambia wabunge waangalie maslahi ya wananchi, wapige kura kwa maslahi ya wananchi na si kwa maslahi ya chama fulani," alifafanua.
Matamko haya yametolewa jana na viongozi wa Chadema walipokuwa wakizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kufungua semina ya siku moja ya viongozi wa chama hicho kutoka katika mikoa 26 ya Tanzania Bara.
Slaa:
"Sisi tuliomba tuonane na rais ili tumshauri aache kusaini katiba ile lakini hatuna uwezo wa kumzuia kwa kuwa katiba yenyewe inamruhusu, hivyo kama ameisaini shauri yake, sisi bado tunaendelea na msimamo wetu wa kuipinga sheria hiyo," alisema.
Alisema kuwa kitendo hicho kimeonesha kuwa Kikwete hakujali hoja za Watanzania na wadau wengine kwa ujumla. Alisema pamoja na yote yaliyotokea, CHADEMA wataendelea kupeleka maoni yao kwa ajili ya marekebisho hayo kama ambavyo walikubaliana kwa pamoja.
Zitto:
"Ni vema juhudi hizi ziendelee, tusikubali kushindwa kupata mwafaka wa kitaifa," alisema Zitto na kusisitiza; "Kwa namna yoyote ile Chadema itaendelea kuchukua hatua zote muafaka kuhakikisha Watanzania wanapata Katiba nzuri na yenye manufaa kwa taifa.
"Watanzania waelewe kwamba hakuna ushindani katika jambo hili. Tunaandaa mazingira mazuri ya kuliandaa Taifa letu liwe na demokrasia zaidi na liweze kutumia rasilimali za nchi kwa maendeleo ya Watanzania," aliongeza.
"Nimewahi kusema na ninarudia kusema tena, Katiba ya nchi inaweza kutafutwa barabarani, lakini kamwe haiandikwi barabarani. Katiba huandikwa mezani kutokana na mazungumzo yanayozaa mwafaka wa Kitaifa," alionya Zitto
Lissu:
"Ninachosema ni kuwa Rais alitukatalia mapendekezo yetu kwa sababu katika kikao kile hatukukubaliana kuwa hataisani muswada huo," alisema Lissu na kuongeza:
"Sisi tunaendelea kufanya efforts (juhudi), kuendelea kusimamia hoja zetu na tunajiandaa kupeleka hoja bungeni kubadilishwa kwa sheria hii," alisema.
"Tutawaambia wabunge waangalie maslahi ya wananchi, wapige kura kwa maslahi ya wananchi na si kwa maslahi ya chama fulani," alifafanua.