The Hunter
JF-Expert Member
- Dec 25, 2010
- 1,049
- 305
Kimsingi tumeshuhudia pilika pilika na mbwembwe nyingi pindi inapotokea uchaguzi mdogo, mambo haya yamekuwa yakienda pamoja na gharama kubwa za maandalizi miongoni mwa vyama vinavyogombea.
Naamini Uchaguzi ujao wa Meru Mashariki, CDM lazima kifanye maamuzi magumu na maandalizi makubwa hii nikutokana na sababu zifuatazo;-
. Meru Mashariki ipo Arusha mkoa ambao CDM ina amini ndio ngome yake, huku CCM kikijaribu kurudisha heshima
. Ni jimbo ambalo 70% ya vijana wake hawana ajira rasmi na hii nikutokana na wengi wao kulazimishwa kuondoka machimboni kule Mbuguni
.Wakina mama wa jimbo lile ndo wafanyakazi wakubwa katika sekta nzima ya kiuchumi, kwani wanaume wengi si wafanyaji kazi
.Ni jimbo ambalo vijana wengi ni wajanja na waliotayari kufanya lolote ili kupata pesa
.Ni jimbo la mtego kwa Mh.Lowasa kwani bila shaka atakuwa kwenye kamati maalumu ya kuhakikisha jimbo linarudi CCM
.Wengi ya wakazi wa jimbo hili ni Wameru,Waarusha, Wamasai,Wachaga na makabila mengine madogo.
. Jimbo la Meru Mashariki lipo karibu na mjini anapotoka Kamanda Lema hivyo CCM wanajua ugumu watakao kumbana nao
Nionavyo
CDM lazima kimpitishe mtu anaekubalika na mwenye kuaminika,
siamini kama kijana wetu alieshindwa 2010 bwana Nasari ni chaguo muhafaka kwa kinyanganyiro hichi
hii ni kutokana na ukweli Sumari hakufanya kampeni lakini alimshinda hii ina leta picha kwamba huyu kijana hakubaliki sana
Ikumbukwe CCM watakuwa radhi kuingia gharama mara mbili ya Igunga ili kushinda jimbo hili
Na ni ukweli usiposhiba jikoni huwezi shibia sebuleni kama 2010 ulishindwa je 2012 ambapo Wapinzani wote wanaangalia jimbo hilo hilo utashinda vipi?
. Mtu alie karibu na anaefamika na kufikika wakati wote
Kuwa mbali na wananchi wako ni jambo jingine ambalo kijana Nasari litamfanya asichagulike,
mfano, Bashe, Shigongo na wengine wengi japo hawakupata nafasi za kupitishwa na vyama vyao still wapo kwenye majimbo yao mara kwa mara wakishiriki na wananchi wenzao shughuli za kila siku.
Naamini Uchaguzi ujao wa Meru Mashariki, CDM lazima kifanye maamuzi magumu na maandalizi makubwa hii nikutokana na sababu zifuatazo;-
. Meru Mashariki ipo Arusha mkoa ambao CDM ina amini ndio ngome yake, huku CCM kikijaribu kurudisha heshima
. Ni jimbo ambalo 70% ya vijana wake hawana ajira rasmi na hii nikutokana na wengi wao kulazimishwa kuondoka machimboni kule Mbuguni
.Wakina mama wa jimbo lile ndo wafanyakazi wakubwa katika sekta nzima ya kiuchumi, kwani wanaume wengi si wafanyaji kazi
.Ni jimbo ambalo vijana wengi ni wajanja na waliotayari kufanya lolote ili kupata pesa
.Ni jimbo la mtego kwa Mh.Lowasa kwani bila shaka atakuwa kwenye kamati maalumu ya kuhakikisha jimbo linarudi CCM
.Wengi ya wakazi wa jimbo hili ni Wameru,Waarusha, Wamasai,Wachaga na makabila mengine madogo.
. Jimbo la Meru Mashariki lipo karibu na mjini anapotoka Kamanda Lema hivyo CCM wanajua ugumu watakao kumbana nao
Nionavyo
CDM lazima kimpitishe mtu anaekubalika na mwenye kuaminika,
siamini kama kijana wetu alieshindwa 2010 bwana Nasari ni chaguo muhafaka kwa kinyanganyiro hichi
hii ni kutokana na ukweli Sumari hakufanya kampeni lakini alimshinda hii ina leta picha kwamba huyu kijana hakubaliki sana
Ikumbukwe CCM watakuwa radhi kuingia gharama mara mbili ya Igunga ili kushinda jimbo hili
Na ni ukweli usiposhiba jikoni huwezi shibia sebuleni kama 2010 ulishindwa je 2012 ambapo Wapinzani wote wanaangalia jimbo hilo hilo utashinda vipi?
. Mtu alie karibu na anaefamika na kufikika wakati wote
Kuwa mbali na wananchi wako ni jambo jingine ambalo kijana Nasari litamfanya asichagulike,
mfano, Bashe, Shigongo na wengine wengi japo hawakupata nafasi za kupitishwa na vyama vyao still wapo kwenye majimbo yao mara kwa mara wakishiriki na wananchi wenzao shughuli za kila siku.