Chadema: Kwanini vyuo vikuu

Mkuu, unachanganya mambo. Wanafunzi wa vyuo vikuu wenyewe ndiyo waliwaalika viongozi wa Chadema kwenye kongamano lao wawahutubie. Chadema inaungwa mkono sana na wanafunzi wa vyuo, wasomi, wafanyakazi na watu wengine walioelimika. Hii ni kutokana na kuwa elimu yao imewafanya waweze kuchambua hoja za Chadema na kuzielewa na kuzikubali. Elimu yao pia imebaini kuwa CCM wametawala nchi hii kwa nusu karne (miaka 50) na kushindwa kuleta maendeleo hivyo ni muda sasa wa kuleta mabadiliko.

CCM bado inaendelea kuungwa mkono na baadhi ya wananchi wa vijijini kutokana na elimu yao duni. CCM wanatumia ujinga wa wananchi wake kuendelea kuwatawala kwa kuwatisha wasilinde kura vituoni, waogope wapinzani kuwa wataipeleka nchi iwe kama Rwanda au Somalia na wajigambe kuwa CCM ndiyo chama pekee cha kuleta amani na utilivu.

Kadri elimu inavyozidi kusambaa ndiyo jinsi CCM inavyozidi kuporomoka madarakani, watoto wa sasa wa primary na sekondari wakifikia umri wa kupiga kura 2015 wakaungana na wenzao wa vyuo ni kiama zaidi kwa CCM.
hizo ni hadithi tu,watanzania wanahitaji huduma za jamii siyo CDM
 
Hawa wanafunzi wetu wengi wanatoka vijijini sasa CDM inatakiwa kuwambia kuwa wawaeleze ndugu zao juu ya umuhimu wa katiba mpya na suala la dowans. Unajua tatizo haliko vyuo vikuu,tatizo liko vijijini ambako kuna uelewa mdogo wa wananchi na huo ndiyo mtaji wa mafisadi.
Na ndicho wanacho kifanya ref; penye red
 
sasa wewe unashangaa nin?hujui km m2 akishafika chuo ndo mtu mzima kamil?hebu kuwa muwaz hapa unachotaka ku2ambia...'elmu kwnz tunakuomba plz'
 
ElimuKwanza, pointi yako ni mzuri sana kwamba CDM kusirudie makosa bali tuwe makini zaidi katika kutumia hii strategy ya kuwakomba wasomi nchini. Great Thinkers, tuwe tunasoma hoja kwa ukamilifu wake kwanza ndio tuweze kuchangia uzuri mawazo yetu.

Wewe ndio ujifunze kusoma hoja, ina maana sisi ni vipofu? ulichoandika hapo sio hoja ya mtoa mada hiyo ni hoja yako wewe, ingekuwa vyema kama ungeianzishia thread yake. mtu yeyote humu anaeandika hoja yake kwa ukamilifu bila mawaa huwa watu wanakwenda straight kwenye kuichaingia haaitaji kuvaa miwani ndio uone kilichoandikwa.
 
Siku za karibuni sasa ni dhahiri CDM wameamua kutumia wanafunzi wa vyuo vikuu katika kile wanachokiita kudai mabadiliko.Mimi kwa mtizamo wangu wasiwe wana take advantage ya matatizo yao kufanikisha malengo yao ya kisiasa.hawa wanafunzi wetu wengi wanatoka vijijini sasa cDMinatakiwa kuwambia kuwa wawaeleze ndugu zao juu ya umuhimu wa katiba mpya na suala la dowans.Unajua tatizo aliko vyuo vikuu,tatizo liko vijijini ambako kuna uelewa mdogo wa wananchi na huo ndiyo mtaji wa mafisadi.

Je umesoma tena ulichoandika kuona jinsi unavyojichanganya? Kwanza umetumia lugha ya "kile wanachokiita kudai mabadiliko". Sasa labda ungetusaidia kwa kutueleza mabadiliko kwa muktadha wako kwanza ili tuone kama mabadiliko unavyoyajua wewe yana tofauti yoyote na kile CHADEMA wanachokiita mabadiliko.

Pili umewalaumu CHADEMA kwa ku "take advantage" ya wanafunzi kufanikisha malengo yao ya kisiasa lakini unawapa ushauri kuwa CHADEMA wanatakiwa wawaambie wanafunzi wawaeleze ndugu zao juu ya umuhimu wa katiba mpya na suala la dowans. Sasa CHADEMA watawaeleza vipi wanafunzi bila kukutana nao kama walivyofanya? Je wanaweza kuwaeleza wanafunzi mambo hayo bila kufanikisha malengo yao ya kisiasa ambayo ni kuwahamasisha wananchi kudai haki zao?
 
mtu mwenye elimu ya chuo huwezi kumdanganya ameisha funguka macho.ccm wanataka watu wasioenda shule ili wapate kuwadanganya.wakati huo umeisha.Nawapongeza CDM kwa muelekeo wao huo.
 
hizo ni hadithi tu,watanzania wanahitaji huduma za jamii siyo CDM

miaka 50 baada ya uhuru. huduma za jamii ni za hovyo au hazipo kabisa.

50 years!!!!?????????????????

tumechoka.

sasa hatutaki tena hizo huduma zenu za kisanii.

Tunataka Chadema!!!
 
hizo ni hadithi tu,watanzania wanahitaji huduma za jamii siyo CDM

Elimukwanza punguza mhemko.

Unaposema wanahitaji huduma sio CDM, hizo huduma zinaletwa na nani???
Watu wakihoji hoja yako ni vema ukajitahidi kufafanua. Kimsingi hoja yako haijaeleweka iwapo unataka CDM wasijihusishe na wanafunzi/wasomi au unawapa tahadhari ya namna wanavyojihusisha na wasomi. Tusaidie kukuelewa kwa kuboresha post yako.

Kwa ufahamu wangu kama hawa wasomi wanatoka vijijini na wanaelewa nini CDM itatetea basi itakuwa rahisi kwao kufikisha ujumbe wa CDM kwa ndugu na jamaa zao walioko vijijini.
Na kwa sasa kazi ya wasomi itakuwa rahisi maana shule za kata ni kitanzi kingine cha CCM. Hawa watoto wanajua kupata habari hata kama ni kwa kutumia simu. Kadri tabaka la wasiosoma linavyopungua ndivyo nguvu ya CCM inavyoisha kwa kasi.

Lakini pia mwaka 2009 - 2010 CDM wamekuwa na operesheni Sangara iliyoanzia kanda ya ziwa (ngome ya ccm) na imewalipa wabunge Musoma, Mwanza, Maswa east and west, Bukombe, Meatu, Shinyanga na Kahama (wakaibiwa). Ukweli kwamba hawa jamaa (CDM) ni jinamizi la mchana kwa watawala na hakuna namna inabidi watulie kama unaponyolewa.
 
Wanafunzi wa Vyuo Vikuu hawataisaidia sana CHADEMA. Wanasoma kwa mkopo na ruzuku ya serikali. Watu watakaoisaidia CHADEMA ni hawa wa mitaani na hasa maeneo ya mijini. Wajue namna ya kuwatumia bila ya kusababisha mauaji kama ilivyotokea Arusha.

CHADEMA wawe na agenda itakayoonekana kuwasaidia vijana hawa wa mitaani. Iwasikilize wao kwanza.

Hawa wa vyuo vikuu ni waoga, wanafiki kama walivyo baba na mama zao walioko CCM.
 
Siku za karibuni sasa ni dhahiri CDM wameamua kutumia wanafunzi wa vyuo vikuu katika kile wanachokiita kudai mabadiliko.

Mimi kwa mtizamo wangu wasiwe wana-take advantage ya matatizo yao kufanikisha malengo yao ya kisiasa. Hawa wanafunzi wetu wengi wanatoka vijijini sasa CDM inatakiwa kuwambia kuwa wawaeleze ndugu zao juu ya umuhimu wa katiba mpya na suala la DOWANS.

Unajua tatizo aliko vyuo vikuu, tatizo liko vijijini ambako kuna uelewa mdogo wa wananchi na huo ndiyo mtaji wa mafisadi.
Mabadiliko ya kweli yanaaanza na wanavyuo. Hata Nyerere alianza siasa za kumuondoa mkoloni chuoni.

Soma historia kwani haijipingi.
 
Wanafunzi wa Vyuo Vikuu hawataisaidia sana CHADEMA. Wanasoma kwa mkopo na ruzuku ya serikali. Watu watakaoisaidia CHADEMA ni hawa wa mitaani
na hasa maeneo ya mijini. Wajue namna ya kuwatumia bila ya kusababisha mauaji kama ilivyotokea Arusha. CHADEMA wawe na agenda itakayoonekana kuwasaidia vijana hawa wa mitaani. Iwasikilize wao kwanza.
Hawa wa vyuo vikuu ni waoga, wanafiki kama walivyo baba na mama zao walioko CCM.


Kwahiyo hapo kwenye RED unataka kutuaminisha kwamba wabunge watarajiwa wataenda kuokotezwa mitaani na sio kwenye kada za wasomi? hivi unadhani CHADEMA ni chama cha mambumbumbu kiache kurecruite wasomi waende mitaani kuokoteza majobless kama Tambwe Hiza? vijaana wa mitaani wanaitaji vijana wenzao ambao wamepata fursa ya kupata elimu nzuri wachukuwe uongozi wa nchi na kuwapelekea kwenye nchi ya maziwa mito na asali. CCM ndicho chama chenye fursa ya watu wa mitaani kupewa vyeo ili waendelee kukiuwa chama.
 
Wanafunzi wa Vyuo Vikuu hawataisaidia sana CHADEMA. Wanasoma kwa mkopo na ruzuku ya serikali. Watu watakaoisaidia CHADEMA ni hawa wa mitaani na hasa maeneo ya mijini. Wajue namna ya kuwatumia bila ya kusababisha mauaji kama ilivyotokea Arusha.

CHADEMA wawe na agenda itakayoonekana kuwasaidia vijana hawa wa mitaani. Iwasikilize wao kwanza.

Hawa wa vyuo vikuu ni waoga, wanafiki kama walivyo baba na mama zao walioko CCM.

Great thinker huyo, si mchezo ati!
 
kumbuka haba na haba...., wakianzia vyuoni, sawa, mitaani poa, vijijini, dole, tabu yako nini, mapambano ndo ameanza, hiyo ndo strategy yao , usitake umaarafu subiri tulia kama unanyolewa,
 
Tunapoweka mikakati huwa tunaangalia maeneo muhimu kimkakati. Wasomi ni moja ya maeneo muhimu katika kujenga mkakati kwa sababu ya uelewa wao mkubwa, uwezo wao wa ushawishi na pia ni watu wasioogopa mabadiliko.

Nadhani CDM wako sahihi sana kufanyia shughuli zao kwenye makundi ya wasomi kama wamekusudia kuleta mabadiliko. Mimi nawapongeza hata kama wangekuwa hawajaitwa na wanafunzi, walipaswa kufanya wanayoyafanya.

Nafurahia ujasiri wa wasomi kuhusu mustakabali wa taifa letu. nafurahia pia uwezo wa ushawishi walionao CDM katika kumtetea mwananchi. Hongera Chadema kwa kuchukua hatua hizi kuelimisha uma. ipo siku kitaeleweka.
 
Siku za karibuni sasa ni dhahiri CDM wameamua kutumia wanafunzi wa vyuo vikuu katika kile wanachokiita kudai mabadiliko.

Mimi kwa mtizamo wangu wasiwe wana-take advantage ya matatizo yao kufanikisha malengo yao ya kisiasa. Hawa wanafunzi wetu wengi wanatoka vijijini sasa CDM inatakiwa kuwambia kuwa wawaeleze ndugu zao juu ya umuhimu wa katiba mpya na suala la DOWANS.

Unajua tatizo aliko vyuo vikuu, tatizo liko vijijini ambako kuna uelewa mdogo wa wananchi na huo ndiyo mtaji wa mafisadi.

Sio CHADEMA liyoamua, bali wanafunzi ndio walioamua kukiunga mkono CHADEMA. CCM ndiyo inalazimisha uhalali wake kwa vyuo vikuu.
 
Siku za karibuni sasa ni dhahiri CDM wameamua kutumia wanafunzi wa vyuo vikuu katika kile wanachokiita kudai mabadiliko.

Mimi kwa mtizamo wangu wasiwe wana-take advantage ya matatizo yao kufanikisha malengo yao ya kisiasa. Hawa wanafunzi wetu wengi wanatoka vijijini sasa CDM inatakiwa kuwambia kuwa wawaeleze ndugu zao juu ya umuhimu wa katiba mpya na suala la DOWANS.

Unajua tatizo aliko vyuo vikuu, tatizo liko vijijini ambako kuna uelewa mdogo wa wananchi na huo ndiyo mtaji wa mafisadi.

Umeshasema kuwa watu wa vijijini wana uelewa mdogo na huku mjini tuna wasomi wenye uelewa mkubwa ambao wanatoka huko vijijini kwa watu wenye uelewa mdogo; huoni kuwa ni sahihi kuwatumia hawa ili wakawaelimishe hao wa vijijini? Na hilo ndio hasa lengo la chadema na huo ndio ukweli wa mambo kwa mtu yeyote aliye makini. Tanzania ina wilaya zaidi ya 120 je vijiji vitakuwa vingapi? Unadhani kuna njia rahisi kwa chadema kuwafikia wananchi wengi wa huko vijijini bila kutumia njia ya wawakilishi? Tafakari kabla ya kuongea!
 
Back
Top Bottom