CHADEMA kuweni makini sana, kilicho nyuma ya pazia hiki hapa!

...du, kuna vitu vyaonyesha haya yana ukweli... Mgombea binafsi, ushindi kuhojiwa mahakamani.... Mbwembwe za Shibuda... Mikutano ya "siri" kati ya Mbowe Jk....
 
Nundu na Kikwete wapi na wapi kwenye U-rais?.Nundu mwenyewe mpaka anatemwa Uwaziri alikuwa analia na Ikulu kumuhujumu kupitia kwa Naibu wake Athuman Mfutakamba.Mkubwa kuona hii ni soo kawapiga wote chini.

''Sihitaki hii, nimeiacha''.
 
...du, kuna vitu vyaonyesha haya yana ukweli... Mgombea binafsi, ushindi kuhojiwa mahakamani.... Mbwembwe za Shibuda... Mikutano ya "siri" kati ya Mbowe Jk....

Mmmmmhhh Hapa pana walakini.....!!??
 
Tiss imegawanyika katika makundi 7 na kila moja linafanya kazi kwa maslahi ya mtu flan lakini wanalipwa na serikali...kundi linalofanya kazi kwa maslahi ya nchi linapingwa vibaya sana na wengi wanapotea kwa formula ya costra nostra ...tangu 2008 kazi za kichunguzi zimekuwa zikifanywa na mashirika ya nje ya kijasus...

Tulifikaje hapo mungu?
 
2. JK ajiuzulu urais mnamo mwaka 2013 hivi ili chini ya Bilal na kwa muda mfupi mabadiliko makubwa yafanyike na CHADEMA waweze kujumuishwa katika serikali hasa Dr Slaa ili kujipanga kukimaliza CHADEMA kwa urais zaidi. Ingawa JK alihofia hii technique kwa maana ya Bilal but hii naona ina mkono wa "wafanyabiashara" wakubwa wa mataifa Fulani ambao wanataka biashara zao ziende vizuri kama JK ataondoka madarakani kwani akiendelea hataweza kumweka mtu wao ili aendelee kulinda 'maslahi Fulani'

taarifa hii inaweza kuwa ya kweli lakini, ngumu JK kuachia ngazi!!!!!!
 
Mambo ya kusadikika haya. Sijapata picha ya lolote kati ya haya kuwa litatekelezeka.

Ngoja tu nisitake na niyaache
Intelijensia... Inabidi akili itulie sana ili kuamini mipango ya aina hii, lakini ni mipango inayowezekana kabisa.
 
Aaaaah....aaaah.The so called ''Hutaki Unaacha'' amefanikiwa sana ku confuse jamvi hapa.Kweli Tanzania bado kuna kazi mbele, kwa hivi vichwa vya panzi! ''Not yet Uhuru''.Stori hizi hazina tofauti na zile ninazozipata kwenye kakijiwe kangu ka kahawa na kashata pale Msimbazi-Kariakoo.

nenda tena hapo kwenye ka kijiwe kisha uwaulize hao wanywaji wenzao juu ya mahali walipo wale vijana waliomkamata maige mwaka jana pale kibo palace akipokea pesa toka kwa wale jamaa wa vitalu akabanwa na kuulizwa na nani amemtuma kisha akutoboa na kueleza siri nzito juu ya biashara za mkuu wa nchi....wakikujibu waulize tena juu ya watu sita waliopelekwa bulgaria..wamekwenda kufanya nini na kwa nini kinaitwa kikosi maalumu kwa ajili ya kuidhibiti chadema kabla ya 2015??

wakiwa na majibu hayo basi nami ntakuja nijiunge
 
Nundu na Kikwete wapi na wapi kwenye U-rais?.Nundu mwenyewe mpaka anatemwa Uwaziri alikuwa analia na Ikulu kumuhujumu kupitia kwa Naibu wake Athuman Mfutakamba.Mkubwa kuona hii ni soo kawapiga wote chini.

''Sihitaki hii, nimeiacha''.


ntantoka nje ya mada kidogo ili kukusaidia..hili ulikuwa unalijua?


Mkapa hakuwa mtu wa JK tokea mwanzo. Lakini pia Mkapa hakuwa na chaguo lolote la wazi. Je ni Kwanini? Ni kwasababu, Nyerere miaka yote amekuwa anamtaka Salim kuwa Rais. Nyerere aliposhindwa kuamsha tena jina hilo chini kwa chini mwaka 1995, Mkapa ndiye akawa "his fallback position" (yani kwa Nyerere). Kwahiyo Mkapa kumbeba mtu mwingine nje ya yule ambae Nyerere alimpenda, ingekuwa kama usaliti kwa mtandao wa Nyerere. Lakini chini kwa chini, Mkapa alimtaka Hassy Kitine kumpokea mwaka 2005. Alianza kwa kuunda nafasi mpya kabisa tangia uhuru ya Uwaziri wa nchi utawala bora (Usalaam wa taifa), na kumfanya kitine kuwa waziri wa kwanza, ili ajijengee mazingira ya 2005. Lakini kina ENL, RO,
waliligundua hili mapema sana na hivyo kummaliza Kitine bungeni kwa kashfa ya kutumia dola elf 60 kwa ajili ya matibabu ya mkewe Canada. Baada ya hayo, Mkapa alibakia anaelea, asijue la kufanya. Isitoshe, hata mabalozi wa
Marekani, Uingereza, na nchi nyingine kubwa walikuwa wanamuonya sana Mkapa kwamba Kikwete hafai, ataingiza nchi katika matatizo.


Mwaka 2005, mkakati wa mkapa inasemekana ulikuwa ni kuwatosa wagombea wote ambao walikuwa na nguvu kubwa kwenye jamii, ili kuepuka mfarakano iwapo kundi moja litaonekana limeonewa. Kwa mfano, Sumaye
alikuwa na kundi kubwa la wakuu wa mikoa, wakuu wa wilaya, na viongozi wengi wa halmashauri za wilaya. Malecela alikuwa na kundi kubwa sana viongozi wa CCM kitaifa, lakini pia wenyeviti na makatibu wa CCM mikoa
na wilaya. Kikwete alikuwa na kundi kubwa sana la viongozi wa kitaifa wa UVCCM, UWT kutokea mwaka 1995 hadi 2005, huku akidokoa dokoa wengine wengi kutoka katika makundi hayo hapo juu. Mikakati ya Mkapa
ikaingia dosari pale ENL, JK, RA, walipotoa msimamo kwamba iwapo Kikwete atatoswa, watahamia Chadema. Ndipo Mkapa akaunda timu ya kutembea nchi nzima kutafiti hilo, chini ya Absom, ambae whether ni kutonana na utafiti wa kweli au uliokwisha andaliwa mapema na kina EL, RA, akamletea taarifa Mkapa kwamba Kikwete akiachwa, CCM itapasuka, na nchi
itaingia katika machafuko. Huu ndio ukawa mwanzo wa Mkapa kulibeba jina la Kikwete kwa mtindo wa kura moja badala ya tatu Dodoma.

hivi unaijua tanzania unayodai ni nchi yako?!! ulikuwa unajua kuwa mkapa alimtka hans kitine amrith?
 
About Private Candidate Am absolutely sure Hutaki Unaacha ameuweka ukweli kwenye mabano ili kunusuru mpasuko ndani ya Chadema japo darubini yangu kali naona kama anaulea na kuumba huo mpasuko.

Ofcourse Massive Political Empass will erupt within the Party b4 2015 na kitakachonusuru huu mpasuko ni kuchelewa kukamilika kwa Katiba Mpya
 
Hutaki unaacha, asante kwa nondo, sisi tunatafakari na kuangalia upepo uvumavyo.

Kitu ninachokubali moja kwa moja ni Chadema kuweni makini, kila clue inayopatikana, kwa watu makini ni jambo la kufanyia kazi.
Nani asiyejua kuwa kura za Dk Slaa zilichakachuliwa? CCM wanajua wazi kuchakachua kura za urais 2015 itakuwa kazi ngumu sana, na yawezekana matokeo ya uchakachuaji kura za urais 2015 yanaweza kuingiza nchi yetu kwenye historia na ukizingatia ICC imeshatinga Kenya, wanatutolea macho Tanzania.



Nimeipenda hii Kamanda!

Mfa maji haachi kutapatapa wajamen!

ccm wapo ICU jamani!
 
Hakuna ukweli hapa, tena chadema wawe makini na hii taarifa maana naona ni yakuwafanya wavimbe vichwa kwamba wameweza tayari kumbe bado kazi ni kubwa sana. Sijaona mkakati hapa zaidi ya kuisifia chadema indirectly
 
Back
Top Bottom