Ng'wanza Madaso
JF-Expert Member
- Oct 21, 2008
- 2,268
- 333
Hili swali nilimuuliza Dr.Slaa jana japo hakunijibu nimefurahi kupata habari hii.Nawashukuru sana CHADEMA kwa kulitambua hili na kuwasaidia wana Kaliua wanaonyanyasika mikononi mwa watoto wa Mafisadi
CHADEMA kuwatetea wakazi Urambo
na Joseph Senga, Tabora
CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimeapa kusimamia kesi zote zinazowakabili wakazi wa jimbo la Urambo Magharibi zikiwamo za manyanyaso, kupigwa na wengine kuuawa na baadhi ya viongozi wa jimbo hilo.
Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dk. Willbrod Slaa akizungumza katika mkutano wa hadhara jana mkoani hapa alieleza kusikitishwa na manyanyaso yanayofanywa na viongozi wa jimbo hilo hususan kwa wananchi wa mji wa Kaliua.
Dk. Slaa alipewa taarifa ya manyanyaso hayo na baadhi ya wananchi wa mji huo kabla ya kuanza kuhutubia mkutano huo uliofanyika katika uwanja wa tarafa ya Kaliua.
Katika majibu yake, Dk. Slaa alisema chama chake kitasimamia kesi zote zinazohusu manyanyaso hayo kwa kuwaweka mawakili, ili wahusika wafikishwe mahakamani.
"Nimesikitishwa sana kwamba dunia ya leo kuna watu bado wananyanyasa wenzao kwa sababu ni vigogo au watoto wa vigogo.
"Sasa CHADEMA tumeapa kuwa tutasimamia kesi zote ambazo zimetupwa na polisi na kuwaweka mawakili ili haki itendeke," alisema Dk. Slaa.
Awali, baadhi ya wananchi waliohudhuria mkutano huo walidai mtoto wa mbunge wa jimbo hilo amekuwa akiwanyanyasa wananchi husasan wale wanaojiunga na vyama vya upinzani.
Walidai mtoto huyo ambaye alikuwapo eneo la mkutano huo, hutumia wadhifa wa baba yake kuwatisha na kuwapiga vijana ambao hukataa kutii matakwa yake na kwamba askari hukwepa kumtia mikononi mwa sheria.
Source:Freemedia.co.tz
CHADEMA kuwatetea wakazi Urambo
na Joseph Senga, Tabora
CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimeapa kusimamia kesi zote zinazowakabili wakazi wa jimbo la Urambo Magharibi zikiwamo za manyanyaso, kupigwa na wengine kuuawa na baadhi ya viongozi wa jimbo hilo.
Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dk. Willbrod Slaa akizungumza katika mkutano wa hadhara jana mkoani hapa alieleza kusikitishwa na manyanyaso yanayofanywa na viongozi wa jimbo hilo hususan kwa wananchi wa mji wa Kaliua.
Dk. Slaa alipewa taarifa ya manyanyaso hayo na baadhi ya wananchi wa mji huo kabla ya kuanza kuhutubia mkutano huo uliofanyika katika uwanja wa tarafa ya Kaliua.
Katika majibu yake, Dk. Slaa alisema chama chake kitasimamia kesi zote zinazohusu manyanyaso hayo kwa kuwaweka mawakili, ili wahusika wafikishwe mahakamani.
"Nimesikitishwa sana kwamba dunia ya leo kuna watu bado wananyanyasa wenzao kwa sababu ni vigogo au watoto wa vigogo.
"Sasa CHADEMA tumeapa kuwa tutasimamia kesi zote ambazo zimetupwa na polisi na kuwaweka mawakili ili haki itendeke," alisema Dk. Slaa.
Awali, baadhi ya wananchi waliohudhuria mkutano huo walidai mtoto wa mbunge wa jimbo hilo amekuwa akiwanyanyasa wananchi husasan wale wanaojiunga na vyama vya upinzani.
Walidai mtoto huyo ambaye alikuwapo eneo la mkutano huo, hutumia wadhifa wa baba yake kuwatisha na kuwapiga vijana ambao hukataa kutii matakwa yake na kwamba askari hukwepa kumtia mikononi mwa sheria.
Source:Freemedia.co.tz