CHAMA Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kimetangaza rasmi kusitisha kuwapokea viongozi wa ngazi zote watakaohama kutoka Chama Cha Mapinduzi (CCM) na vyama vingine, baada ya kutemwa katika kura za maoni kwa lengo la kutaka kuwania nafasi za uongozi ndani ya chama hicho.
Mwenyekiti wa Taifa wa CHADEMA, Freeman Mbowe, alitoa msimamo huo jana alipokutana na wanafunzi wa vyuo vikuu vitatu vya Udom, CBE na St John, katika hafla ya kuwaaga wenzao wanaomaliza masomo yao.
Mbowe alisema kuwa, CHADEMA kinataka sasa kupata viongozi na wanachama wanaosukumwa na uzalendo wa kweli, na wanaoamini itikadi na sera zake, na si wanaotaka kukitumia kama ngazi ya kufanikisha malengo yao.
Alisema wamejifunza kwa kiasi kikubwa hasara ya kuwapokea wanachama, na hasa waliokuwa viongozi wa vyama vingine dakika za mwisho, hususan wakati wa uchaguzi, hivyo kuanzia sasa hawapo tayari kufanya hivyo.
Mbowe alisema wapo tayari na wanawakaribisha wanachama ama viongozi wa CCM ambao wanaona kuwa CHADEMA ni chama makini, kikomavu na wanaoamini kina malengo halisi ya kuikomboa nchi na kuwaletea maendeleo wananchi wote bila kujali itikadi ya vyama, dini, kabila ama eneo la nchi.
"Wale wapambanaji waliochoshwa na matendo ya wenzao ndani ya CCM, na wanaoamini kwa dhati kabisa na kusukumwa na dhamiri ya kweli ya kupigania maslahi ya wanyonge, waje sasa.
"Hakuna haja ya wao kusubiri hadi dakika za mwisho, na hasa pale wanapopigwa chini katika kura za maoni ndio waje. Wajue kuwa wakisubiri muda huo, hawataweza kupokelewa hata kama watakuwa ni wazuri namna gani," alisema Mbowe
Source: Tanzania Daima
My take: Hii itasaidia sana kukwepa kadhia kama ya Shibuda. Na ingekuwa vizuri kwa kila chama. Haiwezakani leo uko chama hiki lakini kesho uko upande wa pili. Unasimamia nini? Tumeona Kenya jinsi siasa zimegubikwa na wakubwa kuhama hama kila mara. Mwishoni mnajikuta vyama vyote viko contaminated maana viongozi wanakuwepo si kwa sababu ya principle bali kuendeleza 'ulaji'. Thanks Shibuda - learned the hard way!
Mwenyekiti wa Taifa wa CHADEMA, Freeman Mbowe, alitoa msimamo huo jana alipokutana na wanafunzi wa vyuo vikuu vitatu vya Udom, CBE na St John, katika hafla ya kuwaaga wenzao wanaomaliza masomo yao.
Mbowe alisema kuwa, CHADEMA kinataka sasa kupata viongozi na wanachama wanaosukumwa na uzalendo wa kweli, na wanaoamini itikadi na sera zake, na si wanaotaka kukitumia kama ngazi ya kufanikisha malengo yao.
Alisema wamejifunza kwa kiasi kikubwa hasara ya kuwapokea wanachama, na hasa waliokuwa viongozi wa vyama vingine dakika za mwisho, hususan wakati wa uchaguzi, hivyo kuanzia sasa hawapo tayari kufanya hivyo.
Mbowe alisema wapo tayari na wanawakaribisha wanachama ama viongozi wa CCM ambao wanaona kuwa CHADEMA ni chama makini, kikomavu na wanaoamini kina malengo halisi ya kuikomboa nchi na kuwaletea maendeleo wananchi wote bila kujali itikadi ya vyama, dini, kabila ama eneo la nchi.
"Wale wapambanaji waliochoshwa na matendo ya wenzao ndani ya CCM, na wanaoamini kwa dhati kabisa na kusukumwa na dhamiri ya kweli ya kupigania maslahi ya wanyonge, waje sasa.
"Hakuna haja ya wao kusubiri hadi dakika za mwisho, na hasa pale wanapopigwa chini katika kura za maoni ndio waje. Wajue kuwa wakisubiri muda huo, hawataweza kupokelewa hata kama watakuwa ni wazuri namna gani," alisema Mbowe
Source: Tanzania Daima
My take: Hii itasaidia sana kukwepa kadhia kama ya Shibuda. Na ingekuwa vizuri kwa kila chama. Haiwezakani leo uko chama hiki lakini kesho uko upande wa pili. Unasimamia nini? Tumeona Kenya jinsi siasa zimegubikwa na wakubwa kuhama hama kila mara. Mwishoni mnajikuta vyama vyote viko contaminated maana viongozi wanakuwepo si kwa sababu ya principle bali kuendeleza 'ulaji'. Thanks Shibuda - learned the hard way!