CHADEMA kutoa uamuzi wa maamuzi ya Mahakama Jumamosi NMC Arusha

Natoa Wito Kwa Chadema wakate rufani.........wakati huu ambao kesi ya rufani unaendelea Lema aendelee kuwatumikia wanannchi ......nakubaliana na aliyesema hapa kuwa hukumu hii mbaya lazima ibatilishwe isije ikaendelea kutafuna haki za watanzania...
 
Sio kazi ya lema kukata rufaa. Huo ubunge ulikuwa sio wa mh. Lema ulikuwa ni wetu wana-arusha. Sisi arusha rufaa yetu tunayo mkononi tunasubiri wakati wa uchaguzi mdogo arusha ndio itakuwa rufaa yetu rasmi. Na hii rufaa tutakayokata wananchi itakuwa na mwangwi mkubwa mpaka kusini mwa tanzania kama kule mtwara, lindi na pengine. Magamba mtajibeba
 
Askofu Lebulu -''vikundi vya watu vinakaa kwa siri na kupanga mbinu za kumwangamiza mtu asiye na hatia na wakati mwingine hata kuhonga mahakama zipotoshe hukumu dhidi ya mnyonge''. Mwananchi newspaper report today
 
Uhuru wa mahakama ni rahisi kuutamka kwa nadharia kuliko Kutenda. Kama kuna mtu atafanya utafiti juu ya uteuzi wa Majaji sina Shaka hatashangaa juu ya vigezo vinavyotumika kuwateua waheshimiwa hawa. Jibu la chagamoto hii ni Kwenye katiba mpya.
Unachosema ni kweli, lakini kwa suala la hukumu hii juu ya Lema haifai kuwa sehemu ya kumbukumbu za sheria za nchi hii. Ninaimani kwa suala hili mahakama ya rufaa itakataa kutumiwa na CCM, na serikali yake na hivyo majaji wataona aibu na kumrudishia Lema Ubunge wake.
 
Kwa mujibu wa M Kiti wa CDM Mhe Freman Mbowe, CDM itatoa kauli rasmi jumamosi hii, kama kitakata rufaa au kitakubali maamuzi ya mahakama. Hii inatokana na kwamba kukubali uamuzi wa mahakama kunaweza kutafsiriwa kama uamuzi huo uko sahihi kabisa. Mhe amesama wanaheshimu taratibu za mahakama, lakini wamepokea uamuzi huo kwa mshituko mkubwa. Ili kuonyesha ulimwengu kwamba hawakutendewa haki basi wanaweza kuamua kukata rufaa. Aliongeza kwamba hawaogopi uchaguzi lakini haki lazima iheshimiwe.

Dr Bana amesema kuna uwezekano mkubwa sana wa CDM kulirudisha jimbo hilo kwa sabau ni ngome kubwa ya CDM

(Mahojiano Redio ya Ujermani leo saa 12)

Soma pendekezo la Mwana JF (Atigi) hapa chini:

Uamuzi wa Chadema na Lema kukata rufaa ni wakurahisha na kupongezwa sana. Katika uzi nilioweka uliosema ''Chadema na Lema lazima wakate rufaa kupinga hukumu'' nilitoa sababu za lazima kwa rufaa hiyo. Lakini nilishambuliwa sana na kuitwa majina mbalimbali. Nilisimama imara kwa kuwa nilijiridhisha kuwa ilikuwa ni lazima kukata rufaa kwa kukuza demokrasia na kulinda hadhi ya mahakama hapa nchini, kumrudishia ubunge wake Lema, kutunga sheria zenye hadhi na kuendeleza M4C. Kwa namna ya pekee namshukuru Superman ambaye alielewa vizuri sana hoja nilizowasilisha. Pia shukurani ziende kwa Phillimoni Michael ambaye naye alitetea hoja nilizowasilisha. Bila kumsahau Mwanakijiji ambaye naye aliona namna jaji alivyoboronga katika hukumu yake. Kwa namna ya pekee nawaomba viongozi wa Chadema akiwemo Dr Slaa wapitie uzi ule niliowasilisha ambao ninauhakika unamasuala ya kufuatilia ili kukuza demokrasia nchini kwetu na kuiendeleza Chadema. Pia natoa changamoto kuwa katika kujadiliana tuwe tunaangalia hoja zilizopo si kuongozwa zaidi na hisia au vinginevyo. Ukifuatilia maneno niliyotupiwa utashangaa na kukubaliana nami kuwa ni vema kuelewa vizuri hoja za wenzetu.
 
atigi,kwanza habari yako. Mimi huwa napenda kuwa muwazi kwa sababu ni njia nzuri tu ya kumsaidia mtu. niombe samahani in advance kwa wale nitakao kuwa nimewakwaza. Naomba mnielimishe kwani nami napenda kujifunza.sina uhakika kama nitakuwa nimechelewa au la. Hoja zako umezigawa sehemu nne nami nitajaribu kutoa mtizamo wangu kwa mtindo huo huo, yaani-(1) haki haikutendeka.(2)kutekeleza M4C (3) kutathimini muhimili wa mahakama (4) kutunga sheria zenya hadhi.HAKI HAIKITENDEKA.Ilikuwa ni vizuri ukatupa dondoo chache za mwenendo wa kesi ambazo kwa mtazamo na sababu zako umeona hazikuwa sahihi. Lakini pia ni vyema tukaelewa tafsiri ya neno TUSI kwenye sheria ya uchaguzi. Naamini kabisa kwamba matusi kwenye kampeni yanaweza kupelekea hukumu kama hii. Nimeshindwa kulitolea mtizamo hili kwa kuwa sina sheria za uchaguzi. Naomba nisaidiwe kwa hilo.Nakunukuu "Mwanasiasa yoyote anayegombea inabidi mwenendo wake wa maisha uhojiwe ili kuona kama anaweza kushika madaraka ya kisiasa".kauli yako hii ni sahihi kabisa,lakini hakuna aliyesema kuwa Mh Lema hakuwa na sifa za kushika madaraka. Kumbuka kuwa baada ya kuonekana kuwa anafaa ndio alipitishwana alienda kuanza kampeni. Kosa hili inasemekana kuwa amelitenda katika kampeni ina maana BAADA ya kuonekana kuwa anafaa kugombea.hapa nafikiri haki ilitendeka.Nakunukuu tena "Wote tunatambua namna maisha ya wagombea wa Chadema yanavyohojiwa wakati wa chaguzi Mbalimbali, za ubunge na uraisi. Na hii ni haki kwa wananchi kujua, siyo kosa". Ni kweli kabisa mkuu wangu kuhoji sio kosa. kilichokuwa kinasemekana NI KUTUMIA lugha ya MATUSI. Nakunukuu tena "Pamoja na mapungufu ya kutungwa kwa kosa, pia hakuna uthibitisho wa nguvu wa hicho kinachoitwa kosa kuwa Lema alikifanya. Ni ushahidi wa kutunga wa maneno, hakuna ushahidi wa maandishi wala sauti katika mkanda wala CD kuwa Lema alitoa matamshi yaliyotungiwa mashitaka". Kaka,hapa unakiri kuwa kulikuwa kuna uthibitisho wa kosa kutendeka lakini haukuwa wa nguvu, nafikiri mahakama ilitumia uthibitisho huo mdogo, ambao wewe unakiri kuwepo, kufikia uamuzi.
kuhusu ushahidi unaousema wa maandishi na CD. Aliyesikia kauli
zinazosemwa kuwa ni matusi anaweza kuja kutoa ushahidi akasimama badala ya CD na ndio ushahidi mzuri, hata hiyo CD bado ingehitaji mtu kuja kuitoa, hivyo katika hili nalo hakuna tatizo.
Ulitumia pia neno ‘kudodosa’. kilichokuwa kinabishaniwa ni lugha inayoitwa ya matusi.nafikiri kudodosa na kutukana ni tofauti.ingawa katika kudodosa unaweza tukana.Hivyo katika eneo lako la HAKI HAIJATENDEKA nimeona hizi zilikuwa ndio sehemu muhimu lakini hujanishwawishi bado na hujaeleza haki haijatendeka vipi.KUTEKELEZA M4C.Hili wala sina ubishi nalo kwani mabadiliko ndio tunayoyataka ili sote tuwe na maisha na mazuri.Big Up.KUTATHIMINI MUHIMILI WA MAHAKAMA.Mhh,sidhani kama CDM ina uwezo huo. Napenda kuwa wazi tu, huwezi kutathimini muhimili wa Mahakama kwa kukata rufaa. Hiyo itakuwa ni kutathimini mwenendo wa kesi na kutafuta mapungufu kwa ajili ya kukata rufaa. Hiyo ni haki ya msingi ya kila mtu na wala sio kigezo cha kutathimini muhimili wa mahakama.Lakini pia nikukumbushe kuwa utakuwa umetathimini utendaji wa Jaji huyo mmoja tu aliyetoa hukumu.Mahakama ya juu kutengua uamuzi wa mahakama ya chini ni katika kutekeleza moja ya majukumu yake kama chombo cha sheria na hata kama haitafanya hivyo haina maana kuwa itakuwa imedhalilishwa. Kukata rufaa si jambo geni limeanza zamani sana na ndio limezaa ‘Case Laws’. Sheria sio hesabu kuwa 1+1=2. Hapana, Sheria ni namna utakavyoweza kutetea hoja yako mahakamani ili kuishawishi mahakama ikubaliane na wewe au ikubaliane na sababu zako za kukata rufaa.lakini hii haina maana kuwa vigezo vya msingi virukwe na mahakama wakati wa kufikia maamuzi kwa sababu tu sheria sio 1+1. Eneo hili ndilo ambalo huwa linaleta matatizo mara nyingi. sasa sijui kwenye kesi hii kama eneo hili halijakuwa temperedMimi sio mtaalamu wa sheria lakini wanaojua sheria watatusaidia ili siku nyingine tuweze kujikwamua na tusitumie sheria za kwenye vijiwe vya kahawa kutoa hoja.lakini naamini kuwa kutathimini muhimili wa mahakama kama unavyosema inahitaji watu wenye upeo wa juu sana wa sheria. ndio maana natia shaka.KUTUNGA SHERIA ZENYE HADHI.Katika eneo hili la kukataa sheria unazosema za hovyo,mimi naona kama kukata rufaa sio kuikataa sheria, sheria inabaki kama ilivyo. Isipokuwa unapinga tafsiri tofauti liyotumika kwenye kufikia maamuzi kinyume na inavyotakiwa na sheria husika.au unapinga mwenendo wa kesi kuwa haukuwa sahihi.Mfano, WIZI maana yake, mtu yeyote atakuwa ametenda kosa la WIZI endapo:· Bila ya halali atachukua mali ya mtu mwingine.· Kwa lengo la kuitaifisha moja kwa moja.· Kitu hicho kiwe na thamani,n.k(Samahani wenye fani yenu)Huu ni mfano tu sina maana kuwa ndivyo vigezo vya wizi.Sasa basi, kama vigezo hivi havijakamilika na hakimu akatoa adhabu. Aah, hapa lazima rufaa ikatwe.lakini Je? Hapa ukikata rufaa unapinga sheria au tafsiri tofauti iliyotumika katika sheria? au mtazamo corrupt wa hakimu muhusika? na je hii sheria ni ya hovyo au hakimu ndiye wa hovyo? Hivyo wananchi hawatakataa sheria za hovyo, bali watakataa matumizi hovyo ya sheria yanayofanywa na wasimamizi wa sheria hizo. Kuhusu suala la kukataa hukumu hii kuingizwa katika nukuu za sheria,nafikiri hapa unamaanisha case laws. Kama maamuzi ya kesi hii yatawekwa kwenye nukuu za sheria,madhara yatategemea maamuzi baada ya rufaa. Kama CDM itashinda basi nukuu itakuwa kwa ajili ya kupinga conviction kwa kesi yoyote ile ambayo itafanana na hii.jambo hili litakuwa zuri kwa wananchi.rufaa Ikishindwa, nukuu itakuwa kwa ajili ya kushindilia hukumu. Hiki nafikiri ndio usichokitaka. Hivyo tusianze kuikataa nukuu kabla ya matokeo ya rufaa. NINI KIFANYIKE. Kwa kuwa mimi si mtaalamu wa sheria.siwezi kusema kuwa ninachokisema ni sahihi sana. ndio maana nasema ni mtazamo wangu.Naamini kuwa CDM wanatafuta mapungufu yaliyojitokeza katika mwenedo mzima wa kesi ili waweze kukata rufaa. Wana wataalamu wa sheria ambao wanajua nini kifanyike na kama kuna upotoshwaji wa sheria LAZIMA watakata rufaa. NAWAAMINIA. wanajua nini wanafanya kuliko tunavyozani mimi na wewe.‘
 
Back
Top Bottom