Jumakidogo
R I P
- Jul 16, 2009
- 1,851
- 417
Huenda alishatega timing bomb huko CDM na anaona linakaribia kulipuka! Haya mambo ya siasa magumu kweli. Watu hatukuamini kama NCCR ingesamabaratika na kubaki historia. Nikikumbuka NCCR ya 1993 ikaja ile ya Mrema ya 1995 na kisha ukaja ule msambaratiko wa Tanga naogopa. Nikikumbuka akina Marando, Selasini na Komu kuwa walikuwepo Tanga siwezi kusema kitu hadi tufike 2015 na kuipita CDM ikiwa salama.
Mkuu bomu lipo tayari, ni Shibuda. CDM wasiposhituka na kulitegua mapema. Anachosema Wasira kitatokea , nadhani mitambo wameshaiseti tayari na pandikizi lao limeanza kutema cheche.