Wakuu habari za weekend. Wiki hii magazeti mengi yameandika habari za Sumaye kuteta na CDM kuhusu mipango yake ya kuangalia kujiunga na CDM. Ikumbukwe Sumaye ndiye waziri mkuu ambaye wakati wa utawala wa awamu ya tatu alisimamia ubinafsishaji wa mali za umma. Na katika hilo mali nyingi alijiuzia ikiwemo MT MERU HOTEL ya Arusha.
Inashangaza sana leo hii huyu ambaye ni fisadi anawesema wenzake kuwa ni mafisadi. Hivi yeye na Lowasa nani ni msafi. Asitake kuwadanganya watanzania kuwa anapigania haki zao wakati alishindwa akiwa waziri mkuu.
Tahadhari tu, iwapo CDM watampokea huyu jamaa, basi wajue ndoto yao ya kuongoza nchi ndiyo mwisho, kwani watu wengi watakimbia na kuona nacho ni chama cha mafisadi.
CDM inatakiwa ijifunze kwa Shibuda, watu wanaojiunga nacho ili wapate uongozi kamwe hawatasaidia Chama zaidi ya kukivuruga kwa uchu wa madaraka.
Inashangaza sana leo hii huyu ambaye ni fisadi anawesema wenzake kuwa ni mafisadi. Hivi yeye na Lowasa nani ni msafi. Asitake kuwadanganya watanzania kuwa anapigania haki zao wakati alishindwa akiwa waziri mkuu.
Tahadhari tu, iwapo CDM watampokea huyu jamaa, basi wajue ndoto yao ya kuongoza nchi ndiyo mwisho, kwani watu wengi watakimbia na kuona nacho ni chama cha mafisadi.
CDM inatakiwa ijifunze kwa Shibuda, watu wanaojiunga nacho ili wapate uongozi kamwe hawatasaidia Chama zaidi ya kukivuruga kwa uchu wa madaraka.