Nimefurahishwa sana na CHADEMA kuichangamkia na kujiorodhesha kwa wingi kuchangia hotuba ya Rais Kikwete aliyoitoa bungeni, kumbe waliipenda. Hapa sasa nimegundua kuwa kumbe ile hotuba ilikuwa nzuri na muhimu kwa mustakabali wa nchi, na nimeshangaa kwa jinsi CHADEMA walivyo ipenda na kujiorodhesha wengi, ambapo ilistahili wale waliokuwemo siku hiyo bungeni ndio walitakiwa waichangie tu. Siku zingine CHADEMA mkae mumsikilize Rais , mnachangia nini sasa ili hali nyie mlikataa hotuba yake ?. Mmeziba nafasi bure za wale ambao walitakiwa halali kuchangia.